Mungu hayupo? Atheist njooni mthibitishe

Mungu hayupo? Atheist njooni mthibitishe

Kwanza kabla ya yote haya unatakiwa kijiuliza Wewe hivi Mungu ni nani?
Yupo je?
Je ana mwili kama sisi wanadamu au vipi anaonekana au vipi

Ukipata majibu ya maswali yako ndo sasa uje ulete mada apa
Sio umepigwa na stress zako za mapenzi ndo unakuja kutuletea kelele apa acha bangi



Si vyote vitakavyowasilishwa vitaafikiana na matakwa yako
 
Kwanza, sijasema Mungu hayupo kwa sababu anatesa watu. Akitesa watu atakuwa yupo, si hayupo.

Nasema Mungu hayupo kwa sababu dhana ya Mungu kuwapo inajipinga yenyewe. Mara unaambiwa Mungu ana upendo mkuu, mara unaona vitoto vichanga masikini vinakufa kwa utapiamlo.

Watu wametunga dhana ya Mungu.

Wakampa Mungu tabia za watu. Ndiyo maana unasikia Mungu anatoa mtihani, Mungu anakasirika, Mungu anaghairi mambo aliyopanga na kuleta mafuriko duniani.

Mungu anakasirikaje wakati anajua kila kitu kitakavyokuwa? Anaghairi nini wakati anajua kila kitu kitakavyokuwa?

Anatoa mtihani ili iweje wakati yeye anajua yote yatakavyokuwa?

Mtihani ni sehemu ya maisha ya dunia ya watu wasio na nguvu zote, uwezo wote wala upendo wote. Kupimana ili kujua nani anajua zaidi. Na hata katika dunia hii, kuna baadhi ya jamii zinaondokana kwenye mifumo ya mitihani.

Sasa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kwanza kwa nini aweke mitihani mibaya sana inayoweza kuumiza watu wake anaowapenda?

Hivi, kuna baba mwenye akili zake timamu, anayewapenda watoto wake, anayesema leo najenga nyumba, naitegeshea mabomu ndani yake, ili wanangu wapate kujua kukwepa mabomu, wakati anaweza kujenga nyumba ambayo haina mabomu?

Hivi, msichana wa miaka 10 anayejiuza mjini Manila Philippines ili apate kula tu, anapewa mtihani wa maisha hayo na Mungu mwenye mapenzi?

Wale Wahutu na Watusti waliochinjana kama kuku, yani Mungu hata kama tunasema anatoa mitihani, alishindwa kuwapa mtihani mzuri ambao hauna mauaji ya kinyama?

Kwa nini Mungu anayejua kila kitu na kuweza kila kitu na mwenye upendo wote ahitaji kuwepo na mtihani, hususan kama mtihani wenyewe unaumiza sana viumbe wke anaowapenda?

Usiongelee mtihani kama kitu ambacho hakiepukiki katika dunia hii tunayoiona, ongelea mtihani kutoka perspective ya Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote.
kwanza kabsa unatakiwa ujue mimi skubaliani na hii hali ya Mungu kupewa sifa hzo sijui hasira kuabudiwa huzuni na mengne mengi hizo ni sifa za mapungufu tambua vitabu vya din ni maono ya watu waliojitambua na kumtambua Mungu japo kuna nyongeza nyingi ya watu flan kwa dhumuni flan lenye sababu maalumu, huo unaosema ni ubaya ni sisi tu bila kuwa na jicho la ndani tunaona niubaya ila kiuhalisia zina sababu maalumu kwa njia ya upendo mkuu.
 
Huelewi sifa za Mungu ni kigezo kikubwa kumtofautisha na mtu?

Mungu ambaye hana uwezo wote na upendo wote unamtofautishaje na mtu?
kumtofautisha Mungu na mtu kivp wakati nimeshasema huko juu sisi ni maumbile ya chini kabsa na frequence ya chini ya hyo nguvu kuu hyo nishati ipo kwenye mwendo , kuna maumbile mengne tu yapo hatuwezi kuyaona kwasababu yapo kwenye speed na frequence ya juu zaid
 
Mtoa mada haueleweki ushasema Mungu hayupo maana yake tayari una tafsiri yako kuhusu uyo Mungu alafu unataka wasioamini waje kuthibitisha kutokuwepo kwa uyo Mungu unaemjua wewe sasa hii maana yake nini?

