Mtwara kimenuka: Mabomu ya machozi yarindima!

Mtwara kimenuka: Mabomu ya machozi yarindima!

mapambano ndo yameanza, viongozi mnaokazana kuuza rasilimali zetu jitayalisheni kuturejeshea, hatutalala mpaka gesi ibaki mtwara, kila kitu dar es salaam kwahiyo tanzania ni dsm peke yake. Alutaaaaaa..........
 
Hawajawahi kufaidika
kivipi? unaweza kuniambia faida za bandari kwa watu wa dar?...Hivi kwa
mfano viwanda kama vingefunguliwa pale Mtwara huoni wananchi wangefaida
lakini unapoitoa wananchi unawanyia furusa na kama unawanyiama kufaidia
moja kwamoja basi uwaambie kwenye mapato ya gesi 7% ya pato lote
litokanalo na gesi litarudi kwenye mkoa na litaendelea kugawanywa mpaka
kufika kwenye kata/wilaya inakopatikana gesi..hivyo hivyo kwa mikoa kama
shy,mwanza,mara,Arusha,Dar..siyo wahuni wanawaachia machimo unazidi
kuneemesha akaunti za kina Riz1,lowasa na wahuni wengine...

Crashwise, Huo utaratibu wa kugawana mapato na kuweka mfukoni ni wa nchi gani? hapa kwetu haupo! Ni sera za Lipumbaf sijaona mimi!
 
Last edited by a moderator:
chadema wanahusika!!!!!!!!
chadema wanahusika kivipi, wakati wabunge wengi mkoani mtwara ni wa ccm na asilimia kubwa ya wakazi wa mtwara wako ccm. Hapo sijakuelewa. Kwa mawazo yangu wabunge wa ccm hawawezi kufuata sera za chama kingine badala ya kunadi sera za ccm.
 
Hii ni safi kabisa, manake hiyo gas ikifika hapa dar mafisadi washaingia mikataba yao na washajiwekea 10% itauzwa bei ghali mara mbili ya ilivyo sasa,hongereni watanzania kwa kujanjaruka kwanini tuwatajirishe watu wachache kwa rasilimali zetu .walio i iba zinatosha sasa basi lolote na liwe ,vyovyote vile kwa gharama yoyote
 
viongozi pangeni sera nzuri za kusimamia rasilimali za nchi zilizopo kwanza kabla ya kurukia nyingine.Kaeni chini mujiulize wanyama wanauwawa serengeti usiku na mchana hakuna hatua zozote za maana zinachukuliwa,faru wamepotea sasa na tembo nao wako mbioni kupotea juzi lori lapembe zimekamatwa huko arusha wenyewe wanajulikana, hivi mnataka sisi wananchi tuwaeleweje nyie viongozi wetu ,kesho kutwa tusipo waunga mkono mtatulaumu kwa mambo yanavyokwenda sasa hivi .Angalieni wenzetu wanatumia weakness zetu kutumaliza mnajikaanga kwa mafuta yenu wenyewe
 
Crashwise, Huo utaratibu wa kugawana mapato na kuweka mfukoni ni wa nchi gani? hapa kwetu haupo! Ni sera za Lipumbaf sijaona mimi!
Wapi nimesema wagawiwe pesa waweke mfukoni?..acheni ukweli ubaki kuwa ukweli maliasli zetu lazima zinufaishe sehemu husika kwanza siyo watu wanachota madini na wanyama kisha mnapewa vyandarua watanzania tuamke tusimamie rasilimali zetu tuache upumbavu wa kuhofia ukihoji utaitwa mdini sijui mkabila....
 
chadema wanahusika kivipi, wakati wabunge wengi mkoani mtwara ni wa ccm na asilimia kubwa ya wakazi wa mtwara wako ccm. Hapo sijakuelewa. Kwa mawazo yangu wabunge wa ccm hawawezi kufuata sera za chama kingine badala ya kunadi sera za ccm.
kama unakumbuka M4C ilipo ingia kule ilibidi mawaziri ambao ni wabunge wa huko warudi kwenye majimbo yao haikuwa bure.. watu walikuwa wanapewa masomo ya bure na inavyoelekea wana mtwara ni wanafunzi wazuri maana wameyashika mafundisho vyema...bado kanda zingine kwenye upande wa kulinda mali...
 
Bado wanamtwara watapigwa changa la macho tu maana Che nkapa ameshauri mazungumzo, hapo ndo watapooza kidogo na hela tayari zimeliwa zipo Swiss
 
Kwan ukwel haujifich gesi yetu ila imeshauzwa kipindi cha mkwele inamaan mmesahau?
 
Back
Top Bottom