Mwalimu Nyerere na ukabila

Mwalimu Nyerere na ukabila

by nature binadamu ni watu huru
hakuna kitu kama too much freedom

huko iraq na libya ni lazima wapitie stages zote za freedom
kama wangekuwa na freedom japo kidogo yasingefika haya

mbona south africa walisema haitaweza kuishi kwa amani
na imewezekana so far

South Africa, its a different story alafu siongelei ubaguzi wa rangi wala kumkandamiza mtu sababu ya imani yake au jinsi alivyo ninachoongelea kuna watu inabidi uwaonyeshe kwamba kuna sheria na kuna state ambayo inabidi ieshimiwe, hakuna ubishi.., good example ni England sasa hivi too much usawa na political correctness imefanya hadi mtoto mdogo anahaki ambapo mzazi inabidi aangalie mara mbili kabla hajamkana.., that is political correctness going mad..., so in Iraq and Libya kama hakuna power ya kuonyesha kwamba you cant just run amok and get out scot free (kama enzi za Saddam)...., maybe all those crazy people will take advantage..., As the saying goes its like Lunatics Running the Asylum
 
Have you finished with Geza Ulole?Nyerere was a super destroyer, he had what, in myths, they call the "midas touch" what he touched turned into stone. Nyerere was scared of everything big, may it be a big tribe or any other major ethnic. Similarly Islam, you can never talk about ethnic descrimination without touching major religious ethnics. Islam being a major religion at the time, nyerere never was ashamed of clipping its wings. By the way, why discuss about unions if you are discussing tribes?

pole sana...........
 
kama alishindwa kufanya hivyo then hakuwa qualified ku-rule the country, kwanini basi, aliomba uhuru maana that means hakuweza ku-meet expectations alizoongelea katika kupigania uhuru! au kwanini asi-resign, he wasnt a hard worker basi kushindwa kujenga hata shule kuwezesha kila Mtanzania kusoma bali kutaifisha zilizopo maana nathani immediately baada ya kupata uhuru alitoa national deveolopment plan kama aliyotoa Kikwete hapo juzi! akisema anatarajia kufanya nini katika miaka kumi!

Ni vizuri tukumbushane kwamba Nyerere hakuomba uhuru kama mtu binafsi bali alifanya hivyo kwa kushirikiana na watanganyika wenzake, na kwa kweli watanganyika wengi sana walitaka wawe huru, kuna vibaraka wachache waliokuwa kwenye utumishi wa serikali ya mkoloni hawakuona haraka ya kupata uhuru.

Hatahivyo ni vizuri kukumbuka kwamba watanganyika wenyewe ndio walimchagua Nyerere awaongoze, hakujichagua mwenyewe.
Kama utasema kwamba haumeet expectations alizoongelea wakati akipigania uhuru nitakwambia hapana, tena hapana kubwa. Kuna mambo mengi sana ya maana na ya kukumbukwa Nyerere kawafanyia watanganyika na watanzania, na hata hivyo alifika mahali akaamua kwa hiari yake kung'atuka, inawezekana ni baada ya kurealise kwamba anahitajika mtu mwingine aje na mawazo yake kwa ajili ya maendeleo ya watanzania, tofauti na viongozi wengine wa kiafrika walioziletea nchi zao uhuru na kugeuza ikulu kuwa mali binafsi ya familia zao, mifano hai ipo huitaji nikutajie.
 
wewe una matatizo ya kuelewasasa ntajaribu tena kukuelewesha labda itasaidia....hakuna sehemu niliposema nyerere alikuwa hafai kuongozaau alikuwa mtu mbaya sanathread inazungumzia nyerere na ukabila na jinsi alivyopinga ukabilahuku akidhibiti makabila makubwanow je nyerere alikuwa na hotuba nzuri zenye manufaaa ?yes alikuwa nazo..je kutokuwepo kwa tv wakati ule kumesababisha hotuba hizo zipoteee,yes kabisa...je baadhi ya idea zake hazikuwa mbaya na finyu kwa maendeleo ya taifa?jibu ni ndio kwa herufi kubwa kabisa....tunapozungumzia matatizo ya utawala wake na mapungufu yake hatusemi hakuna mazuri aliyofanyatunachosema alikosea na kulikuwa na njia nyingine mbadala....kuhusu tv mbona cuba,zanzibar,china ya maona nchi nyingi tu za kisoshalisti zilikuwa na tv?????televisheni ni chombo chenye faida na hasara kwa mujibu ya mnavyotumia na kukidhibitihasara chache haziwezi futa faida zake?mbona internet ina porno kuliko chombo chochote?je ipigwe marufuku???????/angekuwepo nyerere hata jamiiforums isingekuwepo
"Thread inazungumzia Nyerere na ukabila" Halafu kuna jamaa hapo juu asiye na matatizo ya uelewa ameandika hivi: "Nyerere alikuwa na mawazo finyu alizuia tv....!!" Naona kweli kwenye vipaumbele vyake angewawekea tv watu wa mijini wa wakati huo wafaidi maisha!!
 
Nilisikia kwamba na TV pia hakupenda watu binafsi wamiliki!Hicho kitabu kinaitwaje?!Ningefurahi kweli kukipata!!!

Ukisoma historia ya ICT katika TZ, wanasema miaka ya 70 kulikuwa na uhamasishaji mkubwa kuhusiana na matumizi ya redio hadi mashuleni. Kwahiyo sioni kama ishu ilikuwa kuzuia habari. Pia tukumbuke TV zilikuwa banned pamoja na kompyuta kwa wakati mmoja kwa watumiaji binafsi.
 
"Thread inazungumzia Nyerere na ukabila" Halafu kuna jamaa hapo juu asiye na matatizo ya uelewa ameandika hivi: "Nyerere alikuwa na mawazo finyu alizuia tv....!!" Naona kweli kwenye vipaumbele vyake angewawekea tv watu wa mijini wa wakati huo wafaidi maisha!!


wewe kweli una matatizo ya kuelewa
nimeainisha hapo faida za tv nyingi mpaka mashuleni zinatumika
kama zanzibar waliweza kuwa na tv miaka hiyo
we unafikiri tanganyika ingeshindikana vipi????
vipaumbele vingeathiri vipi hilo?
au kipaumbele cha kuchangisha watu pesa za mbio za mwenge we ndo unaona cha maana??????

mnamsifia nyerere hata sifa ambazo sio zake

eti alijenga reli ya kati,na wakoloni waliacha reli ipi?????

kusema tv ni anasa
na magari ni anasa
namatrekta ni anasa ni mawazo finyu mno
period
 
Alichoamini kama hakikua kizuri alifanya kwa faida ya nani?!?!Nani anaejua kwa uhakika kwamba angeruhusu hayo makabila kuongoza huo “undugunization“ ungetawala?!
Umenikumbusha enzi za Gibonsi Mwaikambo aliyekuwa bosi wa benki. Fuatilia habari yake...
 
Hawa sitaki hata kumsikia Mwl Nyerere, alikuwa ana roho mbaya sana nimeuona utawala wake wa kidikiteta. Alimkamata Mzee wangu eti muhujumi uchumi duka lake likikuwa na dazeni kumi za kanga kutoka mwatex, na dola 500, miaka ya 80. Alikuwa mkabila pia alichaguwa waziri mkuu na, mkuu wa majeshi kutoka kwao mkoa wa MARA

Nina wasiwasi huenda mzee wako alikuwa mhujumu uchumi kweli, miaka ya themanini dukani ana khanga ya mwatex na dola 500? alizitoa wapi dolari miaka hiyo? Halafu usiiruhusu chuki uliyonayo dhidi ya mwalimu ukasahau kwamba operesheni ya kuwakamata wahujumu uchumi ilitikisa kila kona ya nchi chini ya usimamizi makini wa Sokoine na mimi binafsi nilishuhudia hao hao wazanaki na wakurya wakisombwa kwenda kizuizini kwa tuhuma hizo hizo za uhujumu uchumi kwahiyo hakuna ukabila hapo!!
 
Ukisoma historia ya ICT katika TZ, wanasema miaka ya 70 kulikuwa na uhamasishaji mkubwa kuhusiana na matumizi ya redio hadi mashuleni. Kwahiyo sioni kama ishu ilikuwa kuzuia habari. Pia tukumbuke TV zilikuwa banned pamoja na kompyuta kwa wakati mmoja kwa watumiaji binafsi.

ukisikia ugonjwa ndo huo
yaani tanzania ilikuwa juu kwa ict wakati computer na tv zilikuwa banned????????
so radio tanzania ndio ilitufanya tuwe juu sio???????/
kipindi cha mikingamo sio?????????
 
Ni vizuri tukumbushane kwamba Nyerere hakuomba uhuru kama mtu binafsi bali alifanya hivyo kwa kushirikiana na watanganyika wenzake, na kwa kweli watanganyika wengi sana walitaka wawe huru, kuna vibaraka wachache waliokuwa kwenye utumishi wa serikali ya mkoloni hawakuona haraka ya kupata uhuru.

Hatahivyo ni vizuri kukumbuka kwamba watanganyika wenyewe ndio walimchagua Nyerere awaongoze, hakujichagua mwenyewe.
Kama utasema kwamba haumeet expectations alizoongelea wakati akipigania uhuru nitakwambia hapana, tena hapana kubwa. Kuna mambo mengi sana ya maana na ya kukumbukwa Nyerere kawafanyia watanganyika na watanzania, na hata hivyo alifika mahali akaamua kwa hiari yake kung'atuka, inawezekana ni baada ya kurealise kwamba anahitajika mtu mwingine aje na mawazo yake kwa ajili ya maendeleo ya watanzania, tofauti na viongozi wengine wa kiafrika walioziletea nchi zao uhuru na kugeuza ikulu kuwa mali binafsi ya familia zao, mifano hai ipo huitaji nikutajie.
Mie naweza kukuhakikishia Mwl Nyerere haku-meet expectations kama alizotarajia! sababu kuu ni kwamba kabla ya uhuru hakuwa na ideologies kama za Ujamaa na self reliance hata chembe maana nina uhakika hata huo uhuru wenyewe usingepatikana kuna sehemu kubwa ya wananchi waliom-support wangempinga! Ni baada ya kuona mambo yanaenda Mrama kila kitu hakiendi na at climax mutiny attempt nathani 1964 ndipo akaenda uchina akarudi na all the ideas za Ujamaa+plus dress code na pia akavunja na jeshi loote...na wafanyabiashara wakawa publicly anounced a great threat to his government alichofanya tofauti ni kuita African socialism ambayo unfortunately was never experimented anywhere ila we were made to be guinea pigs! ili kuwa a bit neutral to the cold war foes!
 
yaani nyerere mawazo yake yalikuwa finyu mpaka na yeye yamem cost

kutokuwepo kwa tv matokeo yake hotuba zake za tv zipo mbili tu....
na zilichukuliwa akiwa sio rais...na ni itv na channel ten tu ndo wanazo....
zingine nzuri hazipo kwenye tv

kitabu ni historia ya edwin mtei kimezinduliwa hivi karibuni

waulize watu wa chadema watakupa

I bet u would kill to just achieve 1% of what Nyerere did!

Sijawahi kuona mwenye akili finyu akipewa "standing ovation" na bunge la SA!
 
Mie naweza kukuhakikishia Mwl Nyerere haku-meet expectations kama alizotarajia! sababu kuu ni kwamba kabla ya uhuru hakuwa na ideologies kama za Ujamaa na self reliance hata chembe maana nina uhakika hata huo uhuru wenyewe usingepatikana kuna sehemu kubwa ya wananchi waliom-support wangempinga! Ni baada ya kuona mambo yanaenda Mrama kila kitu hakiendi na at climax pale baada ya mutiny attempt nathani 1964 ndipo akaenda uchina akarudi na all the ideas za Ujamaa+plus dress code na pia akavunja jeshi loote...alichofanya tofauti ni kuita African socialism ambayo unfortunately was never experimente anywhere ila we were made to be guinea pigs! ili kuwa a bit neutral compared to the cold war foes!

nimegundua humu ndani
watu wa nyerere hawana cha kuzungumza
mbele ya geza ulole.
 
ukisikia ugonjwa ndo huo
yaani tanzania ilikuwa juu kwa ict wakati computer na tv zilikuwa banned????????
so radio tanzania ndio ilitufanya tuwe juu sio???????/
kipindi cha mikingamo sio?????????
hizo redio zilikuwa zinashika masafa yapi? acha uzushi wewe....!
 
Hahahha....mi nilivyosikia ni kwamba hakutaka watuwawe na tv ili wasijue yanayoendelea nje ya sehemu walipo...sasa yeye kwasababu anayo anakuja kuwadanganya ana maono haya na yale kuhusu ulimwengu unapoelekea.Siku ya pili watu wakisikia zile habari kwenye redio au sijui kwenye magazeti basi wanazidi kumwamini maana anajua mambo!!!Ntakitafuta!!!

Myth and speculations!
 
I bet u would kill to just achieve 1% of what Nyerere did!

Sijawahi kuona mwenye akili finyu akipewa "standing ovation" na bunge la SA!

umeona ulivyo finyu na wewe????????
kila anaepewa standing ovation ana mawazo sahihi sio???????
na kila anaekaribishwa white house je????????
we uliona ziara ya mobutu marekani???????
umewahi ona standing ovation za madikteta wengi tu?
hivi unajua hata iddi amin aliwahi kuwa mwenyekiti wa oau??????

manake nyinyi mnawa brain wash watoto eti
nyerere alikuwa mwenyekiti wa oau
ha ha haaa,so what???????hata mobutu na iddi amini aliwahi kuwa
wenyeviti wa oau.
 
mere excuses, tume-fail kwa ville tumekuwa na watawala wanaoturudisha nyuma kwa maslahi yao binafsi ya kuendelea kuwa madarakani not visionary.

Katika Watanzania, wapo ambao walijitahidi kutumikia taifa hili kama wale waliojiweka kwenye ushirika na kulipa kodi na kuliletea taifa hili fedha za kigeni! Je Nyerere aliwasaidia vp? au aliwafanya nini?

Nathani unajua aliwaona threat na aliwakandamiza na kuwalazimisha through dictated economy kuwa kama wale waliolala badala ya kuwaamsha wale walio usingizini kuwa kama wale walio macho! fikra za kijamaa zili-police hata kile kilichokuwa na manufaa kwa jamii kiujumla na kuua hata that goose that lays egg!

Nyerere alikuwa anaamini katika itikadi ya ujamaa, na kama ilivyo itikadi nyengine, itakadi ya ujamaa ilikuwa na misingi yake na mojawapo ni serikali ama dola kuwa muhimili mkuu wa kila shughuli kuanzia shughuli za kiuchumi, huduma za jamii hadi uzalishaji.

Sasa utaona hapo kwamba hao watu wa vyama vya ushirika hakuwakandamiza kwa sababu alikuwa na chuki nao, isipokuwa ni katika kutekeleza sera za ujamaa alizokuwa akiziamini, na kwa misingi ya itikadi hiyo serikali ililazimika kuhodhi nyanja zote.

Na kwakuwa itikadi ya ujamaa imeonekana kuwa ngumu kuitekeleza kutokana na nature ya binadamu pamoja mazingira yote kama alivyoeleza hapo kabla VOR basi utaona kwamba alikuwa akifanya hivyo kwa nia jjema na kwa kusimamia itikadi aliyoiaminina wala si kwa ubinafsi.
 
nimegundua humu ndani
watu wa nyerere hawana cha kuzungumza
mbele ya geza ulole.

Naona unajitahidi kujinasibisha na geza ulole kwa kasi sana.

Rudi kule ukatetee utumbo wako, achana na geza ulole tunakwenda naye vizuri ili kufahamisha na kubadilishana uzoefu na uelewa sio wewe kila saa kurukia ncha ya mkuki wa geza ulole!!
 
Nyerere alikuwa anaamini katika itikadi ya ujamaa, na kama ilivyo itikadi nyengine, itakadi ya ujamaa ilikuwa na misingi yake na mojawapo ni serikali ama dola kuwa muhimili mkuu wa kila shughuli kuanzia shughuli za kiuchumi, huduma za jamii hadi uzalishaji.
Sasa utaona hapo kwamba hao watu wa vyama vya ushirika hakuwakandamiza kwa sababu alikuwa na chuki nao, isipokuwa ni katika kutekeleza sera za ujamaa alizokuwa akiziamini, na kwa misingi ya itikadi hiyo serikali ililazimika kuhodhi nyanja zote.

Na kwakuwa itikadi ya ujamaa imeonekana kuwa ngumu kuitekeleza kutokana na nature ya binadamu pamoja mazingira yote kama alivyoeleza hapo kabla VOR basi utaona kwamba alikuwa akifanya hivyo kwa nia jjema na kwa kusimamia itikadi aliyoiaminina wala si kwa ubinafsi.
wacha we itikadi za ujamaa zilikuja baada ya mambo kubuma! ukiangalia vizuri hata harakati zetu za kupigania uhuru zilitu-exclude na any sort ya totally alignment towards the two cold war players! we were so fortunate unlike the rest of African nations at the time so huwezi kusema alikuwa Mjamaa hapo kabla u r practically misrepresenting facts!
 
Mie naweza kukuhakikishia Mwl Nyerere haku-meet expectations kama alizotarajia! sababu kuu ni kwamba kabla ya uhuru hakuwa na ideologies kama za Ujamaa na self reliance hata chembe maana nina uhakika hata huo uhuru wenyewe usingepatikana kuna sehemu kubwa ya wananchi waliom-support wangempinga! Ni baada ya kuona mambo yanaenda Mrama kila kitu hakiendi na at climax mutiny attempt nathani 1964 ndipo akaenda uchina akarudi na all the ideas za Ujamaa+plus dress code na pia akavunja na jeshi loote...na wafanyabiashara wakawa publicly anounced a great threat to his government alichofanya tofauti ni kuita African socialism ambayo unfortunately was never experimented anywhere ila we were made to be guinea pigs! ili kuwa a bit neutral to the cold war foes!

Mapambano ya kudai uhuru yaliongozwa na TANU chini ya uongozi wa mwalimu. Kwahiyo hoja kwamba uhuru ungekosekana sehemu kubwa ya watunwaliomsupport wangempinga ni hisia zako tu kutokana na mtazamo wako binafsi na wala hakuna uhalisia wowote.
Watanganyika waliokuwa wanadai uhuru hakuwa nyerere peke yake, ukumbuke hadi nyerere anakuja kupewa uenyekiti wa TANU alikuta tayari harakati za kudai uhuru zimeshaanza na zinazidi kupamba moto kwahiyo alichofanya yeye ni kuunganisha nguvu na watanganyika wenzake na kutokana wao kumuamini na kumpa uenyekiti wa chama basi ilibidi aongoze mapambano. Kwahiyo kama uhuru ungekosekana labda tanu ndiyo ingepingwa na si nyerere.
 
Mwita Maranya said:
Kwa kuzingatia kwamba nchi imepata uhuru huku ikiwa na wasomi wachache sana kiasi kwamba ilibidi kuagiza nguvukazi kutoka nje ya nchi ilikuwa ni jambo la busara mno kutaifisha shule za kidini zilizokuwepo ili kujenga taifa la watu wa aina moja. Vinginevyo watu wa aina fulani ndio wangeendelea kupata elimu wakati wenzao wakiangalia. Kwa kuzingatia kwamba pamoja na kutaifisha shule za dini na mashirika mbali walionufaika ni watanzania wote pasipo kujali rangi zao, dini zao, kabila zao na maeneo yao ya kuzaliwa basi jambo hilo haliwezi kutajwa kama kuliwarudisha nyuma kimaendeleo vinginevyo hata mimi huenda ningekuwa sasahivi niko mugumu huko ninachunga ng'ombe na kulima mtama na muhogo, usingenikuta hapa jf, kwa hili mwalimu anastahili pongezi kubwa.

Mwita Maranya,

..binafsi naamini uamuzi wa Mwalimu wa kutaifisha shule za binafsi na madhehebu ya dini ulikuwa na makosa.

..alichopaswa kufanya Mwalimu ni kujenga shule za serikali akielekeza nguvu zaidi maeneo ambayo yalikuwa yameachwa nyuma.

..kosa lingine ni ule utaratibu wa quota system ambapo wanafunzi ambao hawakuwa qualified walipewa nafasi za kuendelea na masomo.

..nakubaliana na dhima nzima ya kutoa elimu kwa wa-Tanzania wote, lakini nadhani juhudi hazikufanyika kuhakikisha kwamba tunatoa ELIMU BORA KWA WOTE, na mipango kama quota system ilikuwa inaficha deficiencies ktk mfumo wa utoaji elimu wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere.

..kitu kinachosikitisha ni kwamba mpaka leo hii usawa haujapatikana na zaidi elimu yetu imeshuka kiwango kiasi cha kutisha.
 
Back
Top Bottom