Binadamu tunathibitisha mambo kupitia senses zetu tano ambazo wote tunazijua.
Linapokuja swala la Mungu, binafsi sijawahi kumuona, kumsikia, kumuonja, kumuhisi wala kusikia harufu yake.
Hii inanipa hitimisho kwamba Mungu ni dhana tu iliyoanzishwa na binadamu walipokosa majibu ya asili ya mambo mbalimbali. Kisha akaingizwa kwenye hadithi mbalimbali na kupewa sifa za mamlaka na zingine za kuogofya.
So naamini Mungu haexist physically ila dhana ya Mungu inaishi kwenye vichwa vya mamilioni ya watu duniani Kwa kuwa stori za Mungu zinasimuliwa toka utotoni na dhana ya Mungu imebidhaishwa na watu mbalimbali Kwa manufaa yao binafsi ya kisiasa, kiuchumi na kadhalika.
Mkuu,
Nakushukuru sana kuelewa Mungu hayupo.
Tunakubaliana katika hilo. Nafurahi kuona tunaokubaliana katika hili tunazidi kuongezeka hapa JF.
Lakini kuna mengine tunapishana. Na hapo najisikia nina wajibu wa kunyambulisha mambo tueleweshane zaidi na kubadikishana mawazo.
Sifikiri kwamba sense pekee zinatosha kusema kitu kipo au hakipo.
Kuna mengi hatuyafahamu kwa sense tano, lakini tunaweza kutambua kuwa yapo kwa kutumia mantiki.
Kesho tunafahamu inakuja, lakini hatujaiona, hatujaisikia, hatujainusa, hatujaigusa, wala hatujaionja.
Kwa hivyo, zaidi ya senses tano, kuna akili, kuna mantiki.
Tunajua 1 + 1 = 2. Lakini hakuna hata mtu mmoja aliyewahi kuiona 1 (namaanisha 1 yenyewe, si chungwa moja, au namba moja inayowakilisha moja yenyewe)
Kwa hivyo, inawezekana kitu kikathibitishwa kimantiki, k8mahesabu, bila kuthibitishwa wala kujulikana kwa senses. Watu wanaofanya mahesabu ya juu wanajua hili. Waliweza kuthibitisha spacetime ina bend ukiwa kwenye high gravity, kwa mahesabu, bila kujua hilo kupitia senses. Kwa mahesabu tu. Ukimsima Albert Einstein na Relativity utaona hilo.
Kwa hivyo, ingawa nakubakiana nawe Mungu hayupo, sikubakuani nawe kwamba tunathibitisha mambo kwa senses tu.
Ukiindoleea senses zote tano, ukapewa uwezo wa jufanya hesabu tu, unaweza kuthibitisha mambo mengi sana kimatiki na kimahesabu.
Tatizo la dhana ya kuwapo Mungu si kwamba haonekani, haonjeki, hanusiki, hagusiki, hasikii.
Kuna vitu havionekani na vipo.
Kuna vitu havionekani, havionjeki, havinusiki, havigusiki nahavisikiki na vipo.
Tatizo la dhana ya kuwapo Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote ni la kifalsafa na kimantiki zaidi.
Tatizo ni kwamba, dhana ya kuwapo kwake haina logical consistency. Tabia zake, tunazoambiwa anazo a zinapingana zenyewe, pia, zinapingana na ulimwengu tunaouona kwa namna ambayo, Mungu huyo angekuwepo, ulimwengu huu tunaouona usingeweza kuwapo.
Unaambiwa Mungu ni kilele cha perfection, halafu unaambiwa Mungu anakasirika.
Kukasirika ni uthibitisho wa impwrfection, sasa Mungu perfect anakasirikaje?
Mungu perfect maana yake hawezi kukasirika. Kukasirika ni imperfection. Halafu hapo hapo unaambiwa Mungu ni perfect, halafu anakasirika. Cintradiction.
Unaambiwa Mungu huyu ni mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote. Logically Mungu huyu ni mwenye kugawa mazuri tu, mabaya hagawi. Ana neema kuu.
Sasa Mungu huyu imekuwaje kaumba ulimwengu ambao unaruhusu mabaya, wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao hauruhusu mabaya?
Kati ya anayeumba ulimwengu unaoruhusu mabaya na anayekuja kujikuta katika ulimwengu huo tu, na kufanya mabaya, lakini hajaumba ulumwengu unaoruhusu mabaya, nani ana kosa kubwa zaidi?
Hivi, huyu aliyeumba ulimwengu ambao unaruhusu mabaya, angeumba ulimwengu ambai mabaya hayawezi jufanyuka, viumbe ambao wangetokea katika ulimwengu huo wangeweza kufanya mabaya?
Kati ya Mungu na viumbe hapa, nani ana makosa makubwa zaidi?
Kuna mtu al8niambia kwamba napinga uwepo wa Mungu kwa sababu sijamuona.
Nikamwambia si kweli, unaweza kwenda jangwani, ukaona mbele yako kuna chemchemi ya maji kwa mirage, kumbe hakuna maji, ni mauzauza ya mwanga nanjoto tu.
Unaweza kuona Bob Marley anaimba mbele yako kwenye TV au computer, kumbe Bob Marley amefariki tangu May 11 1981.
Kwa hivyo, hizi five senses, kuona, kusikia, kuonja, kunusa na kugusa si vitu vya kuhakiki na kuthibitisha kitu kipo.
Vitu vinaweza kuhakikiwa na kuthibitishwa vizuri zaidi kwamba vipo kweli kwa kutumia hizo senses, pamoja na kitu kikubwa zaidi.
Akili. Mantiki.
Logical consistency. Contradictions.
Na pingamizi langu kubwa kabisa dhidi ya hoja ya uwepo wa Mungu, si ka senses, ni la kiakili na kimantiki.
Ninapopinga uwepo wa Mungu kwa kuangalia "the problem of evil", si kwa sababu simuoni, simuonji, simgusi, simsikii wala simnusi.
Babu za babu zangu wote siwaoni, siwaonji, siwagusi, siwasikii na wala siwanusi.
Lakini, kwa kutumia logical consistency, naweza kusema nina uhakika waliishi.
So.
Mungu hayupo.
Si kwa sababu simuoni, simuonji, simgusi, simsikii au simnusi.
Bali, kwa sabaju, habari za kuwapo kwake zina logical inconsistencies na contradictions kibao.