Nyamayao
JF-Expert Member
- Jan 22, 2009
- 6,966
- 2,379
Mimi naungana na Shishi kukwambia kwamba ni bora usiseme chochote maana mumewe wako atachanganyikiwa sana na kujiuliza maswali mengi ambayo wewe huwezi kuyajibu. Atakuuliza maswali kama yafuatayo: Umetembea na huyo jamaa kwa miaka mingapi wakati wa ndoa yenu? Kama mna watoto wengine anaweza kuuliza je na hawa watoto kuna uwezekano kuwa si wangu? Ni wakati gani ambapo mlikuwa mnakutana na mlikutana mara ngapi labda kwa wiki au kwa mwezi? Kama mumeo huwa anasafiri kikazi au kibiashara atakuuliza uliwahi kumleta nyumbani kwenu na mkafanya naye mapenzi labda kitandani kwenu? Na mengine mengi tu.
Kwa kifupi ukimwambia ndio itakuwa mwisho wa ndoa yenu. Najua hiki kitu kinakutesa sana na kukukosesha raha katika maisha yako ya kila siku, lakini siafikiani na wewe kumwambia mumeo. Unajua kwa sababu halinihusu mimi ni rahisi mno kusema mwambie atakusamehe, lakini ukweli mkuki kwa nguruwe kwa mwanadamu ni mchungu. Wanaume tulivyo katika maswala haya hasa kunapokuwa na mtoto aliyemlea miaka yote hiyo akijua kwamba ni mwanae halafu anakuja kuambiwa si mwanae basi inakuwa ni kasheshe ya hali ya juu. Ndio wako wanaume wachache wanaweza kusamehe lakini zaidi ya asilimia 80 ya wanaume hawawezi kusamehe na ndoa inakuwa imeingia dosari kubwa na itadorora na hatimaye huvunjika. Kila la heri lakini kumwambia mumeo IS A NO NO maana ndio itakuwa mwisho wa ndoa yenu. Na huyo taahira fanya juu chini ukate mawasiliano naye kabisa kama mnafanya kazi pamoja basi aanza kutafuta kazi nyingine kwa juhudi zako zote.
well said mpendwa, but hapo kwenye baba wa mtoto naweza sema hawezi kuitwa tahaira hata kidogo, kuna watu wengine damu zao hazipotei hovyo, ndio mana anania na mwanae, na kama huyu mama alishamwambia ni mimba yake then wat do u espect? ana haki zote za kumtaka mwanae, kasheshe ni kwa mume namuonea huruma kweli atakavyokabiliana na hii ctuation, wewe mama mwenzangu hebu roho ikuume ki vyako, ucumize za wenzio, 2lia na hicho kitu! sio kidogo kama unavyofikiria, nakwambia utaachwaaa na watoto wote baba atakuwa na wacwac nao kasheshe aende kupima hiyo DNA kwa wote, hapana ucwaaweke watoto kwenye risk ki hivyo.