Wanafunzi wa vyuo vikuu badilikeni, msikae kisekondari humo vyuoni. Harakati nyingi kokote duniani zinahamsishwa na wasomi wa vyuo vikuu kama ninyi, ingawa utekelezaji wake wawezafanywa na makundi mengine. Ninyi ndo mna macho kwa maana ya akili kujua wapi serikali inakosea. Nachotaka kusema hapa ni kwamba mnatakiwa kuanzisha maandamano ambayo yatasambaa nchi nzima kuitaka serikali kurejesha amani na utulivu ktk vyuo na nchi kwa ujumla. Msisome tu kama kindergaten. Tafadhali, mabadiliko yanaanzishwa na ninyi. Kama msomi analalamika, bibi yangu wa Namanyere au Mbagala maji matitu afanyeje?