mzee mwanakijiji
huu mjadala ungeweza kabisa kuwa mzuri sana na wa kiakili kama watu wataondoa madongo ya kidini na badala yake tuangalie tu ushahidi wote uliopo na kujaribu kuangalia tufanye nini mbele. Binafsi kuna mambo ambayo kwa kweli kabisa naona ni sehemu ya tatizo zima. A
1. Serikali ilifanya makosa sana kuanza utaratibu wa kurudisha mashule na taasisi za dini ambazo zilitaifishwa na nyerere. Nyerere alipotaifisha shule na hospitali n.k alikuwa na sababu na sababu yake ni kuhakikisha kuwa kunakuwa na nafasisawa zaidi za watu kupata elimu na hata ajira n.k inawezekana labda kuna taasisi fulani zingetaifishwa lakini ninaamini ulikuwa ni uamuzi sawasawa. Kwa serikali kurudisha shule kwa mashirika ya dini kimsingi ni kurudisha status quo ya 1967 na ambayo kimsingi iliwapendelea wakristu. Lakini kurudisha status quo ya 1967 ni kurudisha status quo ya 1958 ambayo iliwapendelea wakristu. Kurudisha statuq quo ya 1958 ni kurudisha status quo ya 1940s ambayo iliwapendelea wakristu. Binafsi naamini kwa hili serikali imeenda kinyume kabisa na lengo la kuleta usawa zaidi.
2. Uamuzi huo wa kurudisha mashule na hospitali kwenye taasisi za kidini ulivyofanya na serikali umekuwa na matokeo yake yale yale ambayo yangeweza kutabirika. Taasisi za makanisa za elimu na afya ni nyingi zaidi kuliko zile za misikiti au taasisi za kiislamu.
na uchunguzi mwingine unaonesha kuwa idadi ya wanafunzi wa kikristu kwenye shule za kiislamu ni kubwa zaidi kuliko idadi ya wanafunzi wa kiislamu kwenye shule za kikristu kitu ambacho bado kinaendeleza ile ile status quo.
Haya mawili yanalazimisha kujiuliza ni njia gani basi inafaa kuanglaia hili la imbalance katika fob initiatives nchini?
1. Radical secularism?
Kuna watu wengi ambao hawataki fedha ziende kwenye huduma za kijamii kupitia taasisi na hasa kwenda kwa njia ya makanisa - kama mou inavyoonesha. Hii ni hoja nzuri lakini ni lazim iende kwenye hitimisho lake. Aidha serikali iwe tayari kutoa ruzuku kwa taasisi nyingine za kidini na kwa uwiano unaoendana na shughuli za taasisi hizo au ijitoe kabisa ili kutoonesha kupendelea dini moja au dhehebu moja. Kwenye nchi ambapo makanisa yana shule nyingi na hospitali nyingi ni wazi - haiitaji sayansi ya fizikia kuliona - fedha nyingi zitaenda kwenye taasisi hizo kama inakubaliwa kuendelea na mfumo huu. Njia pekee ni aidha serikali itaifishe na ihudumie taasisi hizo yenyewe na kuzifanya za umma kitu ambacho kitarudisha madai yale yale. Lakini haiwezi kufanya hivyo kwa dini moja bila kufanya kwa dini nyingine. Njia nyingine ni kuwa serikali iseme tu kuwa inajitoa kabisa katika kuchangia moja kwa moja katika gharama za taasisi za kidini zinazotoa huduma ya kijamii. Kila taasisi ijitegemea kabisa kutafuta misaada yake na kujiendesha bila kutegemea serikali kabisa.
je uamuzi huo utamnufaisha nani hasa katika nchi ambayo tayari makanisa yako mbele katika utoaji wa hizo huduma?
2. Affirmative action
kwa vile tayari tunajua kuwa kuna imbalance hii ambayo is historical in nature je ipo haja ya kuanzisha programu ya upendeleo maalum kwa waislamu ili kuongeza idadi ya taasisi zao na wanafunzi katika shule mbalimbali? Je, upendeleo wa namna hiyo unakuwaje kwenye maeneo sema kwa mfeano yenye waislamu wengi tayari au yale yenye waislamu wachache? Na katika kutoa upendeleo huo ni taasisi gani za kiislamu zitakuwa zinahusishwa? Je, ukija na affirmative action unafanya vipi katika ajira kwa mfano ambapo watu wenye elimu sawa na uzoefu sawa wanaomba kazi? Je muislamu apewe nafasi hiyo based on affirmative principle? Na utajuaje kama kiwango cha parity kimefikiwa? Je hii affirmative inahusiana vipi na minority groups? Kwa mfano wahindi, waharabu na baadhi ya makabila nchini yako under-represented katika taasisi mbalimbali za umma je tuna recruit vipi? Inakuwaja kama makabila hayo ni predominantly christian au traditionalist? Na ukianzisha affirmative action itaendelea kwa muda gani kwani haiwezi kuendelea indefinitely.
Lakini tatizo la affirmative action kama ilivyo kwenye baadhi ya nchi ni kuwa matokeo yake yasiyotakiwa ni reverse discrimanation. Kwa mfano, ukianza kuonesha upendeleo wa pekee wa waislamu au watu wa eneo fulani siyo kwamba utaanza kubagua watu wengine huku ukidai kuwa unajaribu kuondoa ubaguzi mwingine? Kwa mfano, ukisema wakristu wasiajiriwe mahali fulani kwamba kiwango hao kimezidi au wachagga wasiajliwe siyo kwamba utakuwa unawabagua wakristu na wachagga? Unaweza vipi kuoanisha basi dhana yako ya kuondoa ubaguzi kwa kutumia ubaguzi mwingine?
Hapa ndipo tunaitwa kutumia uwezo wwetu wa kufikiria na kuona ni jinsi gani tunataka kujenga jamii ya watu walio huru na sawa, wasioonewa au kuonea wengine? Ni vipi tunaweza kujenga jamii ambayo hakuna mtu anayejiona duni au kufanywa duni na watu wengine kwa sababu ya rangi, kabila, au dini yake?
Source:
https://www.jamiiforums.com/jamii-i...atoliki-na-taasisi-nyingine-za-kidini-36.html