Watu wemekuambia uko juu leta iyo tafsiri ya Mungu unaesema hayupo ila ichambuliwe na wewe unawarushia mpira unataka wao ndo watoe tafsiri ya Mungu hivi unajua kweli unachokitaka? Umeianza hoja yako kwa kusema Mungu hayupo sasa leta tafsiri ya uyo Mungu unaesema hayupo ili achambuliwe. Kiranga na Scars Wanajaribu kukuelewesha hapo Mungu ni nini? Au ni nani?

Wewe unataka wao ndo wamchambue Mungu wakati wewe mwenyewe ushasema hayupo, leta tafsiri ya uyo Mungu unaesema hayupo ichambuliwe mbona unafanya mjadala mfupi na rahisi uwe mrefu na mgumu
 
Na wewe thibitisha there is God, lakini sio mapambio tuu na story za wayahudi & waarabu mlizokaririshwa ambazo hata wenyewe wameacha kuziamini
umejuaje wameacha kuamini , ni wapi hawaamin kuhusu Mungu ? usiongee tu kufurahisha uma mimi nmeishi telaviv sjaona hao watu wasio amni nimekutana na waislam na wayahudi , tena wengi wana ujuzi wa hali ya juu na matajir wakubwa.
 
Nimejaribu kupitia comments za watu katika hii thread, Nilichogundua Ni kwamba Kama ambavyo binadamu tulivyo tofauti kimuonekano basi pia tupo tofauti sana kifikra.
Nirudi kwenye mada kwanza kuthibitisha kuwa Kuna mungu au hayupo ni lazima tukubaliane juu ya maana ya Mungu, Kisha ndio tuthibitishe uwepo wake au kutokuwepo.
Pili tuelewe ni ngumu kutenganisha dhana ya uwepo wa mungu na dini yaani uyahudi,uislamu na ukristo.
Nianze na maana ya mungu(N.b kwa jinsi ninavyofahamu Mimi)
Mungu kutoka katika Mwenyezimungu yaani mwenye- enzi -mungu.
Mwenye-mmiliki wa
Enzi- ya kale au mwanzo
Mungu- muweza wa kila Jambo/ anayepaswa kuabudiwa
Hivyo unaposema Mwenyezimungu maana yake -wa mwanzo mwenye kupaswa kuabudiwa au wa mwanzo muweza wa kila Jambo.
Sasa turudi juu ya uwepo wake na kutokuwepo.
Hapa tuelewe kuwa wengi wanao support uwepo wa mungu ni watu wenye dini yaani waislamu,wakristo na wayahudi ndio maana mwanzo nikasema ni ngumu kutenganisha mungu na dini.

Kwa uzoefu wangu wengi wanaopinga uwepo wa mungu (Atheists) wanatumia hoja za kiakili na logic pamoja na ushahidi wa kisayansi kuthibitisha kuwa hakuna mungu na hapo ndipo tatizo limapoanzia, kivipi? ..kuwa makini point inayofuata.

Unapotaka kuthibitisha kuwa hakuna mungu kwa kutumia let say milango ya fahamu yaani macho, pua, masikio n.k hii tunasema ni sayansi kwa maana nyingine ni vipimo vya kupimia vitu vyenye asili ya maada (matters) na mungu sio maada Hivyo kutaka kumpima mungu kupitia vipimo vya kupimia maada ni kosa kwa maana wale Wanaosema mungu hayupo kwa sababu haonekani , hashikiki huwezi kumnusa hoja yao inakosa nguvu automatic kwani wametumia vipimo ambavyo sio sahihi kumpimia mungu yaani ni sawasawa na uchukue mizani ya kupimia uzito alafu unataka kujua kimo cha ndoo hutapata kimo utapata uzito lakini haimanishi hiyo ndoo haina kimo inayo na ukitaka Kupata kimo chake tumia tape measure na sio mizani.

Hoja Ni nyingi Sana ambazo Atheists wanazitumia na Mimi apo nimetoa hoja moja tu na nimeikosoa hoja hio ..mwenye hoja nyingine aweke hapo alafu tuchambue kila hoja
N.b msimamo wangu mungu yupo na linathibitika kiakili, kisayansi na kiimani..​
 
Mtoa mada haueleweki ushasema Mungu hayupo maana yake tayari una tafsiri yako kuhusu uyo Mungu alafu unataka wasioamini waje kuthibitisha kutokuwepo kwa uyo Mungu unaemjua wewe sasa hii maana yake nini? Watu wemekuambia uko juu leta iyo tafsiri ya Mungu unaesema hayupo ila ichambuliwe na wewe unawarushia mpira unataka wao ndo watoe tafsiri ya Mungu hivi unajua kweli unachokitaka? Umeianza hoja yako kwa kusema Mungu hayupo sasa leta tafsiri ya uyo Mungu unaesema hayupo ili achambuliwe. Kiranga na Scars Wanajaribu kukuelewesha hapo Mungu ni nini? Au ni nani? Wewe unataka wao ndo wamchambue Mungu wakati wewe mwenyewe ushasema hayupo, leta tafsiri ya uyo Mungu unaesema hayupo ichambuliwe mbona unafanya mjadala mfupi na rahisi uwe mrefu na mgumu
kwa comment hii mjadala ufungwe
 
kwanza kabsa unatakiwa ujue mimi skubaliani na hii hali ya Mungu kupewa sifa hzo sijui hasira kuabudiwa huzuni na mengne mengi hizo ni sifa za mapungufu tambua vitabu vya din ni maono ya watu waliojitambua na kumtambua Mungu japo kuna nyongeza nyingi ya watu flan kwa dhumuni flan lenye sababu maalumu, huo unaosema ni ubaya ni sisi tu bila kuwa na jicho la ndani tunaona niubaya ila kiuhalisia zina sababu maalumu kwa njia ya upendo mkuu.
Sababu gani maalum?

Ukifuatilia hoja hiyo ya "sababu maalum za upendo mkuu", hata mimi ninaweza kukuambia wewe kuwa mimi ndiye Mungu mwenywe, ila siwezi kukufahamisha vizuri kwa sababu maalum za upendo mkuu.

Utanipingaje ikiwa ushaikubali hoja ya "sababu maalum za upendo mkuu" isiyo na maelezo kuwa inatosha?
 
