Habari
Mimi ni muumini mzuri wa dini ya kikristo, nimezaliwa na kukulia katika dini. Hiyo haikuwa sababu ya kunizuia kusoma maandiko na machapisho ya dini zengine.
Nimesoma Quran pale nilipo bahatika, nikasoma maandiko ya freemasons yale niliyokutana nayo, nimesoma vitabu vya wahindu kwa uchache wake.
Vyote hivyo vinamuelezea Mungu vizuri kabisa na vimejitosheleza. Lakini hawa jamaa "Atheist" watu wasioamini uwepo wa Mungu.
Maandiko yao yamekuwa yakinipa ukakasi sana. Leo naomba Atheist mje hapa nanithibitishie kuwa Mungu hayupo.
Nipe sababu ikikupendeza nielezee kwanini unasema Mungu hayupo, nithibitishie kuwa hakuna, hajawahi kuwa Mungu wa aina yoyote ile.
Thibitisha kuwa Allah hayupo, hayupo Yehovah, hayupo Shiva, Vinshu. Yaani hii dunia haiendeshwi na Mungu