Mtei amefilisika kimawazo - Zitto

Mtei amefilisika kimawazo - Zitto

we Ben ebu acha kujitoa ufahamu..we unafananisha OIC na Vatican?kwa oic ni nchi!mbona tuna uhusiano wa kibalozi na Iran na Saudi Arabia nchi za kiislamu na mioyo yetu myeupe,ndio kama kuwa na uhusiano na Vatican nchi ya kikristo..hapa ishu ni nchi yenye wakristo 70% kuwa mwanachama wa jumuia ya nchi za kiislamu ilo atuwezi kukubali kwani hii nchi sio ya kiislamu.

Mahakama ya kadhi wala hatuwakatazi kuanzisha ata leo wakitaka,si ata mwenzao Jk ameshawaruhusu...tatizo wanataka eti igharamiwe kwa kodi za wananchi ambao asilimia kubwa ni wakristo..ilo atuwezi kukubali kodi zetu zikagharamie IBADA ya kiislamu......wamezugazuga na uyo jk wao wameona hii ndio sehemu ya kukamilisha mission yao..mbona kitaeleweka tu na sisi safari hii tutawaonyesha ubavu wetu,tumeshawanyamazia sana.

Alafu hapa hakuna mtu anaemchukia mtu kwa Dini yake wala Kabila,mtu anachukiwa kwa UNAFIKI wake.

Mkuu Ma2mbo,
Naomba utupe source za hizo takwimu zako za 70% Wakirsto...Waislam ni asilimia ngapi na wasiokuwa na dini ni asilimia ngapi kwa faida ya JF tufahamishe.
 
sasa mlivyokuwa mnalalamika ccm inawatukana kumbe ni mwigulu na lusinde yalikuwa mawazo yao binafsi.
tofautisha mawazo na matusi; mtu hawezi kuhukumiwa kwa kutoa mawazo lakini ccm imekumbatia mafisadi japo inayajua; waachieni chadema wapambane nao.
 
Tuache wananchi waamue.Competency ya wajumbe itumike intellectually bila kuwa biased na imani zao.Kama ingekuwa ni maoni basi maoni yangu ni kwamba serikali iruhusu mahkama za kiimani ila Fedha za walipa kodi zisitumike.

Balozi za Vatican,Saudia,Iran,Malaysia,Pakistan,Israel n.k hazina tatizo.Vatican na Iran ndiyo the only theocracies zinazo-exist so far.Zinaongozwa na viongozi wa kidini.Zinatambulika kwenye sheria za kimataifa.Lateran Pact 1929 kati ya VATICAN na Mussolin iliingiza moja kwa moja VATICAN kwenye utambulisho.Hadi sasa mataifa zaidi ya 200 yana uhusiano wa kidiplomasia na VATICAN,kodi za wananchi wa mataifa husika zinatumika kulipia watumishi wa ubalozi kule vatican zikiwemo kodi za raia ambao ni waumini wa kiislam au wasio na dini.Suala la VATICAN limehusishwa na kujiunga na OIC.Hebu soma maandishi kwa utulivu.

Hizi chuki za kidini zinatuonyesha jinsi waafrika tunavyovamia imani kizuzu tu. Watu haangalii competency ya mtu tunaanza kuangalia imani zao.Ningefurahi sana kama watu wangejenga hoja za msingi kuhusu uwezo wa wajumbe,imani (confidence) kwa wajumbe,uhalali wa kisheria kwa tume kufanya kazi chini ya muongozo wa katiba hii inayompa Rais Mamlaka ya ki-mungu mtu katika mchakato mzima wa katiba

Hivi mbona Tanzania ina uhusiano wa kidiplomasia na VATICAN?Mbona hatupigi kelele?

Tukuelewe vipi? Mbona unauma na kupuliza? Hilo suala la Vatican limehusishwa kujiunga na OIC na nani? Unaishi wapi Tanzania ambako husikii/huoni jinsi udini ulivyoishaota mizizi? Hilo la kodi za waislamu kuwalipia watumishi wa ubalozi wao Vatican linahusiana nini na topic hii?

Unataka tuzungumzie competence ya hao wajumbe. Tutazungumzia based on what? Ushiriki wao katika kuandika Katiba nyingine? Si nyinyi ambao mnadai kuwa Justice si itendeke tu bali ni lazima ionekane kutendeka. Unadhani tume kama hii, hata ikifanya mchakato diligently, kwa uhaki kabisa halafu wakaja na hoja kuwa wananchi wanataka Mahakama ya Kadhi itambulike kikatiba watakuwa na credibility yeyote?

Mahakama ya Kadhi ilikuwepo wakati wa ukoloni kwa sababu tu mhimili mkubwa wa taifa hili alikuwa Malkia wa Uingereza, Mkuu wa Church of England. Kwa wao kilikuwa kitendo cha appeasement ambacho walijua hakina uwezo wa kuathiri utawala wao. Vile vile nchini Kenya, ambako the great majority ni wakristu. Kwa wao, hakuna uwezekano wa chombo hicho kuonekana kama Trojan Horse ya Islamization ya taifa lao.

Sisi ni tofauti. Hasa bara, ambako tumeoleana, tumezaa pamoja na tunaishi katika delicate balance ambapo tukifanya mchezo mmoja wetu anaweza ku-tip the scales upande wake. Tofauti na wakati wa ukoloni au kwa jirani zetu, ni wachache sana kwetu ambao hawana ndugu, rafiki au jirani asie wa dini nyingine. Katika mazingira kama hayo secularism ni imperative. Ndio maana tunasema Mahakama kama hii iundwe nje ya mfumo wa serikali. Mahakama ya kitaifa ni lazima itoe haki sawa kwa raia yeyote bila kujali dini, rangi au jinsia yake. Upendeleo uolewe kwa wale tu ambao sisi sote kama taifa tunakubaliana kuwa wanahitaji kulindwa, k.m wenye ulemavu na watoto.

Badala ya kumkebei Mtei, inabidi tumshukuru kwa kuzungumzia huyo tembo aliye katika sebule yetu. Si kwenye udini tu bali katika uwakilishi wa pande mbili za Muungano. Ni kujidanganya kuwa Muungano wetu uko imara wakati wenzetu wamegeuza Bunge lao kuwa sehemu la kuelekeza mapigo dhidi ya wale wanaowaita machogo. Tatizo si Jussa kuwaita watanzania bara wageni bali ni kwa kiasi gani hoja yake ilikubalika na kuungwa mkono na wenzie bila kujali itikadi zao!

Hap tunazungumzi tume itakayotuongoza katika kupata sheria mama ya taifa letu, sio viranja au wajumbe wa bodi za mashirika. Ni lazima tuzungumzie kwa undani yale yote ambayo tunadhani yanaweza kutufanya tukose imani na uongozi wao, udini na mustakabali wa Muungano vikiwemo.

Amandla.......
 
19 vs 11.

Sawa 19 ni kubwa, lakini je, ingekua 15 vs 15, kuna nini la maana kwa taifa? kwani wanaenda kupigia kura vifungu vya katiba? wanaoingiza udini wanachemka na wanaosisitizia (kwa njia ya kukosoa) pia wanachemka.


Samahani sana, Hivi Kafulila yuko wapi?
 
Tukuelewe vipi? Mbona unauma na kupuliza? Hilo suala la Vatican limehusishwa kujiunga na OIC na nani? Unaishi wapi Tanzania ambako husikii/huoni jinsi udini ulivyoishaota mizizi? Hilo la kodi za waislamu kuwalipia watumishi wa ubalozi wao Vatican linahusiana nini na topic hii?

Unataka tuzungumzie competence ya hao wajumbe. Tutazungumzia based on what? Ushiriki wao katika kuandika Katiba nyingine? Si nyinyi ambao mnadai kuwa Justice si itendeke tu bali ni lazima ionekane kutendeka. Unadhani tume kama hii, hata ikifanya mchakato diligently, kwa uhaki kabisa halafu wakaja na hoja kuwa wananchi wanataka Mahakama ya Kadhi itambulike kikatiba watakuwa na credibility yeyote?

