Mtwara kimenuka: Mabomu ya machozi yarindima!

Mtwara kimenuka: Mabomu ya machozi yarindima!

Hali mijini hapa ni tete! Mabomu yanarindima mjini hapa kuwatawanya wananchi wanaojiandaa na mkutano mkubwa unaotarajiwa kufanyika mjini hapa kuhusu suala zima la gesi.

Chanzo cha mabomu hayo kupingwa ni baada ya umeme kukatika/kukatwa eneo panapotarajiwa kufanyika mkutano huo uwanja wa mashujaa mjini hapa na baada ya kuona hivyo wananchi wakaamua kuandamana kuelekea Tanesco kujua chanzo cha tatizo hilo la umeme na hali hiyo kupelekea polisi kuanza kuvurumisha mabomu ya machozi.

Ifahamike kwamba kumekuwa na mvua kubwa mjini hapa toka usiku wa leo ambayo inaweza ikawa chanzo cha kukatika kwa umeme huo (huu ni mtazamo wangu) ingawa inaweza ikawa hujuma pia.

Eneo nilipo umeme upo hali hii ya sintofahamu imepelekea huduma muhimu za kijamii kama maduka na soko kufungwa.

Acha waonje kipigo kidogo, walitakiwa kutafakari kwanza kuhusu hlo suala la mvua.
 
Yanayotokea Mtwara na sehemu nyingine kama Nyamongo kwenye madini ni matokeo ya kukata tamaa kwa wananchi dhidi ya serikali. Wananchi hawana matumaini tena na uongozi. Watz wengi hasa vijana walikuwa na matumaini makubwa sana na Kikwete alipochukua madaraka mwaka 2005 lakini baada ya kuona hakuna mabadiliko katika maisha yao kwa miaka 5 watu wamekosa matumaini. Kwa hiyo sasa kila mtu anaona ni bora ang'ang'anie rasilimali iliyo karibu nae. Sitoshangaa vuguvugu likianza kule kanda ya Ziwa kwenye madini!! hayo ni matokeo ya wananchi kukosa imani na viongozi wao wa juu!!

kuna sredi nimechangia na kuandika hivi...

kama watanywea ktk hili watakua wamekosa the best opportunity ya kuingia katika historia ya nchi hii kama mapioneers wa kutetea rasrimali za nchi zinufaishe wananchi na sio watawala. na kwa msimamo walioonyesha, ninahakika ndugu zangu wa kanda ya ziwa kwenye madini kemkem kuna kitu wamegundua na watakifanyia kazi. just wait and see! its a matter of time! just a matter of time!

naona tunawaza kitu kimoja mkuu!!
 
kwahiyo unataka gas ianze
kuchimbwa na kusafirishwa kwa hiyo mikataba ya siri na ya kifisadi,huku
wenzetu wa Mtwara wakiendelea kuishi maisha ya KIMASIKINI?Shame on
you!

BBJ, kwani wakiiona hiyo mikataba ndio watawekewa mihela mfukoni? wawajibike sio kukomalia rasilimali ibaki upande mmoja wa nchi ambayo inaweza kunufaisha taifa! Shame on you too!
 
Last edited by a moderator:
Dhambi ya ubaguzi ni sawa na kula nyama ya mtu. Ukishaianza huwezi kuiacha. Itakutafuna milele. Natamani iwapate ili iwe funzo kwa watu/regions zenye vision kama hii.
Swala hili si ubaguzi ila CCM ndiyo wanalitengeneza ili ionekane kama ni ubaguzi...
 
Kwa Habari za uhakika miongoni wawlioonja shubiri ya mabomu ya machozi ni Naibu katibu mkuu CUF Julius Mtatiro.Hivi sasa mabomu yametulia na mkutano unaendelea na Mtatiro yuko jukwaani akihutubiaView attachment 80024

... Asante sana mkuu kwa kutujuza kwa picha' je anasemaje huyu mwanandoa na ccm
 
Mdau katika hili hakuna dhambi yoyote itakayomkamata mtu

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Wakishaifanya dhambi hii ya ubaguzi haitaishia hapo, baadaye wataanza kusema mimi ni Muislam na yule ni Mkristo. Wataanza tena kubaguana kwa misingi ya kabila na rangi. Hii dhambi haitawaacha salama kamwe. Historia ni shahidi mzuri wa hili.
 
BBJ, kwani wakiiona hiyo mikataba ndio watawekewa mihela mfukoni? wawajibike sio kukomalia rasilimali ibaki upande mmoja wa nchi ambayo inaweza kunufaisha taifa! Shame on you too!

Issue siyo gesi ibaki mtwara, ila wananufaikaje na gesi hiyo siyo watu wawe wanachota gesi na kuwaacha na matatizo yao nyie kama mmeshindwa kupigania pesa zenu zilizo welwa huko uswiss na kwingineko ni nyie wao wameamua kukaba mapema...hizi unajua mtwara na lindi kuna watu wana miaka 20 hajawahi kuzaa kiatu siyo kwamba hapendi ni kwasababu hana uwezo huo sasa leo wamebahatika tugesi wawalegezee...
 
TANZANIA KUMEKUCHA, watu wa Mtwara waungwe mkono na mikoa yote hasa sehemu walizodhulumiwa madini kama TANZANITE Manyara, Mara - Buhemba na North Mara Gold Barrick, Mwanza bulyanhulu, kahama, geita na Mwadui.

Mbaya zaidi North Mara wanapigwa risasi, wanatiririsha maji machafu kwenye mito.

Mererani Wana apolo na watanzania walinyang'anywa Vitalu vyenye madini wakapewa makaburu

Sasa tuliona Madaktari walikosa uungwaji mkono na wananchi, Hatimae Dokta Ulimboka akatekwa, akateswa, akasulubiwa.... Mashuka, vifaa tiba na dawa hospitali hakuna

Waalimu nao wakatishwa wakaogopwa, angalia sasa matokeo ya secondari na shule za msingi.

wenye hasara ni wananchi, maana hao mafisadi wanatibiwa nje, watoto wao wanasoma nje.

THIS IS APATHEID HALAFU NI MBAYA KULIKO ILE APATHEID YA MAKABURU SOUTH BOTHA.

kwa sasa wananchi wa mikoa yote tuungane na Wanamtwara, ili hawa watawala wakose upenyo na hata ikiwezekana Maandamano yakomae yatapakae nchi nzima kama Misri, Libya...

We just need coordinator behind scenes ili kuunganisha nguvu, just use mobile phones, FB and social media to mobilize people.

Hapa ndo mwanzo na safari moja huanzisha nyingine.

Maandamano yakipamba moto nchi nzima hakya nani wanajeshi na polisi wataunga wananchi mkono.
 
Nasikia kule agha kan kimeshanuka tujulisheni mlioko pande hizo ili mkutano unoge.
 
Swala hili si ubaguzi ila CCM ndiyo wanalitengeneza ili ionekane kama ni ubaguzi...
Mkuu mimi siiungi mkono approach yao ila nataka madai yao ya msingi yafanyiwe kazi na serikali. Haya ni matokeo ya serikali ya CCM kuwa kama kenge ambaye huwa hasikii hadi umpige atokwe na damu maskioni.
 
Back
Top Bottom