Muombee Adui Yako Njaa; Maandamano Yanayoendelea Kenya Yawafurusha Watalii 800 na Kukimbilia Tanzania.

TODAYS

JF-Expert Member
Apr 30, 2014
13,764
21,237
Mzee RAO anamuangamiza kiuchumi Rais Ruto na makamu wake Gachagua kupitia maandamano.

Meli ya kitalii iitwayo MV Seabourn Sojourn, iliyopo njiani kwenda nchi mbalimbali duniani, ambapo kwa afrika mashariki ilikuwa isimame kwa siku 6 kwenye bandari ya Mombasa, sasa imebadiri uelekeo hadi Tanzania kutokana na maandamano ya upinzani yanayoendelea nchini Kenya.
cruise-seabourn.jpg

Meli hiyo inayotoka Mahe, nchini Shelisheli, ina watalii 800 sasa itatia nanga kwenye visiwa vya Zanzibar na Dar es Salaam kwa siku sita kabla ya kuelekea nchini Afrika Kusini.

Meli hiyo ilianza safari yake huko Miami Florida, mnamo Januari mwaka huu, ambapo safari yao inategemewa itakamilika Mei 27 huko katiak jiji la Barcelona, Uhispania.

Awali Kenya ilikuwa kwenye ratiba ya safari ya Mv. Seabourn Sojourn ambapo ilitegemewa kutia nanga katika bandari ya Mombasa.

Kufuatia hali hiyo nchi hiyo imepata athari kwenye sekta ya utalii huku wadadisi wakisema taifa hilo la Afrika Mashariki linapoteza mamilioni ya dola za kimarekani.

“Tumepoteza pesa nyingi sana, kutokana na matumizi ya awali, kila abiria hutumia angalau usd 200 kwa siku, kwa siku tatu hizo ni usd 600, tumepoteza usd 800,000, tukichukulia kila mmoja angetumia kiasi hicho,” kauli ya Bw Masemo, kutoka nchini Kenya.


Credit: The Citizens
 
Mombasa imetengenezwa katika hali maalumu ya watalii kufurahi, muunganiko wa bandari na sehemu za starehe zipo programed well, Dar yetu cruise ikitia nanga mazingira yanakwaza, atleast zanzibar pako ok!
N. B, IPO HAJA KWA MAMLAKA HUSIKA KULIANGALIA JAMBO HILI KWA AJILI YA CRUISE SHIP TOUR, GATTY LA CRUISE LIJENGWE WAPI, NA WATAKAPOSHUKA WATAELEKEA WAPI PA KUWAPA RAHA, NA SI KUBASE TU SERENGETI NA MBUGANI NI LAZIMA VYANZO VYOTE MUHIMU VIWE ACTIVATED.
 
Mombasa imetengenezwa katika hali maalumu ya watalii kufurahi, muunganiko wa bandari na sehemu za starehe zipo programed well, Dar yetu cruise ikitia nanga mazingira yanakwaza, atleast zanzibar pako ok!
N. B, IPO HAJA KWA MAMLAKA HUSIKA KULIANGALIA JAMBO HILI KWA AJILI YA CRUISE SHIP TOUR, GATTY LA CRUISE LIJENGWE WAPI, NA WATAKAPOSHUKA WATAELEKEA WAPI PA KUWAPA RAHA, NA SI KUBASE TU SERENGETI NA MBUGANI NI LAZIMA VYANZO VYOTE MUHIMU VIWE ACTIVATED.
Mkuu umeandika jambo kubwa na muhimu sana, nadhani kama viongozi wa serikali wanasoma hii basi wasiwe kama wale waliokula pesa ya ndege wakasingizia COVID.

Ukweli ni huo uliousema, ile bandari yetu pale Dasalama siyo ya Cruise ship ni ya cargo ship 🚢, ukiwa pale unaweza kuelewa hilo.

So nadhani kama inaweza kuleta tija basi bagamoyo pajengwe gati maalum la meli za kitalii although bagamoyo yenyewe itakuwa inabeba nia na tija ya kitalii ilihali pale jirani kuna mbuga ya wanyama.
 
Mkuu umeandika jambo kubwa na muhimu sana, nadhani kama viongozi wa serikali wanasoma hii basi wasiwe kama wale waliokula pesa ya ndege wakasingizia COVID.

Ukweli ni huo uliousema, ile bandari yetu pale Dasalama siyo ya Cruise ship ni ya cargo ship 🚢, ukiwa pale unaweza kuelewa hilo.

So nadhani kama inaweza kuleta tija basi bagamoyo pajengwe gati maalum la meli za kitalii although bagamoyo yenyewe itakuwa inabeba nia na tija ya kitalii ilihali pale jirani kuna mbuga ya wanyama.
Mkuu upo sahihi mno, bagamoyo nirahisi pia kusogea saadan kulingana na ratiba zao ambazo huwa ni siku 5-7.
"Bagamoyo is a right place"
 
Tutambue kwamba Kenya kukiwa na vurugu watalii wengi wanaotarajiwa kuja Tanzania pia huahirisha Safari zao kwakuwa ni nchi jirani. Pia baadhi ya ndege zinazobeba watalii wa TZ hupitia Nairobi.

Tushukuru hili vuguvugu linatokea kipindi hiki cha "Low Season".
 
Mkuu upo sahihi mno, bagamoyo nirahisi pia kusogea saadan kulingana na ratiba zao ambazo huwa ni siku 5-7.
"Bagamoyo is a right place"
Shida huwa ni kwa hawa wasimamizi wetu wa serikali, wapo kiwizi wizi sana, yaani mtu kaambiwa kula mwisho hapa ndipo kamba yako inaishia yeye anakata kamba na kuunganisha nyingine ili aibe zaidi, ndiposa anashtukiwa.

Yaani kama wakiangalia hili kwa jicho la future wanaweza kufanya uwekezaji wa kihistoria hapo bagamoyo.
 
Sawa mkuu, basi afadhali waje tu watie nanga bwaga moyo....🤥
Au nasema uongo ndugu zangu....🤷‍♂️
Sasa nikuulize kitu Ushimen, uliwahi fika bagamoyo?.

Kama bado au tayari unaona kuna sehemu ambayo meli inaweza kutia nanga?.

Na kwa mfano; wanakuja watalii 320+ wakishuka wanaelekea wapi kwa 'kuanzia' kabla ya kuanza tour?.
 
Sasa nikuulize kitu Ushimen, uliwahi fika bagamoyo?.

Kama bado au tayari unaona kuna sehemu ambayo meli inaweza kutia nanga?.

Na kwa mfano; wanakuja watalii 320+ wakishuka wanaelekea wapi kwa 'kuanzia' kabla ya kuanza tour?.
Dahhhhh.....
Upo sawa mkuu, pale meli ikitia naga lazima itang'oa tope..😂
 
Back
Top Bottom