Mwalimu Nyerere na ukabila

Mwalimu Nyerere na ukabila

wewe kweli una matatizo ya kuelewanimeainisha hapo faida za tv nyingi mpaka mashuleni zinatumikakama zanzibar waliweza kuwa na tv miaka hiyowe unafikiri tanganyika ingeshindikana vipi????vipaumbele vingeathiri vipi hilo?au kipaumbele cha kuchangisha watu pesa za mbio za mwenge we ndo unaona cha maana??????mnamsifia nyerere hata sifa ambazo sio zakeeti alijenga reli ya kati,na wakoloni waliacha reli ipi?????kusema tv ni anasana magari ni anasanamatrekta ni anasa ni mawazo finyu mnoperiod
Mkuu usiye na matatizo ya kuelewa, nimekubaliana na wewe kuwa ANGEWEKA KUANZISHA TV KWENYE VIPAUMBELE VYAKE ILI WABONGO TUFAIDI, hutaki tena??? Halafu punguza hasira ili uone vizuri, hakuna mahali nimesema kajenga reli ya kati... Mimi ni mmoja wa watu ambao hawaungi mkono hiyo 'mila' ya mwenge, pia sitegemei kwamba nipendezwe na misimamo yake %100, lkn hiyo hainifanyi nimuone mwenye mawazo finyu .
 
 
Last edited by a moderator:
Kwanza unakosea unaposema watu wengi walimpenda sana. Naomba kukufahamisha kuwa mimi nilikuwepo kabla, alipokuwepo, na baada yake. Nyerere hakupendwa na wengi kama unavyotakiwa kufikiria, Nyerere alilazimisha kupendwa, ukionesha kumpinga unapotezwa au unaswekwa ndani. Nyerere kisha koswa kupinduliwa mara nyingi tu kuliko Rais mwingine yoyote wa Tanzania.Mengine hayo utajaza mwenyewe.
wewe ni mwongo mkubwa, kwanza toka lini mtu akalazimishwa kupendwa na watu wakampenda? haina mantiki kabisa, ila walikuwepo wasiompenda kwa sababu zao binafsi au kwa kutofautiana mitazamo na walikuwa wachache na uache uongo wako kusema walikuwa wengi, nadhani ulishuhudia kipindi cha kung'atuka kwake jinsi watu wengi walivyomuaga kwa zawadi mbalimbali, je walilazimishwa? na vipi alipofariki uliona umati wa watu waliojawa na majonzi? taifa lilizizima, je walilazimishwa? acha hizo ndugu yangu hicho ni kisokolokwinyo chako tu! halafu una uhakika hao waliotaka kumpindua ndo waliokuwa wanapendwa na wengi au ni tamaa zao za madaraka!?
 
sijakutukana babu najaribu kukuelewesha...the realities most of us we are fully of incorrect facts

Unapozungumzia historia ya nchi hii kila mmoja anaitazama kutokea katika "angle" tofauti na mwenzake, ndio maana tunajadili ili tufike mahali tukubaliane kukubaliana ama tukubaliane kutokubaliana.

Sasa ndugu yangu unajua hapa tunajaribu kueleweshana na vilevile kubadilishana uzoefu wa historia ya nchi yetu, sioni mantiki ya kutumia maneno ya dharau wakati tumekuwa tukijadiliana kiungwana tangu mwanzo.
 
umeona ulivyo finyu na wewe????????
kila anaepewa standing ovation ana mawazo sahihi sio???????
na kila anaekaribishwa white house je????????
we uliona ziara ya mobutu marekani???????
umewahi ona standing ovation za madikteta wengi tu?
hivi unajua hata iddi amin aliwahi kuwa mwenyekiti wa oau??????

manake nyinyi mnawa brain wash watoto eti
nyerere alikuwa mwenyekiti wa oau
ha ha haaa,so what???????hata mobutu na iddi amini aliwahi kuwa
wenyeviti wa oau.

I wouldn't be surprised if u have never seen the speech. I can feel how light u are and if u are a Manchurian candidate, there is nothing i can do 2 help. About Mobutu's visit to USA, that is a rhetorical question, as well as Idd Amin. Who put Mobutu in power? Who killed P.Lumumba?
 
Unapozungumzia historia ya nchi hii kila mmoja anaitazama kutokea katika "angle" tofauti na mwenzake, ndio maana tunajadili ili tufike mahali tukubaliane kukubaliana ama tukubaliane kutokubaliana.

Sasa ndugu yangu unajua hapa tunajaribu kueleweshana na vilevile kubadilishana uzoefu wa historia ya nchi yetu, sioni mantiki ya kutumia maneno ya dharau wakati tumekuwa tukijadiliana kiungwana tangu mwanzo.
acha hasira babu neno uduanzi siyo baya namna hiyoo niite mie basi...
 
Mwalimu Nyerere kama kiongozi alikuwa na mazuri pamoja na mapungufu, ni kweli alipendwa na watu wengi kwa sababu mbali mbali,hivyo hivyo alichukiwa na watu kwa sababu mbali mbali.Kama kiongozi alikuwa mstari wa mbele wakati wa mapambano ya uhuru wa nchi kusini mwa afrika,na wakati huo huo anataka kujenga ujamaa,vile vile vita vya Kagera,Alijikuta njia panda baada wafadhiri wa IMF,World Bank wakamtema kwa kutofautiana nae.
 
I wouldn't be surprised if u have never seen the speech. I can feel how light u are and if u are a Manchurian candidate, there is nothing i can do 2 help. About Mobutu's visit to USA, that is a rhetorical question, as well as Idd Amin. Who put Mobutu in power? Who killed P.Lumumba?

for the records hiyo hotuba ya nyerere south africa
imeonyeshwa sana na tbc1
nimeiona mara nyingi sana...

tatizo lako unaitazama south afrika kama nchi muhimu sana kwa
kum validate mtu...
sijui umefuatilia jacob zuma anavyojaribu kumuokoa gadafi na anashindwa????????
 
Naona unajitahidi kujinasibisha na geza ulole kwa kasi sana.

Rudi kule ukatetee utumbo wako, achana na geza ulole tunakwenda naye vizuri ili kufahamisha na kubadilishana uzoefu na uelewa sio wewe kila saa kurukia ncha ya mkuki wa geza ulole!!

una tatizo kubwa sana
kuthibitisha nyerere alikuwa mkabila hukuti mtu mwenye jina
la mwita akimpinga nyerere

soma vizuri mwanzo wa thread
alieanzisha topic ya vyama vya ushirika hapa ni mimi
gezaulole alikuja kuongezea data
sasa usijiabishe kwa kuropoka ropoka
 
Mwita Maranya said:
Tukumbuke kwamba shule hizi tunazozitaja zimejengwa na wakoloni hata kama tutawaita wamishenari, lengo alo kubwa lilikuwa ni moja tu, kutafuta mbinu bora ya kututawala na kwa msaada wa sisi wenyewe weusi.

Mwita Maranya,

..kuna maeneo Wamishionari walifundisha useremala, ufundi uashi, etc etc. pia yapo maeneo walianzisha zahanati.

..pia yapo maeneo ambayo wazazi walishiriki ktk ujenzi wa shule za misioni haswa za msingi.

..binafsi siyaelewi-elewi haya madai kwamba Wamishionari walitoa elimu ili Watanganyika watawalike kwa urahisi. nasema hivyo kwa kuzingatia kwamba yapo maeneo walikuwa wanatoa elimu ya nadharia na vitendo kama kufundisha useremala, etc etc.
 
Nyerere alifanya mambo mengi mazuri especially kwenye issue ya usawa ila lazima tukubali kwamba alikuwa na vi elements vya udikteta. Aliminya sana uhuru wa kutoa/kupata habari ingawa yeye mwenyewe alikuwa na Runinga ikulu!!
Hauwezi ku justify altaka marais watoke kwenye makabila madogomadogo tu eti kwa sababu marais karibu wote wametoka kwenye makabila madogo!!
Sweke,
Nyerere hakuwa na runinga ikulu. Siku hizo hata ungekuwa na tv ungekuwa unatizama nini? TV Zanzibar? Ila mwaka 1977 baada ya ziara yake rasmi Marekani kuzungumzia harakati za ukombozi Rhodesia, Mzee Bomani alimnunulia video player pamoja na TV yake ili aweze kuona video mbalimbali ambazo ubalozi wa Tanzania Washington DC uliweza kumtumia. Nadhani hiyo ndiyo imepelekea watu kusema Nyerere alikuwa na tv ikulu. Ilikuwa ni TV ya kuangalia video. That is a fact.
 
  • Thanks
Reactions: 911
Your might have a point but I don't think this is Mwl Nyerere we know for all these years. Ndio mwalimu sio mtu sahii na kuna vitu vingi vya kumkosoa lakini katika kuishi kwake na maisha yake yalionyesha wazi kwamba yeye sio mkabila. This issue unayoizungumzia hapa really it's not relevant katika maisha yetu ya Watanzania kwa sasa. Why I am saying this, Tanzania sasa kila Mtanzania anayetoka kabila lolote lile anayonafasi ya ku-archive anything they want na opportunities are there. Tatizo lilipo sio maneno ya Nyerere ila ni ccm iliopo ambayo tunaona uozo, wizi, violations za human rights tunazoziona, kikwete na majangiri wenzio ndio wanaharibu Taifa sasa. Yes some of it Nyerere is to blame, Mtanzania yeyote anayehamu politics tunajua wazi kwamba political figure kama Nyerere alikuwa na opportunity kubwa ya kuweka foundation ya true democracy na kwa hili he did come short. Nyerere ange-focus kwenye constitution inayolenga true democratic society and not favouring ccm only, tunajua Nyerere alikuwa na influence kubwa katika kutengeneza hii constitution but he didn't. Tunaona matokeo yake ccm na kikwete wanatumia hii hii constitution to oppress Wananchi na oppositions. In short, Nyerere did a lot for Tanzania and he was largely good political figure but he has many many short comings. Thats Nyerere for you, yes he is human and he had at least leadership integrity compare to Mwinyi, Mkapa and huyu fisadi kikwete.

'One thing to remember Nyerere's short falls can be summarized this way, he did want to protect his legacy and he though ccm will continue and flourish and not deminizing Tanzania this way'


Habari zenu jamani?!

Naomba nianze kwa kusema ukweli kwamba mimi sikuwepo kipindi cha utawala wa Mwl na hata alipofariki nilikua mdogo sana hivyo sikuwahi kujua kwanini watu wengi walikua wanampenda sana huku bado kukiwa na mambo mengi hasi yanayosemwa juu yake.Nafurahi kwamba mwaka huu nimeweza kutumia muda wangu kiasi nikasoma vitabu kadhaa kumhusu...makusanyo ya hotuba zake pamoja na vitabu alivyoandika mwenyewe.Kutokana na niliyoyasoma niliridhika kwamba sifa zote anastahili...pia kukosolewa maana yeye kama mtu mwingine yeyote yule makosa hatuwezi tuyakwepa.

Katika vitu ambavyo Mwl alivisimamia haswa ni usawa.Hakutaka kabila moja lijione/jisikie liko juu ya jingine na kutengeneza matabaka.Sasa swali langu nnaloomba mnisaidie ni hili....ule msemo au sijui niyaite madai ya kwamba Mwl aliwahi kusema makabila fulani hayafai kupewa uongozi wa juu wa nchi ni wa kweli au ni propaganda za waliomchukia?!Nauliza hivi kwasababu niliyoyasoma juu yake hayaendani kabisa na madai haya...na wala haileti maana kusikia kwamba aliyepigania usawa ndie aliyekua wa kwanza kutengeneza matabaka lilipokuja swala la uongozi!!!

Naomba majibu kama yapo yawe na vielelezo na yasiwe maneno ya kusikika na kufikirika tu ili tusiojua tujifunze kitu.
Asanteni!
 
una tatizo kubwa sana
kuthibitisha nyerere alikuwa mkabila hukuti mtu mwenye jina
la mwita akimpinga nyerere

soma vizuri mwanzo wa thread
alieanzisha topic ya vyama vya ushirika hapa ni mimi
gezaulole alikuja kuongezea data
sasa usijiabishe kwa kuropoka ropoka
Hapo pia umeteleza. Katika njama za mapinduzi za mwaka 1970 alikuwemo mwanajeshi Marwa aliyehusishwa na njama hizo. Jaribu kingine.
 
hakuna kitu kama hicho aliweka Wakurya kumlinda madarakani ukiangalia vizuri kabola Wazanaki ni la kufikirika yaani ni sehemu ya Wakurya!
Geza Ulole,
Hapana. Wazanaki si sehemu ya Wakurya. Wazanaki walitoka Rwanda/ Burundi wakati Wakurya inasemekana wametokea Ethiopia. Lakini hii ya kuwa na Wakurya wengi jeshini na Wanyakyusa haikutengenezwa na Mwalimu. Ilianzia enzi za KAR.
 
Sweke,
Nyerere hakuwa na runinga ikulu. Siku hizo hata ungekuwa na tv ungekuwa unatizama nini? TV Zanzibar? Ila mwaka 1977 baada ya ziara yake rasmi Marekani kuzungumzia harakati za ukombozi Rhodesia, Mzee Bomani alimnunulia video player pamoja na TV yake ili aweze kuona video mbalimbali ambazo ubalozi wa Tanzania Washington DC uliweza kumtumia. Nadhani hiyo ndiyo imepelekea watu kusema Nyerere alikuwa na tv ikulu. Ilikuwa ni TV ya kuangalia video. That is a fact.
ina maana unataka kusema ikulu nzima haikuwa na Dish kuangalia newz kama BBC? siamini! alikuwa anapata wapi habari za nje?
 
well nakuelewa sasa baada ya kuyapinga, then kwanini aliua vyama vyao vya ushirika through nationalization ambavyo ni jasho lao yaani KNCU na KCU?
Geza Ulole,
Katika interview moja na jarida The Internationalist, Mwalimu alikiri kuwa lilikuwa kosa kuua vyama vya ushirika. He admitted to the mistake.
 
Mwita Maranya,

..kwani hizo shule na hospitali alizotaifisha resources zilitoka wapi?

..pia matatizo kama hayo yanahitaji mikakati endelevu kuyatatua.

..nimeeleza ktk post yangu iliyopita kwamba vilikuwepo vyanzo mbalimbali ya mapato kwa serikali lakini tulivivuruga kutokana na sera zetu kama Azimio la Arusha na operesheni vijiji.

..alichopaswa Mwalimu ni kuongeza vyanzo vipya vya mapato, siyo kwenda kuvuruga vile ambacho tayari vilikuwepo.


..
Mkuu joka kuu, ngoja namimi niulize hivi serikali ya kikoloni iliyokuwepo ukianza na ya wajerumani halafu waingereza ilijenga shule zipi?
 
Geza Ulole,
Hapana. Wazanaki si sehemu ya Wakurya. Wazanaki walitoka Rwanda/ Burundi wakati Wakurya inasemekana wametokea Ethiopia. Lakini hii ya kuwa na Wakurya wengi jeshini na Wanyakyusa haikutengenezwa na Mwalimu. Ilianzia enzi za KAR.
kuna kitu kinaitwa kinship ni sawa leo hii Mbowe awe Rais halafu jeshini ajaze Wameru, Waarusha na Wamasai halafu aseme hatushaabiani au si jamaa! still utaona kuna sort of nepotism maana hizi jamii ziko karibu zaidi kuanzia kimila hata tamaduni! nathani unapata gist ya nilichomaanisha! Mbona asijaze Wanzanzibari jeshini?
 
kumbe helewi kitu wewe uliza tukwambie, Nyerere aliona ili kuua nguvu ya vyama vya ushirika kama VFCU, ilibidi awatenge viongozi wa vyama hivyo na chama chenyewe, alimchukua Bomani na kumpeleka Dar kuwa waziri wa Ushirika na Kilimo, akalazimisha kila eneo la kazi lazima kuwe na tawi la TANU! Akachukua vimwana-TANU viherehere toka vitokako akaviweka kila mahali kuwa vikatibu vya hayo matawi, na mameneja wa maeneo hayo kuwa wenyeviti.

Hapo ndipo siasa ilipo ingilia nyanja ya uzalishaji. Wale makatibu wa matawi ya TANU wakawa ni watendaji wakuu na ndipo Chama Kushika Hatamu ikatangazwa rasmi. Pesa zikawa zinachotwa toka viwandani na kwenye vyama vya ushirika na kupelekwa TANU/CCM. Wanasiasa wakatamalaki kila upande na uzalishaji viwandani ukazorota na mashirika mengi kufa.

Bomani kwa kujua ama kutokujua lengo la Mwl. lilikuwa ni kummaliza nguvu za umaarufu, alikubaliana na mawazo ya Mwl. akasahau na kwao, akenda kuoa huko huko viongozi wengi wapuuzi wasipenda kwao wanako-oa! CCM ikavuruga uchumi wa nchi, ilipo ona mashirika mengi yamekufa ikaanzisha shirika lake la uchumi, weeh kwa vile walizoea kula bila kuzalisha halikuchukua round wakalikomba pyuuu! CCM ikauza mashirika yaliyokufa ili wapate pesa, walipoyamaliza wakaingilia BOT, wakalamba kwa style ya EPA. Historia ni ndefu, naomba kuwasilisha!
Anko Sam,
Bomani alioa Uchagani hata kabla ya uhuru. That is a fact.
 
Hee babu lile, waislaam kawanyanyasa sana, kumbe hata makabila mengine alikuwa anayanyanyasa? ndio maana ile hotuba yake moja anawasannif wakara? mungu amuweke anapostahili.
Na wewe umefunguliwa lini? Nitakata rufaa kwa mods urejeshwe lupango!
 
Back
Top Bottom