Mwanafunzi chuo kikuu UDSM apigwa risasi- Afariki

Mwanafunzi chuo kikuu UDSM apigwa risasi- Afariki

Status
Not open for further replies.
Ni mwendawazimu tu ndie atakae husisha tukio hili na kauli ya Mha. Waziri mkuu. Mungu amponye msomi wetu.
 
Pole sana Mwanafunzi Mwenyezi amponye ampe afya ,Kwa kauli ya PINDA(Pm) sijui jamaa alikuwa mbishi hakutii amri" akapigwa tu"na wakaidi wapigwe tu-lakini na hao vibaka wameshindwa kwenda kuvunja benk wanakuja kwa wachumia njaa wenzao?si kuna kituo cha polisi pale chuo utawala hawakufika?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

poleni sana wanafunzi wote wa chuo cha mlimani. nchi yetu haina amani polisi wapo busy na chadema cha wanyonge. poleni sana Mungu awatie nguvu.
 
poleni sana wanafunzi wote wa chuo cha mlimani. nchi yetu haina amani polisi wapo busy na chadema cha wanyonge. poleni sana Mungu awatie nguvu.
 
Ndugu jf kwa masikitiiko makubwa mwanafunzi wa chuo kikuu aliyepigwa risasi usiku wa leo na majambazi amefariki dunia asubuhi mapema leo..
R.I.P Alex
 
Poleni ndugu, jamaa na watanzania wote kwa kumpoteza mtanzania mwenzetu
 
....kwa habari iliyonifikia hivi punde, wanafunzi wakiwa darasani maeneo ya Yombo-UDSM ghafla wamevamiwa na majambazi waliofanikiwa kuwapora laptop zao na kumjeruhi mwanachuo mmoja wa mwaka wa Nne-Sheria kwa risasi ambaye inasemekana yuko mahututi....japo amekimbizwa Hospitalini. Ni taaruki tupo sasa Chuoni hapo, na Walinzi wa Chuo haonekani hata mmoja.

Kwa habari kamili tutaendelea kujuzana, kwa kadri nitakavyo kuwa nazipata

Hii ndio habari ilio kamilika...sio ya juu!
 
OMG
RIP Alex
Uzembe wa watawala kwenye uwajibikaji wa majukumu ndio sababu ya watanzania kuteketea!
 
Mungu amlaze mahali pema peponi, ninaamini hapo ndo kazi ya polisi ilitakiwa kufanyika, nguvu kubwa ilipelekwa Arusha kutibua mkutano wa CHADEMA
 
Inasikitisha sana, tumepoteza NGUVU KAZI muhimu ya TAIFA kwani alikuwa akijiandaa kuhitimisha masomo ya shahada katika sheria. Tunaomba serikali isikie vilio vya wanafunzi wa elimu ya juu, kwani wamekuwa wakivamiwa kila mara na kuporwa mali zao pamoja na kudhuriwa. Serikali inajukumu la kuchukua hatua madhubuti kuhusiana na uhalifu kuongezeka sana katika vyuo vya elimu ya juu.

Nawapa pole wale wote walioguswa na msiba huu mchungu, Mungu awaoe faraja zake na ujasiri wa kulikubali tukio hili. Mungu amlaze pema mpendwa wetu Alex.
 
Ndugu jf kwa masikitiiko makubwa mwanafunzi wa chuo kikuu aliyepigwa risasi usiku wa leo na majambazi amefariki dunia asubuhi mapema leo..
R.I.P Alex

Poleni sana. Inawezekana ulishaileta tena hii stori, hebu tukumbushe... Ni yupi, wa chuo gani, ailikuwaje, nk...
 
Hivi hawa policcm kazi yao ni nini. Hii siyo mara ya kwanza kwa wanafunzi kuvamiwa, kuibiwa mali zao, kujeruhiwa, kufanyiwa kitu mbaya-IFM. Ni hivi karibuni matukio ya kutisha yametokea katika taasisi za elimu nchini mfano Chuo cha Uuguzi DOM, AIA,IFM na sasa UDSM. Cha kushangaza wanaofanya mambo haya hawakamatwi. Je; hawa policcm ni mpaka Kamanda wao avamiwe ndio usikie kuna watu wamekamatwa?
MKUU hujui? Kazi yao ni kuidhibiti CHADEMA
 
Inasikitisha sana, tumepoteza NGUVU KAZI muhimu ya TAIFA kwani alikuwa akijiandaa kuhitimisha masomo ya shahada katika sheria. Tunaomba serikali isikie vilio vya wanafunzi wa elimu ya juu, kwani wamekuwa wakivamiwa kila mara na kuporwa mali zao pamoja na kudhuriwa. Serikali inajukumu la kuchukua hatua madhubuti kuhusiana na uhalifu kuongezeka sana katika vyuo vya elimu ya juu.

Nawapa pole wale wote walioguswa na msiba huu mchungu, Mungu awaoe faraja zake na ujasiri wa kulikubali tukio hili. Mungu amlaze pema mpendwa wetu Alex.

Kama alivyoagiza Mr. Handsome wa ccm Mh. Pinda kwamba hao waombolezaji wa huyo mwanafunzi mwenzao hawatakiwi kuuliza chochote, wala kukusanyika wala kwenda kuzika, kwa sasa polisi watakuwa bussy wakiendelea na uchunguzi wa huyo JAMBAZI, hivyo ole wao wasitii amri ya Polisi, WAPIGWE TUUUU!!!!!

 
Msiba wetu wote huu, mambo yakuanza kulaumu Serkali hayana tija nikama muendelezo wa siasa chafu. Tuache kufanya siasa mpaka kwenye misiba.
 
Wakikaidi KUPORWA WATAPIGWA TU NA WAPIGWE TU.. Ee Mungu kwa nini umetupa viongozi kama hawa.
 
Ni matokeo ya awali kabisa ya majibu ya waziri wetu mkuu.
 
polis wao adui ni chadema na nguvu kibwa naweka kupambana na chadema badala ya kuwalinda raia.
 
Kwanza kabisa niwape pole wanafunzi wa UDSM kwa yaliyotokea, pili niwapongeze kwa umoja na mshikamano usiyoangalia maswala ya siasa kama wengi wetu tunaochangia ujinga katika maswala ya msingi. Nawapongeza maana baada ya tukio lenyewe wanafunzi walikimbia mbiyo kali mpaka kituo cha afya cha chuo kuomba msaada wa ambulance bahati nzuri mwanafunzi mwenzao anayeishi hall six alichukua gari yake akamuwahisha pale dispensary akapewa huduma ya kwanza haraka iwezekanavyo na kukimbizwa Muhimbili.

Kwa masikitiko makubwa nachukua nafasi hii kuwaasa wana JF kuwa makini na statements zinazotuweka katika hali tunayodhani ni sifa kuzitamka au ni kumkomoa mtu au chama kumbe ni kujipalia makaa ya moto. Eti tanzania siyo sehemu nzuri ya kuishi alafu wewe uko wapi? wewe ni mtanzania kweli? au ndicho chama chako kinachokufunza kushadadia? Eti Pinda amesema watu wapigwe tu hivyo majambazi nao wapige waue tu maana wameruhusiwa na pinda, unadhani chama chako kikiingia madarakani ndiyo utakuwa mwisho wa ujambazi, USA hamna ujambazi? chama chako kikiingia madarakani mtaandamana na kuvunja amani bila polisi kuwazuia? Lets think positive as wazalendo siyo kumwaga unga, ugali na mboga.

Mh. John bukuku wa Full Shangwe, mimi nilifika pale hosipitali ya chuo wakati huyu bwana alivyokua ameshapelekwa Muhimbili, ila askari walifika baadae, ni kweli kulikua na uzembe kwa askari. Hilo la kwamba uongozi wa chuo ulipigiwa simu haukufika kutoa msaada kwa wakati si kweli maana walimpeleka hosipitali ya chuo walisema hawakuanza kazi ya kufatuta uongozi wa chuo bali kazi ya kumpeleka mwenzao hosipitali na lilifanyika kwa haraka. Kumbuka baada ya kusikia risari imepigwa vijana walitaharuki na kutawanyika kwanza ndipo wakaanza makelele kuwaita wenzao huku wengine wakikimbia kituo cha afya chuoni kuomba msaada wa usafiri lakini kumbe huku nyuma mwenzao aliyepo hall six kama nilivyoeleza awali alijitokeza na kutoa usafiri kwenda hosipitali na kwenda kituo cha polisi kupata PF3 wakati mwenzao anapewa huduma ya kwanza na hilo lilifanywa kaw haraka sana. Manesi wa Chuo walifanya kazi ya ziada maana ni muda mfupi tu mfanyakazi wa chuo alikua amepelekwa hapo na kufariki kwa ugonjwa.

