saidoo25
JF-Expert Member
- Jul 4, 2022
- 602
- 1,407
Wiki hii tumeshudia bungeni wabunge na mawaziri wakiringishiana viwango vya elimu wengine wakitamba na PHD zao kwamba ni za darasani sio za kupewa na wengine wakiambiwa hawana elimu ni waganga wa kienyeji.
Ni muhimu Spika wa Bunge kuruhusu uhakiki wa vyeti vya elimu kwa wabunge ili kujua ukweli wa elimu ambazo zimekuwa zikitajwa bungeni kama kinga ya kutisha wengine na watanzania wajue ukweli kuhusu wawakilishi wao.
Uhakiki huo ukague cheti cha Darasa la 7, Kidato cha 4, Kidato cha 6, Astashahada, Stashahada, Shahada, Shahada za uzamili, Shahada za Uzamivu nk.
Pia TCU ihakiki vyeti vya waliodaiwa kusoma nje ya nchi na kupata ukweli kuhusu elimu zao na uhalali wao.
Ni muhimu Spika wa Bunge kuruhusu uhakiki wa vyeti vya elimu kwa wabunge ili kujua ukweli wa elimu ambazo zimekuwa zikitajwa bungeni kama kinga ya kutisha wengine na watanzania wajue ukweli kuhusu wawakilishi wao.
Uhakiki huo ukague cheti cha Darasa la 7, Kidato cha 4, Kidato cha 6, Astashahada, Stashahada, Shahada, Shahada za uzamili, Shahada za Uzamivu nk.
Pia TCU ihakiki vyeti vya waliodaiwa kusoma nje ya nchi na kupata ukweli kuhusu elimu zao na uhalali wao.