Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 11,622
- 20,570
Kuna stori kuwa Columbus alipokuwa anaondoka kisiwa fulani huko Amerika aliwaambia wenyeji wampe chakula cha safari. Wakagoma. Akasema mkigoma kesho nitafanya miujiza. Nitautia mwezi giza. Kweli kesho yake mwezi uliingiwa giza. Wenyeji wakamsujudu Columbus na kumpa chakula. Waliona miujiza mtu kuutia mwezi giza. Lakini Columbus alitumia sayansi. Alijua habari za kupatwa kwa mwezi na mzunguko wake.
Binadamu anaweza kurusha mzinga na ukaenda kutua sehemu anayotaka. Anaangalia umbali alipo adui, spidi ya mzinga, joto, mgandamizo wa hewa, spidi ya upepo nk. Anaingiza yote haya(Variables)kwenye formula na kupata angle anayopaswa kuweka mzinga wake. Na kweli mzinga unaenda kutua alipopanga.
Si Mungu naye anapotabiri mambo hutumia formula kama hiyo. Anapotabiri mfano kifo anaingiza mabilioni ya variables kumhusu mtu huyo kwenye formula. Alichokula, mawazo yake(Brain waves) maneno anayoongea, afya yake, watu wanaomzunguka, hali ya hewa. . . Yaani anaingiza kila kitu kinachomhusu mtu huyo kwenye formula kisha anapata jibu kuwa kesho Absalomu mwana wa Daudi atakufa kwa kunaswa kwenye mti. Hafanyi miujiza, anafanya hesabu. "Miujiza" inawezekana bila sayansi?
Binadamu anaweza kurusha mzinga na ukaenda kutua sehemu anayotaka. Anaangalia umbali alipo adui, spidi ya mzinga, joto, mgandamizo wa hewa, spidi ya upepo nk. Anaingiza yote haya(Variables)kwenye formula na kupata angle anayopaswa kuweka mzinga wake. Na kweli mzinga unaenda kutua alipopanga.
Si Mungu naye anapotabiri mambo hutumia formula kama hiyo. Anapotabiri mfano kifo anaingiza mabilioni ya variables kumhusu mtu huyo kwenye formula. Alichokula, mawazo yake(Brain waves) maneno anayoongea, afya yake, watu wanaomzunguka, hali ya hewa. . . Yaani anaingiza kila kitu kinachomhusu mtu huyo kwenye formula kisha anapata jibu kuwa kesho Absalomu mwana wa Daudi atakufa kwa kunaswa kwenye mti. Hafanyi miujiza, anafanya hesabu. "Miujiza" inawezekana bila sayansi?