BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Asanteni kwa ushauri wenu mzuri. I am still caught up between the two - nicheme nichicheme? Nakubali nisingesema kwa biological father, ila nilichanganyikiwa wewee, sikujua nifanye nini. Na kwa kweli kutoa mimba sikuwahi kufikiria.
Kwa kweli hata kama naachika leo singependa mtoto akae na biological father, alelewe na mama wa kambo? Nina reservations katika hili, pamoja naye pia. Halafu pia mtoto akijua na ukija kumkanya akikosea baadae atasema-wewe na baba nyote hamna akili!
Bado nahitaji muongozo wa kisheria, wajua siwezi kwenda kwa lawyer juu ya hili. Kama nimeelewa, mnasema mtoto kisheria ni wa biological father unless anakuwa adopted. Naomba kama kuna mtu anaijua hiyo sheria aniambie ni ipi niitafute.
Abunuwasi hongera sana, I wish ningekutuma wewe uongee na mume wangu. Ila sina uhakika kama mzee anafanana na Chuma au la, maana amesema angenisambaratisha kwanza, maskini mie.
Hivi wababa mnaopeleka watoto wa nje home inakuwaje, au nyie ni mteremko tu, unampiga mama kiswahili na doti ya Khanga / Wax basi.
Kuna mtu aliuliza umri wa mtoto, naomba nisiseme maana wanaume wote humu ndani wataenda kukagua watoto wao wa umri huo, mwajuaje mzee ni mwana JF?
Ukishafanya uamuzi useme au usiseme basi tufahamishe pia. Na kama utaamua kumwambia mumeo pia tungependa kujua matokeo ya hili bomu utakalomuangushia. Bado ushauri wangu ni ule ule kwamba usimwambie mumeo.