Mungu hayupo? Atheist njooni mthibitishe

Mungu hayupo? Atheist njooni mthibitishe

Hutapanga nini nifanye ama nini nisifanye.

Kama unaona kufanya hivyo ni sahihi fungua mada kisha weka ‘facts’ then “opposers waje na reasons zao”
Sijaelewa why umereply kwa ukali hivyo. Ila ni kawaida, ukianzisha mada lazima wewe uwe na upande, na huo upande lazima uwe na hoja zako ambazo zitafungulia mada, huwezi anzisha mada kwa heading tu
 
ixo ni theory tu mkuu hazima uthibitisho, juzi darubini mpya imeprove big bang theory ni uongo mkubwa
Kwanza kabisa darubini kubwa haija prove hilo, kama unataka tujadili hilo, weka source zako.

Pili, hata wewe uwepo wako unaweza kuelezewa kwa theory, je, hilo linamaanisha wewe haupo kikweli kwa sababu umeweza kuelezewa na theory?

Tatu, unapotumia simu inayotumia electromagnetic waves, minara, satellite, internet, unatumia vitu vinavyothibitisha theories kama Relativity, je unafahamu hilo? Utasema hapa tunawasiliana kwa theory tu?

Nne, hata kama hizo ni theories tu, bado hujathibitisha Mungu yupo, unakubali kwamba kw muktadha wako wa kudogosha theory Mungu naye ni theory tu hajathibitishwa?

Einstein's Relativity imethibitishwa tangu mwaka 1919 na inaendelea kupsi mitihani ya uthibitisho mpaka mwaka huu.

Unajua hilo?
 
sukari kwenye miwa ,machungwa, na ladha kwenye magimbi, iliwekwa na wanasayansi ,kwa mujibu wa Kiranga
Wapi nimesema hilo? Naomba link unioneshe, ama sivyo wewe ni muongo unaniwekea maneno ambayo sikusema.

Zaidi, hoja yako ni nini? Kwamba kama hatujui sukari imeingiaje kwenye miwa (kitu ambacho tunajua) basi ni lazima imewekwa na Mungu?
 
Hapana si vitu nivionavyo mimi kwani tangu nizaliwe nina miaka michache sana hapa duniani, haifiki hata hamsini kwahiyo huwezi sema nivionavyo mimi.
“kabla yetu” kirahisi waweza sema kabla ya Big Bang, Kabla ya kuumbwa mwanaadamu (kama waumini watavyosema) au kabla hatuja-evolve kama wanasayansi watavyosema, wakati wetu ni tangu Binaadamu aifaye Dunia kuwa makazi yake, baada yetu- (hii ni possibility) kwa maana hakuna ajuae kwa hakika nini kitafuata, kama wanaadamu watatoweka na kutokea viumbe wengine au namna gani…

Nafikiri kwa makusudi kabisa unajaribu kutafuta chochoro.
Wakati kabla yetu na vilivyo kabla yetu na vijavyo baada yetu ni dhana rahisi kuelewa sijui vipi huelewi.

Ila si mbaya.

Vizuri kabisa, twende kwa ufinyu huu huu niliokuja nao wa dhana ya “vyote” kama nilivyoisema awali, pasina Msingi wa kiulimwengu (kama ambavyo wewe unaufahamu huo Ulimwengu, ukiweza nitafurahi ukinipa maana yake)

Si wote,

Si nusu tu, hata theluthi itakuwa ngumu, ndiyo maana kwa makusudi nikasema “tunavyovijua, tusivyovijua na ambavyo hatutakuja kuvijua”

Kwa maana ile ile unayoiita “finyu” ya dhana ya “vyote” tafadhali nijibu swali hili tufunge mjadala huu, na kama hauna jibu si ubaya kukiri.

Je, tunaweza hitimisha kuwa kwako wewe Bwana Kiranga dhana ya Mungu (ikimaanisha Muumba kwa vyote-kwa “Ufinyu wa kiparokia” wa dhana hii) ni batili na kiumbe, nguvu, mtu au chochote kinachinasibishwa na dhana hiyo si halisi ila uzushi???
Sasa unataka tuongelee muumba vyote wakati hata hatujui vyote ni nini?

Tutaongeleaje hilo?

Yani hivi vichache tunavyoviona na kuvifahamu tu vinakanusha kuwepo kwa convergence kutokea Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, halafu unataka kuviongeza vyote ambavyo hatuvijui?

Let's talk about time.

Do you understand that the concept of time is not fundamental and absolute, and that it is relative and not absolute, and that your question of "before, now, and after" is rather anthropic?

Wewe ni kama mtu uliye katika gari linalokimbia kwa kasi, unafikiri kila mtu yupo katika gari anakwenda kwa mwendo wa kasi.

Hujui kwamba hilo gari kwenda kwa mwendo wa kasi ni a derivative of a still background that does not necessarily move.

Time is neither fundamental nor absolute.

Sasa utasemaje kilichopita, kilichopo na kinachokuja wakati dhana nzima ya sasa inategemeana na mtizamaji ni nani?

Kilichopita kwa nani? N nakwa nini kwa huyo?

Unajua kwamba baba yako aliyekuzidi miaka 40 anaweza kukuacha hapa leo akafanya safari na kurudi yuko kijana kwa miaka mingi kuliko wewe, kwa sababu ya effects za time dilation at near relativistic speeds?

Time is relative, neither fundamental, nor absolute.

Why are you making it fundamental and absolute?
 
Dini zilikuwepo tangu enzi na enzi, jamii za wanaadamu zimekuwa zikiabudu vile wanavyoviita Mungu kwa miaka mingi sana hili halina ubishi.

Uwepo wake miaka mingi haina maana ni sahihi kuwepo wake maana hata uongo usipodhihirika huonekana ukweli miaka yote mpaka ukweli utakapofahamika.

Ila kuna sehemu ya watu kwenye jamii wamekuwa wakitilia mashaka na kukosoa wazo lenyewe la kuwepo kwa huyo anaeitwa Mungu. Wanaoamini (imani yoyote tu ‘as long as’ wanamuabudu wanachokiita Mungu) wanasistiza kuwa yupo na uwezo wake ni Mkuu sana.

Hoja za waumini nazifahamu baadhi, ila hoja za Atheist sijazielewa.

Ningependa kuwaelewa zaidi Atheists, Karibuni hapa Atheist walau mthibitishe (kama mtaweza) kuwa huyo wa kuitwa Mungu hayupo.

Lakini kwanza ni lazima tufafanue nini maana ya MUNGU, kwa maana kukurupuka kujibu swali ilhali hatujui maana ya dhana ya msingi wa swali itakuwa ni uhayewani wa kiwango cha juu sana.

Karibuni sana!
View attachment 2355249
Thibitisha kwamba hayupo wewe unayedai hivyo. Unakuja na madai na unamtupia mwingine kazi ya kuthibitisha.
 
Dini zilikuwepo tangu enzi na enzi, jamii za wanaadamu zimekuwa zikiabudu vile wanavyoviita Mungu kwa miaka mingi sana hili halina ubishi.

Uwepo wake miaka mingi haina maana ni sahihi kuwepo wake maana hata uongo usipodhihirika huonekana ukweli miaka yote mpaka ukweli utakapofahamika.

Ila kuna sehemu ya watu kwenye jamii wamekuwa wakitilia mashaka na kukosoa wazo lenyewe la kuwepo kwa huyo anaeitwa Mungu. Wanaoamini (imani yoyote tu ‘as long as’ wanamuabudu wanachokiita Mungu) wanasistiza kuwa yupo na uwezo wake ni Mkuu sana.

Hoja za waumini nazifahamu baadhi, ila hoja za Atheist sijazielewa.

Ningependa kuwaelewa zaidi Atheists, Karibuni hapa Atheist walau mthibitishe (kama mtaweza) kuwa huyo wa kuitwa Mungu hayupo.

Lakini kwanza ni lazima tufafanue nini maana ya MUNGU, kwa maana kukurupuka kujibu swali ilhali hatujui maana ya dhana ya msingi wa swali itakuwa ni uhayewani wa kiwango cha juu sana.

Karibuni sana!
View attachment 2355249
Nani alikudanganya kuwa,kama dini zimedanganya basi hakuna Mungu?
 
Nani alikudanganya kuwa,kama dini zimedanganya basi hakuna Mungu?
Sawa, inawezekana dini zikadanganya na Mungu akawapo.

Inawezekana pia dini zikadanganya na Mungu akawa hayupo.

Kwa hivyo dini tu si muhimu, maana hazitupi jibu lisilohojika kuhusu Mungu, inawezekana zinadanganya, inawezekana hazidanganyi.

Sasa unathibitishaje Mungu yupo nje ya dini? Maana tushaona dini hazina jibu lisilohojika kimantiki.
 
Sawa, inawezekana dini zikadanganya na Mungu akawapo.

Inawezekana pia dini zikadanganya na Mungu akawa hayupo.

Sasa unathibitishaje Mungu yupo?
Naweza pia nikashindwa kuthibitisha uwepo wa Mungu halafu akawa yupo...

Naweza pia kushindwa kuthibitisha akawa hayupo...

Kwahiyo?
 
Naweza pia nikashindwa kuthibitisha uwepo wa Mungu halafu akawa yupo...

Naweza pia kushindwa kuthibitisha akawa hayupo...

Kwahiyo?
Utajuaje Mungu yupo kweli na hiyo habari si imani yako tu wakati kiukweli hayupo?
 
Utajuaje Mungu yupo kweli na hiyo habari si imani yako tu wakati kiukweli hayupo?
Iwe naweza kujuwa au siwezi,bado haiwezi kubadili ukweli kwamba yupo au kinyume chake...

Jambo tunalolifanya hapa ni kubadilishana mawazo ya namna mimi napna yupo lakini wewe unaona kinyume na mimi japokuwa sababu ni hizo hizo zinazokufanya wewe uone hayupo na mimi nione yupo...

Yote hayo hayabadili ukweli ambao huenda wote hatuujuwi au mmoja wetu anaujuwa...


Jambo ambalo nilitaka kumsaidia niliyemnukuu ni kuonesha makosa ya kufikiri kwamba kama dini zimekosea basi anayesemwa na dini hizo hayupo...

Ni kama mtu atoe taarifa ya mafuriko sehemu fulani halafu aseme kulikuwa pia na maghorofa milioni moja eneo hilo...

Habari ya uwepo wa maghorofa inaweza kuwa siyo ya kweli lakini haimaanishi kwamba taarifa ya mafuriko ni uwongo...
 
Atheism ni kukataa kuwepo Mungu nje ya dhana na fikra, hivyo ukiniuliza atheists tunaielewaje dhana ya Mungu, tunaielewa kama kitu cha kufikirika ambacho hakipo katika uhalisia nje ya kufikirika.

Ni kama dhana ya "pembetatu ambayo pia ni duara" katika Euclidean geometry planes.Unaweza kuisema, unaweza kuifikiria, lakini haipo katika uhalisia.

Kuhusu dhana ya Mungu kwa upana wake, nakuomba usome hiki kitabu "Philosophy of Religion: An Anthology".

Kimeelezea vizuri sana, kisomi, kutoka pande zote, za watu wanaoamini uwepo wa Mungu na wasioamini uwepo wa Mungu. Nakiambatanisha.
THIBITISHA uwepo wa hewa/upepo kimwonekano wa macho na kiumbo/visibility/physically/tangible ilihali ndivyo nguvu ya uhai (roho) kiumbe chochote kinachoishi ktk sayari hii (dunia).
 
THIBITISHA uwepo wa hewa/upepo kimwonekano wa macho na kiumbo/visibility/physically/tangible ilihali ndivyo nguvu ya uhai (roho) kiumbe chochote kinachoishi ktk sayari hii (dunia).
Kwa nini nithibitishe jambo ambalo sijalitolea madai?

Je, nikishindwa kuthibitisha hilo, hilo litathibitisha Mungu yupo?
 
Kwanza kabisa darubini kubwa haija prove hilo, kama unataka tujadili hilo, weka source zako.

Pili, hata wewe uwepo wako unaweza kuelezewa kwa theory, je, hilo linamaanisha wewe haupo kikweli kwa sababu umeweza kuelezewa na theory?

Tatu, unapotumia simu inayotumia electromagnetic waves, minara, satellite, internet, unatumia vitu vinavyothibitisha theories kama Relativity, je unafahamu hilo? Utasema hapa tunawasiliana kwa theory tu?

Nne, hata kama hizo ni theories tu, bado hujathibitisha Mungu yupo, unakubali kwamba kw muktadha wako wa kudogosha theory Mungu naye ni theory tu hajathibitishwa?

Einstein's Relativity imethibitishwa tangu mwaka 1919 na inaendelea kupsi mitihani ya uthibitisho mpaka mwaka huu.

Unajua hilo?



ivi unajua gravity bado ni tatizo kubwa?,
 
nimekutana na comment moja uko ulimwenguni naona niwadokeze. kwamba adam ni mtu wa kwanza mweupe na sio mtu wa kwanza duniani, ANU ndio muumbwa wa wafrica wana wa ANU yani ANU NNAKI,sasa ukitafuta usibitisho wa ANU kuwa yupo au alikuwepo unaupata mchana kweupe.
 
Mungu anatafsirika kwa sifa zake.

Mungu ni nini?
Mungu anatafsirika kwa sifa zake
Hatuwezi kutoa fasiri ya Mungu kwa kumnasibisha na kitu, vitu au hali au kiumbe mfano hatuwezi sema mungu ni mtu .......
au mungu Ni kitu...... au mungu Ni Hali...... Kwanini hatuwezi sema hivyo ni kwa sababu hakuna aliyewahi kumuona mungu, Ila kutokuonekana kwake hatushindwi kutoa maana ya Mungu kwani tunaweza kumueleza kwa sifa zake.

Hivyo basi mungu anaelezeka kwa sifa zake na hivyo basi maana ya mungu ni mwenye kupaswa kuabudiwa kwa haki, muwezawa wa kila kitu, asiyeshindwa na lolote, mwenye kuumiliki ulimwengu na sifa nyingine nyingi tu anazo.
I mentioned just few attributes as an examples.
 
Maswali ya msingi sana
sababu ya wewe kusema hakuna mwanzilishi wa haya yote nini? nakama unauhakika hakuna je ni nan kafanya haya yote kwa ustadi mkubwa hivyo ? nn chanzo cha uhai , na uhai una dhumuni gani?maisha ni nini ? mwisho wa maisha upo kwa dhumuni lip ili iweje ? ikishakua kwa sababu gan?wewe ni nan umetoka wap? upo kwa dhumuni gani ? ukifa unaenda wap ? kwa sababu gani . pia kumbuka hakuna jambo lolote lisilokua na sababu.
 
Imani, imani imani.
Sina shaka imani hiyo hukuzwa na sababu fulani fulani, hiyo ndiyo ‘focus’ yetu.

Kipi kinakufanya UAMINI YUPO?
au
Kipi kinakufanya UAMINI HAYUPO?

Ila kabla hatujafika huko tuanze na maana ya dhana yenyewe ya MUNGU.
Mungu ni kila kitu na kila kitu ni Mungu..imani ni Mungu..kutokuwa na imani pia ni Mungu Atheist pia ni Mungu shetani pia ni Mungu..Mungu pia ni shetani...pia kuhoji na kuuliza Mungu ni nini? Pia ni Umungu vile vile...
 
Dini zilikuwepo tangu enzi na enzi, jamii za wanaadamu zimekuwa zikiabudu vile wanavyoviita Mungu kwa miaka mingi sana hili halina ubishi.

Uwepo wake miaka mingi haina maana ni sahihi kuwepo wake maana hata uongo usipodhihirika huonekana ukweli miaka yote mpaka ukweli utakapofahamika.

Ila kuna sehemu ya watu kwenye jamii wamekuwa wakitilia mashaka na kukosoa wazo lenyewe la kuwepo kwa huyo anaeitwa Mungu. Wanaoamini (imani yoyote tu ‘as long as’ wanamuabudu wanachokiita Mungu) wanasistiza kuwa yupo na uwezo wake ni Mkuu sana.

Hoja za waumini nazifahamu baadhi, ila hoja za Atheist sijazielewa.

Ningependa kuwaelewa zaidi Atheists, Karibuni hapa Atheist walau mthibitishe (kama mtaweza) kuwa huyo wa kuitwa Mungu hayupo.

Lakini kwanza ni lazima tufafanue nini maana ya MUNGU, kwa maana kukurupuka kujibu swali ilhali hatujui maana ya dhana ya msingi wa swali itakuwa ni uhayewani wa kiwango cha juu sana.

Karibuni sana!
View attachment 2355249
Kuwepo na kutokuwepo kwa Mungu pia ni Mungu..Mungu ni kila kitu na kila kitu ni Mungu, Atheist pia ni Mungu...imani pia Mungu.. shetani ni Mungu na Mungu ni shetani..mwanzo ni Mungu na mwisho ni Mungu.
 
Back
Top Bottom