Waziri wa Afya kazi imemshinda tishio la Hospitali binafsi kuikataa NHIF

masopakyindi

Platinum Member
Jul 5, 2011
17,882
13,172
1709287275118.png

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu

Sakata la Hospitali binafsi kuingia mgogoro na NHIF juu ya huduma itolewayo na NHIF kutokidhi gharama halisi ilinaendelea kurindima.

Kinachojitokeza ni kwamba srikali, hasa Wizara ya Afya inaonekana kulega ega katka sekta inyoisimamia.

Waziri wa Afya hatujamsikia akitoa neno katika swala hili. Wagonjwa watadhurika, na wengine kupoteza uhai, huku wavaa tai wakilumbana.

Umahiri wa kisiasa wa Ummy Mwalimu sasa ndio unatakiwa uonekane, kuwasaidia watanzania, hasa wale walio vitandani mahospitalini na wanaougua.
 
Hospital za binafsi ni wezi , wezi , wezi wakubwa , siku zoto wanabambikizia bili watu wenye bima . Ukiwa medical personel utagundua wanavyowaibia walala hoi.. Tatizo ni serikali kutokuwa na chombo kinachowafuatilia . Kama huamini nenda hospital tatu ukawaambia una tatizo fulani , utaona unavyobambikiziwa vipimo vikumba visivyo na tija ili ulipe hela nyingi
 
Huyo dada hiyo wizara sio size yake kabisa, kuna mengi ya kumlaumu kwenye ubovu wa huduma (she is just clueless). Lakini ili la NHIF huu sio mzigo wake ni wa serikali nzima, kumlaumu hapo nikumuonea.
 
Hospital za binafsi ni wezi , wezi , wezi wakubwa , siku zoto wanabambikizia bili watu wenye bima . Ukiwa medical personel utagundua wanavyowaibia walala hoi.. Tatizo ni serikali kutokuwa na chombo kinachowafuatilia . Kama huamini nenda hospital tatu ukawaambia una tatizo fulani , utaona unavyobambikiziwa vipimo vikumba visivyo na tija ili ulipe hela nyingi
Sasa kazi ikikushinda si utaibiwa tu?
 
Serikali si inasema Iko vizuri Kila Secta😂.
Kila mtu ashinde mechi zake.
Hiyo NHIF Tunazisikiaga kwenye familia za watumishi.mnaposema Walala hoi,wakati hiyo ni huduma ya Walala heli.

Hiyo wanyonge hauwahusu hata kidogo.

Tunalipaga kesho sisi,hakuna migogoro wowote hapo,maana wao wanatumia hela zao kujiendesha.

Hela Yao,Bado mnataka kuwawekea Sheria jinsi ya kuzitumia🤣.
Serikali iache janja janja,wanakusanya hela ya uchaguzi sio😏.
Hilo ni lenu Walala heli,sisi Walala hoi tunalipa keshi.
Sio kwamba tunawaonea wivu,hapana maana maisha haya yanahitaji mahesabu tu.
 
Nadhani wewe Huna kadi ya NHIF Huna clue yeyote ile ya process ya kutumia hiyo card.
 
Tatizo lishatengenezwa...

Sasa subiri muda si mrefu watatoka na tamko la kuwapa ujiko...
 
Ati Waziri katoa oreder kwa hospitali binafsi kupokea wagonjwa. Failure of negotiations, huwezi ku rely on orders.
 
Bila kupoteza muda sasa ni wakati wa VIKOBA vya AFYA, tutunze pesa kwaajili ya matibabu, dalili sio nzuri huko tuendako.
 
Pana mawili hapa,kutofautiana bei NHIF wana bei zao ambzo kwa hospital binafsi haziwalipi kurejesha gharama ya manunuzi ya dawa,.au NHIF hawazilipi hospital binafsi pesa kwa wakati
 
Pana mawili hapa,kutofautiana bei NHIF wana bei zao ambzo kwa hospital binafsi haziwalipi kurejesha gharama ya manunuzi ya dawa,.au NHIF hawazilipi hospital binafsi pesa kwa wakati
Ndio maana hospitali binafsi wamesuggest wagonjwa wenye NHIF waende hospitali za serikali.
Serikali yenyewe jnashindwa kuendesha hospitali zake kwa weledi.
 
View attachment 2921272
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu

Sakata la Hospitali binafsi kuingia mgogoro na NHIF juu ya huduma itolewayo na NHIF kutokidhi gharama halisi ilinaendelea kurindima.

Kinachojitokeza ni kwamba srikali, hasa Wizara ya Afya inaonekana kulega ega katka sekta inyoisimamia.

Waziri wa Afya hatujamsikia akitoa neno katika swala hili. Wagonjwa watadhurika, na wengine kupoteza uhai, huku wavaa tai wakilumbana.

Umahiri wa kisiasa wa Ummy Mwalimu sasa ndio unatakiwa uonekane, kuwasaidia watanzania, hasa wale walio vitandani mahospitalini na wanaougua.
Hospitali binafsi ni jipu. Mgonjwa unapewa dawa nyingi zingine hata hazihitajiki lengo wao ili wapige pesa.
 
Back
Top Bottom