MahinaVeterani
JF-Expert Member
- Aug 8, 2013
- 710
- 257
Mkuu Morning Glory, sikumbuki kama nilichangia kwenye uzi wako wa mwanzo ambao, kama sikosei, ulitoa kwenye Jukwaa la MMU.
Kwa kuwa ni hulka yetu kumtanguliza MUNGU hasa tunapokwama, hivyo, na mimi, usiku huu wa manane ninamtanguliza MUNGU kwenye ushauri wangu mfupi.
Kukosa ajira kwa Mumeo huenda ni Mpango wa MUNGU. Huenda MUNGU amekusudia makubwa katika Maisha yenu lakini sio kupitia ajira rasmi ya Mumeo ya Mshahara kwa kila mwisho wa Mwezi, Mkataba wa Kazi, kuripoti kazini kila kukicha, kuvaa Shati na Suruali - mkanda nje, kupokea Salary Slip kila tarehe 25 ya mwezi, kukimbizana na Mikopo ya Benki kwa Wafanyakazi, n.k., n.k.
Huenda MUNGU anawaepushia mabaya kwa kukosekana kwa ajira hiyo.
Jaribuni kuliangalia suala hili kwa mtazamo tofauti - mtazamo chanya. Cha msingi ni kuangalia fursa nyingi zilizopo na kuingia huko. Mwanzo siku zote ni mgumu, lakini uvumilivu na kumtumainia MUNGU ndiyo silaha. Hakuna haja ya kuanza parefu, anzieni chini - mdogomdogo. Jishusheni ili mpande. Hiyo PGD (haijalishi ni ya Masomo yepi) ni Mtaji kwa kuwa upana wa kuyaona na kuyapembua mambo pengine ni mkubwa kuliko wasio na kiwango hicho cha Elimu.
Kuna Mtu ninamfahamu. Alisoma Digrii ya Uchumi hapo UDSM na kuongezea Vyeti kadhaa baada ya hiyo Digrii. Aliacha yote, akaenda kusoma Kozi ya Mwaka mzima ya Kilimo kwenye Chuo kimoja cha Kilimo hapa Nchini. Akaanza kwa Bustani ndogo ya kukodi hapo Dar. Sasa hivi ingawa siyo Tajiri wa kusifiwa kwenye Vyombo vya Habari ana Mradi wa Shamba na Mifugo wa kutosha kabisa huko Arusha unaoifanya Familia yake iishi maisha ya neema na Watoto wasome Ulaya. Hii siyo fiksi - ni ukweli!
Sijui kama ninaeleweka. Hivyo ninaomba niishie hapa!
Ningeandika mengi!
Kwa kuwa ni hulka yetu kumtanguliza MUNGU hasa tunapokwama, hivyo, na mimi, usiku huu wa manane ninamtanguliza MUNGU kwenye ushauri wangu mfupi.
Kukosa ajira kwa Mumeo huenda ni Mpango wa MUNGU. Huenda MUNGU amekusudia makubwa katika Maisha yenu lakini sio kupitia ajira rasmi ya Mumeo ya Mshahara kwa kila mwisho wa Mwezi, Mkataba wa Kazi, kuripoti kazini kila kukicha, kuvaa Shati na Suruali - mkanda nje, kupokea Salary Slip kila tarehe 25 ya mwezi, kukimbizana na Mikopo ya Benki kwa Wafanyakazi, n.k., n.k.
Huenda MUNGU anawaepushia mabaya kwa kukosekana kwa ajira hiyo.
Jaribuni kuliangalia suala hili kwa mtazamo tofauti - mtazamo chanya. Cha msingi ni kuangalia fursa nyingi zilizopo na kuingia huko. Mwanzo siku zote ni mgumu, lakini uvumilivu na kumtumainia MUNGU ndiyo silaha. Hakuna haja ya kuanza parefu, anzieni chini - mdogomdogo. Jishusheni ili mpande. Hiyo PGD (haijalishi ni ya Masomo yepi) ni Mtaji kwa kuwa upana wa kuyaona na kuyapembua mambo pengine ni mkubwa kuliko wasio na kiwango hicho cha Elimu.
Kuna Mtu ninamfahamu. Alisoma Digrii ya Uchumi hapo UDSM na kuongezea Vyeti kadhaa baada ya hiyo Digrii. Aliacha yote, akaenda kusoma Kozi ya Mwaka mzima ya Kilimo kwenye Chuo kimoja cha Kilimo hapa Nchini. Akaanza kwa Bustani ndogo ya kukodi hapo Dar. Sasa hivi ingawa siyo Tajiri wa kusifiwa kwenye Vyombo vya Habari ana Mradi wa Shamba na Mifugo wa kutosha kabisa huko Arusha unaoifanya Familia yake iishi maisha ya neema na Watoto wasome Ulaya. Hii siyo fiksi - ni ukweli!
Sijui kama ninaeleweka. Hivyo ninaomba niishie hapa!
Ningeandika mengi!