Mahakama ya Kadhi ilikuwepo wakati wa ukoloni kwa sababu tu mhimili mkubwa wa taifa hili alikuwa Malkia wa Uingereza, Mkuu wa Church of England. Kwa wao kilikuwa kitendo cha appeasement ambacho walijua hakina uwezo wa kuathiri utawala wao. Vile vile nchini Kenya, ambako the great majority ni wakristu. Kwa wao, hakuna uwezekano wa chombo hicho kuonekana kama Trojan Horse ya Islamization ya taifa lao.

Sisi ni tofauti. Hasa bara, ambako tumeoleana, tumezaa pamoja na tunaishi katika delicate balance ambapo tukifanya mchezo mmoja wetu anaweza ku-tip the scales upande wake. Tofauti na wakati wa ukoloni au kwa jirani zetu, ni wachache sana kwetu ambao hawana ndugu, rafiki au jirani asie wa dini nyingine. Katika mazingira kama hayo secularism ni imperative. Ndio maana tunasema Mahakama kama hii iundwe nje ya mfumo wa serikali. Mahakama ya kitaifa ni lazima itoe haki sawa kwa raia yeyote bila kujali dini, rangi au jinsia yake. Upendeleo uolewe kwa wale tu ambao sisi sote kama taifa tunakubaliana kuwa wanahitaji kulindwa, k.m wenye ulemavu na watoto.

Badala ya kumkebei Mtei, inabidi tumshukuru kwa kuzungumzia huyo tembo aliye katika sebule yetu. Si kwenye udini tu bali katika uwakilishi wa pande mbili za Muungano. Ni kujidanganya kuwa Muungano wetu uko imara wakati wenzetu wamegeuza Bunge lao kuwa sehemu la kuelekeza mapigo dhidi ya wale wanaowaita machogo. Tatizo si Jussa kuwaita watanzania bara wageni bali ni kwa kiasi gani hoja yake ilikubalika na kuungwa mkono na wenzie bila kujali itikadi zao!

Hap tunazungumzi tume itakayotuongoza katika kupata sheria mama ya taifa letu, sio viranja au wajumbe wa bodi za mashirika. Ni lazima tuzungumzie kwa undani yale yote ambayo tunadhani yanaweza kutufanya tukose imani na uongozi wao, udini na mustakabali wa Muungano vikiwemo.

Amandla.......


Duh,

Naelewa ni ngumu kwako kuwa objective kwenye mjadala kama huu ulioburuza watu wengi kuingia kwenye hisia

Hivi mkuu huoni connection yoyote ya VATICAN,OIC na labda ili uelewe vizuri Jumuiya ya Madola ambayo mkuu wake ni Malikia ambaye ni mkuu wa kanisa la Anglican?Waislam wakijenga hoja katika ulinganisho huo bado hutaelewa?
 
Duh,

Naelewa ni ngumu kwako kuwa objective kwenye mjadala kama huu ulioburuza watu wengi kuingia kwenye hisia

Hivi mkuu huoni connection yoyote ya VATICAN,OIC na labda ili uelewe vizuri Jumuiya ya Madola ambayo mkuu wake ni Malikia ambaye ni mkuu wa kanisa la Anglican?Waislam wakijenga hoja katika ulinganisho huo bado hutaelewa?

Hivi ni nini kirefu cha OIC ?
 
Hivi ni nini kirefu cha OIC ?

Molemo,

Hata hili unauliza?basi ndiyo maana hapa watu hawataelewana......

Tafadhali hebu soma international treaties halafu concentrate kwenye Concordats kwa Holy Sea-vatican halafu usome maudhui ya OIC ili uwe objective katika michango yako yako kaka
 
Molemo,

Hata hili unauliza?basi ndiyo maana hapa watu hawataelewana......

Tafadhali hebu soma international treaties halafu concentrate kwenye Concordats kwa Holy Sea-vatican halafu usome maudhui ya OIC ili uwe objective katika michango yako yako kaka

Mkuu Ben,
Itakuwa ni ngumu mno kwa maana kuna wenzetu wanakuwa radicals kiasi kwamba ni muhimu kwao kujenga upinzani dhidi ya hoja badala ya kujenga hoja dhidi ya hoja yenyewe(fact to fact). Imagine, watu wanajiandaa kupinga jambo ambalo hata halijawasilishwa.! Tunawachagulia watu maoni au mchango wa kutoa kwenye katiba mpya! Nauliza,hii ndio katiba mpya wanayoitaka watanzania? Katiba ya kuwachagulia watanzania mambo ya kusema, au kufikiri? Katiba iliyotanguliza siasa,ubinafsi,ukabila,udini mbele ya uzalendo na utaifa?. We still have a long way to go. And this explains why akitokea mpinzani akikubali jambo,au kwa katoa mawazo yanayoshabihiana na fulani,hata kama kuna mantiki,tunamshangaa na kumtukana kwa nini kakubali,eti kwa kuwa yeye ni mpinzani!!
 
Mnatuchanganya na sio adabu kujibishana hadharani, kwani hamna vikao vyenu mkayaongea, CDM toeni msimamo wenu kuhusu tume na awepo msemaji mmoja sio kila mtu anajidai ana uhuru wa kuongea kama kila mtu ana mawazo yake anzisheni vyama tofauti, kwa kuwa chama cha siasa ni watu wenye mtizamo mmoja wamekutana na kuanzisha chama, msituchanganye.
 
Kama ni kweli Mzee Mtei aliongea kauli hiya ya idadi ya Waislam basi amepotoka kweli!!! Hivi Dr Salim ana idenity ngapi?
Sasa tuanze kuzungumzia pia idadi ya Wanawake.

Mimi si mwanachama wa Chadema wala chama kingine chochote cha siasa. Lakini naegemea upande wa Chadema. Mzee Mtei hata kama si kiongozi lakini anabeba ngao ya uasisi na ushawishi mkubwa juu ya taswira ya Chadema. Sasa, ikiwa nitajiridhisha kuwa mtazamo wa Mzee Mtei ndiyo mtazamo wa wengi wa viongozi wa Chadema pamoja na wanachama wake basi nitaondoa moyo wangu toka Chadema (Na sitaunga mkono wezi (CCM)). Najua kura yangu ni moja tu lakini Chadema hawataistahili.
 
Kama source ni Jambo leo si shangai hilo ni gazeti la magamba hawana cha kuandika zaidi ya kutafutia wenzao chokochoko
 
Wakuu zangu nitawapa majibu yote ktk maswala haya kikatiba..Na nataka muelewe vema kwamba SIKUBALINI na Mahakama ya Kadhi kwa sababu tofauti kabisa na hizi mnazoandika hapa japokuwa waislaam wanayo haki ya kudai mahakama ya kadhi. Nawaomba sana mfahamu kwamba tunaongozwa na katiba na ndio maana Zanzibar wanayo mahakama ya kadhi kama katiba inakataza Zanzibar wasingekuwa na mahakama hiyo kwa sababu sehemu ya tatu ya katiba ni swala la muungano..

Nitarudia tena kusema mahakama ya kadhi sio serikali ni muhimili wa Mahakama ambao hauna mahusiano kabisa na serikali isipokuwa kikatiba na KATIBA ya Juamhuri inasema wazi ktk sehemu ya tatu - haki ya Usawa kifungu cha 6 a) kinasema hivi:- 6) Kwa madhumuni ya kuhakikisha usawa mbele ya sheria, Mamlaka ya Nchi itaweka taratibu zinazofaa au zinazozingatia misingi kwamba -
(a) wakati haki na wajibu wa mtu yeyote vinahitaji kufanyiwa uamuzi wa mahakama au chombo kinginecho kinachohusika, basi mtu huyo atakuwa na haki ya kupewa fursa ya kusikilizwa kwa ukamilifu, na pia haki ya kukata rufaa au kupata nafuu nyingine ya kisheria kutokana na maamuzi ya mahakama au chombo hicho kingenecho kinachohusika.

Kwa hiyo kutokuwepo kwa mahakama ya kadhi huku Bara ni kutokana na upinzani tu wa kijinga ambao unafanywa na baadhi wakristu kwanza haiwahusu. Pili, hakuna mahala popote ndani ya katiba iliyopo kunapokataza kufunguliwa kwa OIC au mahakama ya kadhi isipokuwa ni pingamizi linalotokana na UDINI tulonao kama mnavyotaka kuwaingilia hata Zanzibar wachague wajumbe wakristu wakati hawana wajumbe hao, haiwahusu na wala hamuwezi kuwataja mnaowataka kutoka Zanzibar ni kina nani. Hawasaidii kitu isipokuwa kupinga tu maadam ni cha waislaam wakati bara mna wajumbe wengi wakristu hamjasikia hata Muislaam mmoja akilitazama hilo kama ni kosa...tunawaamini kina Warioba, Beregu, Butiku, Jaji Augustine na wengineo kusimamia maslahi ya bara.

Naanza kuamini kwamba kumbe kweli kuna MFUMO KRISTU ktk utawla wetu na sasa hili swala la katiba mpya linaanza kuwagusa. haiwezekani watu muanze kushuku uchaguzi huu wakati sheria inasema wazi kwamba wajumbe wa Zanzibar watapatikana kutokana na ushauri kutoka kwa rais wa Zanzibar, na hawa ni wazanzibar wanaowakilisha upande mmoja wa Muungano ambao unahusika sana ktk utunzi wa katiba ktk maswala yasiyo ya muungano na yaliyo ya muungano.. Katiba yetu inagusa sehemu zote hizi mbili muhimu na sio dini za watu lakini watu mnataka kulazimisha iwe swala la kiimani kwa sababu pengine huko nyuma mlitumia sana imani zenu. katiba ni katiba tu haijalishi kama taifa lina watu millini moja au 40 maneno yatakuwa yale yale kinachotuunganisha sote ni Muuungano wa nchi mbili sio idadi ya watu.
 
Wakuu kama haya ndio mawazo ya wasomi walioko kwenye bunge la JF basi kuna haja kubwa sana ya wazo la Mzee Mtei kufanyiwa kazi haraka iwezekanavyo kabla mambo hayajaharibika zaidi. Kwa bahati mbaya sana wengi wa waislamu wanashare this misconception, kwao kuliko KCMC, Bugando, Marangu, Haydom, Huruma na hospitali nyingine nyingi zinazoendeshwa na makanisa ziwepo ni afadhali zifutwe tukose wote, hata kama hospitali hizi zinahudumia wenye dini na wasio na dini. Huu ni ulimbukeni na ndio unaofanya wengi wetu tuwe na shaka na tume iliyoundwa. Whats wrong to have religious institutions which provide healthcare services to all citizens without religious discrimination? What is preventing our muslim brothers to build a referal hospital in Dodoma so that we wananchi from central areas of the country can have these kind of services too? Kama thinking ya waislamu ndio hii ambayo siamini kama kweliwengi wana mtizamo huu,kushindwa kutenganisha dini yao na maswala yasiyohitaji dini tutarajie matatizo makubwa kwenye tume ya katiba.

Ndio maana nimesisitiza wajumbe wa hii tume wawe waislamu au wakristo wasahau kama wana dini, wasahau kama wananchi wa Tanzania wana dini, ndio njia pekee ya kuwa na katiba ya maana. Kama huu hautakuwa msingi wa tume hii, tumekwisha maana sioni ni kwa namna gani tume yenye wajumbe wengi wa dini ya kiislamu wataacha kuingiza maswala la mahakama ya kadhi kwenye katiba. It is unconceivable to believe religious beliefs will not influece thinking and decision making, and whoever wants people not to talk about this is short sightened. We need to caution members of the committee to abandon their beliefs and ideologies so that they can discuss issues with much needed freedom and perspectives. Their reliogious beliefs will without any doubt constrain their ability to thnk and digest issues the way they are supposed to.
Mkuu labda nikujibu tena na tena. Nachosema Hospital za Bugando KCMC na nyinginezo zijiendeshe zenyewe kama private Hospital na wananchi wanaotibiwa hapo ndio wapewe nafuu kwa kulipiwa kiwango fulani cha huduma zipatikanazo. Tunachopinga sisi ni serikali kuwa mbia na kanisa wakati katiba inapinga swala hilo. Sasa kama wameweza kurudisha shule na hospital zote za makanisa wameshindwa nini kurudisha shule za AghaKhan kama Tambaza?.. na iweje shule za waislaam na watu wengine waliojitolea kufungua shule na kutoa huduma kwa watu wote zisiwe na fungu la kupewa fedha isipokuwa zile za kanisa? Tazama shule za waislaam na Private nyinginezo zinapokea tu watoto waliofail mitihani na kuwapa nafasi ya kujiendeleza wakati za kikristu zinachukua walioshinda mitihani kwa ushirika na serikali kwa kutumia fedha za walipa kodi lakini zile nyingine kila mtu anajitegemea yeye mfuko wake..Huoni kasoro hapo halafu unasema ni Huruma?

Kila mara mnapenda sana kuepa ukweli, wewe huwezi kuishi nyumba ya kupanga ati kwa sababu unapewa huduma hiyo, utapenda ujenge chako na wewe uwe na sehemu yako. Unafikiri shule na hospital nyinginezo hawapendi kuziboresha hospital zao ili wapate kuhudumia watu wote kwa ufanisi bila kuwatenga kwa dini au makabila yao?.. Eeeh, nakuuliza wewe inakuwaje serikali bado inajenga shule na Hospital zake ambazo ziko chini ya kiwango halafu tunaambiwa ati walishindwa kuzihudumia ndio maana makanisa wakarudishiwa, sasa zile za waislam au za watu private serikali iliweza kuzihudumia au ndio wametengwa kiaina.

_ Namalizia kwa kusema muafaka wa MoU haufai, aidha shule na hospital zote nchini ziwe na mfumo mmoja na wapewe wote nafasi sawa za kifedha na kadhalika au kila shule na hospital isiyokuwa ya serikali ijiendeshe yenyewe (ktk ushindani) na serikali ijikite ktk kuwasadia wananchi wanaokwenda kusoma au kutibiwa huko.
 
Kama ni kweli Mzee Mtei aliongea kauli hiya ya idadi ya Waislam basi amepotoka kweli!!! Hivi Dr Salim ana idenity ngapi?
Sasa tuanze kuzungumzia pia idadi ya Wanawake.

Mimi si mwanachama wa Chadema wala chama kingine chochote cha siasa. Lakini naegemea upande wa Chadema. Mzee Mtei hata kama si kiongozi lakini anabeba ngao ya uasisi na ushawishi mkubwa juu ya taswira ya Chadema. Sasa, ikiwa nitajiridhisha kuwa mtazamo wa Mzee Mtei ndiyo mtazamo wa wengi wa viongozi wa Chadema pamoja na wanachama wake basi nitaondoa moyo wangu toka Chadema (Na sitaunga mkono wezi (CCM)). Najua kura yangu ni moja tu lakini Chadema hawataistahili.

Kura yako watastahili Magamba mkuu.
 
Mkuu Ma2mbo,
Naomba utupe source za hizo takwimu zako za 70% Wakirsto...Waislam ni asilimia ngapi na wasiokuwa na dini ni asilimia ngapi kwa faida ya JF tufahamishe.

Izi takwimu zinajulikana ulimwenguni kote...shughulisha ubongo wako au subiri sensa ya mwezi Agosti utabaini ukweli.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom