Mwakyembe apuuza data za JamiiForums!

Mwakyembe apuuza data za JamiiForums!

Status
Not open for further replies.
Naomba nikusahihishe ili kuondoa upotoshaji. Mwakyembe hajatamka: "Ndiyo tatizo la kuchukua data kwenye JamiiForums", bali ametamka:

"...hilo ndio tatizo la kutegemea sana JamiiForums"; binafsi sioni ubaya wa kauli hii kwani mbali ya kupata habari JF au chanzo kingine chochote, ni vizuri to verify na vyanzo vingine kabla haujawa na uhakika na unachokisema. Vinginevyo Dr. Mwakyembe ni dhahiri anaheshimu sana JF kama chombo cha habari na hii ilidhihirika wakati ule anaugua.

Mkuu mbona unakomaa sana kutetea kauli ya Mwakyembe. Kuna uzi umemwaga mboga kuhusu hii issue fuatilia ili ujue JF chanzo cha uhakika au kanjanja.
 
Mkuu mbona unakomaa sana kutetea kauli ya Mwakyembe. Kuna uzi umemwaga mboga kuhusu hii issue fuatilia ili ujue JF chanzo cha uhakika au kanjanja.

Nilikuwa nasikiliza bunge leo siku nzima na hivyo ndivyo nilivyosikia; nacho ongelea hapa ni kauli yake kwa Mh. Wenje na sio kitu kingine. Masuala mengine yanayozungumziwa humu yanasimama kama yalivyo.
 
masikini....mwakyembe..amesaau mchango wa jf kipindi kile ameumwa..binadamu bwana we hacha tu..
 
Nafikiri sumu sasa ndo imekimbilia kwenye medura .akumbuke kuwa kabla ajapewa sumu taharifa za tukio hilo zilishahanikwa hapa. kama hangekua anasoma hapa yasingempata hayo. jamii forum ni zaidi ya ukweli
 
Mwakyembe aombe radhi kwakosa lipi? Jf imefilisika hoja nimajungu,uzandiki,nachuki hakuna chamaana huku nikuchafua watt tu! Jf hainamuelekeo wala dira watu wakiwa nachuki zao wanakuja kuchafuana jf. Kwasasa jf haina mvuto inadharaurika sana

DU! mbona bado uko memba?
 
Hiyo bahari ya batter trade waliyopendekeza wachina waliotaka kujenga terminal three alishaisema Zitto tangu kikao cha April ndio zikafika hapa JF. Wenjer na yeye amekuwa mvivu tu wa kuuliza vema swali lake
Wacha kumzulia mheshimiwa Wenje! yeye akiuliza swali kwa kumtaka Mwakyembe atolee ufafanuzi wa kauri iliyotolewa na kambi rasimi ya upinzani bungeni juu ya bandari ya Mtwara, Mwakyembe kwa nia ya kutaka kuidharirisha hotuba ya upinzani ndio akaja na kauri ya kifedhuri kuwa hiyo ndio tatizo la kutegemea sana data za JF. Sasa hapo mvivu ni nani, kama sio yeye Mwakyembe kushindwa kufuatilia ukweli wa wapinzani. Wapinzani wanataarifa na ushahidi wa kutosha juu biashara hiyo haramu na ilisha semwa kwenye vikao vya bunge wakati yeye Mwakyembe akiwa ananyonyoka nywele kule India.
 
Nafarijika kuona JF inazungumziwa tena bungeni.....
 
Nilikuwa nasikiliza bunge leo siku nzima na hivyo ndivyo nilivyosikia; nacho ongelea hapa ni kauli yake kwa Mh. Wenje na sio kitu kingine. Masuala mengine yanayozungumziwa humu yanasimama kama yalivyo.


Mchambuzi,

..tatizo ni DHARAU za Mwakyembe.

..mfuatilie vizuri utakubaliana na haya ninayoyasema.
 
Alichosema ni kwamba "...hilo ndio tatizo la kutegemea sana JamiiForums"; binafsi sioni ubaya wa kauli hii kwani mbali ya kupata habari JF au chanzo kingine chochote, ni vizuri to verify na vyanzo vingine kabla haujawa na uhakika na unachokisema.
Agreed with you 100%.
 
Mchambuzi,

..tatizo ni DHARAU za Mwakyembe.

..mfuatilie vizuri utakubaliana na haya ninayoyasema.

Nadhani ana self-pride iliyopitiliza. Wanaolijadili hilo huku mitaani wanasema ni kawaida ya wanyakyusa, so I don't know.
 
Pia ana self-esteem kiwango ambacho ni unreasonable, au tuseme pride iliyopitiliza. Wanaolijadili hilo huku mitaani wanasema ni kawaida ya wanyakyusa, so I don't know.

ana majigambo sana.. na anapenda kushughulikia mambo madogo madogo sana.....hivi inawezekana njian abria wasichimbe dawa? kutakuwa na vyoo maalumu?
 
Ni mara ngapi?na ni data zipi ziliwekwa jamii forum ni za uongo??


Hivi data inawekwa na mtu ambae jina lake hata alieleweki wala details zake'wewe ungekuwa waziri utabeba hizo data kama ushahidi?je ukiambiwa tuletee huyo mwenye data utampata wapi? Mwakyembe yuko right kabisa
 
Uzuri wa mwakyembe akiwa mzima ni mwepesi wa kusahau fadhira. Akiumwa atajirudi na kuikumbuka tena jf. Angekuwa anajua sinia la kumuombea dua lilikuwa hapa jf asinge padhihaki.

Kwanza anatakiwa kutambua kuwa jf ni mahali patakatifu panapo beba watu wenye sauti tofauti, rangi tofauti, dini tofauti na makabila tofauti kwa wakati mmoja 24/7 kwa 365 tofauti na bunge ambalo lina vipindi maalumu na mambo huzuiwa kujadiliwa kwa kusingizia kuingilia uhuru wa mahakama. Sisi hapa hatuna hayo.
 
Lakini kuna kaukweli flani. Kuna habari nyingine zinazorushwa humu ni full c.r.a.p!

Mimi nimemuelewa Mwakyembe katika angle nyingine. Pamoja na mambo yote yanayosemwa kuhusu JF, yawe mazuri ama mabaya, jambo moja la msingi sana ni kwamba hawa wakubwa wanazidi kudhihirisha kwamba JF inawafikia huko waliko.
Kwahiyo wakiitaja kwa uzuri ama kwa ubaya bado wanakuwa wamei-recognize kama chombo mahiri cha habari kwakuwa hakuna chombo chochote cha habai kisichokosea iwe radio, tv stations, magazeti na hata mitandao ya kijamii (social digital media).
Big up Mwakyembe kwa kutambua nguvu ya JF. Wadau tuendelee kumkoma nyani kama kawaida.
Wale mabingwa wa kutema pumba tuwasaidie waweze kuweka machekecheo ili kuiboresha JF!
 
ana majigambo sana.. na anapenda kushughulikia mambo madogo madogo sana.....hivi inawezekana njian abria wasichimbe dawa? kutakuwa na vyoo maalumu?

Kwa hili la kuchimba dawa hata mimi nimeshangaa sana; wabunge wengine hoja zao hazina msingi na sio kila kitu waziri lazima akubaliane nacho, unatakiwa unakipima na wewe; suala la kuchimba dawa madereva huwa wanafanya msaada tu, vinginevyo from an economic stand point, tajiri anaingia hasara kwa kupoteza muda barabarani; sasa mpaka wajenge hivyo vyoo, kuanzia sasa ina maana breki ya kwanza kwa mfano njia ya Arusha - Dar ni njia panda/kwa maana nyingine ukipanda basi saa kumi na mbili asubuhi, jipange kujisaidia saa sita mchana to saa saba mchana; next time ni ukifika ubungo au Arusha; na ni muhimu ule msaada wa maji ya kunywa wanayopewa abiria wawe wana taadharishwa kabisa kwamba kusimama hapa ni baada ya masaa sita hadi saba.

Vinginevyo Mawaziri na wabunge wao pia ni mabingwa wa kuchimba dawa wanaposimama huko njiani kununua mahindi ya kuchoma na karanga za kuchemsha.
 
kama ni kweli amesema hivyo basi amekosea mzee wa watu, pengine ni madhara ya ile sumu aliyopewa na maadui zake, kwa kuwa JF ni waungwana bora tumsamehe bure hasa wakati huu wa mfungo na toba
 
Nadhani ana self-pride iliyopitiliza. Wanaolijadili hilo huku mitaani wanasema ni kawaida ya wanyakyusa, so I don't know.

Mchambuzi,

..I dont appreciate ur comments about Wanyakyusa.

..nina marafiki zangu Wanyakyusa na sijashuhudia hiyo "self-pride iliyopitiliza" unayoizungumzia.

..particularly, nimewahi kukutana na Prof.Mwakyusa, na hana hata chembe ya kiburi alichonacho Dr.Mwakyembe.

..I doubt it kama Dr.Mwakyembe angetoa kauli kama hizo kama muuliza swali angekuwa mbunge wa CCM.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom