Mkuu swala la kutaifisha shule soteb tunajua wazi kwamba shule zilitaifishwa nyingi zilikuwa za kikristu na sababu yake ilikuwa kuondoa matabaka ambayo yaliathiri UMOJA wetu, hata ukienda Zimbabwe au South Afrika utaona waliowekeza zaidi ni wazungu na waliofaidika vile vile ni wazungu..Hivyo huwezi kuleta usawa katika nchi hizo kwa kutazama nani ataumia zaidi..1. Hivi ni shule ngapi za wakristu na ngapi za waislamu zilitaifishwa? Tukizungumzia sekondari, mimi najua katika maeneo ya Dar es Salaam, kanisa lilikuwa na shule za sekondari zifuatazo:
a. St. Xavier ambayo ilitaifishwa ikaitwa Kibasila.
b. St.Joseph iliyogeuzwa na kuitwa Forodhani.
c. St. Andrews iliyotaifishwa na kuitwa Minaki.
d. St. Francis iliyotaifishwa na kuitwa Pugu.
Katika hizi ni Forodhani peke yake iliyorudishwa.
Waislamu mlikuwa na shule za sekondari zifuatazo:
a. Aga Khan Boys Secondary iliyotaifishwa na kuitwa Tambaza.
b. Aga Khan Girls Secondary iliyotaifishwa na kuitwa Zanaki.
c. Mzizima Secondary ambayo haikutaifishwa.
d. Kinondoni Muslim ambayo haikutaifishwa.
Ukienda Moshi, wakatoliki walikuwa na Weruweru na Ubwe. Katika hizi, ipi wamerudishiwa?
Katika hizo, ninavyojua, Zanaki amerudishiwa Aga Khan. Hapa ni nani kaonewa? Huyo aliyetaifishiwa shule 4 akarudishiwa moja au yule aliyetaifishiwa mbili akarudishiwa moja? Wewe unaesema wakristu walipendelewa, unaweza kunitajia shule ya sekondari ya kikristu ambayo haikuwa seminari ambayo haikutaifishwa?
Ukweli ni kuwa ukiangalia idadi ya shule, vyuo na hospitali zilizokuwa zikimilikiwa na kanisa ni chache ambazo wamerudishiwa.
2. Kwa vile inaelekea hii MoU imekuwa ni ishu sana kwenu basi hebu tuiweke tuone wapi mnakwazika. Hii hapa kama alivyoileta mwenzenu: https://www.jamiiforums.com/jamii-i...a-katoliki-na-taasisi-nyingine-za-kidini.html
Ukiangalia article XII inazungumzia kutaifishwa kwa shule, hospitali au chombo chochote kinachotoa huduma ya afya au/na elimu kinachomilikiwa na kanisa. Hii ilikuwa ndiyo sababu kubwa ya MoU hii, kuwalinda wale ambao waliishang'atwa na serikali wasing'atwe tena. Hayo hayo ambayo wakina Mkandara wanataka kurudia.
Article XIII ambayo imekuwa underlined inasema serikali ita-endeavour (ITAJITAHIDI) kuingiza suala la misaada kwa ajili ya institutions hizi za kanisa katika majadiliano yao na nchi zinazotufadhili haswa Ujerumani. Watajitahidi na si lazima.
Sasa nyie mnaosema kuwa MoU hii inataka serikali itoe ruzuku kwa kanisa katika utoaji wa huduma hizi, tuonyesheni article inayoelezea hivyo. Mnataja bilioni kumi bila kutuambia kwa uhakika imetoka wapi kwenye bajeti!
2. Naam, kweli shule za kikristu zitakuwa na mlengo wa kikristu kama vile ambavyo zilivyo za kiislamu. Lakini hakuna shule inayotambulika na serikali (isipokuwa zile zinazowatayarisha wahudumu wa baadae wa imani hizi) inayozuia muumini wa dini nyingine kujiunga nazo. Waislamu wengi walikataa kwenda kwenye shule za kikristu kwa sababu ya kuhofia kuwa watabadilishwa dini au uwezo mdogo wa kipesa. Pamoja na haya, ni wengi tu ambao wameelimishwa katika shule hizi bila kuathirika, rais wetu akiwa mmoja wao. Wakristu wengi hawapeleki watoto wao katika shule za kiislamu kwa wasiwasi wasi huo huo. Lakini nao kama shule hizo zina matokeo mazuri kama Feza, Al Muntazir n.k. hawachelei kuwaruhusu binti zao kuvaa hijab ili mradi wanapata elimu.
Kusingizia kuwa waislamu wanaathirika kutokana na shule hizo kurudishwa kwa wakristu ni uchimvi maana waislamu wamekuwa wakilega nyuma kielimu hata wakati karibu shule zote zilikuwa ni za serikali. Badala ya kutafuta visingizio kama hivi ( incl. kuibiwa mitihani), waislamu mnatakiwa kujiangalia wenyewe na kuhimizana kwenda shule.
Huko kubaguliwa mnakodai kunafanyika katika shule hizo za kikristu dhidi ya waislamu inabidi mtolee mifano. Au mnazungumzia seminari ambazo hata mkristu wa dhehebu lingine hapewi nafasi kwa sababu lengo ni kuelimisha watu watakaokuwa makasisi, mapadri n.k.?
3. Mnazungumzia hadithi za alinacha. Hata kama mlipewa ili kuwapooza juu ya MoU, ukweli unabaki kuwa MLIPEWA BURE. Itakuwa vyema kama mtatutolea mfano wa namna ambavyo hayo mabilioni serikali inayotoa kwa kanisa mnayoyazungumzia yamewafaidia vipi wa kristu kwa kuhudumia shule na hospitali wanazoelimishwa na kutibiwa peke yao. Tutajieni shule au hospitali moja inayopokea ruzuku hiyo ambayo inahudumia wakristu peke yao. Moja tu.
4. Waberoya amewapa mfano wa Mbagala Mission lakini hamtaki kumsikia. Au mnataka kutuambia kuwa katika maeneo yenye waislamu wengi hakuna shule au dispensari za kanisa? Hamna hata aibu!
5.Yale yale. Insinuations bila substantiation. Toa ushahidi wa shule au chuo kinachopewa ruzuku na serikali ambayo inatoa huduma zake kwa kupendelea waumini wa dini yake.
Amandla......
Tatizo linakuja ni kwamba kama kutaifisha mashule na Hospital ilikuwa kuondoa ubaguzi uliokuwepo toka mkoloni kwa nini leo tumeurudia tena kule na Udini umerudi?. tatizo lako unazungumzia kwa niaba ya makanisa wakati sisi tunahoji serikali sio wakristu ama Ukristu. Nakumbuka vizuri sana kwamba Lake socondary - Mwanza, Shaaban Robert, Mzizima - Dar, na kadhalika hizi hazikutaifishwa kwa sababu zilikuwa za watu binafsi kwa hiyo haikuwa kutaifisha hovyo tu bali zile zilizosababisha kutugawa. Kinondoni Sec na Seminary hazikutaifishwa kwa sababu zilitakiwa kuwa shule za DINI zikifundisha pia elimu dunia. Kwa nini tumebadilisha mfumo huu?.
Nitakupa hadithi moja ya kweli nayoikumbuka vizuri. baba mmoja katika kuendesha familia yake alimpeleka mwanaye wa kiume shule akamwacha wa kike kwa sababu alitegemea huyo ni mwanamke na mwisho wake ataolewa na hivyo kuwa ktk familia nyingine lakini wa kiume ataendele kulinda jina la familia hata akioa. Miaka imeenda mzee akamwandikishia mtoto wa kiume nyumba yao kama urithi, yule mtoto wa kike akamuuliza baba yake kulikoni umrithishe nyumba mtoto wa kiume..
Wakati akisubiri jibu, mtoto wa kiume akadakia na kusema "Dah! leo nimeelewa, kumbe dada yangu mwenyewe hupendi mafanikio yangu? mbona nyumba yenyewe tunaishi wote sijakubagua leo umefikia kuhoji hata kuandikishwa mimi jina langu?.."
Yule binti akasema "Kaka haihusiani kabisa na mapenzi yangu kwako, isipokuwa sielewi kwa nini baba hakunipeleka shule na sasa imefika hadi urithi anakupa wewe kwnai mimi sii mwanaye?"
Kaka mtu akasema "Aaah si unajua wewe utakuja olewa na kuondoka, lakini mimi kama mwanamme nitaendeleza mali za baba na kuilinda familia ndilo jukumu nililopewa na utamaduni wetu." Dada mtu akasema "Basi kama hofu yenu ndio hiyo bora uniowe wewe maanake navyojua mimi nikiolewa tutapewa mahari ya millioni 10 na ukioa wewe tutatozwa mahari ya millioni 10 nani anayeigharimu familia?"
Ubishi ukawa ubishi na nisemavyo sasa hivi yule kijana yuko Marekani, nyumba aliuza na sasa mzee wa watu analelewa na mtoto wa kike ambaye hakujaliwa kuolewa ila anafanya kazi nzuri tu Benki kuu na kamjengea baba yake nyumba nyingine anakoishi sasa hivi.
Habari hii ni kukuonyesha kwamba hakuna sababu ya kushinda hapa kati ya waislaam na wakristu, sisi sote ni ndugu na tunachohoji sisi ni serikali, serikali kuwa na Ubia na kanisa wakati katiba yetu inakataza kutokana na experience tuloipata enzi za mkoloni kufikia mwaka 1966. Haijalishi kabisa nini malengo ya kanisa wala wanafanya nini kwa sababu hata zile zisizo za kanisa zinalenga kuwaelimisha na kuwatibu watu wote bila kujali dini na makabila yao. Kwa nini uundwe muafaka kama huu pasipo kuvihusisha vyombo vyote?.. hili kosa jamani..Mbona sote tunatazama kwa makini uundwaji wa Katiba mpya tukitaka asasi zote za kijamii zihusishwe? kwa nini seikali isifanye jambo hili na asasi mojawapo tu ambayo itakuwa na malengo ya kulinufaisha Taifa zima?..