Kamanda Pilitoni,
People's.....
Kwa kweli unatumia nguvu kubwa sana kumsafisha Mh. ZZK. Lakini msiba wa kujitakia, hauna kilio.
Mh huyu amekuwa chanzo cha anguko lake mwenyewe. Kwa kuwaruhusu watu kama wewe kumtetea, kumsafisha na kumsifia. Baadhi ya makosa yake ni haya hapa chini:
1. Mwaka 2009/2010 wakati anaandikwa na gazeti la Mwananchi kila uchao huku akisifiwa kuwa "anatembea na barua ya kujiuzulu kwenye mkoba", aliona hiyo ni sifa kubwa sana. Akavimba kichwa.
2. Mwaka huu, kulijitokeza kundi la watu waliokuwa wanatumia jina la TUNTEMEKE kushambulia viongozi wakuu wa Chama, hususan Dkt. Slaa. Hawa walikuja na shutuma nyingi ikiwemo ya kuondolewa kwa Mhasibu wa Chama, Malipo ya Dkt Slaa wakati wa kuhudhuria kesi, Mkopo wa Nyumba, Kulipwa posho kwa Heche, Josephine na akaunti package, uchaguzi wa Iringa uliomuweka Chiku Abwao madarakani, John Mrema na feasibility study Arumeru n.k. Hawa wote walionekana dhahiri kupingana na watu maalum kwenye chama. Wakafikia hatua ya kumkejeli na kumtukana Dkt Slaa, personally and specifically hapa JF na Facebook. Kosa alilolifanya Zitto ni walau kukemea hali hiyo. Alishindwa kuandika hata mstari mmoja kukaripia hali hiyo na dhihaka hizo!
3. Alipopewa tuhuma na Saanane na Mamuya, badala ya kujibu hoja, aliandika kwa hasira, kihuni na kosa kubwa alilolifanya ni kuzungumza wazi wazi Imani ya kishirikina. Maneno kama kuaga kwetu, panya kutokusalimika n.k. hayakuwa maneno ya kuzungumzwa na ROLE MODEL ambaye ni RAIS MTARAJIWA.
4. Baada ya sekeseke la 18/12/2012 na kuendelea, wakajitokeza watu wengi JF ambao wao wakawa wanamtetea Zitto. Kuna Taswira ambaye alikuwa anakesha JF na kujibu kila post. Wakajitokeza watuhumiwa ambao walijiunga usiku wa manane wa tarehe 19/12/2012. Hawa wakaibuka na kumtetea Zitto wazi wazi kwa kuelezea kuwa ni kiongozi shupavu, ni role model na wakaenda mbali zaidi kuanza kumsema kwa dhihaka Katibu Mkuu - Dkt. Slaa. Slaa hakuhusika au hakutajwa popote kwenye PM 7. Why Shonza aliamua kumtaja bila hata sababu? Hawa wakamuharibia zaidi Zitto.
5. Tangu 18/12/2012, kumekuwepo posts nyingi - kama hii yako - zote zikiwa na lengo la kumsafisha Zitto. Bahati mbaya, hasafishiki kwa kuwa alijichafua mwenyewe.
6. Zitto amekuwa akitoa matamshi ya kibaguzi na kichochezi. Kila mara amekuwa akirejea maneno ya ukabila na ukanda. Lakini majuzi ameeleza maneno mengine mazito. Maneno ambayo si wote waliyaelewa. Alijitetea (nadhani ni wakati aidha anamjibu Nyerere au Mamuya), kuwa yeye ni mwaminifu kwa CHADEMA na kuwa yeye ameitumikiwa CHADEMA maisha yake yote na amekuwa mwaminifu. Kwa kuwa tunajua na kuamini kuwa yeye hakuwahi kuwa chama kingine chochote cha siasa zaidi ya CHADEMA, basi anamaanisha kuwa yeye ni bora kuliko 'viongozi wenzake ambao walikuwa CCM huko nyuma na sasa wako CCM; tena viongozi wenyewe wana kadi mbili"(si uanachama wa vyama viwili. Hapana. Kadi mbili!)". Hili ni kosa jingine kubwa alilolifanya Zitto.
7. Kosa jingine la Zitto ni kutokushiriki kabisa kwa uwazi (labda kwa kificho) kwenye M4C. Kila alipokuwa anaulizwa, alikuwa anasema kuwa anakuwa anakiimarisha Chama kwa njia nyingine. Kampeni za Udiwani Songea au Mwanza. Lakini kweli hata kutokea kwenye harambee moja tu? Naibu Katibu Mkuu? Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi? Naibu KUB?
Makosa ni mengi, walau kwa usiku huu tunapokula kuku mnafu hapa Makao Mapya, halafu tukale na Smaki Nick's Pub kushangilia NURU kuishinda GIZA, tuyatazame makosa haya.
Msiba wa kujitakia, hauna kilio.
Nakala
Taswira,
PhD,
Mungi, [MENTION]Ecolli[/MENTION],
Rejao,
chama,
Mungi