Uchaguzi 2020 Mwana JF, be the first to know kuwa CCM ndio mshindi wa jumla wa Uchaguzi huu

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,494
113,590
Wana JF,

Maadam JF ni ukumbi wetu, na sisi humu JF, tuko members wengi, na tumefanya mengi, hivyo mimi member mwenzenu Pascal Mayalla, naomba niwe wa kwanza, kuwajulisha wana JF wenzangu, ili kuwapa ile JF advantage ya wewe kama Mwana JF, be the first to know kuwa CCM ndio inakwenda kushinda uchaguzi mkuu huu kwa a landslide victory ya ushindi wa kishindo, kwa pande zote mbili za Muungano!

Ushindi huu ni kufuatia mimi mwana JF mwenzenu, Pasco Mayalla, nimesikia sauti ndani ya moyo wangu, yaani voices from within, kuwa katika uchaguzi huu, mshindi ni CCM!. Hii voices from within, is never wrong, maana ni sauti yake YEYE mwenyewe!

Kwa upande wa Tanzania Bara, CCM itashinda kwa kishindo kwasababu ya track record ya Magufuli, itaibeba CCM na kushinda kwa kishindo.

Kwa upande wa Zanzibar, kwa mujibu wa katiba, rais wa Zanzibar ni mjumbe wa cabinet ya JMT, Muundo wa serikali ya JMT, hatuna serikali ya mseto, ushindi ni by a simple majority, hata akishinda kwa kura moja, ni mshindi, and the winner takes it all. Hivyo mshindi wa Zanzibar lazima iwe ni CCM!.

