Mwanafunzi wa Feza ashangaa wanaofeli mtihani wa NECTA

Mwanafunzi wa Feza ashangaa wanaofeli mtihani wa NECTA

Dogo mbona km kashaleft group mapema sana?!, anyway, hapo hamna cha maana alichoongea zaidi ya kiburi, dharau, majigambo.
Maisha ya watoto na wadogo zetu hayafanani na yake. Wadogo zetu wengi wao ndo baba, ndo mama nikiwa na maana ya wanajitafutia kula, wanajitafutia ada, n.k.
Wewe nd umeamua kuangalia swala negatively kwa makasiriko kwa dogo ambae kwanza ni mtoto na unamsingizia na mambo ya kijinga na ajabu na umasikini nd changamoto yako. Dogo alichozungumza hata shuleni tulikuwa tunazungumza hivo hivo kuwa tujitahidi labda mock exams au mitihani ya walimu kwa kuwa necta ni nyepesi sana. Nd maan hata dogo kasema mtu asifocus na necta maan ni nyepesi ila ajikite kwenye mazoezi mengi kwa kufanya mitihani ya kutosha ya kujipima na nd jinsi elimu za shule nyingi zinazojitambua zinafanya hivo kuna hadi ile mitihani ya kutungiana wanafunzi kwa wanafunzi.
 
Sema kweli kufeli NECTA kwamba ukose 1,2,3 hata 4 ya kwenda certificate inashangaza sana tena hasa kwa kizazi hiki cha form 4 cha utawala wa Mwendazake na kuendelea na hii haijalishi umesoma kayumba au laah.
Kipindi tunamalizia advance Kuna paper ya adv mathematics ilikua ya motoo Hadi walimu wetu wakalalamika kuwa aliyetunga mtihani akuzingatia vigezo.
Na vigezo alivyotaja mwalimu ni kuwa alitakiwa aweke maswali yenye kupima slow middle na fast learners
Kwahiyo unaona hapo Kila mtu alitakiwa apate angalau hata S tu
 
Nyie wapuuzi mnaosema huyo mtoto kaleft group.

Mnakosea tena Mnakosea Sana
Mnataka mtu aweje mseme ili mridhike kwenye nafsi zenu, Binafsi ushoga naupinga sana tuu. Lakin siwez kujitoa akili na kusema huyo mtoto ni Shoga. Watu hamna Exposure kabisa hamjakutana na vitu tofauti, hamjaona watu tofaut. Kila siku mko na watu wa level zile zile hapo mnajifunza nini ??

Huyo ni mtoto mdogo tuu around 16 or less bado hajakomaa kama wewe hapo, Maisha yake ni tofauti na yale uliyokulia wewe huko kwenu(analala pazuri, anakula vizuri, hana stress za kipuuzi, hateswi kwao, ana malengo yamenyooka)

He speaks his mind with honestly voice. Kama umekosa cha kusema ni bora useme huyu mtoto NI PHYSICALLY WEAK na sio eti KALEFT GROUP mlaaniwe wote mliosema hivyo.

Watu Kama Benjamin Fernandes mmiliki wa Nala pia mtasema Ni shoga sababu tu ya tone yake ya kuzungumza and being humble guy. Watu wajinga kama hao huko juu wanatak u'act rude eti ndio kidume

Imeniuma Sana, kwa kweli badirike Jaribuni kua " Open minded " msisemee watu vibaya tofaut na uhalisia
 
Dogo yuko sahihi, mitihani ya NECTA iko predictable, inalenga more kwenye reproduction of knowledge than application of knowledge.

A smart student hawezi ku-fail. Mimi nilifaulu mitihani yote na watoto wangu hawafanyi hiyo mitiani.

Mwisho, mimi siamini kama mitihani ni kipimo sahihi cha kupima uelewa. Nadhani imewekwa ili ku shortlist wanafunzi kwakua nafasi za masomo huko mbele ni chache

System nzuri ni kuwa na continuing assessments not examinations. Nadhani nchi zilizoendelea wanaondoa mitihani kwenye mifumo yao ya elimu
 
Wakati nipo O level mpaka form four sikuwai dhani eti kuna issue za kutafuta credits...kwanza unaanzaje hata kupata C grade kwenye somo?

Mimi nilikua najua kufaulu ni lazima tu, labda kwasababu ya shule niliokuwapo.
 
Watu wamekasirika wakati dogo kaongea ukweli tupu.
Kwa sasa mwanafunzi hapaswi feli wakati notisi zimejaa kila mahali.

Wazazi hawafatilii maendeleo ya watoto wao hivyo mtoto aende au asiende shule haiwahusu.

Watawala na watawaliwa huandaliwa na wazazi
Ni kweli notes kila mahali, lugha ya kuzielewa imo?
 
binafsi nimesoma kwenye moja kati ya hizo shule kubwa, msifuate sana mkumbo wa kupeleka watoto shule hizo, wanachagua watoto wenye akili tu. Nakumbuka interview tulikua tunafanya watu zaidi ya 5000 tanzania nzima, lakini tukachukuliwa 180 tu.... walisema wanaangalia waliofaulu hisabati kuanzia alama ya 85% kwenda juu, halafu wanachukua top 180 kutoka hapo.....

Ingekua wanachukua watoto ambao wako taratibu kujifunza halafu wanawafaulisha, basi hapo ndo wangekua wako vizuri. Wanachuja wanafunzi wazuri ili wafaulishe sana, halafu hii dhana waitumie kwenye marketing....
 
Back
Top Bottom