Mtoto wa nje ya ndoa

Mtoto wa nje ya ndoa

Ndugu yangu Msanii

Tatizo hapa ni the emotional battle that will ensue ... facing the situation ... how long the recepient will take to digest the situation ... the emotional trauma ... mengine ya sheria yatakuja later after mumewe recovering and accepting the situation

Maana anybody can be given any news lakini there is limitation this is what this lady is worried about ... the aftermath of the situation

I suggest maybe amlishe limbwata kwanza ... maana hapa hata kumface simba afadhali
 
Ndugu yangu Msanii

Tatizo hapa ni the emotional battle that will ensue ... ...............I suggest maybe amlishe limbwata kwanza ... maana hapa hata kumface simba afadhali

Ah kwa mwendo huo natamani ningeoa mke wa aina hiyo wa kulisha limbwata. Hebu Naima nipe shule namna limbwata linavyoandaliwa ili sie kina baba tulile? pls naima
 
wakuu achana na stori ndefu za sheria na vitu gani sijui..nini maana ya DNA..hivi kweli leo uambiwe huyu siyo baba yako? ni baba wa kambo? mzee hata kama unaishi paradiso..damu nzito kuliko maji! hata kama jamaa atakupenda vipi..you will always feel that you belong somewhere else. Hapa naomba watu tutofautishe pale mtu anapomkana baba yake kwa kumtelekeza..I mean baba yako alikukataa, au aliikataa mimba kwamba hahusiki au aliwatupa na mama yako (hapa mama yako hana hata iota of blame kabisa..)..hapo ni possible ukawa na attachment kubwa kwa yule aliyekusaidia hata kama ni baba kambo!

. Lakini kwa hili la mama kukuficha na kugundua baadaye? the story is different! Kumbuka, inawezekana kabisa jamaa ana nia ya kumsaidia mtoto wake.

Hapa cha muhimu ni kumwambia jamaa, this is what I did and it was accidental (ingawa ataconfirm kwamba wewe ulikuwa unacheat, all along). Then yeye ataamua either akupe talaka (au umpe talaka maana siku hizi hata wanaume wanaolewa..).

Swala la custody hapa haliji kabisa, maana jamaa hajakataa kumtunza mwanae. Harafu naturally, hata mtoto iwe namna gani ata feel more attached to her biological father..unless ni wale watoto wa dot. com ambao wamezoea maisha mazuri wanaogopa shida, incase kama msure (presumptive) hana kitu! its all about opportunities...

Otherwise dada pole, we jitahidi uende kwa mshenga au msimamizi wa ndoa umwambie..ila please, please have a PLAN B incase of anything! Hii information ni nzito sana mtu kuhandle.
 
No no maidamaida.
Please dont tell him wanasema sometime good comes from bad.No in the really world my world no no.

Kila mtu ana haki ya kupewa news lakini kwa hili usimwambie hata yule mume wa ni threat kwako usijaribu kumwambia hata kidogo.Kuna vitu vingine ni vyema kufa navyo kama balali tu kwa manufaa ya wote walio baki...
Hii ni benefit kwa mtoto na baba unaweza kuwambia baba akakutosa wengine kama mie huwa sina tatizo kuanza maisha mapya as long as hujanilonga nikapoteza uwezo wa kufanya kazi...kama kupewa libwata.

Mtoto nae ataanza kuwa hana imani,amani,uwezo yaani fulll kuchanganyikiwa.So kufa nalo hilo ni la kwako kama umeweza kukaa nalo muda wote basi unaweza kukaa nalo milele.I dont wish this to happen kwangu nikioa.Yaani kama analo akae nalo kwa kweli milele.

That all i can say,kana ka nsungu nategegemea kukuona hapa.
 
wakuu achana na stori ndefu za sheria na vitu gani sijui..nini maana ya DNA..hivi kweli leo uambiwe huyu siyo baba yako? ni baba wa kambo? mzee hata kama unaishi paradiso..damu nzito kuliko maji! hata kama jamaa atakupenda vipi..you will always feel that you belong somewhere else. Hapa naomba watu tutofautishe pale mtu anapomkana baba yake kwa kumtelekeza..I mean baba yako alikukataa, au aliikataa mimba kwamba hahusiki au aliwatupa na mama yako (hapa mama yako hana hata iota of blame kabisa..)..hapo ni possible ukawa na attachment kubwa kwa yule aliyekusaidia hata kama ni baba kambo!

. Lakini kwa hili la mama kukuficha na kugundua baadaye? the story is different! Kumbuka, inawezekana kabisa jamaa ana nia ya kumsaidia mtoto wake.

Hapa cha muhimu ni kumwambia jamaa, this is what I did and it was accidental (ingawa ataconfirm kwamba wewe ulikuwa unacheat, all along). Then yeye ataamua either akupe talaka (au umpe talaka maana siku hizi hata wanaume wanaolewa..).

Swala la custody hapa haliji kabisa, maana jamaa hajakataa kumtunza mwanae. Harafu naturally, hata mtoto iwe namna gani ata feel more attached to her biological father..unless ni wale watoto wa dot. com ambao wamezoea maisha mazuri wanaogopa shida, incase kama msure (presumptive) hana kitu! its all about opportunities...

Otherwise dada pole, we jitahidi uende kwa mshenga au msimamizi wa ndoa umwambie..ila please, please have a PLAN B incase of anything! Hii information ni nzito sana mtu kuhandle.

ukikuta kibao kimekataza kupita mahala fulani halafu ukakamatwa ukikatiza, unadhani sheria itakulinda kuwa hujui kusoma?? au ukijitetea kuwa mbona njia yenyewe ni ya lami itakulinda??? Masuala ya hisia ni mbali na mambo ya kisheria. Au mzee umepita mahala nini??

Jamii isiyofuata sheria inafanana na jamii ambayo inajichukulia sheria mkononi kuhukumu pasipo utaratibu....
leo nipo safarini sijatembea na bibli zangu za sheria ila nitkuletea vifungu next time mkee.

Halafu we buswelu acha mawazo wa kizamani. endapo akikaa kimya huku ameshajiumbua upande mmoja, itakuwa soo endapo jamaa atakuja kumdai mtoto. Ndiposa nimemshauri Maindainda apige moyo konde amweleze mumewe lkini kwa timing kali ili kumweka sasa, hata wengine wamesema apige starter ya limbwata ili kurekebisha koo.
 
Da Mainda kumbuka kitanda hakizai haramu! Mtoto kisheria baba yake ni mumeo wa ndoa, piga ua hata mkipima DNA huyo mwizi hawezi kupewa mtoto!

Wewe Kakalende: UNASEMA "Mtoto kisheria baba yake ni mumeo wa ndoa, piga ua hata mkipima DNA huyo mwizi hawezi kupewa mtoto", hivi wewe umemaliza darasa la saba kweli, au ni wale mbumbu " (Low IQ Family), unaelewa maana ya DNA, KAMA MTOTO SI WAKWAKO HUNA MAMLAKA NAYE KISHERIA AU KIMILA LABDA UFANYE ADOPTION. KAMALIZIE DARASA LA SABA KWANZA. KWELI NCHI HII TUNAKAZI KWELIKWELI AU INABIDI UENDE NGUMBALU
 
Mama pole sana kwani napenda kukutia moyo uwe tu mkweli kwa mumeo. Mimi haya yalikuta miaka 18 iliyopita baada ya mamsapu wangu kufanya tendo kama lako na akazaa mtoto ambaye kwa kweli ni kijana mzuri sana na mwenye akili sana> Nimemsomesha na hata sasa yuko USA kwenye chuo kikuu huko. Hili pendo lilitokea baada ya mke wangu kunieleza ukweli na kunisihi sana nimfichie hii siri kama mwenzanke kwenye ndoa inayotambulika tulifanya hivyo and now the boy is 21 yrs old. Baadaye nilizunguza na Bilogical father wake kuhusu hili jambo na kuwa kijana anatumia sir yangu. Huyu bwana naye kanishukuru sana na kuniomba hata mtoto asiambiwe yaliyopita yasije yakamfanya akaumia roho. Hivyo kama mumeo ni mtu aliyekomaa kindoa naona hili halitakuwa jambo la ajaabu kwake na bila shaka atalipokea kwa moyo wa kutaka kukusaidia pia maana ni kitu ambacho uanakijutia hadi leo.
 
"Come ye all who are heavily laden with sins and your sins shall be as white as snow"

Ninanachokushauri ni kwamba ndoa yako bado changa, pamoja na kwamba imetimia miaka 10, kipindi hiki huwa bado kinaitwa kipindi cha misukosuko katika ndoa. na kuachika kwa kosa kama hilo ni 99% confidence interval. Hivyo basi, umemkosea mmeo na Mungu pia. Tubu kwa Mungu wako kama unaamini ili ubaki na amani, kwa usalama wa ndoa yako, kama mnaishi vizuri na mmeo nyamaza milele zote hadi mauti. Kumbuka hata wakati unafunga ndoa nyote wawili hakuna aliysema kwamba aliwahi kenda nje ya ndoa na hata mashahidi waliambiwa kama kuna jambo lolote wanalolijua ili nyie msiunganishwe kwa ndoa, na wakanyamaza, basi vivyo hivyo, na wewe unayamaze milele zote.

Pili huyo, biological father wa mtoto, never, meet him. Usi intertain kuonana.

Point yangu ni kwamba ungama kwa Mungu pekee ndiye atakusamehe dhambi zako zote ikiwamo hiyo ya usaliti wa ndoa yako, na kisha endelea na maisha yako na mume wako, lakini, dhambi usitende dhambi tena. Never, never tell your husband. Wanaume tunatofautiana sana na kupokea shocking news kama hiyo itakuwa na madhara makubwa kuliko faida. Sasa mimi nikipima naona hasara ya kumwambia ni kubwa kukilko kutokumwambia. So, don't tell him.
 
Dada Maindainda, pole sana ila huu ni mwiba wa kujidunga! maoni yangu ni nyamaza hivyo hivyo,, kama miaka na miaka imepita ya nini kusema sasa. u need to think abt the repurcussions becoz this is the highest form of betrayal, sijui kama mumeo atakusamehe na hata akikusamehe huyo mtoto atakuwa a constant reminder of your infidelity
Na huyo biological father anakutishia tu, ana uhakika gani, mmefanya DNA testing? yeye yuko tayari kuweka ndoa yake on the line?? kwa sababu akiharibu yako na ya kwakeje?

the other thing is kwa sababu you are really sorry and remorseful about what you did, letting it out will give you some piece of mind. but u need to be careful how u do it.

My advice tread carefully.. na kila la kheri!

dont worry unaona signature hapa that s****t happens, to good pple most of the time..........

Mimi naungana na Shishi kukwambia kwamba ni bora usiseme chochote maana mumewe wako atachanganyikiwa sana na kujiuliza maswali mengi ambayo wewe huwezi kuyajibu. Atakuuliza maswali kama yafuatayo: Umetembea na huyo jamaa kwa miaka mingapi wakati wa ndoa yenu? Kama mna watoto wengine anaweza kuuliza je na hawa watoto kuna uwezekano kuwa si wangu? Ni wakati gani ambapo mlikuwa mnakutana na mlikutana mara ngapi labda kwa wiki au kwa mwezi? Kama mumeo huwa anasafiri kikazi au kibiashara atakuuliza uliwahi kumleta nyumbani kwenu na mkafanya naye mapenzi labda kitandani kwenu? Na mengine mengi tu.

Kwa kifupi ukimwambia ndio itakuwa mwisho wa ndoa yenu. Najua hiki kitu kinakutesa sana na kukukosesha raha katika maisha yako ya kila siku, lakini siafikiani na wewe kumwambia mumeo. Unajua kwa sababu halinihusu mimi ni rahisi mno kusema mwambie atakusamehe, lakini ukweli mkuki kwa nguruwe kwa mwanadamu ni mchungu. Wanaume tulivyo katika maswala haya hasa kunapokuwa na mtoto aliyemlea miaka yote hiyo akijua kwamba ni mwanae halafu anakuja kuambiwa si mwanae basi inakuwa ni kasheshe ya hali ya juu. Ndio wako wanaume wachache wanaweza kusamehe lakini zaidi ya asilimia 80 ya wanaume hawawezi kusamehe na ndoa inakuwa imeingia dosari kubwa na itadorora na hatimaye huvunjika. Kila la heri lakini kumwambia mumeo IS A NO NO maana ndio itakuwa mwisho wa ndoa yenu. Na huyo taahira fanya juu chini ukate mawasiliano naye kabisa kama mnafanya kazi pamoja basi aanza kutafuta kazi nyingine kwa juhudi zako zote.
 
Mama pole sana kwani napenda kukutia moyo uwe tu mkweli kwa mumeo. Mimi haya yalikuta miaka 18 iliyopita baada ya mamsapu wangu kufanya tendo kama lako na akazaa mtoto ambaye kwa kweli ni kijana mzuri sana na mwenye akili sana> Nimemsomesha na hata sasa yuko USA kwenye chuo kikuu huko. Hili pendo lilitokea baada ya mke wangu kunieleza ukweli na kunisihi sana nimfichie hii siri kama mwenzanke kwenye ndoa inayotambulika tulifanya hivyo and now the boy is 21 yrs old. Baadaye nilizunguza na Bilogical father wake kuhusu hili jambo na kuwa kijana anatumia sir yangu. Huyu bwana naye kanishukuru sana na kuniomba hata mtoto asiambiwe yaliyopita yasije yakamfanya akaumia roho. Hivyo kama mumeo ni mtu aliyekomaa kindoa naona hili halitakuwa jambo la ajaabu kwake na bila shaka atalipokea kwa moyo wa kutaka kukusaidia pia maana ni kitu ambacho uanakijutia hadi leo.

Wanaume kama wewe katika dunia ya leo ni nadra sana kukutana nao. Hongera sana.
 
Bubu ataka kusema; [COLOR="Red" said:
Na huyo taahira fanya juu chini ukate mawasiliano naye kabisa kama mnafanya kazi pamoja basi aanza kutafuta kazi nyingine kwa juhudi zako[/COLOR] [/COLOR]zote.[/size][/color]

Kosa moja alilolifanya huyu dada ni kumjulisha huyu jamaa kuwa kapata mimba kutokana na encounter yao. ukiwa unajua una mumeo jamani ni bora kunyamaza tu, Ndio maana sasa anatishia kuja kumchukua 'mwanae' hana hata chembe ya proof, and if that happened he's a mere sperm donor. na wako teletele wa sampuli yake,

kama Bubu ataka kusema, hilo jina nalo, haya we! cut all ties and any form of communication naye kabisa tena mwambie live kuwa he has no right to even think about it na asikuharibie familia. maswali utakayoyazua kwa mumeo na mwanao pia hayana kipimo, na hata hao watoto wengine atakuwa anashuku kama ni wake, dont even talk abt trust, hawezi tena kukutrust and huo ndio utakuwa mwanzo wa mwisho wa ndoa yenu. like i said hapo juu kidogo, weigh the pros and cons of telling and not telling him, dont rush and get enaf shock absorbers kwa sababu u will need them in case u decide to speak.

this will affect your son alot, atakuwa hana imani na wanawake hata kidogo and i know u dont want to do that.

omba msamaha kwa mwnyezi mungu, na nyamaza kimya dadangu.
 
Duh....Ama kweli wanawake mnatuweka pabaya sana.....ila for Me Sina simile...naweza hata kukusambaratisha...umeniharibia program zangu kibao...

1. Sijui wewe DINI gani...lkn kwa jinsi jina ulivyoliweka inaonekana unatoka Usambaani. ni vema ukamtafuta Kiongozi wa DINI yako akupe ushauri.....ila tafuta wa Mbali, maana wa karibu anaweza teta..then tetesi zaweza fika home kwako.

2. Inavyoonekana ULIZINI ukiwa ndani ya Ndoa...Kidini hili ni KOSA LA JINAI.(Unanielewa nikisema kosa la Jinai)...

3. Unaproof gani huyo MZINIFU MWENZA ni mwanae?...sura..tabia..mwili? DNA? au wewe wajua siku ulipozini ndio uliopata mimba?

4. Kesi kama Hii ilishawahi kutokea Mazense...kuna Jamaa nilikuwa nafanya nae kazi aliileta story. Kiufupi MZINIFU MWENZA alikwenda kuwaambia dada zake, kuwa amezaa na Dada XYZ, wakati huyo dada anaishi na Mume wake. na jamaa alimlea mtoto kwa kipindi chote hicho...madada wa MZINIFU Mwenza wakaanza kwenda kumwambia yule mwanamke wanamhitaji mtoto wao, later thru vikao mbalimbali MZINIFU MWENZA alipewa Mtoto/.....for your case angalia huyo MZINIFU MWENZA asije kuwaambia dada zake...ambao hawapendi NDOA idumu..watakuja kusema live mbele ya Mumeo, then MUMEO itabidi aanze UDADIDISI na hapo ndipo utakapojua kusuka au kunyoa.

5......more ushauri to come....kama ukirespond hapo juuu....
 
Asanteni kwa ushauri wenu mzuri. I am still caught up between the two - nicheme nichicheme? Nakubali nisingesema kwa biological father, ila nilichanganyikiwa wewee, sikujua nifanye nini. Na kwa kweli kutoa mimba sikuwahi kufikiria.

Kwa kweli hata kama naachika leo singependa mtoto akae na biological father, alelewe na mama wa kambo? Nina reservations katika hili, pamoja naye pia. Halafu pia mtoto akijua na ukija kumkanya akikosea baadae atasema-wewe na baba nyote hamna akili!

Bado nahitaji muongozo wa kisheria, wajua siwezi kwenda kwa lawyer juu ya hili. Kama nimeelewa, mnasema mtoto kisheria ni wa biological father unless anakuwa adopted. Naomba kama kuna mtu anaijua hiyo sheria aniambie ni ipi niitafute.

Abunuwasi hongera sana, I wish ningekutuma wewe uongee na mume wangu. Ila sina uhakika kama mzee anafanana na Chuma au la, maana amesema angenisambaratisha kwanza, maskini mie.

Hivi wababa mnaopeleka watoto wa nje home inakuwaje, au nyie ni mteremko tu, unampiga mama kiswahili na doti ya Khanga / Wax basi.

Kuna mtu aliuliza umri wa mtoto, naomba nisiseme maana wanaume wote humu ndani wataenda kukagua watoto wao wa umri huo, mwajuaje mzee ni mwana JF?
 
Ah kwa mwendo huo natamani ningeoa mke wa aina hiyo wa kulisha limbwata. Hebu Naima nipe shule namna limbwata linavyoandaliwa ili sie kina baba tulile? pls naima


I will teach you offline ... maana ume beg sana ... BUT PLEASE DONT TRY THIS AT HOME OR AT SCHOOL.
 
3. Unaproof gani huyo MZINIFU MWENZA ni mwanae?...sura..tabia..mwili? DNA? au wewe wajua siku ulipozini ndio uliopata mimba?


NI WA KWAKE, MPAKA KUPIGA MIAYO WANAFANANA. HAPO HAMNA MASWALI. NDIO TATIZO LA WATOTO WA NAMNA HII, NA HILI LINANIDUHI NA KUHUZUNISHA, MAANA NAMUONA JAMAA KILA SIKU KATIKA MTOTO HUYU, NAKUMBUKA MAKOSA YANGU
 
Kuna mtu aliuliza umri wa mtoto, naomba nisiseme maana wanaume wote humu ndani wataenda kukagua watoto wao wa umri huo, mwajuaje mzee ni mwana JF?

Isije kuwa ni mimi...let me xcheck with my boys..! ulisema ni mtomto gani tena..a boy or a girl?
 
3. Unaproof gani huyo MZINIFU MWENZA ni mwanae?...sura..tabia..mwili? DNA? au wewe wajua siku ulipozini ndio uliopata mimba?


NI WA KWAKE, MPAKA KUPIGA MIAYO WANAFANANA. HAPO HAMNA MASWALI. NDIO TATIZO LA WATOTO WA NAMNA HII, NA HILI LINANIDUHI NA KUHUZUNISHA, MAANA NAMUONA JAMAA KILA SIKU KATIKA MTOTO HUYU, NAKUMBUKA MAKOSA YANGU

Dada, Kila jambo lina chanzo chake. Ndio maana huwa wanasema, lazima mtu awe makini na decisions za maisha yake wakati wowote ule,kwasababu mtu huvuna kile anachopanda. Ukipanda uharibufu, utavuna uharibifu....hata ukilia sana, lazima uyale yale matunda ya uharibufu kwanza yaishe ndo maisha mazuri yawepo. Labda, Mungu aweza kukusamehe, ila kwa vitu halisi kama hivyo(mtoto katokea), itabidi ujikaze ule hiyo pilipili hadi iishe, na ikiisha, ndo utaanza maisha ya kawaida ya kula sukari..yaani utaanza upyaaa, maisha mapya. ukijua kuwa yale ya zamani yameshavurugika kabisa na utaanza chapter mpya.

sisemi ili kukuumiza. ukweli ni kwamba, itabidi umwambie huyo jamaa haraka sana ili asiendelee kujiridhisha na mtoto akijua ni wake kumbe sio. unavyozidi kunyamaza ndo unavyozidi kuongeza pilipili kwenye mboga. bora hapo ulipofikia upate adhabu ya hapohapo na uanze maisha mapya kuliko kuja kuanza hayo maisha mapya baadae na jamaa akijua kuwa wewe ni mtu mbaya sana kwani siku zote hizo ulikuwa unamfanyia unafiki. atajua kuwa wewe unao uwezo hata wa kumuua wakati wowote kama unao uwezo wa kuweka mambo hayo moyoni kwa muda wote huo, inamaana haikuumi?

itabidi uwe responsible for your faults. kwetu sisi wanaume, hasa ukiona tunawapenda sana, huwa tunaumia sana kama mkitudanganya. kwa ufupi, jamaa anaweza hata akakuua kama ni kwenye sport na akasingizia ni "provocation" ambayo kisheria hata haendi ndani. wale wanasheria mnajua hili. lakini itabidi tu, umwambie ili kama noma na iwe noma mapema. kama kukusamehe akusamehe mapema, kama kukuacha akuache mapema. ili uanze maisha mapya starting from where jamaa atafikia. ni kweli, kama akiamua kukuacha, hauwezi kumlaumu kwasababu wewe mwenyewe unajua kuwa ni kosa lako, hovyo utaanza na wewe maisha mapya....na kama ataamua kukusamehe, ndo hivyo tena.

Lakini hili liwe fundisho kwa wanawake wengine humu ndani, kwasababu, kwa wanaume wengine, kama mkewe ndo kafanya hivyo, hata akikusamehe, ujue na wewe anaweza akakutafutia watoto wa nje ya ndoa hata watano ili tu akukomeshe. sio rahisi kwa mwanaume wa kawaida kukusamehe hivihivi,ndo maana nasema uwe tayari kula matunda ya yale uliyoyafanya, na wala usipate shida, wewe mwenyewe nenda yachume anza kuyala hadi yaishe....na hauna mtu wa kumlaumu. ila nakushauri, unapomwambia,usiwe peke yako, uwe na watu kama wanne ivi hasa wanaume na wenye nguvu, jamaa asije akachanganyikiwa na hasira akakuchinja. Pole sana. Mrudie Mungu, Okoka, nenda kanisani ukaombewe, na Mungu anaweza akapunguza hiyo sumu, ukashangaa mambo yameenda vizuri tu lakini. ila ukienda kichwakichwa, kuna mawili. .......
 
Wewe Azimio weweee, usitafute matatizo, shauri yako, pamoja na kusema kuwa uko simple, sijui kama kuna mwanamme simple katika kujua kuwa mkeo amefanyausaliti huu. Siwezi kutoa details zingine za mtoto, sorry.
 
Kidzogolae,
Yaelekea wewe umeshatoa adhabu kabisa maana unavyoonekana ni ungempa talaka mkeo tu akaanze maisha mapya, hayo unayoyasema.

wanaume mnajifanya mna mahasira sana, na ndio maana hamuambiwi jambo. Busara zenu tuzione katika vitendo na maneno yenu na sio MANGUMI na KUCHINJANA. Mbona sisi wanawake tunawafumania na bado tunawaandalia chakula na kuwatunzia siri? Hapa sitafuti sympathy, nataka tu kuonyesha kuwa mko tofauti.

Sijui kama umesoma alivyosema Abunuwasi - yeye ana wake baba mkubwa sasa na anamtunza. Labda "kifua" chako kidogo tu.

Nataka kujaribu kumpa mume wangu mtihani kumpima pressure kabla sijampa ishu, any idea how?.
 
Back
Top Bottom