Mwanafunzi wa Feza ashangaa wanaofeli mtihani wa NECTA

Mwanafunzi wa Feza ashangaa wanaofeli mtihani wa NECTA

Sio kazi yake kuzungumzia aliyeshinda nafasi ya kwanza na ya pili, tafuta mahojiano yao ujue wamesema nini. Yeye kahojiwa katoa hoja zake na kajibu maswali yake.

Yeye kashangaa kwanini watu wanafeli, ni sawa na mtu mwingine akishangaa kwanini watu wanaenda kwa waganga na mwingine anashangaa kwanini wanaenda kwa Mwamposa. Hakuna sehemu kadhihaki mtu.

Na katoa maoni juu ya mitihani ya NECTA ilivyo. Mnalazimisha mtoto awe na hekima ambazo wazee wengine humu hawana. Mnalazimisha atambue maisha yenu ambayo hayajui ndio maana kasema anashangaa. Mnalazimisha ajue umaskini wa wengine ambavyo sio kazi yake na hana haja ya kuujua kwa umri wake.

Mtoto mdogo mnamletea hasira na kumuombea mabaya
Dogo yupo sahihi
 
Ni kada muhimu sana kwa vijana wenye ujuzi na maarifa ya mashindano mbali mbali ya michezo kama mpira wa miguu ambapo vijana hao hutumia ujuzi na maarifa yao kubashiri matokeo ya michezo mbali mbali na kujipatia pesa halali ya kujikimu

View attachment 2622183
Nimecheka sana wallahi. Maelezo uliyoweka hapo na picha husika ya tukio vimeshindwa kulandana

Picha inaashiria kuwa Betting ni adhabu inayomkabili St Kayumba
 
Nyie wapuuzi mnaosema huyo mtoto kaleft group.

Mnakosea tena Mnakosea Sana
Mnataka mtu aweje mseme ili mridhike kwenye nafsi zenu, Binafsi ushoga naupinga sana tuu. Lakin siwez kujitoa akili na kusema huyo mtoto ni Shoga. Watu hamna Exposure kabisa hamjakutana na vitu tofauti, hamjaona watu tofaut. Kila siku mko na watu wa level zile zile hapo mnajifunza nini ??

Huyo ni mtoto mdogo tuu around 16 or less bado hajakomaa kama wewe hapo, Maisha yake ni tofauti na yale uliyokulia wewe huko kwenu(analala pazuri, anakula vizuri, hana stress za kipuuzi, hateswi kwao, ana malengo yamenyooka)

He speaks his mind with honestly voice. Kama umekosa cha kusema ni bora useme huyu mtoto NI PHYSICALLY WEAK na sio eti KALEFT GROUP mlaaniwe wote mliosema hivyo.

Watu Kama Benjamin Fernandes mmiliki wa Nala pia mtasema Ni shoga sababu tu ya tone yake ya mazungumzo and being humble guy. Watu wajinga kama hao huko juu wanatak u'act rude eti ndio kidume

Imeniuma Sana, kwa kweli badirike Jaribuni kua " Open minded " msisemee watu vibaya tofaut na uhalisia
Hao ni vilaza, wachawi, wenye wivu na husda. Pia wapewe kombe au kama vipi serikali ianzishe tuzo ya maskini bora wawe wanashindana maana haiwezekani binadamu mwenye akili timamu ajivunie shida na umaskini. Ni punguani tu atajisifia ujinga na kumponda aliyefanikiwa.

Hapa angekuwa wa mwisho na kupata dungu hao wangekuja kumpongeza, akili zao ziko reverse.
Kwanza huyo dogo hapo alipo tiyari anawazidi akili na uzee wao. Katoa ushauri, maoni na kajibu maswali ila wanamkasirikia kama vile kaweka sheria.
1. Kasema wanafunzi wajipime na mitihani mingine maana NECTA ni rahisi. Kama mtu unaona ni upuuzi sio kesi, kawaazishie wanao ligi ya singeli na kucheza rede wasubiri NECTA.

2. Kasema NECTA ni rahisi. Ni maoni yake, kama unapinga mwambie mwanao NECTA ni ngumu akiingia kwenye mtihani azimie.

3. Kashangaa wanaofeli. Ajabu iko wapi? Mbona humu kuna watu mnashangaa wanaofaulu kama yeye, tena yeye hajawatafutia visingizio waliofeli ila nyinyi mnataja mara umaskini, mara yeye kisa wana hela.

Au serikali ianzishe tuzo ya umaskini maana watu wanaupenda sana. Ndio maana mwanasiasa akijiita mnyonge raia wanajigaragaza mtaani, wakati familia yake haijui shida.
 
Simshangai huyo mtoto.Mimi mwenyewe nilipokuwa mdogo nilikuwa nashangaa mtu anafeli vipi.Mpaka namaliza chuo kikuu sikuwahi kufeli.Ila maisha yamenipiga na kitu kizito kichwani najiuliza waliotajirika wamewezaje?🤣🤣🤣
Pole mkuu
 
Watu wamekasirika wakati dogo kaongea ukweli tupu.
Kwa sasa mwanafunzi hapaswi feli wakati notisi zimejaa kila mahali.

Wazazi hawafatilii maendeleo ya watoto wao hivyo mtoto aende au asiende shule haiwahusu.

Watawala na watawaliwa huandaliwa na wazazi
Sasa mzazi kutwa kufatilia mambo ya kina mondi kajala konde kiba na kwa upande wa baba kutwa kubishana mambo ya mpira
Mtoto atatoboa kweli

Ova
 
Sasa mzazi kutwa kufatilia mambo ya kina mondi kajala konde kiba na kwa upande wa baba kutwa kubishana mambo ya mpira
Mtoto atatoboa kweli

Ova
Na hili swala litaendelea kuwepo kadri siku zinavyoenda, wazazi wasipoona umuhimu wa shule, hawawezi somesha watoto wao na kuwakazania wasome
 
Back
Top Bottom