Mwisho nawasihi ndugu zangu tuache kuchangia mada kiitikadi au kwa kushabikia siasa, tuangalie mustakabali ya nchi yetu kwanza vyama baadae.
 
Kwanza kabisa niwape pole wanafunzi wa UDSM kwa yaliyotokea, pili niwapongeze kwa umoja na mshikamano usiyoangalia maswala ya siasa kama wengi wetu tunaochangia ujinga katika maswala ya msingi. Nawapongeza maana baada ya tukio lenyewe wanafunzi walikimbia mbiyo kali mpaka kituo cha afya cha chuo kuomba msaada wa ambulance bahati nzuri mwanafunzi mwenzao anayeishi hall six alichukua gari yake akamuwahisha pale dispensary akapewa huduma ya kwanza haraka iwezekanavyo na kukimbizwa Muhimbili.

Kwa masikitiko makubwa nachukua nafasi hii kuwaasa wana JF kuwa makini na statements zinazotuweka katika hali tunayodhani ni sifa kuzitamka au ni kumkomoa mtu au chama kumbe ni kujipalia makaa ya moto. Eti tanzania siyo sehemu nzuri ya kuishi alafu wewe uko wapi? wewe ni mtanzania kweli? au ndicho chama chako kinachokufunza kushadadia? Eti Pinda amesema watu wapigwe tu hivyo majambazi nao wapige waue tu maana wameruhusiwa na pinda, unadhani chama chako kikiingia madarakani ndiyo utakuwa mwisho wa ujambazi, USA hamna ujambazi? chama chako kikiingia madarakani mtaandamana na kuvunja amani bila polisi kuwazuia? Lets think positive as wazalendo siyo kumwaga unga, ugali na mboga.

Mh. John bukuku wa Full Shangwe, mimi nilifika pale hosipitali ya chuo wakati huyu bwana alivyokua ameshapelekwa Muhimbili, ila askari walifika baadae, ni kweli kulikua na uzembe kwa askari. Hilo la kwamba uongozi wa chuo ulipigiwa simu haukufika kutoa msaada kwa wakati si kweli maana walimpeleka hosipitali ya chuo walisema hawakuanza kazi ya kufatuta uongozi wa chuo bali kazi ya kumpeleka mwenzao hosipitali na lilifanyika kwa haraka. Kumbuka baada ya kusikia risari imepigwa vijana walitaharuki na kutawanyika kwanza ndipo wakaanza makelele kuwaita wenzao huku wengine wakikimbia kituo cha afya chuoni kuomba msaada wa usafiri lakini kumbe huku nyuma mwenzao aliyepo hall six kama nilivyoeleza awali alijitokeza na kutoa usafiri kwenda hosipitali na kwenda kituo cha polisi kupata PF3 wakati mwenzao anapewa huduma ya kwanza na hilo lilifanywa kaw haraka sana. Manesi wa Chuo walifanya kazi ya ziada maana ni muda mfupi tu mfanyakazi wa chuo alikua amepelekwa hapo na kufariki kwa ugonjwa.

Mwisho nawasihi ndugu zangu tuache kuchangia mada kiitikadi au kwa kushabikia siasa, tuangalie mustakabali ya nchi yetu kwanza vyama baadae.

well said. lakin ukwel ni kwamba polis hawafanyi kazi kwa weledi, nguvu kubwa ya polis inatumika kisiasa, tupo tunayaona wanavyo tumika, kuna vitu vingine sio mpaka uambiwe ni kujionea tu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom