Mume wa mtu huyu mbona haniachi jamani?

Mume wa mtu huyu mbona haniachi jamani?

mwambie akuoe,nijuavyo mm ukiristo hauna maandishi/neno/aya ya kuzuia wakristo wacoe mke zaidi ya mmoja.
 
Tena Biblia ndo kabisa ( mke ama mume wako ni yule aliyepiga Hodi na kuondoa Buki............... wengine wote wazini. Je mnaondika hapa ni wangapi hamkufanya kabla ya ndoa? je mliooolewa ni wangaoi waume zenu ndo waliondoa utando? je kwa wanaume milikuwa hamjaona utupu wa mwanamke yeyote kabla? et baada ya kuoa sasa mnatulia!!!!
mie nakushauri binti mweleza huyo jamaa kuwa unahitaji ndoa sasa!! full stop akikueleza kuwa namuacha mke wake hafai!!!! maana atakuacha kwa mwingien as well. mpe black and white. shida misaada unayondelea kupata!! na ushauri unaoomba!! KATA!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Wewe umeshakunywa gongo? sikuelewi unachoandika.
 
Amekuwa akinisaidia sana katika maendeleo yangu mume wa mtu huyu ndie mshauri wangu hata iweje yupo mbele yangu kunijali ananipenda
Jingine umesema Anakujazaga mapesa anakusaidia kwa hali na mali unaposema utaendelea kumtumikia hadi lini ilhali unapokea vyake ,ckuelewi ujue mbona usiseme mtatumikiana hadi lini!

Mimi nilazima nitakuwa na familia Yangu tutaishi maisha haya mpaka lini na tangu tujuane huu ni mwaka wa 6 najitahidi kumuacha .

Una uhakika gani kusema ni lazima nitakuwa na familia yangu!Hebu ona miaka 6 unapiga deiwaka kama hajajitokeza akafika bei wewe endelea kupiga kazi na jamaa.
 
Habari ndugu zangu,

Nashindwa kuelewa mpaka sasa nimetokea kupendwa na mume wa mtu tangu niingie kwenye mahusiano sijawahi kuwa na mahusiano na mwanaume ambaye yupo single,

Amekuwa akinisaidia sana katika maendeleo yangu mume wa mtu huyu ndie mshauri wangu hata iweje yupo mbele yangu kunijali ananipenda sana mara nyingne nawaza siwezi kufika naye mbali tayari yeye ameshakuwa na familia yake na Mimi nilazima nitakuwa na familia Yangu tutaishi maisha haya mpaka lini na tangu tujuane huu ni mwaka wa 6 najitahidi kumuacha lakini jamaa na yeye anapigana kutokuniacha mke wake mpaka leo hajui kama mume wake ana mchepuko nje, nishaurini nahitaji na Mimi kuwa na maisha yangu nimpata mume wangu nitamtumikia huyu jamaa mpaka lini? Nipeni hata njia mbadala matata ili niachane naye.

Mi naona umeshagundua hilo ni tatizo kwahiyo una uwezo wa kuamua kulitatua. Unaweza kuanza kubadilisha utegemezi wako juu yake. Ujione upo single ufanye mambo yako peke yako. Huenda pengine kwa kukusaidia kifedha umekua mtumwa wake. Socialize na marafiki wengine maana kwa kujumuika na wale wa siku zote utapata shida kubadili tabia. Pia waweza tafuta mabadiliko yoyote kielimu(anza kusoma course flani) au anza kutafuta ajira nyingine etc.
Change is good. It keeps you away from your habits.
 
Wala sitetei my dear ila najaribu kuonesha tu kuwa haya mambo sio simple sana sababu yashaleta madhara tayari sababu kuna watu wanawekeza mioyo,roho,figo ,mawazo,hisia na kila kitu ujue!!!!!

Mi naamini kqbisa huyo jamaa alikuwa anajua kuna siku ataambiwa tu kuwa bi dada anataka kuolewa so ni yeye kujipanga na kueleza hoja na kuzisimamia!!

Muite masai dada akupe kisa yake hapa!!!!

Mmmmmmmm yaani leo nimepata kitu kipya kabisa!
 
Last edited by a moderator:
Hatari sana! Ila hayo mapenzi ya Nyumba ndogo huwa ni mazito kuliko ya nyumba kubwa sijui kwa nini! ingetokea akakuoa atabadilika kabisaa
Yanakuwa tight sababu wengi wanakuwa ni kama asylum seekers!!!!!
 
mwambie akuoe,nijuavyo mm ukiristo hauna maandishi/neno/aya ya kuzuia wakristo wacoe mke zaidi ya mmoja.

"Ujuavyo wewe"! Bora umejenga hoja yako kwenye hilo! Pia hakuna mstari wowote unaosema wanaume waoe mke zaidi ya mmoja!
 
Unamfanyia vituko mtu uliyetuambia hapa hapa kuwa anakusaidia, anakushauri na mengine mengi mengi mengi!!!!!!!!!!!!!!!!!!Ama kweli fadhili mfadhili Mbuzi binadamu.......we acha tu. Back to the topic..... kama kweli unafikiri kuwa unataka kuwa huru uendelee na maisha yako fanya hivi. Mtoe out mtu wako, sehemu tulivu na siyo kwenye mafuriko ya Dar kama uko huko. Siku hiyo gharama zote kwako. Mle, mnywe na ikiwezekana mjirushe kwa roho zenu. Mwisho wa siku mweleze jinsi unavyompenda. Mkumbushe jinsi alivyokuwa msaada kwako kwa muda wote huo. Mkumbushe mlivyoanza mahusiano yenu, magumu na marahisi mliyoyapitia mpaka hapo mlipofika. Mwambie unavyojua kuwa anakupenda na mwambie kuna mambo huku nyuma ulimfanyia lkn hayakuwa ya kiungwana na in advance mwombe msamaha akusamehe. Then mwambie lengo mahsusi la ww kumtoa out ni kama ifuatavyo; Muite jina lake halisi na siyo lile jina ulilozoea kumuita. Kama ni Chacha kama jina langu basi muite..... hivi wanaume kama nyinyi bado mpo duniani!?!
 
Mmmmmmmm yaani leo nimepata kitu kipya kabisa!

Ts gud kama unajifunza! !!!!
Wengi huingia kwa sababu A au B na kudhani ni jambo rahisi ila watu wazima baadhi huwa wanamaanisha long term!!!!
 
Hata me naona anatafuta excuse ya kuendelea kuwa na huyo mwanaume, hakuna kitu kinaitwa kushindwa kumuacha mtu tena mtu mwenyewe mume wa mtu, usitudanganye bwana

halafu bidada naona hajielewi na umri una muenda atafte mume wa kuoa na inaonyesha hana mwanaume six years na mume wa mtu utakuwa bibi ucfikirie anavo kupa kila kitu ndo unapendwa kama angekuwa hvo angekuoa tafta wako ucje vuta blanketi kumekucha mana za mwizi arobaini
 
kama unaona huwezi mwacha vunja ndoa yake then uolewe na huyo jamaa maana ndo unataka ushauriwe hivyo
 
Habari ndugu zangu,

Nashindwa kuelewa mpaka sasa nimetokea kupendwa na mume wa mtu tangu niingie kwenye mahusiano sijawahi kuwa na mahusiano na mwanaume ambaye yupo single,

Amekuwa akinisaidia sana katika maendeleo yangu mume wa mtu huyu ndie mshauri wangu hata iweje yupo mbele yangu kunijali ananipenda sana mara nyingne nawaza siwezi kufika naye mbali tayari yeye ameshakuwa na familia yake na Mimi nilazima nitakuwa na familia Yangu tutaishi maisha haya mpaka lini na tangu tujuane huu ni mwaka wa 6 najitahidi kumuacha lakini jamaa na yeye anapigana kutokuniacha mke wake mpaka leo hajui kama mume wake ana mchepuko nje, nishaurini nahitaji na Mimi kuwa na maisha yangu nimpata mume wangu nitamtumikia huyu jamaa mpaka lini? Nipeni hata njia mbadala matata ili niachane naye.
Nowadays mume wa mtu anaweza kuwa bora kuliko huyo single, uzuri wanawake wengi wanaelewa tabia za wanaume trust me hakuna mwanaume ambaye hana mchepuko suala ni kujua, wewe zaa naye kabisa ili akujengee nyumba na akununuliye na gari.
Vile vile jaribu kucheki furaha yako unapata wapi kama anakupa furaha go ahead, maisha hayana formula wewe unafikiri kumpata mume ni jambo jepesi kuna wanawake kutwa kuwinda waume za watu lakini hawawapati you are luck.
Tatu mume wa mtu hakuzuii kumpata huyo single mbona wanawake wengi wanaolewa wanakuwa wameshatembea na waume za watu kibao, as longer as wanamke hujamkuta bikira ujue she has a long story to tell and never ask.
Hiyo ni fursa kamata na uitumie.
 
We tulia tuu kama umeshindwa kumuacha tindikali itakuusu tutaona kama hutamuacha!!

si bora tindkal! Huyu dawa ake achanwe na viwembe hlo liuso lake! Nobody is perfect,lakin bi dada umezidi miaka 6 yote jamaa anakuchmba huko down!khaa muonee mke mwenzio huruma umwachie mme wake! Karma is ...! #okbye
 
weka namba zako hapa uone kama kweli umtaki zikiingia sms usifute azione cm pokea mbele yake,usituzingue fanya hivyo kama kweli humtaki
 
Hatari sana! Ila hayo mapenzi ya Nyumba ndogo huwa ni mazito kuliko ya nyumba kubwa sijui kwa nini! ingetokea akakuoa atabadilika kabisaa
angeniua yule mwanaume, sijawahi kuona mwanaume wa ajabu kama yule. Alifanya nini sijui kwa tigo akawa anasikia simu zangu zote.
Anafanya fujo kwa rafiki zangu hapo baada ya kutaka kuachana nae. Wala sitaki kumkumbuka tena.
Kibaya nlikuja kujua kama kaoa baada ya kama 7 months coz mkewe alikuwa mbali nae na mie naishi dar, alivyorudi ndo akanambia nlilia sana na kuumia but ndo hivyo tena nlirudiana nae hapo ndo nikawa nyumba ndogo rasmi ila yalinishinda coz nina wivu na napenda ku-chat na kuongea nae kila muda nikihitaji kitu ambacho hakikuwezekana. Nikaamua tuachane yeye hataki, hapo ndo vitisho na vurugu viliniandama.
Nashkuru kwa kweli ni zaid ya 3 yrs now tangu tumeachana na sijawahi kumuona tena hadi leo
 
Najua siyo vyema kula tonge la mtu nimelijua hilo ndio maana nilijitahid kumuacha siyo vyema kabisa Lakin mwanaume ndio mgumu kuniacha nafanya vituko Vingi ili nimuuzi anichoke aondoke kwangu ndio nimeshindwa nikaja kwenu mnishauri

Nenda kamsemee kwa mkewe kama upo siriaz
 
Hapo utakuta una na mshkaji pembeni..mademu wengine nyie dah
 
Back
Top Bottom