Nimejaribu kupitia comments za watu katika hii thread, Nilichogundua Ni kwamba Kama ambavyo binadamu tulivyo tofauti kimuonekano basi pia tupo tofauti sana kifikra.
Nirudi kwenye mada kwanza kuthibitisha kuwa Kuna mungu au hayupo ni lazima tukubaliane juu ya maana ya Mungu, Kisha ndio tuthibitishe uwepo wake au kutokuwepo.
Pili tuelewe ni ngumu kutenganisha dhana ya uwepo wa mungu na dini yaani uyahudi,uislamu na ukristo.
Nianze na maana ya mungu(N.b kwa jinsi ninavyofahamu Mimi)
Mungu kutoka katika Mwenyezimungu yaani mwenye- enzi -mungu.
Mwenye-mmiliki wa
Enzi- ya kale au mwanzo
Mungu- muweza wa kila Jambo/ anayepaswa kuabudiwa
Hivyo unaposema Mwenyezimungu maana yake -wa mwanzo mwenye kupaswa kuabudiwa au wa mwanzo muweza wa kila Jambo.
Sasa turudi juu ya uwepo wake na kutokuwepo.
Hapa tuelewe kuwa wengi wanao support uwepo wa mungu ni watu wenye dini yaani waislamu,wakristo na wayahudi ndio maana mwanzo nikasema ni ngumu kutenganisha mungu na dini.
Kwa uzoefu wangu wengi wanaopinga uwepo wa mungu (Atheists) wanatumia hoja za kiakili na logic pamoja na ushahidi wa kisayansi kuthibitisha kuwa hakuna mungu na hapo ndipo tatizo limapoanzia, kivipi? ..kuwa makini point inayofuata.
Unapotaka kuthibitisha kuwa hakuna mungu kwa kutumia let say milango ya fahamu yaani macho, pua, masikio n.k hii tunasema ni sayansi kwa maana nyingine ni vipimo vya kupimia vitu vyenye asili ya maada (matters) na mungu sio maada Hivyo kutaka kumpima mungu kupitia vipimo vya kupimia maada ni kosa kwa maana wale Wanaosema mungu hayupo kwa sababu haonekani , hashikiki huwezi kumnusa hoja yao inakosa nguvu automatic kwani wametumia vipimo ambavyo sio sahihi kumpimia mungu yaani ni sawasawa na uchukue mizani ya kupimia uzito alafu unataka kujua kimo cha ndoo hutapata kimo utapata uzito lakini haimanishi hiyo ndoo haina kimo inayo na ukitaka Kupata kimo chake tumia tape measure na sio mizani.
Hoja Ni nyingi Sana ambazo Atheists wanazitumia na Mimi apo nimetoa hoja moja tu na nimeikosoa hoja hio ..mwenye hoja nyingine aweke hapo alafu tuchambue kila hoja
N.b msimamo wangu mungu yupo na linathibitika kiakili, kisayansi na kiimani..​
mimi naona sayansi yenyewe inadhibitisha Mungu yupo , tusinge ijua mifumo tata iliyopangiliwa madhubuti bila sayansi , Sayansi itakosa maana kama kilichowekwa na Mungu hakipo , ukitumia sayansi kumpnga Mungu ni sawasawa umetumia mkono wako kujipiga kofi
 
Sababu gani maalum?

Ukifuatilia hoja hiyo ya "sababu maalum za upendo mkuu", hata mimi ninaweza kukuambia wewe kuwa mimi ndiye Mungu mwenywe, ila siwezi kukufahamisha vizuri kwa sababu maalum za upendo mkuu.

Utanipingaje ikiwa ushaikubali hoja ya "sababu maalum za upendo mkuu" isiyo na maelezo kuwa inatosha?
umesema watu wanapata shida , wengne wanakufa kwan nini kimekuonyesha kufa ni tatizo , ebu ondoa matatzo yote then yafikirie maisha bila changamoto.
 
kumtofautisha Mungu na mtu kivp wakati nimeshasema huko juu sisi ni maumbile ya chini kabsa na frequence ya chini ya hyo nguvu kuu hyo nishati ipo kwenye mwendo , kuna maumbile mengne tu yapo hatuwezi kuyaona kwasababu yapo kwenye speed na frequence ya juu zaid
Hoja haizingumzii mumbile, hoja imezungumia sifa au uwezo

Ikiwa Mungu sio muweza wa yote, mjuzi wa yote wala mwenye upendo wote, utamtofautishaje na binadamu?
 
yote umemaanisha nn ? toka mwanzo sija zungumza Mungu kiupersonality zaid Kwa nini unamlocalize Mungu mahal fuln ? yani anaongoza kutokea eneo fulan kma mfalme fuln? hicho tunachoita mungu kipo kila mahali kwenye kila maumbile , maumbile yote ni nishati.
 
umesema watu wanapata shida , wengne wanakufa kwan nini kimekuonyesha kufa ni tatizo , ebu ondoa matatzo yote then yafikirie maisha bila changamoto.
Kwa nini nifikirie maisha bila matatizo wala changamoto?

Unaelewa maisha yasiyo na matatizo wala changamoto maana yake Mungu hahitaji kuwaadhibu watu kwa kufanya mabaya, na kwa kuwa Mungu anawaadhibu watu kwa kufanya mabaya, hapo umeshaonesha maisha yana matatizo tayari?

Unaelewa Mungu huyu mnayemsema yupo dhana ya kuwepo kwake haina logical consistency?
 
Si hivyo tu.

Leo nikikaa na kuangalia angani naona nyota ambazo hazipo, zimetoweka mamilioni ya miaka iliyopita, lakini mwanga wake nauona leo. Naweza kukuonesha ile pale nyota ipo, na wewe unaiona na kukubali kwamba ipo, kwa sababu unaiona. Lakini nyota ishalipuka na kutoweka mamilioni ya miaka iliyopita.

Je, hizo nyota zipo, kwa sababu nauona mwanga wake, au hazipo kwa sababu zimetoweka mamilioni ya mika iliyopita?

Kuna sehemu ya ulimwengu hatuijui na daima hatutakuja kuijua, kwa sababu ulimwengu unapanuka kwa kasi kubwa kuliko mwanga wa hiyo sehemu unavyosafiri na kuweza kutufikia.

Je, tunaposema "vyote" huko nako tunakuhesabu? Tunakujuaje?

Unaposema vyote unamaanisha nini? Na unajuaje hivyo ndivyo vyote?

Inawezekana hii dhana ya "vyote" nayo ni mauzauza ya kufikirika tu?

Vyote kwa wapi, lini, na msingi gani?

Vyote kwa wapi, lini, na msingi gani?

Kama siyo, utajuaje hapa umemaliza vyote?

Kama ndiyo, ikiwa hatujui vyote ni nini, tutasemaje huyu ni Mungu muumba vyote?
“Vyote” niliyoisema hapa ni ile inayoaminishwa na waumini…

Vyote ile ya tuvijuavyo, tusivyovijua na ambavyo hatutakuja kuvijua.

je, tunaweza hitimisha kuwa kwako wewe Bwana Kiranga dhana ya Mungu (ikimaanisha Muumba wa vyote- kama nilivyosema hapo juu) ni batili na kiumbe, nguvu, mtu au chochote kinachinasibishwa na dhana hiyo si halisi ila uzushi???
 
Kwa nini nifikirie maisha bila matatizo wala changamoto?

Unaelewa maisha yasiyo na matatizo wala changamoto maana yake Mungu hahitaji kuwaadhibu watu kwa kufanya mabaya, na kwa kuwa Mungu anawaadhibu watu kwa kufanya mabaya, hapo umeshaonesha maisha yana matatizo tayari?

Unaelewa Mungu huyu mnayemsema yupo dhana ya kuwepo kwake haina logical consistency?
nikupe mfano mwingne Mungu nikama kisu , kiuhalisia kisu ni kizuri kinamsaada mkubwa sna , ila kisu hicho hicho mtumiaji anaweza kitumia kuua mtu , tatzo sio kisu tatzo ni mtumiaji wa kisu ,. unapomlaumu Mungu kaleta ubaya ni sawasawa na kulaumu kisu kimeua unaacha kulaumu mtumiaji wa kisu kua kakitumia kwenye matumiz mabaya.
 
Mtoa mada haueleweki ushasema Mungu hayupo maana yake tayari una tafsiri yako kuhusu uyo Mungu alafu unataka wasioamini waje kuthibitisha kutokuwepo kwa uyo Mungu unaemjua wewe sasa hii maana yake nini? Watu wemekuambia uko juu leta iyo tafsiri ya Mungu unaesema hayupo ila ichambuliwe na wewe unawarushia mpira unataka wao ndo watoe tafsiri ya Mungu hivi unajua kweli unachokitaka? Umeianza hoja yako kwa kusema Mungu hayupo sasa leta tafsiri ya uyo Mungu unaesema hayupo ili achambuliwe. Kiranga na Scars Wanajaribu kukuelewesha hapo Mungu ni nini? Au ni nani? Wewe unataka wao ndo wamchambue Mungu wakati wewe mwenyewe ushasema hayupo, leta tafsiri ya uyo Mungu unaesema hayupo ichambuliwe mbona unafanya mjadala mfupi na rahisi uwe mrefu na mgumu
Daah nasikitika sana kuona mtu makini kama wewe humu ndani kutonielewa.

Uiseme “haueleweki” sema “mimi sijakuelewa” maana kuna watu wamenielewa na tunakwenda vizuri sana.

Mbona bwana Scars, Den Xiaping, Kiranga tunaelewana uzuri sana?

Wacha nijaribu kukuelewesha.
Hicho kichwa cha habari kinasema “MUNGU HAYUPO: Atheists njooni mthibitishe”

Hiyo “Mungu Hayupo” ei hoja yangu (wengi kama wewe hapo hawajaniewa) ni madai ya atheists…

Kisha hapo mbele nimewaalika waje wathibitishe…
Lakini kabla ya kupokea uthibitisho wao nimewaomba wanifafanulie maana ya dhana ya Mungu kwa mujibu wao wenyewe (hapa bwana kiranga alieleza kuwa wao sio dini, hawana msahafu hivyo kila mmoja atakuja na maana yake. Suala ambalo lina ‘make sense’).

Majibu nimepata toka kwa wadau kadhaa
Scars amesema Huyu Mungu asemwaye na ‘mainstream religions’ si halisi ila tafiti zinahitajika zaidi kumjua wa kweli

Den Xiapoing yeye kasema hafahamu

Kiranga kadai Mungu huyu wa ‘mainstream religions’ anakosa ‘logic consistency’ kwanini? Kaeleza…

Min - me Na wengine ambao sijawataja wamenijibu uzuri tu.

NB: Mada hizi hazitaki presha, kukariri wala mihemko. Sababu ktk kujadili bila shaka hoja zako msingi zinaweza kosolewa vikali. Mihemko ikizidi ndo matusi unakuta yanaanza.

Karibu Mkuu, Kama umenielewa mawazo yako ktk mjadala huu yatakuwa ya thamani sana🙏
 
“Vyote” niliyoisema hapa ni ile inayoaminishwa na waumini…

Vyote ile ya tuvijuavyo, tusivyovijua na ambavyo hatutakuja kuvijua.

je, tunaweza hitimisha kuwa kwako wewe Bwana Kiranga dhana ya Mungu (ikimaanisha Muumba wa vyote- kama nilivyosema hapo juu) ni batili na kiumbe, nguvu, mtu au chochote kinachinasibishwa na dhana hiyo si halisi ila uzushi???
Kama hatuwezi hata kujua "vyote" ni nini, dhana ya "muumba wa vyote" ni batili.

Yani unaruka kitu kimoja, kabla hujakielewa vizuri, unakwenda kujishaua kuwa unaelewa kilichokisababisha ni kipi.
 
Kama hatuwezi hata kujua "vyote" ni nini, dhana ya "muumba wa vyote" ni batili.

Yani unaruka kitu kimoja, kabla hujakielewa vizuri, unakwenda kujishaua kuwa unaelewa kilichokisababisha ni kipi.
Sijui wapi hujaelewa, umeuliza maana ya “vyote” nimekujibu vyote ni vyote vilivyokuwepo kabla yetu, vilivyo wakati wetu, vitakavyokuwa baada yetu.
Vyote tulivyovijua, tunavyovijua, tutakavyovijua, tusivyovijua, tusivyokua kuvijua…. Vilivyo, vilivyokuwa na vitakavyokuwa kote ulimwenguni ambapo ulimwengu kwa kasi yake haukutanuka, unakotanuka na utakapotanuka…

Umeelewa maana hiyo ya vyote?

Yaani wataka tujue “vyote” kila kimoja kilichopo ulimwenguni ndo tuhitimishe kuwa dhana ya Mungu (kwa mujibu wa Uislam na Uyahudi) ni batili?

Haya nauliza tena,
je tunaweza hitimisha kuwa kwako wewe Bwana Kiranga dhana ya Mungu (ikimaanisha Muumba wa vyote KAMA NILIVYOELEZA HAPO JUU) ni batili na kiumbe, nguvu, mtu au chochote kinachinasibishwa na dhana hiyo si halisi ila uzushi???
 
Back
Top Bottom