mkuu unamaanisha man..ba..katutoka?
ndivyo nilivyouliuliza je? We umejibu au umeuliza?
mkuu unamaanisha man..ba..katutoka?
Nafikiri wote tumeuliza ila katika namna tofauti.ndivyo nilivyouliuliza je? We umejibu au umeuliza?
Huyu ni punda au twiga au ni PUTWI:llama:Sema Kiongozi nani alitarajiwa kuhutubia Mkutano huo?
Hakuna haja ya kuwapiga wenye nchi mabomu! Mara zote nasema suala la gas na wanamtwara litamalizwa na serikali na wanamtwara wenyewe endapo tu serikali ikikumbuka kuwa kuna kitu kiitwacho meza ya mazungumzo. Hatutegemei kusikia siasa au mabomu tena!!
We Mnyisanzu mjinga embu fikiria jinsi wananchi wanaozunguka mbuga za wanyama,na wanavyo athirika na Kuaribiwa,mazao na mara zingine kujeruhiwa, hata Kupoteza maisha!!!!Lakini akiingia hata Mbugani kuwinda Digidigi, akikamatwa,adhabu yake ni kuamrishwa kula Nyama mbichi,na hata kupigwa risasi! Ajabu Waarabu na Mafisadi wanawawinda wanyama kuwaua,na kuwasafirisha nje ya nchi wakiwa hai.!!!!!na hawafanywi kitu.sasa wanakusini wamegundua hilo ndio maana wanasema GESI KWANZA UHAI BAADAE.,,,lazima wanufaike wao kwanza,na sio Mafisadi Wa Ccm.,,,,,,Upo hadi hapo?Rasilimali za taifa ni kwa ajili ya manufaa ya taifa zima. Kusema GESI HAITOKI MTWARA ni ubinafsi uliopitiliza. Hakuna justification yoyote inayoweza kuhalalisha hilo.
hali mijini hapa ni tete! Mabomu yanarindima mjini hapa kuwatawanya wananchi wanaojiandaa na mkutano mkubwa unaotarajiwa kufanyika mjini hapa kuhusu suala zima la gesi.
Chanzo cha mabomu hayo kupingwa ni baada ya umeme kukatika/kukatwa eneo panapotarajiwa kufanyika mkutano huo uwanja wa mashujaa mjini hapa na baada ya kuona hivyo wananchi wakaamua kuandamana kuelekea tanesco kujua chanzo cha tatizo hilo la umeme na hali hiyo kupelekea polisi kuanza kuvurumisha mabomu ya machozi.
Ifahamike kwamba kumekuwa na mvua kubwa mjini hapa toka usiku wa leo ambayo inaweza ikawa chanzo cha kukatika kwa umeme huo (huu ni mtazamo wangu) ingawa inaweza ikawa hujuma pia.
Eneo nilipo umeme upo hali hii ya sintofahamu imepelekea huduma muhimu za kijamii kama maduka na soko kufungwa.
updates:
wakuu nimetoka kwenye mkutano umefanyika hapo mashiujaa kiukweli sikuweza kuendelea kuwaletea live kutokana na hali ya mvua pale uwanjani. Kifupi mkkutano umehutubiwa na wazungumzaji kadhaa wakiwepo wasanii na wabunge, wasanii walikuwa ni afande sele na kala pina kwa upande wa bunge nimagdalena sakaya, sulemani bungala (bwe.ge) na barwan, wazuinguzaji wengime walikuwa ni katani na mtatiro
wote kwa hakika wamezungumza mengi sana na wote wameungana na wanamtwara katika kuhakikisha rasilimaliya gesi inawanuifaisha watu wa mtwara nakusini kwa ujmla kwa upande wa wasanii hakika afande sele amejitahidi sana kuongea kwa kujenga hoja. Pamoja na kuwa nahali ya mvua wananchi hawakuondoka pale uwanjani kwa kweli serikali isipuuze haya madai ya watu wa mtwara kwa mfano kwa jinsi inavyoonekana vijana wako tayari kwa lolote serikalli iache kiburi. Katika mkutano huo kumekusanywa saini za watu 26,000 na kuwatuma wabunge kupeleka bungeni madai yao na munge wa lindi mjini ameeleza mara baada ya mkutano huo wa bunge kma madi ya wanantwara na kusini yote watakutana lindi kwa maandamano makubwa yatakayo fanyika tarehe 23 februari mwaka huu hadi kieleweke
lakini pia kulikuwa na jambo la kusikisha, kumetokea ajari pale njia panda ya kuelekea eapot ya mtwara gari lililokuwa linatokea tandahimba likiwa na wananchi limepata ajali na watu watatu kuumia nakupelekwa hosptali ya mkoa ligula na mmoja inaelezwa hali yake sinzuri anatakiwa kupelekwa muhimbili kwa matibabu zaidi, jambo ambalo lilimfanya bwana katani kuumba umati mkubwa uliohudhuria kutoa mchango kuwezesha safari hiyo na wananchi kuitikia jambo hilo ni hayo tu wakuu. Picha zitafuata punde.
Huyu ni punda au twiga au ni PUTWI
Issue siyo gesi ibaki
mtwara, ila wananufaikaje na gesi hiyo siyo watu wawe wanachota gesi na
kuwaacha na matatizo yao nyie kama mmeshindwa kupigania pesa zenu zilizo
welwa huko uswiss na kwingineko ni nyie wao wameamua kukaba
mapema...hizi unajua mtwara na lindi kuna watu wana miaka 20 hajawahi
kuzaa kiatu siyo kwamba hapendi ni kwasababu hana uwezo huo sasa leo
wamebahatika tugesi wawalegezee...
tozi yupo njian kuelekea ufaransa, nasikia kuna show ya koffi olomide kule paris, anaiwahi na my wife wake....
ni kwerli kabisa mkuu jamaa wakibanwa hutafuta sababu na hoja dhaifu katika kupindisha ukweli lakini bahati mbaya safari hii wamekutana na ngangari.wataisoma tu namba.gesi kwanza ukanda,ukabila,udini,uamsho etc baadae!!!!!!!!!!!!!.Swala hili si ubaguzi ila CCM ndiyo wanalitengeneza ili ionekane kama ni ubaguzi...
kuna sredi nimechangia na kuandika hivi...
kama watanywea ktk hili watakua wamekosa the best opportunity ya kuingia katika historia ya nchi hii kama mapioneers wa kutetea rasrimali za nchi zinufaishe wananchi na sio watawala. na kwa msimamo walioonyesha, ninahakika ndugu zangu wa kanda ya ziwa kwenye madini kemkem kuna kitu wamegundua na watakifanyia kazi. just wait and see! its a matter of time! just a matter of time!
naona tunawaza kitu kimoja mkuu!!
Yaani Nchi hii ina viongozi Mburula sana,gesi igunduliwe Mtwara then ipelekwe bagamoyo!shwain
TANZANIA KUMEKUCHA, watu
wa Mtwara waungwe mkono na mikoa yote hasa sehemu walizodhulumiwa madini
kama TANZANITE Manyara, Mara - Buhemba na North Mara Gold Barrick,
Mwanza bulyanhulu, kahama, geita na Mwadui.
Mbaya zaidi North Mara wanapigwa risasi, wanatiririsha maji machafu
kwenye mito.
Mererani Wana apolo na watanzania walinyang'anywa Vitalu vyenye madini
wakapewa makaburu
Sasa tuliona Madaktari walikosa uungwaji mkono na wananchi, Hatimae
Dokta Ulimboka akatekwa, akateswa, akasulubiwa.... Mashuka, vifaa tiba
na dawa hospitali hakuna
Waalimu nao wakatishwa wakaogopwa, angalia sasa matokeo ya secondari na
shule za msingi.
wenye hasara ni wananchi, maana hao mafisadi wanatibiwa nje, watoto wao
wanasoma nje.
THIS IS APATHEID HALAFU NI MBAYA KULIKO ILE APATHEID YA MAKABURU SOUTH
BOTHA.
kwa sasa wananchi wa mikoa yote tuungane na Wanamtwara, ili hawa
watawala wakose upenyo na hata ikiwezekana Maandamano yakomae yatapakae
nchi nzima kama Misri, Libya...
We just need coordinator behind scenes ili kuunganisha nguvu, just use
mobile phones, FB and social media to mobilize people.
Hapa ndo mwanzo na safari moja huanzisha nyingine.
Maandamano yakipamba moto nchi nzima hakya nani wanajeshi na polisi
wataunga wananchi mkono.
.......... do you really expect to rule Tanzanians through coercion, When there is no hope, and then expect that they will sit quiet in peace? .......... Unless these people are fools. ...... Tanzanians would be fools, ******, if they continued to accept to be oppressed by minority in their own country....