Habari hii ni ya kweli kwa mujibu wa mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Msimbati. Pengine nyie mliopo mbali na Mtwara na Msimbambati kwa ujumla hamna habari za kutosha na vyombo vya habari kwa kiasi kikubwa vinapotosha yale yanayojili huku hasa vyombo vya habari vya serikali na ccm, (gezeti la habari leo na uhuru). Bibi yupo na ana umri unaokadiliwa kuwa ni miaka 116 na mtoto wake ambaye anamsaidia kuongea na wageni wote wanaokwenda hapo kwake ana umri wa miaka 70 na wote bado wana nguvu kiakili, hawajapoteza network bado.
Kilichotokea, afisa usalama huyo wa taifa alifika Msimbati jana jioni inayoelekea kuwa usiku kwa nia ya kuonana na bibi ili amchukuwe ampeleke dar, kwa hiyo alikaribishwa hapo nyumbani na mtoto wa huyo bibi lakini afisa usalama alitaka kuongea na bibi huyo kwa faragha hivyo alitaka mtoto wa huyo bibi awapishe, mtoto wa bibi alimwambia afisa usalama kuwa haiwezekani kwani yeye ndiye humsadia bibi kwa mawasiliano yoyote yanayofanywa na wageni wote wanaofika hapo nyumbani, ndipo afisa aliposema amekuja kumchukua bibi anatakiwa dar na viongozi wa serikali, akijibiwa kuwa kutokana na umri wa bibi kuwa mkubwa na hali yake ya kiafya kutokuwa mzuri sana bibi huyo haendi kokote, afisa usalama akasema atwachukuwa wote akaambiwa haiwezekani pia. wakati hayo yakijiri wanakijiji waalianza kujikuasanya hapo nyumbani wengine wakalizinguka gari na wengine wakawa wanafutilia mazungumzo hayo kupitia dirisha la nyumba. afisa akashtuka na kutoka nje kutahamaki akakuta anahojiwa yeye na kila mwanakijiji akawaambia kuwa hawezi kuzungumza na wote alipoona kibano kinazidi na maisha yake yapo hatarini, akatimua mbio, kilichofuata ni wanakijiji kulichoma moto gari lakini afisa usalama amefinikiwa kusepa. Kwa mujibu wa m/kiti wa kijiji anasema afisa huyo ni kijana mzaliwa wa msimbati lakini hajafika hapo msimbati miaka mingi na haishi Mtwara.
Watanzania tunaomba mtambuwe kwamba wakati umefika kuwa wananchi wana haki zote za kunufaika na rasirimali za asili zinazopatikana katika maeneo yao na serikali inawajibu wa kujenga mazingira wezeshi kwa wananchi kunufaika na rasirimali zao, Kama tunavyodai ujenzi wa mtambo wa kufua umeme wa megawatt 300 na kujenga mtambo wa kuchakata gesi hapa Mtwara.
Kujengwa kwa mitambo hiyo kutavutia wajasiriamali wa kimataifa kuja kuwekeza katika viwanda mbalimbali vinavyotumia malighafi (by-product) zinazotokana na gesi asilia, viwanda hivyo ni vya fertilizer, antifreeze, plastics, pharmaceuticals and fabrics. It is also used to manufacture a wide range of chemicals such as ammonia, methanol, butane, ethane, propane and acetic acid. Many manufacturing processes require heat to melt, dry, bake or glaze a product. Natural gas is used as a heat source in making glass, steel, cement, bricks, ceramics, tile, paper, food products and many other commodities. Natural gas is also used at many industrial facilities for incineration.
Viwanda vya uzalishaji wa bidhaa hizo hapo juu vitafanya Mtwara kuwa mji wa viwanda kama mh. rais Dr. Jakaya Kikwete alivyoahidi wakati wa kampeni ya uchaguzi 2010 kama utekelezaji wa ilani ya chama cha ccm. Nchi bado itanufaika kwa makusanyo ya kodi lakini pia serikali zetu za mitaa zitanufaika kwa kodi inayotokana na viwanda hivyo kuwepo katika mikoa yetu ya kusini, kutakuwa na ajira za kutosha kwa watanzania wote na Mtwara itakuwa economic hub of Tanzani miaka 15 had 40 ijayo. inakadiliwa kuwa kuwepo kwa viwanda hivyo kutatengeneza nafasi za ajira za moja kwa moja 1,500,000 na zisizo za moja kwa majo 2,84,7000. Mtwara kuchele mwanzo wa mapinduzi ya kifikra.
Lakini watanzania lazima mjuwe pia kwamba Kilagani ambaye ni mtendaji mkuu wa shirika la maendeleo ya petrol Tanzani ndiye chanzo cha mgogoro huu, huyu ameiambia kamati ya ushauri ya Mkoa wa Mtwara katika warsha iliyofanyika katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mtwara tarehe 20/07/2012 kuwa "mafanikio makubwa iliyoyapata TPDC ni kishawishi na kushauri serikali kuihamisha gesi asilia ya Msimbati Mtwara na Songosongo Kilwa kwa kuisafirisha kwa njia ya bomba hadi Dar" yeye kwake haya ni mafanikio makubwa ambayo sasa ni zahama kwa serikali ambayo haiheshimu kauri na ahadi zake, serikali ambayo imeahidi kuwatumikia wananchi wake kwa uadilifu mkubwa.
WanaJF na watanzania ufisadi wa maliasili sasa basi na Mtwara ndo tumelianzisha, inayezadhani kuwa ni swala la kisiasa na umaarufu wa kisiasa aje sasa Mtwara naye aupati huo umaarufu. mimi ni ccm kwa hili hatuna chetu huku, tujipange tena.