Mtei amefilisika kimawazo - Zitto

Mtei amefilisika kimawazo - Zitto

Ivi unaweza kulinganisha context ya lusinde (kwenye jukwaa la kisiasa)wakati wa kampeni na Katibu mkuu wa chama alipoulizwa akadefend na mawazo ya Mtei (sio kiongozi wa chama) tena akiwa nyumbani kwake??

:focus:
Ivi kawa wewe Ritz ni mrefu nikasema wewe ni mrefu natakiwa kuomba radhi sio?? Hebu geuzia upande wa pili wangekuwa ni kina john wamezidi kwenye hiyo tume si kila ijumaa kungekuwa na maandamano?? Humu si kungekuwa hakutoshi? Shukuruni mungu huu upande wa pili kuna ustaarabu na hata mteuzi najua ameliona hilo.

Ingawa waleta thread wote wametunyima nukuu sahii ya alichokisema Mzee Mtei ili tuweze kupima context (muktadha) wa kile ambacho mzee alikikusudia kama kila chembechembe ya udini wa la hasha. Lakini kusema Zanzibar inawakilishwa na Waislamu tu kuna ubaya gani kama sio kuwa Watanzania tunataka kukuza kitu. Call a spade a spade. Ukweli unabaki palepale kuwa kati ya wajumbe wote 15 toka Zanzibar hakuna Mkristo. Huo ndio ukweli kama Wakristo wenye vigezo vya kuingia kwenye committee hawapo tumwachie aliyewateua aseme kwenye muktadha wa mzee Mtei. Wachangiaji wote pamoja na mimi hapa kwa bahati mbaya tunaangalia form of what mzee said and we are falling short of the context. Tunatakiwa tuzame kwenye context ya mzee Mtei halafu ndio tutoe mawazo ambayo contractive kewa ajili ya ustawi wa Taifa letu.

Je, tukikuta mzee alikuwa na nia nzuri tena yenye faida ya dini zote mbili tutafanyaje? Maana hizi ndio dini zenye wafuasi wengi hapa Tanzania na duniani kwa ujumla. Ni kutaka kuishi kwenye falsafa ya ngamia kuficha kichwa na hali kiwiliwili kiko nje tukifikiri kunaweza kuwa na amani bila watu wa dini hizi kukaa pamoja kwa maelewano. N amuafaka wowote ule lazima uzingati equity kwenye representation ya population ya dini hizi. Watanzania wenzangu tena wana great thinkers nafikiri mzee Mtei kuna watu wako karibu naye ebu tumwombe aeleze muktadha a kile alichokusudia. Siamini sana kuwa mzee mwenye busara na akili kama Mtei anaweza sema kitu hali mradi.

Na swala kuangalia uwakilishi wa dini lipo nchi msikatae. Mfano ambao bado upo katika kumbukumbu zetu ni pale Waziri Mkuu mstaafu-Sumaye alipounda board of parole. Ilionekana ilikuwa na Wakristu wengi. Waislamu wali raise alarm na Rais wakati huo Mkapa akaliona na akavunja ile board ya awali na kuiunda upya. Kama Wakritiu nao wanaona hakuna equal represenatation kwenye hii tume walalamike ili uwakilishi uangaliwe upya. Kunungunikia chini kwa chini sio vizuri.

Nawakilisha
 
Nioneshe popote niliponukuliwa kusema unavyosema hapa.

Sijawahi kumjibu Mtei moja kwa moja hata siku moja. Kwenye suala hili msimamo wangu niliuweka wazi hat kabla Mtei Hajasema.
Walioandika wameunganisha tu tweets zangu na kauli ya Mtei ambayo siiungi mkono hata kidogo. Mzee was mistaken.
Tume ya Katiba imeteuliwa kwa mujibu wa sheria. Haina Udini. Ina wajumbe ninaowaheshimu sana. Twende tukatoe maoni. Tuache maneno yasiyo na maana yeyote.

Mie nilijua tu haya ni maneno ya kupikwa................Bora umekuja kutuweka wazi hapa.
 
Sasa mlivyokuwa mnalalamika CCM inawatukana kumbe ni Mwigulu na Lusinde yalikuwa mawazo yao binafsi.

Mkuu pale jamaa walikuwa wanafanya kampeni kwa niaba ya CCM! Hivyo walikuwa wakiwakilisha mawazo na sera za CCM ili chama kiweze kuchaguliwa (kupitia kwa mgombea wake).
 
Zito anaweza akawa amesema ukweli kwa maoni ya watu wengi, lakini si kila ukweli unapaswa kusemwa kwa namna hii na kuwekwa hadharani. Huku ni kukosa adabu kwa hali ya juu kabisa. Ili unielewe, fikiria kwamba kuna ukweli juu ya baba au mama yako ambao watu wanaufahamu lakini ambao wewe hutapenda wauseme hadharani, japo ni ukweli.
 
Sasa mlivyokuwa mnalalamika CCM inawatukana kumbe ni Mwigulu na Lusinde yalikuwa mawazo yao binafsi.

Ok, tuchukulie kuwa Jambo Leo limetoa habari hiyo kwa ufasaha (ingawa bado si la kuaminika); Unaweza kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Mtei?
Hiyo habari (kama ni ya kweli) Mtei kazungumza nyuma ya pazia maana, wakati Lusinde kazungumza mbele ya kadamnasi (in public).
 
Kuna jambo moja linalonivutia kuhusu Waislam. Siku zote wanapopenyeza mambo yao ukiwasema mara moja huishia kudai una udini!!
Kumbuka habari ya yule mkuu wa wilaya; Kumbuka habari ya JK kushindwa kudhibiti matumizi [wanamsema kwa sababu ni muislam-Masheikh].
Binafsi nitaamini kuwa tume haina sura ya udini pale watakapoacha kuchomeka kwenye katiba mambo ya OIC na Kadhi
 
Ingawa waleta thread wote wametunyima nukuu sahii ya alichokisema Mzee Mtei ili tuweze kupima context (muktadha) wa kile ambacho mzee alikikusudia kama kila chembechembe ya udini wa la hasha.
Hiki ndicho alichokisema Mtei, tafakari
Licha ya kwamba J.K. kajitahidi kuwa na vigogo kweli kweli, na Katiba ya sasa imezingatiwa ktk kuandaa m'badala wake, muundo wa hii Tume umedhihirisha kwamba demokrasia ya kweli ni ndoto kwa Watanzania wa leo. Kama tunanuia kwa dhati kuwa na Demokrasis ya kweli, itabidi Watanzania wanaoamini kwamba hilo ni muhimu, waendelee na juhudi za kuandaa hata Mabadiliko kwa Katiba Mpya ijayo.

Kwa mfano ni jambo la kichekesho kwamba Tanzania Bara ambayo ina Watu takriban 42 milioni iwakilishe na wajumbe sawa na Tanzania Zanzibar ambayo ina watu wasiozidi 1.5 milioni. Mfano wa pili ni kwamba, licha ya kwamba Tanzania siyo nchi inayozingatia dini katika maamuzi yake ya kisiasa, ni lazima tukubali kuwa madhehebu ya dini yana influence katika mchakato na hatimaye maamuzi. Nikihesabu Waislamu katika hii Tume kwa kuzingatia majina naona zaidi ya theluthi mbili ni Wao. Wengine ni Wakristo au watu wasiokuwa na dini yoyote.

Hata kama ni lazima tujali Muungano wa Jamhuri yetu, hatuwezi kupuuza ukweli kuwa sasa kuna matatizo ya umilikaji wa raslimali maliasili (e.g. gas), na kuna wananchi wamediriki hata kwenda Umoja wa Mataifa kudai Zanzibar ijiondoe.

Haya ni mambo mazito na nimeona ni vema niyataje sasa, siyo tu yajadiliwe na Tume, bali ikiwa ni lazima, basi mjadala uendelee hata baada ya Tume kutoa taarifa na Bunge Maalum kupitisha Katiba Mpya.
 
Nioneshe popote niliponukuliwa kusema unavyosema hapa.

Sijawahi kumjibu Mtei moja kwa moja hata siku moja. Kwenye suala hili msimamo wangu niliuweka wazi hat kabla Mtei Hajasema.
Walioandika wameunganisha tu tweets zangu na kauli ya Mtei ambayo siiungi mkono hata kidogo. Mzee was mistaken.
Tume ya Katiba imeteuliwa kwa mujibu wa sheria. Haina Udini. Ina wajumbe ninaowaheshimu sana. Twende tukatoe maoni. Tuache maneno yasiyo na maana yeyote.
Mkuu zito watu wanataka wakutumie kama daraja la mfarakano ndani ya chama chetu CDM hao wote ni magamba na bora umesema wewe Mzee Mtei was mistaken nakuunga mkono mia kwa mia. naona baada ya kujibu magamba wote wamekimbia kutafuta thread nyingine za uchochezi wameangukia pua
 
Ritz na Rejao kuna thread nyingine inayosema "Nassari hajaonekana bungeni kuapishwa" nenda mkachangie na huko kwasababu ndio mnazo zipenda
 
zito sasa anakoelekea siko,huwa simuamini kwenye mambo yake.amekaa kishushu na kauli zake zenye contradictions
 
Kwani kauli ya Mtei ndio kauli ya Chadema?? Nadhani hayo yalikuwa ni mawazo yake binafsi, na pia Zitto yupo sahihi kabisa.
 
Jamani kwani katika sheria inayoongoza kwenye haya, kuna kipengele kinachobainisha idadi ya wajumbe na sifa zao? Kama nakumbuka vizuri issue ilikuwa kutoruhusu rais achague wajumbe kama anavyotaka yeye!!! Wakakubaliana na CDM rais apelekewe orodha inayojumuisha wajumbe watarajiwa kutoka katika makundi tofauti tofauti, lakini hakubanwa aangalie pia dini!!!

Hebu tusaidiane hapa...
 
Kuna mambo ya msingi lazima tuyaelewe kwenye decision-making process. Reasonable and rational people reach their deliberations by argumentation without being influenced by personal interests and values. The convincing arguments prevails and the weak ones are abandoned along the way. Swali la kujiuliza je kwa mazingira yetu ya Tanzania, do we have people who act free of their vested personal interests, be it religious beliefs, political ideologies etc? Decision-makers wa Tanzania wanaweza kuitwa rational and reasonable?

Reasonable people are those who take into account the interests of others in the pursuit of their ends, they are impartial individuals. Rational people are those who opt for the most effective means to achieve certain goals. Issue nzima inakuwa ngumu zaidi kama maamuzi ya tume katika hayo watakayokuwa wanayajadili yatakuwa yanafikiwa kwa njia ya kupiga kura badala ya mtu kuwa convinced na arguments. Kwa urahisi tu ni kwamba religious believes will distort peoples thinking and will influence many issues related or connected directly or indirectly to religion. Kwa mfano mtakuja kuona kuwa katiba ijayo itakuwa na vitu kama hivi: Raisi akitoka Tanganyika makamu atoke Zanzibar, Zamu hii Raisi akitoka Tanganyika wakati ujao ni zamu ya Zanzibar, mbaya zaidi ni issues kama mahakama za kadhi kuingizwa kwenye katiba japokuwa nchi haina dini na haiendeshwi kwa misingi ya dini.

Kwa wanaom beza Mtei, he has a point japokuwa ameipresent in a very radical way. Tume lazima ifanye kazi bila kuwa polarized with values which are deeply seated to its members, which inmy opinion is very difficult in Tanzania settings. Imagine issue ya mahakama za kadhi itakavyopolarize tume, hili tutalishudia muda si mrefu na kwa namna tume ilivyo you can even tell what will happen if and only if members are not rational and reasonable.Na solution yake sio kuwa na tume yenye uwiano wa kidini bali wahusika wasahau dini zao na maslahi yoyote, watengeneze draft as if nchi hii haina dini wala kabila wala political ideologies etc.

Kama Mh Zitto kasema Mtei kafilisika kimawazo, nafikiri yeye ndio hajataka kutumia akili yake in its full capacity to see the obvious. We will be lying ourselves if we believe the commitee members will act free of their long standing beliefs and values. These are kind of difficult issues which need alot of thinking and not giving simple solutions.
 
Zitto anaivuruga CDM, au chadema inamvuruga zitto?? Zitto anapanbana na maadui zake ndani ya chadema wasiotaka kuona chama kinatoka minoni mwa wenye malengo !! Mtoeni zitto ili chama chuenu kife ili tanzania iendelee kuwa na amani
Sidhani? CDM kufa kwa ajili ya mabishano ya Mtei na Zitto. Kwani kusema waislamu wengi ni Kosa? ni mawazo yake! tujiulize kwani Zanzibar wakristu ni wawili tu? ukiangalia Mkuu anapenda kubalance, mara dini mara jinsia. Mimi naudhani akiangalia utendaji hata wawe waislamu wote ama wakristu ili mradi wanabeba Maslahi ya nchi hii hamna shida. Kwani katiba ni Imani? Katiba ni makubalianao yanayotekelezeka na kuhakikiwa. Imani zetu za dini zinapangika lakini hazihakikiki. Unaweza kusema kwamba mtu akitenda mema anakwenda Akhera ama Mbinguni, ama anakwenda kuonana na Yesu na Bikira Maria, Je nani anaweza kuthibitisha kuwa utaonana nao. Lakini Katiba 2nahitaji watu watakaosema haka ka nchi na watu wao watawezaje kuishi kwa amani na kuheshimu sheria? Lakini ni lazima kuwa makini na chaguzi zinazoweza kuzaa mashaka.
 
Mbunge wa Kigoma Kaskazini-CDM amesema Mzee Edwin Mtei amefilisika kimawazo kwa kauli yake kwamba tume ya Katiba ina Waislam wengi kuliko wakristo.

Source:JAMBO LEO.

Hivi Zitto ni dini gani??? Tunajua ni Mwislamu. Kwa kawaida ya Waislamu ni watu wenye munkari,chuki,hasira na wasio wavumilivu. It is the same spirit of Islamic religion trying to defend its dominion.

Zitto ni kiongozi mwenye jazba za kipuuzi. Zitto ni Mropokaji na hana subira. Zitto ni mtaka sifa na kujikweza kuliko hata viongozi wake ndani ya Chama. Zitto ni Kafulila type,no difference.Kuropoka kwamba ati Mtei amefilisika kimawazo kwa mtazamo wake kuhusu Wajumbe wa Tume ya Katiba siyo sahihi. Hii ni DHARAU KUBWA SANA KWA MWASISI WA CHADEMA. Kuna haja ya kumfuatilia Zitto kwa karibu ili kujua kwanini huwa anapenda kutoa KAULI ZENYE UTATA NDANI YA CHAMA. Juzi tu tumesikia anadai kugombea Urais wa nchi hii mwaka 2015! Yawezekana kabisa Zitto anatumiwa na Chama Cha Magamba-CCM kutaka kuivuruga CHADEMA. Tulishasikia habari za yeye Zitto kuwa karibu sana na baadhi ya Vigogo wa Serikali akiwemo Rais Kiwete!

Kila mtu anakumbuka Zitto alipokataa kuunga mkono Walk out ya Wabunge wa CDM mwaka 2010 wakipinga kuburuzwa na CCM na Katiba mbovu ya nchi.Zitto ni wa ku-watch out. Huyu jamaa anaweza kukisambaratisha chama in future asipoangaliwa na kudhibitiwa. Tuanomba Mhe. Mbowe na Dr. Slaa wamemfuatile Zitto nyendo zake.Shame on him!
 
Hivi Zitto ni dini gani??? Tunajua ni Mwislamu. Kwa kawaida ya Waislamu ni watu wenye munkari,chuki,hasira na wasio wavumilivu. It is the same spirit of Islamic religion trying to defend its dominion.

Zitto ni kiongozi mwenye jazba za kipuuzi. Zitto ni Mropokaji na hana subira. Zitto ni mtaka sifa na kujikweza kuliko hata viongozi wake ndani ya Chama. Zitto ni Kafulila type,no difference.Kuropoka kwamba ati Mtei amefilisika kimawazo kwa mtazamo wake kuhusu Wajumbe wa Tume ya Katiba siyo sahihi. Hii ni DHARAU KUBWA SANA KWA MWASISI WA CHADEMA. Kuna haja ya kumfuatilia Zitto kwa karibu ili kujua kwanini huwa anapenda kutoa KAULI ZENYE UTATA NDANI YA CHAMA. Juzi tu tumesikia anadai kugombea Urais wa nchi hii mwaka 2015! Yawezekana kabisa Zitto anatumiwa na Chama Cha Magamba-CCM kutaka kuivuruga CHADEMA. Tulishasikia habari za yeye Zitto kuwa karibu sana na baadhi ya Vigogo wa Serikali akiwemo Rais Kiwete!

Kila mtu anakumbuka Zitto alipokataa kuunga mkono Walk out ya Wabunge wa CDM mwaka 2010 wakipinga kuburuzwa na CCM na Katiba mbovu ya nchi.Zitto ni wa ku-watch out. Huyu jamaa anaweza kukisambaratisha chama in future asipoangaliwa na kudhibitiwa. Tuanomba Mhe. Mbowe na Dr. Slaa wamemfuatile Zitto nyendo zake.Shame on him!

We mgeni chadema ZITTO ndiye aliyekijenga chama, hao wakina slaa ni wageni chadema,
Zitto ana haki ya kumkosoa MTEI kwa kukiharibu chama.
Zitto anapaswa kupongezwa kwa kukemea maovu katika chama bila kujali superiority ya mtu.
 
We mgeni chadema ZITTO ndiye aliyekijenga chama, hao wakina slaa ni wageni chadema,
Zitto ana haki ya kumkosoa MTEI kwa kukiharibu chama.
Zitto anapaswa kupongezwa kwa kukemea maovu katika chama bila kujali superiority ya mtu.

Pumba za mafisadi wa chama cha magamba zinachekesha sana
 
Jamani kwani katika sheria inayoongoza kwenye haya, kuna kipengele kinachobainisha idadi ya wajumbe na sifa zao? Kama nakumbuka vizuri issue ilikuwa kutoruhusu rais achague wajumbe kama anavyotaka yeye!!! Wakakubaliana na CDM rais apelekewe orodha inayojumuisha wajumbe watarajiwa kutoka katika makundi tofauti tofauti, lakini hakubanwa aangalie pia dini!!!

Hebu tusaidiane hapa...

Mkuu upo sahihi!
Tatizo limekuja kutokea baada ya baadhi ya watu kama Mzee MTEI kuona maslah binafsi yake hayatotimizwa! Hili ni tatizo kwa kuwa sisi tunaangalia maslah ya TANZANIA sio ya mtu binafsi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom