Mwalimu Nyerere na ukabila

Mwalimu Nyerere na ukabila

Mwita Maranya,

..binafsi naamini uamuzi wa Mwalimu wa kutaifisha shule za binafsi na madhehebu ya dini ulikuwa na makosa.

..alichopaswa kufanya Mwalimu ni kujenga shule za serikali akielekeza nguvu zaidi maeneo ambayo yalikuwa yameachwa nyuma.

..kosa lingine ni ule utaratibu wa quota system ambapo wanafunzi ambao hawakuwa qualified walipewa nafasi za kuendelea na masomo.

..nakubaliana na dhima nzima ya kutoa elimu kwa wa-Tanzania wote, lakini nadhani juhudi hazikufanyika kuhakikisha kwamba tunatoa ELIMU BORA KWA WOTE, na mipango kama quota system ilikuwa inaficha deficiencies ktk mfumo wa utoaji elimu wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere.

..kitu kinachosikitisha ni kwamba mpaka leo hii usawa haujapatikana na zaidi elimu yetu imeshuka kiwango kiasi cha kutisha.
you say it man, hakafu wale waliokuwa victimized na quota system leo hii wana utitiri wa shule za wazazi or binafsi na hata vyuo binafsi ukiacha kujikita katika sekta binafsi huwezi kumzuia binadamu mwenye bidii katika ku-achieve what he or she rightful believe its her or his obligation to have!
 
wacha we itikadi za ujamaa zilikuja baada ya mambo kubuma! ukiangalia vizuri hata harakati zetu za kupigania uhuru zilitu-exclude na any sort ya totally alignment towards the two cold war players! we were so fortunate unlike the rest of African nations at the time so huwezi kusema alikuwa Mjamaa hapo kabla u r practically misrepresenting facts!

Kwahiyo hapo mwanzo alikuwa na itikadi gani.., anyway hata kama upo sawa ni kwamba alisimamia policy alizoziamini and as a good leader alijitahidi zifanikiwe kwahiyo alikuwa na good motives, kutokufanikiwa kwa India does not make Gandhi a bad leader au kufanikiwa kwa Libya does not necessarily make Ghadafi an Angel
 
Mwita Maranya,

..binafsi naamini uamuzi wa Mwalimu wa kutaifisha shule za binafsi na madhehebu ya dini ulikuwa na makosa.

..alichopaswa kufanya Mwalimu ni kujenga shule za serikali akielekeza nguvu zaidi maeneo ambayo yalikuwa yameachwa nyuma.

..kosa lingine ni ule utaratibu wa quota system ambapo wanafunzi ambao hawakuwa qualified walipewa nafasi za kuendelea na masomo.

..nakubaliana na dhima nzima ya kutoa elimu kwa wa-Tanzania wote, lakini nadhani juhudi hazikufanyika kuhakikisha kwamba tunatoa ELIMU BORA KWA WOTE, na mipango kama quota system ilikuwa inaficha deficiencies ktk mfumo wa utoaji elimu wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere.

..kitu kinachosikitisha ni kwamba mpaka leo hii usawa haujapatikana na zaidi elimu yetu imeshuka kiwango kiasi cha kutisha.

Nashukuru kwa maoni yako mkuu,

Labda unisaidie jambo moja kwenye hoja yako, resources za kujenga mashule katika maeneo yote yaliyokuwa nyuma kielimu na kujemga hospitali katika maeneo yote yaliyokuwa nyuma katika huduma za afya zingepatikana wapi na kwa muda mfupi kiasi gani ili watanzania wote waweze kufaidika?
 
Mapambano ya kudai uhuru yaliongozwa na TANU chini ya uongozi wa mwalimu. Kwahiyo hoja kwamba uhuru ungekosekana sehemu kubwa ya watunwaliomsupport wangempinga ni hisia zako tu kutokana na mtazamo wako binafsi na wala hakuna uhalisia wowote.
Watanganyika waliokuwa wanadai uhuru hakuwa nyerere peke yake, ukumbuke hadi nyerere anakuja kupewa uenyekiti wa TANU alikuta tayari harakati za kudai uhuru zimeshaanza na zinazidi kupamba moto kwahiyo alichofanya yeye ni kuunganisha nguvu na watanganyika wenzake na kutokana wao kumuamini na kumpa uenyekiti wa chama basi ilibidi aongoze mapambano. Kwahiyo kama uhuru ungekosekana labda tanu ndiyo ingepingwa na si nyerere.
nathani huijui historia vizuri baada ya Kifimbo kuwa Mjamaa alienda hata kutaifisha assets za Rupia ni Mzee kunambi aliyethubutu kwenda kumkemea Mwl na kumwambia hivi huyu mtu alivyotusaidia namna hii kirasilimali katika harakati za ukombozi leo hii unataifisha hata nyumba zake? Jamaa akaona noma akaamuru ku-exlude assets za Rupia kutaifishwa though wengine waliokuwa si wanamtandao wakaula wa chuya! hata leo hii uduanzi huu upo baba katika siasa!
 
Nashukuru kwa maoni yako mkuu,

Labda unisaidie jambo moja kwenye hoja yako, resources za kujenga mashule katika maeneo yote yaliyokuwa nyuma kielimu na kujemga hospitali katika maeneo yote yaliyokuwa nyuma katika huduma za afya zingepatikana wapi na kwa muda mfupi kiasi gani ili watanzania wote waweze kufaidika?
we acha uduanzi at that time kulikuwa na settlers wengii na baadhi ya wazawa wachache waliokuwa na mashamba makubwa ya Mkonge, kahawa, pamba na mazao mengine ya biashara ukiachia mbali wahindi waliokuwa na viwanda vya kati waliokuwa wanalipa kodi! Mwl aliwatimua katika ku-implement his ujamaa na kujitegemea policies!
 
Mwita Maranya said:
Hivi nchi ndo punde tu imepata uhuru, ilikuwa na vyanzo vingapi vya mapato ambavyo vingeiwezesha serkali kutekeleza mahitaji ya watanzania kwa mara moja?? Kulikuwa na wafanyakazi wangapi ambao wangelipa kodi na kuiongezea seriali kipato?

Unafahamu fika kwamba kipindi cha utawala wa mwalimu ndicho kipindi pekee katika historia ya marais wa nchi hii ambapo fedha ya serikali ilikuwa haiwezi kuchezewa kirahisi rahisi kama tunavyoshuhudia wakati huu wa ufisadi na mikataba feki.

Kwa kuzingatia kwamba nchi imepata uhuru huku ikiwa na wasomi wachache sana kiasi kwamba ilibidi kuagiza nguvukazi kutoka nje ya nchi ilikuwa ni jambo la busara mno kutaifisha shule za kidini zilizokuwepo ili kujenga taifa la watu wa aina moja.

Mwita Maranya,

..vilikuwepo vyanzo vichache vya mapato lakini Mwalimu alivivuruga kutoka na AZIMIO LA ARUSHA na OPERESHENI VIJIJI.

..utaifishaji mashamba makubwa uliporomosha sekta ya katani/mkonge nchini.

..operesheni vijiji ulivuruga kilimo cha korosho mikoa ya kusini na hali ya uchumi kusini haijatengemaa tangu wakati huo.

..baada ya korosho na katani kuanguka tukaanza kutegemea kahawa na pamba kama mazao makuu ya biashara.

..tena Mwalimu akaja kuvunja vyama vya ushirika kama KNCU na Nyanza Cooperative taasisi ambazo zilikuwa wadau wakubwa ktk kilimo cha kahawa na pamba.

..kwa msingi huo mchango wa kahawa na pamba ktk pato la taifa uliathirika pamoja na hali ya maisha ya wakulima wa mazao hayo.

..MWALIMU ALIKUWA NA NIA NJEMA KABISA ILA NADHANI TATIZO LAKE ALIKUWA TOO IN-EXPERIENCED. TUANGALIE UZOEFU WAKE WA KAZI KABLA HAJAPEWA MADARAKA YA KUONGOZA TAIFA CHANGA NA MASKINI KAMA TANGANYIKA.
 
you say it man, hakafu wale waliokuwa victimized na quota system leo hii wana utitiri wa shule za wazazi or binafsi na hata vyuo binafsi ukiacha kujikita katika sekta binafsi huwezi kumzuia binadamu mwenye bidii katika ku-achieve what he or she rightful believe its her or his obligation to have!

Sidhani kwamba kulikuwa na suala la kuvictimize mtu au kikundi cha watu katika hili, Je kama nchi tulikuwa na resources za kutosha kuwafikia wale waliokuwa wamesahauliwa na mkoloni kwa haraka kiasi gani. Tukumbuke kwamba shule hizi tunazozitaja zimejengwa na wakoloni hata kama tutawaita wamishenari, lengo alo kubwa lilikuwa ni moja tu, kutafuta mbinu bora ya kututawala na kwa msaada wa sisi wenyewe weusi.

Kwahiyo walianzisha shule maeneo kadhaa waliyotaka kwa malengo yao, sasa baada ya kupata uhuru ilikuwa ni lazima kuondoa ule ubaguzi uliokuwepo enzi ya mkoloni, uwe ni ubaguzi wa kwenye elimu, afya na hata ubaguzi wa misingi ya dini. Kwa mantiki hiyo ilibidi serikali itaifishe huduma hizo na kuziweka chini yake ili watu wote pasipo kujali kabila lake ama dini yake waweze kusaidika na kunufaika na huduma hizo.
 
Ukweli ni kwamba Ujamaa doesnt work..., lakini mimi na wewe tunajua hayo because of hindsight, baada ya kuona from history, na ujamaa haufanyi kazi sio sababu ya utekelezaji, bali ni sababu binadamu ni wachoyo na tuna ubinafsi, hatukuwezi kuishi wote sawa na kugawana mali kwa usawa, umimi ni mwingi kwahiyo hata King Solomon angekuwa ndio kiongozi sidhani kama anaweza akafanya Ujamaa a Success..,

Kuhusu kuwaweka watu pamoja na kuweletea huduma haikuwa flawed.., kama ingetekelezwa it was a good idea..., hii nchi ni kubwa wasambaze watu nchi nzima wapelekee huduma zote muhimu ili tuondoe Ujinga, na Umaskini... After All Umoja ni Nguvu Utengano ni Dhaifu..... (If only it can work)

Ujamaa haukupewa nafasi ya kusimama. Ulaya ukiwa communist watu walikunyanyapaa, ilikuwa kama ukoma enzi za Yesu! Lakini hata hivyo, ubepari mpaka leo haujafanikiwa afrika na amerika kusini (F. Castro)
 
Ujamaa haukupewa nafasi ya kusimama. Ulaya ukiwa communist watu walikunyanyapaa, ilikuwa kama ukoma enzi za Yesu! Lakini hata hivyo, ubepari mpaka leo haujafanikiwa afrika na amerika kusini (F. Castro)
Ujamaa is very good on paper.., lakini sababu ya ubinadamu na uchoyo na umimi its very hard to implent it..., Hata Cuba ambako wamejaribu ila kuna wa-Cuba wengi sana wanakimbilia Marekani ili wakapate neema.

Tukiangalia Africa Mashariki kiuchumi tuna Kenya na Tanzania..., nadhani kwa mifano hiyo miwili tunaweza tukasema ubepari umefanikiwa kuliko ujamaa.....
 
Have you finished with Geza Ulole?Nyerere was a super destroyer, he had what, in myths, they call the "midas touch" what he touched turned into stone. Nyerere was scared of everything big, may it be a big tribe or any other major ethnic. Similarly Islam, you can never talk about ethnic descrimination without touching major religious ethnics. Islam being a major religion at the time, nyerere never was ashamed of clipping its wings. By the way, why discuss about unions if you are discussing tribes?

So Muslims were better of during colonial era than after independence? Major religion in what sense-population,political influence, better living conditions?
 
Unaona comment yako hapo kwenye red;

nathani huijui historia vizuri baada ya Kifimbo kuwa Mjamaa alienda hata kutaifisha assets za Rupia ni Mzee kunambi aliyethubutu kwenda kumkemea Mwl na kumwambia hivi huyu mtu alivyotusaidia namna hii kirasilimali katika harakati za ukombozi leo hii unataifisha hata nyumba zake? Jamaa akaona noma akaamuru ku-exlude assets za Rupia kutaifishwa though wengine waliokuwa si wanamtandao wakaula wa chuya! hata leo hii uduanzi huu upo baba katika siasa!

Kumbe ulikuwa unatafuta njia mazee hatimaye ukaamua kushusha pumzi!

we acha uduanzi at that time kulikuwa na settlers wengii na baadhi ya wazawa wachache waliokuwa na mashamba makubwa ya Mkonge, kahawa, pamba na mazao mengine ya biashara ukiachia mbali wahindi waliokuwa na viwanda vya kati waliokuwa wanalipa kodi! Mwl aliwatimua katika ku-implement his ujamaa na kujitegemea policies!

Dah, ngoja tu nikuache upite na zako leo sikwambii chochote.
 
Sidhani kwamba kulikuwa na suala la kuvictimize mtu au kikundi cha watu katika hili, Je kama nchi tulikuwa na resources za kutosha kuwafikia wale waliokuwa wamesahauliwa na mkoloni kwa haraka kiasi gani. Tukumbuke kwamba shule hizi tunazozitaja zimejengwa na wakoloni hata kama tutawaita wamishenari, lengo alo kubwa lilikuwa ni moja tu, kutafuta mbinu bora ya kututawala na kwa msaada wa sisi wenyewe weusi.

Kwahiyo walianzisha shule maeneo kadhaa waliyotaka kwa malengo yao, sasa baada ya kupata uhuru ilikuwa ni lazima kuondoa ule ubaguzi uliokuwepo enzi ya mkoloni, uwe ni ubaguzi wa kwenye elimu, afya na hata ubaguzi wa misingi ya dini. Kwa mantiki hiyo ilibidi serikali itaifishe huduma hizo na kuziweka chini yake ili watu wote pasipo kujali kabila lake ama dini yake waweze kusaidika na kunufaika na huduma hizo.
so hizo shule zilijengwa kule kutokana na circumstances zinazofahamika na wakoloni wenyewe sio? hao wazawa wa huko hawaku-influence chochote sio? Je, how do u rectify that problem? Kwa akili za mtu asiye visionary na mwenye kwanini na anayeshindana na historia anaona bora anyanganye hizo shule au aweke quota systme ili woote wakose na si kujenga au ku-initiate muamko wa kwenda shule kwa wale waliokosa ili ku-meet the demand! By doing so ana-prevent the nation from fully realizing its potentials! Btw kama nilivyokuambia hao walionyanganywa nafasi still walitafuta means ya ku-survive ndo maana kuna sehemu shule za ushirika, dini na wazazi zikafumuka! hata vyuo...
 
Unaona comment yako hapo kwenye red;



Kumbe ulikuwa unatafuta njia mazee hatimaye ukaamua kushusha pumzi!



Dah, ngoja tu nikuache upite na zako leo sikwambii chochote.
sijakutukana babu najaribu kukuelewesha...the realities, most of us are fully of incorrect facts
 
wewe acha uwongo wewe
huo mpango wa kumpindua zilikuwa njama zake nyerere za kudhibiti
wote waliopigania uhuru
ili wasimkumbushe makubaliano ya kabla ya uhuru

yaani hata baraza la wazee la tanu lilitaka kumpindua nyerere???????/

So it is ur word against mine!? yours is a hearsay,mine is based on court conviction.
 
Ujamaa is very good on paper.., lakini sababu ya ubinadamu na uchoyo na umimi its very hard to implent it..., Hata Cuba ambako wamejaribu ila kuna wa-Cuba wengi sana wanakimbilia Marekani ili wakapate neema.

Tukiangalia Africa Mashariki kiuchumi tuna Kenya na Tanzania..., nadhani kwa mifano hiyo miwili tunaweza tukasema ubepari umefanikiwa kuliko ujamaa.....

Nakubaliana na wewe kabisa kwamba ujamaa ni mzuri kwenye makaratasi lakini when it comes practically ni zero.

Inafahamika wazi kwamba china inafuata mfumo huu wa ujamaa, sasa wamefikaje hapo walipo leo hadi wamekuwa tishio kwa wazungu wa ulaya ma marekani?

Cuba wanahitaji msaada gani kutoka nchi za kibeberu ambacho wao wameshindwa kufanya?? huoni hao watu wanaokimbilia marekani ni kutokana na msukumo wa marekani kutaka kuivuruga cuba?
 
Ujamaa is very good on paper.., lakini sababu ya ubinadamu na uchoyo na umimi its very hard to implent it..., Hata Cuba ambako wamejaribu ila kuna wa-Cuba wengi sana wanakimbilia Marekani ili wakapate neema.

Tukiangalia Africa Mashariki kiuchumi tuna Kenya na Tanzania..., nadhani kwa mifano hiyo miwili tunaweza tukasema ubepari umefanikiwa kuliko ujamaa.....
in short huwezi ku-dictate hulka ya mtu au self determination ndo maana usawa hamna kinachoweza kufanyika ni at least kuwezesha basic needs kuwepo kwa kila mtu! huwezi kumfanya Matonya awe sawa na Mengi leo hii kwa vile unaamini katika usawa! thats crayz ni kuharibu uchumi huko!
 
Mwita Maranya said:
Nashukuru kwa maoni yako mkuu,

Labda unisaidie jambo moja kwenye hoja yako, resources za kujenga mashule katika maeneo yote yaliyokuwa nyuma kielimu na kujemga hospitali katika maeneo yote yaliyokuwa nyuma katika huduma za afya zingepatikana wapi na kwa muda mfupi kiasi gani ili watanzania wote waweze kufaidika?​


Mwita Maranya,

..kwani hizo shule na hospitali alizotaifisha resources zilitoka wapi?

..pia matatizo kama hayo yanahitaji mikakati endelevu kuyatatua.

..nimeeleza ktk post yangu iliyopita kwamba vilikuwepo vyanzo mbalimbali ya mapato kwa serikali lakini tulivivuruga kutokana na sera zetu kama Azimio la Arusha na operesheni vijiji.

..alichopaswa Mwalimu ni kuongeza vyanzo vipya vya mapato, siyo kwenda kuvuruga vile ambacho tayari vilikuwepo.


..
 
ukisikia ugonjwa ndo huo
yaani tanzania ilikuwa juu kwa ict wakati computer na tv zilikuwa banned????????
so radio tanzania ndio ilitufanya tuwe juu sio???????/
kipindi cha mikingamo sio?????????

Nenda kasome kwanza historia ya ICT Tz ndo utaelewa ninachozungumza. Kwa kifupi kumpyuta zimeanza kuja Tz in 60s na zikawa banned late 70s na early 80s.
 
Nakubaliana na wewe kabisa kwamba ujamaa ni mzuri kwenye makaratasi lakini when it comes practically ni zero.

Inafahamika wazi kwamba china inafuata mfumo huu wa ujamaa, sasa wamefikaje hapo walipo leo hadi wamekuwa tishio kwa wazungu wa ulaya ma marekani?

Cuba wanahitaji msaada gani kutoka nchi za kibeberu ambacho wao wameshindwa kufanya?? huoni hao watu wanaokimbilia marekani ni kutokana na msukumo wa marekani kutaka kuivuruga cuba?
nathani wewe hauko update na yanayoendelea raul anajisalimisha uko ameanza ku-loosen up a tight control of state on business na ku-implement free-market economic policies! sasa naomba umuulize amekosa nini wakati anakula kuku kila siku labda anahofia uprise kutoka kwa Cubanas
 
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom