Mtoto wa Shekhe Yahaya akiongelea Majini

Mtoto wa Shekhe Yahaya akiongelea Majini

sir chief bila ya shaka utakuwa muumini wake tu, narudia kusema tena mwenye uwezo wa kujua la kesho ni MUNGU peke yake period!

sio kweli, kuna mtu anaitwa clairvoyant huyu anajua kitakachotokea kesho lakini pia hio clairvoyance ni uwezo ambao hata wewe unaweza kuwa nao provided kwamba unajitambua, umeacha kufata mkumbo na umeacha kukariri.
 
Last edited by a moderator:
Superman, kwa iman yangu ya dini ya kiislam haliwezekani, kesho ni ya mungu na hata leo ni ya mungu sbb sijui nn kitatokea dk moja ijayo
 
Last edited by a moderator:
Si kawaida yangu kuangalia kipindi cha nyota kinachoendeshwa na mtoto wa Marehemu Shekhe Yahaya channel ten. Lakini juzi nilivutiwa na alivyokuwa akielezea majini, jinsi wanavyoweza kukuletea pesa, jinsi ya kuwaita nk.

Lakini alipokuja kwenye mbinu ya Kuwafukuza alisema, Majini yanaweza kuuawa au kufukuzwa kwa Kuyakemea huku ukitaja jina la Yesu. Pia akasema binadamu wote wanapozaliwa huwa wanaguswa na Shetani, lakini mtoto pekee ambae hakuguswa na Shetani ni mtoto Yesu.

Huyo ni Mshenzi tu kama yule TB Joshua wa Nigeria ila tofauti yao yule amekuwa ni mtu wa kuwalia Kondoo hela zake. Uislam hauruhusu ujinga huu hata kidogo ni ameingia katika "SHIRKI"
 
Alipotabiri kwamba rais ajae atakuwa January Makamba mlimsifia na kumwona mungu. Hizi double standards hizi!!!!

Double standards za wapi?Imekuaje unaniaunganisha na makundi ya kishabiki?
 
Uchawi ni majini na uislamu unapromote majini kwenye Qur'an kuna aya special dedicated kwa waislam inayohusu majini na wanasali nayo na wanaposali popote huyakalia mabegani ndivyo Qur'an inavyosema sasa kuja hapa na kusema hamtambui hayo mapepo maimuna maruhan zainab na mapepo mengine mnashangaza wakati mpaka mnashare majina.

Mtakubalije shehe yahaya na mwanae waongoze ibada yenu na kutambulika na uongozi wa juu kama hamumuungi mkono eti mnampinga wakati anawaongozeni.

Me nijuavyo mganga wa kienyeji ni shehe aliyeiva sababu waganga wengi ni waislam tena mashehe sijawahi kumuona mganga wa kienyeji mchungaji au askofu.
 
Yuko sahihi.Hata katika Biblia imeandikwa.Hakuna jina jingine walilokirimiwa wanadamu liwapasalo kuokolewa kwalo ila jina la YESU.Yaani hapo majini hayana ujanja.Sasa kama hata shekh anatambua hilo we maamuma unabisha nini?
 
Ramli isiyomzuru mtu ni moja ya dini zetu za jadi ambazo zilikemea uchawi.Mbona waislamu wana albadili lakini hamuipingi?

Think critically.
 
Si kawaida yangu kuangalia kipindi cha nyota kinachoendeshwa na mtoto wa Marehemu Shekhe Yahaya channel ten. Lakini juzi nilivutiwa na alivyokuwa akielezea majini, jinsi wanavyoweza kukuletea pesa, jinsi ya kuwaita nk.

Lakini alipokuja kwenye mbinu ya Kuwafukuza alisema, Majini yanaweza kuuawa au kufukuzwa kwa Kuyakemea huku ukitaja jina la Yesu. Pia akasema binadamu wote wanapozaliwa huwa wanaguswa na Shetani, lakini mtoto pekee ambae hakuguswa na Shetani ni mtoto Yesu.

Hakwenda mbali zaidi kusema kwa nini iwe Yesu tu!? By @Nyerere

cc
Mahmood Ishmael
 
TAHADHALI YA UONGO NA UTAPELI WA WATABIRI WA NYOTA

Ningependa kuzindua Baadhi ya watu kuusu hao matapeli waongo na Washirikina ambao wanatumia mwamvuli wa Dini kwaajili ya Maslahi yao Binafsi Ewe Usiyejua Zinduka sasa ya kuwa Hakuna anayejua Elimu ya Ghaibu ( mambo yalifichikana kama kujua kesho itakuwaje) Isipokuwa Allah (Subhanaw Wataala )

Mwenyezi Mungu anasema

" Na kwake yeye ndiko kwenye funguo za ghaibu hakuna anayejua isipokuwa yeye ( yaani Mwenyezi Mungu) "
[Al- An a'm: 59]

Amesema Mtume Swallallahu Alayh Wassallam Amesema

" Hakuna anayejua Ghaibu isipokuwa Allah "

amepokea Imam Twabaran

Kuusu Matumizi ya Nyota Je nini Uislam unatufundisha


َِِْ Al-Bukhaariy
amerekodi katika Swahiyh yake: Qataadah amesema: “Allaah Ameumba hizi nyota kwa malengo matatu;

(i) mapambo ya mbingu

(ii) vimondo vya [kuwafukuza na kuwapiga] shaytwaan,

(iii) alama za kuongoza njia (wasafiri wa majangwani na baharini).

Basi atakayefasiri vingine amekosea na atakuta patupu Akhera (atakosa thawabu) kwani atakuwa amebeba asio na elimu nayo kwa kuchupa mipaka ya ujuzi wake”.

Mwisho wa kunukuu.

Nini Hukmu ya kumwendea Mganga, Kuhani /Watabiri wa mambo ya Ghaibu

Kutoka kwa Abee Hurarya (Radhiallahu Anhu) Kutoka kwa Mtume ( Swallallahu Alayh Wassallam )
Amesema

" (yeyote) Atakeyemwendea Kuhani ( mtabiri wa mambo ya Ghaibu) kisha akamswadikisha Yale anayomwambia basi atakuwa ameyakufuru Yale aliyotemeremshiwa Muhammad (Swallallahu Alayh Wassallam )

Ktk Hadith nyingine Atakaye mwendea Mganga au Kuhani

Kwaiyo hao waganga WATABIRI wa Nyota wako Mbali na Mafundisho ya Dini ya Kiislam kwa watu waogope Kuwaendea watu hao ni waongo mno wala sio Mashekh hao ni Mashehena ya Ushirikina

Dhambi ya kuua, Kuzini ,Kula Riba na Kuasi wazazi wa wawili hakufikii madhambi ya kumwendea Mganga au Mtabiri kwa sababu ukimwendea Mganga au Mtabiri utakuwa Umeshirikisha Mola wako na Shirk ni Dhambi ambayo haina Msamaha

Kwaiyo watu wajitaahadhari na watu hao ni waovu mno
 
Si kawaida yangu kuangalia kipindi cha nyota kinachoendeshwa na mtoto wa Marehemu Shekhe Yahaya channel ten. Lakini juzi nilivutiwa na alivyokuwa akielezea majini, jinsi wanavyoweza kukuletea pesa, jinsi ya kuwaita nk.

Lakini alipokuja kwenye mbinu ya Kuwafukuza alisema, Majini yanaweza kuuawa au kufukuzwa kwa Kuyakemea huku ukitaja jina la Yesu. Pia akasema binadamu wote wanapozaliwa huwa wanaguswa na Shetani, lakini mtoto pekee ambae hakuguswa na Shetani ni mtoto Yesu.

= Majinni

Labda Yesu hakuguswa na shetani utotoni lakini alikumbwa na shetani kwa siku arubaini, sijui ilikuwa ukubwani au utotoni? Jibu wewe.

Kumbuka hilo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom