Mtwara: Gari la 'Afisa Usalama' lapondwa mawe Msimbati

Mtwara: Gari la 'Afisa Usalama' lapondwa mawe Msimbati

Chasoda

Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
66
Reaction score
33
Habari za uhakika nilizozipata sasa hivi toka Msimbati zinasema kuwa kuna gari ya afisa usalama wa taifa mmoja toka Dar linapondwa kwa mawe na wananchi wenye hasira.

Afisa usalama huyo inadaiwa ametumwa na viongozi wa juu wa serkali ili aje amshawishi bibi mmoja anaedaiwa kuwa na uwezo wa kuizuia gesi isitoke kwenda Dar kwa njia ya bomba.

Bibi huyo inasemekana ndio mwenye kijiji hicho alishasema wazi kuwa gesi HAITOKI Mtwara kauli iliyowafanya hata viongozi kupata wasiwasi ivo kumtuma mtu huyo ili amshawishi gas itoke.

Wakati akiongea na bibi huyo aliwaita wajukuu zake ili wamsikilize. NDIPO Vurugu kubwa ikaibuka na mwanausalama akatimua mbio na kuliacha gari yake maana watu walikuwa wengi.

Na habari zilizonifikia sasa ni kwamba gari hiyo imechomwa moto.
 
Nchi hii kuna watu wanaamini kiasi hiki ushirikina?
 
Mpaka bibi ameichoka serikali ya chama cha mapinduzi na ahadi zao hewa na sasa kakataa kudanganyika, basi ujue 2015 ccm inazikwa mazima.

Nakupa Hongera sana bibi yetu kazia hapohapo gesi isitike Mtwara, nasi tupo nyuma yako.
 
Hebu tufafanulie kidogo:- Huyo bibi kamilikishwa hicho kijiji kiserikali au anakimiliki kimila?- Bibi huyo ana ushawishi kiasi gani kwa wanakijiji?- Tittle yake hapo kijijini ni nani?- Je, anatumia ushawishi wa hoja au anayo njia nyingine!NB: Isijekuwa 'muungwan' aliwatengenezea viongozi wetu madaraka sasa wanajua akiaribu nao wamearibikiwa!!!
 
mambo ya kaburi ia kiyeyeu haya au kakobe na umeme wa ngereja ?
 
Nchi hii kuna watu wanaamini kiasi hiki ushirikina?
Sio ushirikina, ni uhujumu wa miundombinu ya gesi (sabotage). Vikongwe wa namna hiyo wana ushawishi mkubwa na wanaheshimika!
 
Mpaka bibi ameichoka serikali ya chama cha mapinduzi na ahadi zao hewa na sasa kakataa kudanganyika, basi ujue 2015 ccm inazikwa mazima.

Nakupa Hongera sana bibi yetu kazia hapohapo gesi isitike Mtwara, nasi tupo nyuma yako.

Kumbuka huyu ni bibi asiyejua kusoma wala kuandika na hajui kiswahili zaidi ya neno moja la kuotea.
 
serikali ingetumia wanauslama kutaka kujua majina ya wezi wa pesa zetu walizoficha uswiss kwanjia kama hii, basi tungefika mbali. lakini kutumia njia hii eti kumshawishi bb aruhusu gesi ije mzizima, ni bado wakomunisti!!!!
 
Habari za uhakika nilizozipata sasa iv toka msimbati zinasema kuwa kuna gari ya afisa usalama wa taifa mmoja toka dar linapondwa kwa mawe na wananchi wenye hasira. Afisa usalama huyo inadaiwa ametumwa na viongozi wa juu wa serkali ili aje amshawishi bibi mmoja anaedaiwa kuwa na uwezo wa kuizuia gesi istoke kwenda dar kwa njia ya bomba.bb huyo inasemekana ndio mwenye kijiji hicho alishasema wazi kuwa gesi HATOKI mtwara kauli iliyowafanya hata viongozi kupata wasiwasi ivo kumtuma mtu huyo ili amshawishi gas itoke .wakati akiongea na bb huyo aliwaita wajukuu zake ili wamsikilize.NDIPO Vurugu kubwa ikaibuka na mwanausalama akatimua mbio na kuliacha gari yake maana watu walikuwa wengi. Na habari zilizonifikia sasa ni kwamba gari hiyo imechomwa moto.
huyu bibi ni shujaa kitaifa kuliko mkwawa, isike au kinjekitile! kaza uzi bibi weeeee!
 
hata Askofu kakobe alitishia umeme wa nguzo za Tanesco atauzuia kupita kwa maombi kanisani kwani lakini bado ukapita
 
Back
Top Bottom