Mume wa mtu huyu mbona haniachi jamani?

Mume wa mtu huyu mbona haniachi jamani?

Aina ya wanaume unaokuwa nao hutegemea na jinsi we ulivyo.
Study waume za watu=) Ni wanaume ambao tayari wana experience na maisha/mapenzi. Kwa hiyo kimapenzi hujua vizuri namna ya kuwa na wewe. Kimaisha ni kiongozi mzoefu na kama we ni mchepuko basi ameshajijenga kiasi cha kuweza kutunza mchepuko. Ni mwanaume ambaye hahitaji kitu toka kwako kwa sababu akipitia magumu mkewe ndo msaidizi wake, mkewe ndiye anayekuwa naye. Maisha yakiwa stable ndo huja kutumia na wewe.
What does this make u then? Inamaana mostly wewe ni mpokeaji. Na kama mahusiano yako yamekuwa ni ya namna hii(kama ulivyosema) ina maana mchango wako kwenye mahusiano ni mdogo ama hakuna(RECEIVER).

Ukija kwa mwanaume single, demand zake ni vyingi tofauti na huyo aliyeoa. Huyu hata mawasiliano huhitaji mda mwingi muwasiliane kuliko yule aliyeoa. Hata kama ni kiongozi mzuri kwenye mahusiano bado experience ya ups and downs anazijua mume wa mtu. Hapa itakucost kushiriki kujenga mahusiano, kujenga uchumi pamoja, mipango wa maisha. Kiukweli kama umeshazoea raha za kwa waume za watu(ambazo by the way nusu ni nguvu za wanawake wenzio ndo zimetumika kumjenga alivyo) mahusiano na a single man ni changamoto hivyo inabidi uwe umedhamiria kweli.

Ujue ukiwa na mume/mke wa mtu ni kama parasite(mbu, minyoo na mimea fulani inayojishikiza kwa mingine). Wenzi wao wanajitahidi kulisha na kufight nao kimaisha kisha wewe unajifaidia matunda ya kazi zao (Naturally you give nothing to them since sex does not count as something to offer). Tabia hii sasa kiukweli huendana na laana fulani since kula jasho la mtu ni kitu ambacho hakikubaliki(kama unamjua Mungu. Hata ushauri anaokushauri alistahili akili hiyo na muda huo akampe faraja mkewe kwa magumu ya maisha). Kuna msemo usemao, "He who LIVES by the sword DIES by the sword".

USHAURI: Jenga tabia ya kujitegemea...taka vitu vyako. Own ur life. Kama kwenu ulidekezwa jua sasa umekua na wewe ndo unatakiwa ujitegemee financially, socially, career-wise and emotional-wise. Ukishakuwa na independent characters utaona tu single men wanakutafuta since wanakuona ni mwanamke ambaye mwanaume anaweza kujenga maisha side by side. Ukiwa unatabia tegemezi ndo utatafutwa na hao wataka michepuko since hawahitaji more than sex from you(And basically any woman can provide that so ur not that important if someone wants you for that)
 
Miaka 6 yaani nyie tayar mna ndoa yenu, unakula vya mwenzio kama vya kwako, mwenzio anakonda na dagaa tu, wew unakula kuku, ngoja na mumeo sasa
 
Bibie utakuja kushtuka too late. Miaka 6 yote hiyo, yeye yupo na mkewe wakati wewe upo nae huyo mume wa mtu.
Za wenzio kweli changanya na zako. Jiulize angekuwa anakupenda kama usemayo, kwanini asingekuhalalisha mpaka leo hii? Miaka yote hiyo???
Tafuta wako mjenge wote maisha.
 
Ndugu yangu unatenda dhambi, achana naye huyo jamaa. Usitegemee atamuacha mke wake. Karma is a b.itch! Itakurudia tu maradufu. Unanikumbusha mke wa mtu mmoja alikuwa kila akija kupewa uroda anamponda mume wake kuwa hamjali ingawa jamaa was doing so much for her materially and emotionally. Ilifika point nikamwambia if you wanna come to me to *** please stop talking about your hubby coz it is a turn-off. Mkiamua kula bata mle bata lakini msiwaseme waume zenu ili kuhalalisha uzinzi wenu.
 
naona komaa nae tu ili uwe mke mdogo maana najua hata ukolewa na mwingine bado utachepuka tu na huyo pedeshee
 
Ni ajabu sana mtu anafanya tendo akiwa na akili timamu anagundua kuwa ni kosa baada ya miaka sita. We sema umri umeenda sasa umegundua kuendelea kuendekeza tamaa zako za kuhongwa na mume wa mtu sasa basi. Laana yake ni kuwa ukitoka kwa huyo mume wa mtu utakutana na maplayer watakuvalisha pete na kukutosa hadi unafikisha miaka 40. Hivi unafikiri huyo mke halali hamuombi Mungu amlaani mwizi wa mumewe. Hebu fikiria maombi ya miaka sita laana yake itakuwaje?
 
Habar ndugu zangu, Nashindwa kuelewa mpk sasa nimetokea kupendwa na mume wa mtu tangu niingie kwenye mahusiano cjawahi kuwa na mahusiano na mwanaume ambaye yupo single, amekuwa akinisaidia sana katka maendelea yangu mume wa mtu huyu ndie mshaur wangu hata iweje yupo mbele yangu kunijali ananipenda sana mara nyingne nawaza siwez kufika naye mbali tayar yy ameshakuwa na familia yake na Mimi nilazima nitakuwa na familia Yang tutaishi maisha haya mpk lini na tangu tujuane huu ni mwaka wa 6 najitahidi kumuacha lakini jamaa na yeye anapigana kutokuniacha mke wake mpk leo hajui kama mume wake ana mchepuko nje, nishaurini nahitaji na Mimi kuwa na maisha yangu nimpata mume wangu nitamtumikia huyu jamaa mpk lini? Nipeni hata njia mbadala matata ili niachane naye

Dunia kweli inabadilika na vijana ujasiri unazidi kutujaa, yani unammiliki mume wa mtu kwa miaka 6. Unafurahia huduma tuu unazopata nawe bila aibu unjikubali kwamba wewe ni MCHEPUKO. Haya jiandae kutafuta njia kuu yako nawe uanze kujua machungu ya kuliwa mumeo na kutekwa kabisa hata miezi sita bila kuonekana nyumbani. Muosha huoshwa.
Usijifariji kwamba mkewe hajui kitu, hilo unajidanganya. Kuna wanawake wengine wanajitambua kimya tuu wala hawana papara ila ipo siku utamjua vizuri anga zake zipoje.

ALL THE BEST IN THIS FU...KN WORLD.
 
Haya bibie tumekuelewa njia yako ni nzuri kweli ya kutafuta mchumba wataku PM na utaachana na huyo mume wa mtu.
 
Kaa hivyo hivyo usiolewe haustaili na ukiolewa utatendwa mara millioni, nahamu ukamatwe na huyo mke as za mwizi arobaini then akufundishe adabu.

Na pia ulimwengu ukufundishe adabu tabia mbaya sana halafu unakuja kuomba ushauri. Tamaa umechuma umechoka haya na umesema hujawahi tembea na single man. Mfyuuuuuuu
 
kikamatishe kwa mkewe amgundue mwizi wake kila kitu kiwe wazi hapo mahusiano yataisha
 
Najua siyo vyema kula tonge la mtu nimelijua hilo ndio maana nilijitahid kumuacha siyo vyema kabisa Lakin mwanaume ndio mgumu kuniacha nafanya vituko Vingi ili nimuuzi anichoke aondoke kwangu ndio nimeshindwa nikaja kwenu mnishauri

0713 mhhh!
 
UKIWA umwambia kwa upole hawez kukuelewa,kwakuwa atajua utani wa kimahaba,kwahiyo nakushauri uwemkali na kuwa mbali naye
 
Haya bibie tumekuelewa njia yako ni nzuri kweli ya kutafuta mchumba wataku PM na utaachana na huyo mume wa mtu.


Huwezi ku mpm mchepuko mkuu. Huyu hafai, labda abadilishe ID
 
Usimwache maana umekula hela yake na ukateka mali zake. Iweje baada ya kushiba unataka kumdharau?
 
Back
Top Bottom