Sasa kwa faida ya wasionijua, mimi Pasco Mayalla, ili muweze kuamini ninachowaambia ni kitu cha kweli na ndio kinachokwenda kutokea, naomba niwape ushuhuda wa nimewahi kuwa wa kwanza kwenye mambo mengi tu, je wewe mwana JF mwenzangu, wajua mimi Mwana JF mwenzako Pasco Mayalla, nimewahi kuwa Mtanzania wa kwanza kwenye mambo mengi tuu, ikiwemo humu JF, mimi ndiye Mwana JF wa kwanza kuwa kada wa Chama Cha Siasa? Tuanzie hapa
  1. Tangu kuanzishwa kwake, japo JF ina members wengi wa fani tofauti tofauti, lakini Pascal Mayalla, ndiye member wa kwanza kuwa recognized na modes wa JF kuwa ni kada wa chama cha siasa, hivyo kwenye nikipost chochote humu JF, chini kuna maandishi hutokea automatically yameandikwa "Pasco Mayalla sasa ni Kada wa Chama cha Mapinduzi, CCM", hii haina maana humu JF, kada wa chama cha siasa ni mimi tuu peke yangu, but it just happened, mimi ndie the first member wa JF, kuwa kada wa chama cha siasa!. Japo najua tuna makada wengi humu wa vyama vya siasa, na sijawahi kuona kada yoyote akiandikwa so and so ni kada wa chama fulani, then this means, mimi ndiye the first JF member to be kada wa chama cha siasa!
  2. Tangu Primary, na sekondari, somo la siasa, nilipata A, hivyo nilikuwa wa kwanza kwenye siasa, hata Chuo Kikuu, UDSM, kitivo cha sheria, somo la Katiba, lilifundishwa na Prof. Shivji, mimi somo lake nilipata A, na hata degree yangu ya sheria LL.B ya UDSM ni (hons), na iko tuu kabatini, mimi nikiendelea kuwa mwandishi wa habari, na inawezekana mimi ndie mwandishi wa habari wa kwanza, mwenye LL.B Hons, ambaye naendeleo kuandika and get nothing, badala ya kuwa wakili na kupiga pesa ndefu!.
  3. Nilipokuwa JKT Makotupora kwa mujibu wa sheria, mimi ndiye niliongoza somo la Range, na Parade, kwenye kupiga parade mwendo wa haraka, wakati wa kutoa heshima, mguu wangu huku umenyooka, ulipiga heshima kwa 90 degrees, hivyo kumaliza JKT, niliunganishwa moja kwa moja kujiunga na JWTZ, kule tukapigishwa depo mpya, kwa vile wito wangu haukuwa kuwa mjeda, niliaga rasmi JWTZ, nikajiunga na TSJ kusomea uandishi wa habari.
  4. Baada ya kuhitimu TSJ, nikajinga na RTD, kule nikashauriwa niende newsroom, kwasababu enzi hizo, kwasababu nilipenda utangazaji, nikawa ni mtangazaji wa kwanza wa RTD kuingia utangazaji na Diploma, enzi hizo watangazaji wengi ni form IV tuu.
  5. Nikiwa RTD, enzi hizo tukilipwa mshahara dirishani, kuna mahali moyo wangu ulimdondokea mtu, hivyo kuna siku baada ya kupokea bahasha ya mshahara, nilimkabidhi mtu, bahasha hiyo hivyo ilivyo, hivyo kuwa mtangazaji mpya wa kwanza aliye ...mshahara wake wote shauri ya kupenda!
  6. Nilijiunga Televisheni ya DTV mwaka 1995, na mimi ndie mtangazaji wa kwanza wa TV Tanzania kuhost TV Talk Show, ikiitwa "Mada Moto" kuzungumzia uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi. Kipindi hicho, kiliandaliwa na Mjerumani mmoja akiitwa Wolfgang Baraniek akishirikiana na Mtanzania, Beatrice Mugishagwe na kilidhaminiwa na wafadhili mbalimbali wa kimataifa, nilikuwa navuta TZS 1.M, mwaka 1995!, naomba msiniulize nilifanyia nini hizo pesa, ila mwaka huo ndio nilioa, na honeymoon yangu ni London nchini Uingereza!.
  7. Mimi ndio mwandishi wa Kwanza kutangaza matokeo yasiyo rasmi ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar ile 1995 kana kupelekae sheria kutungwa ni marufuku media kutangaza matokeo ya urais yasiyo rasmi
  8. Baada ya uchaguzi, ndipo Nikachukuliwa na Masai Studios, kuendesha kipindi cha Kiti Moto, nikiwa tena pioneer host wa talk shows za ukumbini, reality show.
  9. Mimi ndiye mwandishi wa kwanza wa Tanzania kuripotia Local TV, mikutano ya UNGA from New York kwa miaka mitano mfulululizo.
  10. Mimi ndiye mwandishi wa mwisho kufanya mahojiano na Baba wa Taifa kabla hajaugua, ambayo tuliyafanya The Bundes House, nchini Uswisi, na mimi ndiye mwandishi pekee wa Tanzania aliyekwenda kumtembelea Mwalimu hospitali ya St. Thomas inchini Uingereza, na kisha kuja kumzika Mwitongo.
  11. Mimi ndie the first journalist kutumia big bike kukusanyia habari, bike yangu ilikuwa kubwa na haina kiti cha abiria bali ina sanduku lenye video camera na still camera.
  12. Ni mimi ndie mwandishi wa kwanza kuripoti vurugu za Mwembe Chai.
  13. Mimi ndio mwandishi wa kwanza kuripoti vurugu za uchaguzi wa Zanzibar na kutiwa ndani kituo cha Mwembe Madema na Ali Saleh wa BBC
  14. Mimi ndiye mwandishi wa kwanza wa Tanzania kufanya VJ, yaani video journalist, unaandika mwenyewe, unapiga picha mwenyewe, unajirekodi mwenyewe, una edit mwenyewe, na unatuma story yenye piece to camera huku kila kitu umefanya mwenyewe
  15. Mimi ndiye mwandishi wa kwanza wa private media, kuandamana na misafara ya ziara za rais nje ya nchi, hivyo nimeandamana na rais Mkapa, na JK katika ziara kibao, kutokana na uwezo wa multi task.
  16. As a freelance journalist, mimi ndiye freelance wa kwanza nchini Tanzania kualikwa press conference za Ikulu, na kuuliza maswali magumu.
  17. Mimi ndio mwandishi wa kwanza wa habari nchini Tanzania, kuitwa na Kamati ya Bunge na kuhojiwa kutokana na Makala Zangu
  18. Humu JF, mimi ndiye mtu wa kwanza kuwaeleza watu humu Magufuli ndio atakuwa rais 2015!. Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli
  19. Mimi ndio the 1st kuwaeleza watu humu Makonda atakuwa RC wa DSM. Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam
  20. Mimi ndio the first kuwaeleza watu humu kuwa Mwanasheria mkuu wa Zanzibar atafutwa kazi. Dr. Shein Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Kabla Hajamwaga Sumu Hii
  21. Kwenye siasa, mimi ndiye mwandishi wa kwanza kuaga rasmi fani ya uandishi na kusema nitajiunga na siasa. Nimeamua Kustaafu Rasmi JF, Utangazaji na Uandishi wa Habari Baada ya Kuhudumu Miaka 30. Niko Free Kujiunga Siasa, Nimejiunga CCM na Nitagombea Ubunge
  22. Siku naanga rasmi media, mimi ni mwandishi wa kwanza kuaga rasmi from studio nikiwa live.
  23. Kumbe kuwa the 1st, pia kuna faida zake na hasara zake, kufuatia kuwa the 1st kwenye mengi, nilipojitokeza kutangaza nia Kawe, baada ya kupata the 1 vote, ikagomea hapo hapo!
  24. Kuna mambo mengi nimeyaeleza humu na yakatokea,
  25. Hivyo leo ninapowaeleza humu mshindi wa uchaguzi huu ni JPM na CCM, naombeni mniamini, na kwa msio amini, subirini October 28 ndipo mtaamini.

Nawatakia maandalizi mema ya October 28, sio kwenda kuchagua, bali kwenda tuu kuthibisha kilichochaguliwa tayari kwa ajili tuu ya kukamilisha taratibu za mchakato wa kukamilisha uchaguzi, kama ni kuchagua, watu siku nyingi, wameisha chagua mioyoni mwao, tarehe 28 ni kukamilisha tuu taratibu.

Pasco,
The First
 
CV yako haiondoi ukweli kuwa uko biased!

Isitoshe,hatuna chombo huru cha kusimamia na kuendesha uchaguzi ulio huru na wa haki hivyo huna uhalali wa kusema kuwa CCM atashinda.

Kazi yako kubwa hapa JF ni kufanya propaganda kwa lengo la kutaka kuwaaminisha watu(kuwaanda kisaikolojia) kuwa CCM itashinda kihalali wakati ukweli unaujua.

Mtu anayeogopa ushindani ndani ya chama chake ndio unakuja kutuambia atashinda?
 
Ulipata kura 1 bw. Mnafique,

Ndio maana jamaa yangu aliniambia ulikuwa miongoni wa washauri CCTV camera zing'olewe kufuta ushahidi, nikamgomea. Sasa naanza kuamini.

Unashangilia 'kura' za 'maruhani?' Wizi?! Kaibeni kura, mjitangaze

Wana JF jifunzeni kutofautisha "paka" na "kimburu". Haitawapa shida mkisoma ujinga wa Pasco.
 
Baki na CCM yako sisi tumeshashtuka

Mungu ibariki CHADEMA

Mungu ibariki Tanzania

Mungu mbariki Tundu Lisu

Screenshot_20201026-071802.jpg
 
CV yako haiondoi ukweli kuwa uko biased!

Isitoshe,hatuna chombo huru cha kusimamia na kuendesha uchaguzi ulio huru na wa haki hivyo huna uhalali wa kusema kuwa CCM atashinda.

Kazi yako kubwa hapa JF ni kufanya propaganda kwa lengo la kutaka kuwaaminisha watu(kuwaanda kisaikolojia) kuwa CCM itashinda kihalali wakati ukweli unaujua.

Mtu anayeopgopa ushindani ndani ya chama chake ndio unakuja kutuambia atashinda?!
 
Baada ya kuona kampeni imekwisha, naona umeporomosha CV ya kutafutia uteuzi. Aiseee!!

Magufuli hawezi kushinda Uchaguzi huu, hata mke wake katika mazingira ya uhuru kabisa hawezi na hataweza kumpigia Kura.

Labda, possibly uwezekano uliopo ni yeye kutangazwa mshindi katika mazingira magumu.

Anyway, ushaanza JF Star TV lini ?
 
Back
Top Bottom