Mtei - Mbowe - BoT; Connecting the dots...

Kutolipa kodi ni UHALIFU uliopitiliza!!

Kumiliki mali yoyote mahali popote duniani kwa njia halali si UHALIFU!!

Ukiwauliza CCM adui yao mkubwa kabisa anayehatarisha uwepo wao,utawala wao sasa na siku za usoni ni nani; jibu litakuwa ni hili CHADEMA tu chini ya MBOWE, Saidi Arfi, Dr Slaa, Zito Z.K, Mnyika, Marando Tundu Lissu nk,nk

Ukiwauliza how to cut them off? Majibu haya yatakuja
  • Bambika kesi za uhaini na ugaidi
  • Ua (kill them) because sisi ni serikali tuna polisi,jeshi,mahakama,Ma - RC, Ma - DC,watendaji wa kata na vijiji ........Hivi ndivyo wanavyojinadi hawa wanaojiita chama cha magamba,chama tawala!!
  • Waite wachochezi kila wanapojaribu kuikosoa serikali ya chama tukufu......utukufu ule wa kishetwani

HOJA SASA NI HII:

Hivi nyinyi ma CCM kama kweli Mbowe na Chama chake anachokiongoza angekuwa na uchafu huu unaosema.....kutolipa kodi za serikali, kumiliki mali iwe ni Uswiss au USA au UK angekuwa salamaaaaa mapaka leo?????
 
Nimeweka haya hapa nikidhani kuwa Field Marshall ES=Le Mutuz=w.j.malecela..... Ebu chunguzeni utetezi wa Le Mutuz juu ya umilikiwa wa mali za John Samwel Malecela....na Je utetezi huu unafaa kutumika kuelezea Mali anazomiliki Mh. Mbowe ? Utetezi huu aliutoa wakati akimjibu member wa JF aitwaye joka Kuu Source: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-john-samwel-na-legacy-yake-9.html#post105511
 
Last edited by a moderator:
Nimeweka haya hapa nikidhani kuwa Field Marshall ES=Le Mutuz=w.j.malecela..... Ebu chunguzeni utetezi wa Le Mutuz juu ya umilikiwa wa mali za John Samwel Malecela....na Je utetezi huu unafaa kutumika kuelezea Mali anazomiliki Mh. Mbowe ? Utetezi huu aliutoa wakati akimjibu member wa JF aitwaye joka Kuu



Source: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-john-samwel-na-legacy-yake-9.html#post105511
 
Tufafanulie hayo mabilioni anayomiliki Mbowe ni mangapi, na kodialiyolipa ni ngapi, tueleze pia ni lini na wapi Mtei aliagiza kuwa hakuna mtu mwingine from no where kama unavyosema asiwe mwenyekiti wa chadema,vinginevyo utaonekala fara tu, mvivu wa kufikiri unaishia kusema mambo ya kusikia, kuambia,na kutaarifiwa, hivyo kuleta hoja za majungu hapa. Toa vielelezo
 
Kwani Mbowe kuwa na nyumba Dubai ni dhambi tatizo magamba mlishazoea wanasiasa masikini wa kuwapa tisheti kanga na buku tano.

MBOWE NI MFANYABIASHARA MKUBWA NDANI YA NCHI HII NA NI MLIPA KODI MZURI SANA,WEWE UNAJUA BILCANAS TU KUNA AISHI,BROTEA TANZANIA DAIMA,SAMBA LA MAUA,HISA KAMPUNI ZISIZOPUNGUA 100,MAJENGO YA KUPANGISHA,KAMPUNI YA UTALII INAYOPANDISHA WATALII MLIMA KILIMANJARO NK.USIWE MBULULA KUWA NA NYUMBA DUBAI SIO DHAMBI KAMA MTU ANALIPA KODI ZOTE ZA SERIKALI TULITEE MADA KUWA MBOWE AJALIPA KODI SIO MAMBO YA KUWA NA NYUMBA HATA FUKO ANA NYUMBA NON SENSE MACCM
 
politicians! ni wale wale hata kama wengine wana unafuu, but haya mambo ya kuwa ni tajiri na kumiliki majumba nje ya nchi kama umeyapata kihalali sawa, lkn wengine nao wakimiliki bila kuthibitisha ufisadi nao msiwalalamikie!
 

acha kelele unatakiwa kuwashukuru wachina kuwafichia ile siri yenu ya mtoto wa mfalme, si unajua naye uwa anafadhili shughuli za vijana wenu.
 
Ungetuwekea kiasi cha kodi kinacholipwa na kila kiongozi wa chama au mbunge mwenye biashara ndio tungekuwa na nafasi nzuri ya kujadili hoja na kumhukumu Mbowe.
 
Kwa mtindo huu basi kila mtu ni fisadi. Hivi maana halisi ya ufisadi ni nini ? Kuwa na mali, kuiba ama kudhulumu ? bado nimeachwa hapo
 

Hii inaitwa fishing without a bait.
 
Hakuna shetani anayefukuza mashetani, Mbowe na CHADEMA tukimbizieni hao wezi wa CCM, hatuwataki IKULU hata Saa moja baada ya 2015
 
Hicho ndo ulichoona? Mbona mabilioni ya EPA, Ndege ya Rais, Chenchi ya rada mabilioni ya Uswis husemi?
Hatuwe kijibu hoja za ufisadi kwa ufisadi. Ila ninchojua ni kwamba Mbowe katokea kwenye familia ya wenye uwezo. Baba yake alikuwa tajiri na yeye anaendeleza. Tuendelee kuchunguza, but I trust the guys.
 
Kuna tatizo gani STD Seven tena DJ kuwa na bilioni? Sasa ile taasisi ya SELF iliyoko chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais ina umuhimu gani kwa taifa? Kama ameiba mbona mahakama always ziko open? Kama kesi za ugaidi ziliweza kufunguliwa, za wizi wa mabilioni zinashindikana nini? Serikali ifungue kesi za wizi mahakamani (tena public hearing) ili watu wapeleke ushahidi wao badala ya kuwahoji watu kwa siri.
 
Hatuwe kijibu hoja za ufisadi kwa ufisadi. Ila ninchojua ni kwamba Mbowe katokea kwenye familia ya wenye uwezo. Baba yake alikuwa tajiri na yeye anaendeleza. Tuendelee kuchunguza, but I trust the guys.

Rostam Aziz ametoka kwenye familia tajiri zaidi.
 

inamaaana mbowe alizaliwa peke yake??
 

Aisee ni kweli mkuu usemacho.Heshima kwako.
 
mkuunngu007, kukimbizana na kichaa aliyekuibia taulo kutakuumiza kichwa.achana nae.
 
Nalazimika kuandika kuelezea maisha na utumishi wangu kwa umma na taifa letu, kutokana na juhudi za wahasimu wangu ku-"connecting the dots...." kumfikia Mbowe.

Inavyofahamika, nilibahatika kuteuliwa na Mwalimu Nyerere kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha 9 Septemba 19064. Binti yangu Lilian' ambaye alikuwa mtoto wetu wa pili, alizaliwa 29 Sept 1964 na ameolewa na Mbowe. Yeye Freeman alizaliwa 14 Sept., 1961 na wazazi wake walimpa jina hilo alipobatizwa siku yetu ya Uhuru, 9 Decemba, 1961.

Mwalimu Nyerere aliniteua kuanzisha sarafu yetu na Benki Kuu Octoba 1965 na shughuli za BoT zilianza rasmi tarehe 14 Juni, 1966. Niliachia u-Gavana Aprili 1974 nakawa Katibu Mkuu EAC (Phase I) Charles Nyirabu akinuridhi kama Gavana. Februari 1977 nikateuliwa Waziri wa Fedha ambapo kufuatia kutokubaliana na boss wangu kuhusu sera za fedha na uchumi, nilijiuzulu Novemba 1979 nikahamia Arusha kuwa mkulima wa kahawa 1980 mpaka leo.

Itaonekana ni upotoshaji usiopingika kwamba nikiwa Gavana 1965 hadi 1974, Freeman na Lilian walikuwa watoto wachanga wakisoma shule za chekechea na primari na wasioweza kuhusishwa na miradi.

Serikali ya Mwalimu iliniteuwa IMF Executive Director Novemba 1982, nikaweza kuhamia Washington D.C, na wanangu wakaweza kumalizia sekondari na university huko Merikani, isipokuwa Lilian ambaye baada ya sekondari aliamua kurudi Tanzania kusomea udaktari Muhimbili ambapo alifaulu vizuri sana. Nahisi ni wakati huu walifahamiana na Freeman, na wakaoana Augost 1991.

Harakati za siasa za vyama vingi zilishika kasi mwanzoni mwa 1992, Francis Nyalali alipokabidhi ripoti yake. Mimi binafsi nilijitwika mzigo wa kulea Chadema nilichoshiriki kuasisi. Nilihamia Dar es Salaam, hadi 1998, nikiishi kwa mapato yangu binafsi, nikitumia magari yangu na ya waasisi wenzangu na washaabiki wetu kuzuru na kutembelea kila wilaya Tanzania Bara isipokuwa Makete, Ngara na Ukerewe. Kila wilaya niliyozuru niliacha ofisi au tawi la Chadema. Mara nyingi nilikuwa mgeni wa wanachama wapya. Zanzibar nilizuru pia, lakini ungozi wa CDM huko ndio walisimika Chadema.

1998 niliachia uenyekiti kwa Bob Makani, ndipo nikaweza kurudia shamba na mashughuli yangu mengine. Inafahamika kwamba Freeman Mbowe aliongoza Vijana wa Chadema tangu mwanzo; na ameongoza chama kama Chairman tangu 1993, Makani alipoachia uenyekiti, na akishirikiana hasa na Dr. Willibrod Slaa wamesimika Chadema Tanzania. Najisikia raha sana na kuwa na matumaini kwamba ukombozi wetu u karibu, hasa nikiona jinsi vijana wenye uzalendo wa hali ya juu, wenye ujasiri na umakini wakimiminika kwa wingi kutuunga mkono. Kauli mbiu zetu za "Peoples' Power" na " Hakuna Kulala, Mpaka Kieleweke" zimenisisimua sana na kunipa matumaini ya Ushindi mapema.
 
Wewe sio miongoni mwa waliomshangilia Dr. Slaa alipotoa list of shame pale Mwembeyanga? Mbona unamtukana Dr. Slaa kwa post yako hii...



kwa hiyo unataka fananisha uzi wako huu na ile list? mbona liko wazi sana ya kuwa ni vitu viwili tofauti mkuu Zemarc... yako imekaa kitaarabu zaidi wakati ya Dr. ilikaa kizalendo na utaifa ndani yake.

 
Sitaki niharibu uhusiano wangu na mzee Edwin Mtei kwa ajili ya siasa;
Mzee mtei nakukukumbuka wakati wako ukijitahidi kutetea bei ya kahawa;
Ukijaribu kupita huku na huku kuokoa soko la kahawa; japo baada yako
bei ya kahawa ilianguka sana kwenye soko la dunia ikafikia hata wazee wetu
kukataa kuyaendeleza yale mashamba.

................. Nilichojihakikishia ni kwamba mke wa mbowe ni binti yako.
Hapa kwangu imenitosha kabisa.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…