Kwa nini unafikiri nina majibu haya au hata ninaweza kuwa na majibu ya maswali haya?
Kwa nini mtazamo wangu uwe muhimu kuliko utaalamu uliokubalika na kuchunguzwa na mchakato mzima unaorejewa na kuthibitishwa na dunia ya kisayansi?
Mimi ni atheist. Atheism ni kukataa uwepo wa Mungu. Si kusema kwamba tunajua dunia imeanzaje, maisha yameanzaje.Sijawahi kusema najua majibu ya maswali haya nje ya kusema kwamba najua Mungu si jibu sahihi, kwa sababu hayupo.
Ninachojua ni kwamba hatumhitaji Mungu kuelezea yote hayo, in fact theory ya Mungu inakuwa contradicted na dunia tunayoiona, watu wanavyoishi na kufa.
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote angekuwepo, wote tungekuwa na uelewa mzuri na hata mjadala juu ya uwepo wake usingekuwepo na kusingekuwepo na kifo.
Kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambao kumjua yeye tu ni jambo lenye utata mwingi sana na ugomvi mwingi sana, mpaka watu wanauana kwa vita vya kidini? Kwa nini hajafanya dunia yote imjue kiukweli na usawa bila utata wala kuhitaji kitabu, mahubiri, tafsiri, mijadala ya JF, na kadhalika?
Kifo kibaya, kinatenganisha wanaopendana.Kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote aruhusu ulimwengu ambao unaweza kuwa na kifo na kutengenisha viumbe wake anaowapenda na wanaopendana? Huyo Mungu anayeachia viumbe wake wafe wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao hauwezi kuwa na kifo ana upendo gani?
Wewe Baba yako akiwa na uwezo wa kufanya familia yenu mtu asife, wote muishi vizuri tu miaka yote, ana uwezo wa kutatua tatizo lolote, halafu akaruhusu ndugu zako wote wafe, utasema huyo Baba yako ana upendo kweli?
Dunia ilianzaje?
Scientists can use modern rocks, moon samples and meteorites to figure out when and how the Earth and moon formed, and what they might once have looked like.
news.uchicago.edu
Tunakufa na hatuwezi kuzuia kifo kwa sababu seli zetu zinakufa kwa kufuata second law of thermodynamics
We die naturally because our cells die.
www.livescience.com
Jumuiya ya sayansi inachunguza chanzo cha maisha bado, lakini kuna ushahidi mkubwa kwamba maisha yalianza baada ya replication ya RNA au molecule kama RNA.
Even before Charles Darwin proposed his theory of evolution in 1859, scientists the world over had been trying to understand how life got started. How did non-living molecules that covered the young…
beta.nsf.gov
Habari zote hizo hazimuhitaji Mungu, ukimuingiza Mungu hapo unalazimisha tu.