Mtu anaanzaje kumchukia ndugu yake?

Mtu anaanzaje kumchukia ndugu yake?

Umeandika ukweli mkuu
Ubinafsi ni sifa ya nafsi kila nafsi yajitakia mema kwanza yenyewe
Ila kulijua hili na kuona utapambana nalo vipi ndio point amabayo tumetofautiana sana
Baadhi hawajui kabisa kuhusu hili hivyo upelekea nafsi zao kuwa hifadhi ya chuki na hasadi...na kwa kweli hamna maradhi mabaya kama maradhi ya hasadi.

Hasadi ni kutamani Baraka au neema ambazo mwenzio kazipata kutoka kwa mungu wake zimuondokee.

wengine ndio hivyo wanatamani hata wenzio wapate ajali au wapoteze na uhai kabisa...lakini chuki na hasadi kiuhalisia humchoma na kummaliza zaidi yule alievihifadhi
 
Hama yako umenunua bei gani,hongera kwa kumiliki ndinga kali
 
Nilikuwa naendesha gari langu kwa kasi, macho mbele bila kutazama tazama kushoto au kulia kwa barabara. Ndugu yangu aliniona akanisimamisha nimpe lifti lakini bahati mbaya mimi sikumuona nikampita. Tulipoonana uso kwa uso alikuwa amejaa hasira, akaniuliza kwanini siku ile alinisimamisha sikusimama. "Kwakuwa siku hizi umenunua Hummer, unatuona sisi ndugu zako hatufai, eeh? Hutaki hata kutusalimia njiani. Haya, we endelea tu." Ndugu yangu alinifokea kisha akaondoka. Japo sikuona kosa langu nilimfuata nikaenda kumuomba msamaha yaishe.

Siku nyingine ndugu yangu huyo alinipigia simu kuniomba nimkopeshe milioni mbili. Nikamjibu kuwa hapa nilipo hata laki mbili sina. Pesa nilizokuwa nazo zimetumika kukarabati nyumba yangu. Kabla sijamaliza kujieleza alikata simu kwa hasira, baadaye akanifuata nyumbani na kuanza kunigombeza: "Sema leo tujue moja, undugu umevunjika? Kwanini siku hizi hutaki kuwasaidia ndugu zako?"

Dawa ya moto sio moto, nikamjibu kwa upole kuwa ni kweli sina pesa. Nikipata nitampa hata bila kudai anirudishie. Aliondoka kwa hasira huku akiongea mwenyewe njia nzima mpaka mtaa wetu wakajua tumekosana. Huo ni mfano tu wa maisha ya ndugu na ndugu wanaokosana na kuchukiana hata kwa mambo madogo madogo.

Najiuliza mtu anaanzaje kumchukia ndugu yake? Anaanzaje kupanga kulipa kisasi au kumfanyia fitina ndugu yake kwa sababu ya mambo kama hayo huku anakiri kwamba yeye ni mcha Mungu? Katika 1Yoh 3: 14-15 tunaambiwa kwamba mtu asiyempenda ndugu yake anakaa mautini. Na kwamba yeyote amchukiaye ndugu yake anafananishwa na muuaji, na kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. Katika 1 Yohana 4:20 tunaambiwa pia kwamba Mtu akisema, anampenda Mungu, huku anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.

Ulishawahi kuchukiwa na ndugu yako au jirani yako? Ulichukua hatua gani?
Ndugu lawama

Unashangaa mtu mwenye chuki kwenda kanisani?
Hata wachawi uwa wanaenda kusali kanisani..!
 
Jipende mwenyewe ndo ujifunze kumpenda mwingine...hii ndo falsafa yangu
 
Kumbe umeamua kuleta mambo ya familia yetu humu ndani? Kea kuwa umenunua gari aina ya nyundo ndiyo unipite bila kunisalimia?kwa hili sitokubali tutakutana jumamosi kwenye kikao cha familia
 
Ndugu wakweli siku hizi ni mke, watoto zako, baba&mama na washkaji. Mbali na hapo tegemea maumivu tu.

Mimi siongei na mdogo wangu na wajomba zangu chanzo mali zangu na kazi yangu. Wanatamani nifukuzwe kazi, nimepeleleza wanasema najisikia naringa nimekuwa sasa.
 
Ndugu wakweli siku hizi ni mke, watoto zako, baba&mama na washkaji. Mbali na hapo tegemea maumivu tu.

Mimi siongei na mdogo wangu na wajomba zangu chanzo mali zangu na kazi yangu. Wanatamani nifukuzwe kazi, nimepeleleza wanasema najisikia naringa nimekuwa sasa.
Kazi ipo
 
Kumbe umeamua kuleta mambo ya familia yetu humu ndani? Kea kuwa umenunua gari aina ya nyundo ndiyo unipite bila kunisalimia?kwa hili sitokubali tutakutana jumamosi kwenye kikao cha familia
Duh, jino kwa jino
 
Mkuu huyo ndugu yako anayekufokea hivyo una uhusiano gani naye??
Ni kaka, mjomba, shangazi au nani?

Hata baba yangu mzazi siwezi mruhusu anipande kichwani kiasi hicho aisee.
 
Nilikuwa naendesha gari langu kwa kasi, macho mbele bila kutazama tazama kushoto au kulia kwa barabara. Ndugu yangu aliniona akanisimamisha nimpe lifti lakini bahati mbaya mimi sikumuona nikampita. Tulipoonana uso kwa uso alikuwa amejaa hasira, akaniuliza kwanini siku ile alinisimamisha sikusimama. "Kwakuwa siku hizi umenunua Hummer, unatuona sisi ndugu zako hatufai, eeh? Hutaki hata kutusalimia njiani. Haya, we endelea tu." Ndugu yangu alinifokea kisha akaondoka. Japo sikuona kosa langu nilimfuata nikaenda kumuomba msamaha yaishe.

Siku nyingine ndugu yangu huyo alinipigia simu kuniomba nimkopeshe milioni mbili. Nikamjibu kuwa hapa nilipo hata laki mbili sina. Pesa nilizokuwa nazo zimetumika kukarabati nyumba yangu. Kabla sijamaliza kujieleza alikata simu kwa hasira, baadaye akanifuata nyumbani na kuanza kunigombeza: "Sema leo tujue moja, undugu umevunjika? Kwanini siku hizi hutaki kuwasaidia ndugu zako?"

Dawa ya moto sio moto, nikamjibu kwa upole kuwa ni kweli sina pesa. Nikipata nitampa hata bila kudai anirudishie. Aliondoka kwa hasira huku akiongea mwenyewe njia nzima mpaka mtaa wetu wakajua tumekosana. Huo ni mfano tu wa maisha ya ndugu na ndugu wanaokosana na kuchukiana hata kwa mambo madogo madogo.

Najiuliza mtu anaanzaje kumchukia ndugu yake? Anaanzaje kupanga kulipa kisasi au kumfanyia fitina ndugu yake kwa sababu ya mambo kama hayo huku anakiri kwamba yeye ni mcha Mungu? Katika 1Yoh 3: 14-15 tunaambiwa kwamba mtu asiyempenda ndugu yake anakaa mautini. Na kwamba yeyote amchukiaye ndugu yake anafananishwa na muuaji, na kwamba muuaji hana uzima wa milele ndani yake. Katika 1 Yohana 4:20 tunaambiwa pia kwamba Mtu akisema, anampenda Mungu, huku anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.

Ulishawahi kuchukiwa na ndugu yako au jirani yako? Ulichukua hatua gani?

CHANZO CHA HIZI CHUKI ZOTE ZA NDUGU NI WIVU
Kasome visa vya hawa ndugu na wengine
1.Kaini alimuua Habili
2.Yusufu na ndugu zake
3.Rahel na Lea
4.Yakobo na Esau (mapacha)
 
Ndugu wakweli siku hizi ni mke, watoto zako, baba&mama na washkaji. Mbali na hapo tegemea maumivu tu.

Mimi siongei na mdogo wangu na wajomba zangu chanzo mali zangu na kazi yangu. Wanatamani nifukuzwe kazi, nimepeleleza wanasema najisikia naringa nimekuwa sasa.
Mh! mke ni ndugu siku hizi tayari ushatengenezwa wewe!
 
Back
Top Bottom