mkalamo
JF-Expert Member
- Sep 7, 2013
- 324
- 347
Kabla ya kifo cha Rais wa awamu ya tano,chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema),kilio chao kikuu kilikuwa ni kupatikana kwa Tume huru ya uchaguzi kwa ajili ya kuendea Upatikanaji wa Katiba mpya.
Katika kuhakikisha jambo hili linafanikiwa vijana wao katika maeneo mbali mbali walizunguka wakiwa na madai ya kupatikana Tume huru ya Uchaguzi, kilio kilichokuwa pia kimebebwa na vyama vingine wakati huo huku kila mmoja akipambana kwa namna yake.
Msimamo wao haukubadilika wakati wote huo hata pale baadhi ya viongozi wao wakuu walipoondoka nchini kwa sababu mbali mbali dhidi ya serikali.
Viongozi hao wakiwa nje ya nchi kwa kushirikiana na baadhi ya wanaharakati wakaweka mijadala mbali mbali kati ya katiba na tume huru ya Uchaguzi na kwa bahati nzuri hoja ya kuanza na tume huru ikapata uungwaji mkono na watu wanaoheshimika ndani na nje ya chama hicho.
Mahubiri yakabaki kuwa ni kupatikana Tume huru, na fulana zikatengenezwa wakavalishwa watu wa aina mbali mbali kwenye matukio tofauti(Hapa ilisemwa inafanyika kwa maslahi ya nchi)
Waungwana hawa waliendelea na madai yao mpaka siku za mwisho za kuelekea Uchaguzi mkuu wa 2020 na kufanya baadhi ya wafuasi wao wakamatwe,akiwemo Twaha Mwaipaya(alikamatwa Singida)
Baada ya Uchaguzi wa 2020,madai ya Katiba mpya yakabaki kwa wanaharakati na wanasiasa wakabaki na Tume huru kwanza hadi kifo cha Rais Dk Magufuli kilipotokea,waungwana hawa wakaona wamepata mwanya wa kuanza upya kuidai katiba na wale wanaodai Tume huru kuelekea kwenye katiba mpya hawana maana
Hapa zikaungana nguvu mbili za wanaharakati wanje ya chama kikubwa na wale wanaojinasibisha hawana chama madai yakawa ni katiba tu.
Ni wakati huo pia Rais wa awamu ya sita aliposema kuna mambo yanazungumzika na yanahitaji muda lakini ni vema watu wajue kwanza wanataka kitu gani badala ya kuanza “Choko choko”
Miongoni mwa vyama vilivyobaki na msimamo wa kuanza na Tume huru ni Pamoja na ACT Wazalendo, na baadhi ya watu maarufu akiwemo Mwanasheria nguli nchini kwa sasa Peter Kibatala,ambaye alieleza hoja zake kisheria juu ya umuhimu wa kuanza kwa Tume huru.
Kibatala alisema ili kuwe na katiba yenye uhalali wawananchi ni lazima kwanza mfumo mzima wa Tume ya Uchaguzi uwe huru kwa bara na visiwani,kwa kuwa wananchi wanaweza kuwa na mapendekezo yao na tume isiyo huru ikatangaza mapendekezo mengine juu ya katiba.
Hoja hii ya kibatala ikaendana na hoja ya ACT wazalendo,wenye akili wakapima uzito wa watoa hoja na hoja zao na hatimaye Rais akiwa katika mkutano wa TCD akaeleza kuna umuhimu wa kuipata Tume huru na baadhi ya mabadiliko ya sheria ya vyama vya siasa pia kufanyiwa kazi.
Hoja hii ilipoonekana imekubaliwa na RAIS kutoka kwa Chama cha ACT Wazalendo,kwa mtazamo wao wanaharakati wa kisiasa wakaona inaenda kumjenga adui yao namba moja kwenye siasa Zitto Kabwe kuwa uongozi wake wa TCD na chama chake cha ACT Wazalendo kimefanikisha jambo litakaloweka historia mpya ya kisiasa nchini.
Kwamba wakiunga mkono kwa maslahi ya Taifa watampa ushindi Zitto na wakifanikiwa kukwamisha watamkwamisha Zitto na si kwa maslahi ya Taifa.
Katika mazingira kama haya sasa ni wajibu wa wenye akili kujiuliza hawa wanaopinga tume huru sasa je ni kwa sababu yupo ZItto Kabwe kwenye madai hayo au ni kwa maslahi ya Taifa
Tafakari na jiulize
Pichani ni makada na viongozi wa Chadema wakihimiza upatikanaji wa Tume huru ambayo Rais ameridhia kwa kuunda kikosi kazi kitakachopendekeza namna bora ya kuwa nayo.
hadi pale walipoingia wanaharakati katika mitandao ya kijamii na kubadilisha mwelekeo wao,
Katika kuhakikisha jambo hili linafanikiwa vijana wao katika maeneo mbali mbali walizunguka wakiwa na madai ya kupatikana Tume huru ya Uchaguzi, kilio kilichokuwa pia kimebebwa na vyama vingine wakati huo huku kila mmoja akipambana kwa namna yake.
Msimamo wao haukubadilika wakati wote huo hata pale baadhi ya viongozi wao wakuu walipoondoka nchini kwa sababu mbali mbali dhidi ya serikali.
Viongozi hao wakiwa nje ya nchi kwa kushirikiana na baadhi ya wanaharakati wakaweka mijadala mbali mbali kati ya katiba na tume huru ya Uchaguzi na kwa bahati nzuri hoja ya kuanza na tume huru ikapata uungwaji mkono na watu wanaoheshimika ndani na nje ya chama hicho.
Mahubiri yakabaki kuwa ni kupatikana Tume huru, na fulana zikatengenezwa wakavalishwa watu wa aina mbali mbali kwenye matukio tofauti(Hapa ilisemwa inafanyika kwa maslahi ya nchi)
Waungwana hawa waliendelea na madai yao mpaka siku za mwisho za kuelekea Uchaguzi mkuu wa 2020 na kufanya baadhi ya wafuasi wao wakamatwe,akiwemo Twaha Mwaipaya(alikamatwa Singida)
Baada ya Uchaguzi wa 2020,madai ya Katiba mpya yakabaki kwa wanaharakati na wanasiasa wakabaki na Tume huru kwanza hadi kifo cha Rais Dk Magufuli kilipotokea,waungwana hawa wakaona wamepata mwanya wa kuanza upya kuidai katiba na wale wanaodai Tume huru kuelekea kwenye katiba mpya hawana maana
Hapa zikaungana nguvu mbili za wanaharakati wanje ya chama kikubwa na wale wanaojinasibisha hawana chama madai yakawa ni katiba tu.
Ni wakati huo pia Rais wa awamu ya sita aliposema kuna mambo yanazungumzika na yanahitaji muda lakini ni vema watu wajue kwanza wanataka kitu gani badala ya kuanza “Choko choko”
Miongoni mwa vyama vilivyobaki na msimamo wa kuanza na Tume huru ni Pamoja na ACT Wazalendo, na baadhi ya watu maarufu akiwemo Mwanasheria nguli nchini kwa sasa Peter Kibatala,ambaye alieleza hoja zake kisheria juu ya umuhimu wa kuanza kwa Tume huru.
Kibatala alisema ili kuwe na katiba yenye uhalali wawananchi ni lazima kwanza mfumo mzima wa Tume ya Uchaguzi uwe huru kwa bara na visiwani,kwa kuwa wananchi wanaweza kuwa na mapendekezo yao na tume isiyo huru ikatangaza mapendekezo mengine juu ya katiba.
Hoja hii ya kibatala ikaendana na hoja ya ACT wazalendo,wenye akili wakapima uzito wa watoa hoja na hoja zao na hatimaye Rais akiwa katika mkutano wa TCD akaeleza kuna umuhimu wa kuipata Tume huru na baadhi ya mabadiliko ya sheria ya vyama vya siasa pia kufanyiwa kazi.
Hoja hii ilipoonekana imekubaliwa na RAIS kutoka kwa Chama cha ACT Wazalendo,kwa mtazamo wao wanaharakati wa kisiasa wakaona inaenda kumjenga adui yao namba moja kwenye siasa Zitto Kabwe kuwa uongozi wake wa TCD na chama chake cha ACT Wazalendo kimefanikisha jambo litakaloweka historia mpya ya kisiasa nchini.
Kwamba wakiunga mkono kwa maslahi ya Taifa watampa ushindi Zitto na wakifanikiwa kukwamisha watamkwamisha Zitto na si kwa maslahi ya Taifa.
Katika mazingira kama haya sasa ni wajibu wa wenye akili kujiuliza hawa wanaopinga tume huru sasa je ni kwa sababu yupo ZItto Kabwe kwenye madai hayo au ni kwa maslahi ya Taifa
Tafakari na jiulize
Pichani ni makada na viongozi wa Chadema wakihimiza upatikanaji wa Tume huru ambayo Rais ameridhia kwa kuunda kikosi kazi kitakachopendekeza namna bora ya kuwa nayo.
hadi pale walipoingia wanaharakati katika mitandao ya kijamii na kubadilisha mwelekeo wao,