Mtajeni Mwanasiasa Aliyetema Pumba Zaidi 2012

Mtajeni Mwanasiasa Aliyetema Pumba Zaidi 2012

Mulugo aka mzee wa Zimbabwe na 'one nineteen sixty four'
 
Ni huyu hapa
[h=1]Nnauye Jr
user-offline.png

Banned
verified.png

reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
[/h]
Na moderators kuzingatia utoaji wake wa pumba, wamempa zawadi ya kufungia mwaka. BAN!
 
Aaa wapi ! Usukani umeshikwa na ndugu STEVEN MASATU WASIRA ( Dr slaa alikula hela za mapokezi ya papa ) , Lingine ni la CDM kufa mwisho wa mwaka 2012 , bado siku 7 wala hata dalili za Cdm kufa sizioni ! Ndiyo kwanza wanarudishiwa walivyodhulumiwa .
 
Muhongo..."Hakuna mgao wa umeme Tanzania."....really!!! seriously!!!
 
Lusinde na mwigulu wazee wa migomba ina ra ngi ganii? Mpunga una rangi ganii? Mahindi yakiota yana rangi gani!? Bendera ya ccm ina rangi gani? Tuchague ccm coz uoto wote ni wa kijani na maneno yao majukwwani lusinde bila kusifia mkewe hajahutubia na kutaja ch*pi mf mpwapwa kwenye udiwani na wape maembe mabichi wasionyoosha mikono maana wana mimba. Nape mulugo wassira hawawezi kosa kwa top 5

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Wakati tukisaka wanasiasa bora na waliofanya kazi zaidi mwaka 2012, nadhani ni bora tuwataje pia wanasiasa waliotia fora kwa pumba nyingi zaidi. Tupendekeze majina halafu nitawaweka kwenye poll. Mimi binafsi nampendekeza Cyprian Majura Musiba kama mwanasiasa aliyetema pumba zaidi mwaka huu. Naomba majina mengine wadau

Joshua Nassari:- JK asikanyage AR, mie ndio rais wa huko. "This was pumba ya mwaka".
Wassira:-Esther wassira sio mwanangu ni mtoto wa mdogo wangu. "Pumba pia, mtoto wa mdogo wako kwani sio mwanao?"
 
Lema, Voda mkituhujumu, tutapita mtaani na Kuzikusanya laini Zenu Zote tuzitupe.
 
Ni Lusinde,mbunge wa CCM,Mtera aliyemwaga matusi wakati wa Uchaguzi wa Ubunge Arumeru Mashariki,mbaya zaidi chama chake hakijamchukulia hatua yoyote ya kinidhamu hadi hivi sasa,kwa maana nyingine walikubaliana na matusi ya huyu Mbunge.
 
Kwaheri 2012: Mwaka wa Upumbavu wa Ujana!

Ningepewa nafasi ya kuubatiza jina Mwaka 2012 ningeuita Mwaka wa Upumbafu wa Ujana. Ningeuita hivyo kutokana na kuwa mwaka uliodhihirisha UJANA/RIKA/UMRI ni vigezo vya kipuuzi kabisa katika Uongozi wowote nchini mwetu. Haya yamethibitishwa na ufanisi finyu wa vijana walioaminiwa katika nafasi mbalimbali za Kitaifa (Japo hili halimaanishi kuwa hakukuwa na vijana waliotoboa kwa excellent performance). Orodha ya walioliahibisha rika la vijana katika nafasi za kitaifa ni pamoja na Waziri Mahige (Ushamba wa Pesa taslimu), Waziri Ngereja (Ufanisi zero katika Wizara nyeti), na Waziri Malima (Uhuni na ubwanyenye).

Katika kilele cha aibu kuna hawa vijana wawili kutoka vyama tofauti ambao wamedhihirisha kuwa, kama watachukuliwa wao kama wawakilishi wa vijana wote, basi vijana wa Tanzania hawajui wanataka nini, hawajui matamshi wanayotoa au maana ya maandishi wanayoandika, na wanasimamia kile wasichokisema wala kukiamini. Mbaya zaidi hawajui ama hawataki kukubali kuwa hawajuhi. Vijana hawa ni Nape Nnauye na Zitto Kabwe.

Nape aliteka hisia za watu wote wazalendo (nami nikiwemo) wa nchi hii kwa kujipambanua dhidi ya ufisadi na mafisadi. Akaenda mbali zaidi kuendesha kampeni ya kuvua magamba (mafisadi). Lakini kilichotokea sote ni mashahidi kuwa siku zilizitolewa kwa magamba kuvuliwa zilikwisisha, magamba hayakuvuliwa na mwisho Nape Nnauye kajikabidhi mwili na roho kwa Mkuu wa aliowaita mafisadi. Sasa anaimba kama kasuku wimbo wa "Umoja na Mafisadi ni Ushindi!"
…. BABAANGU JEETU PATEL…..
. Nnauye Jr sasa kwa fikra zake anaamini kuwa, karatasi ya manila iliyochapiswa kama kadi ya ccm na kumilikiwa na Dr. Slaa ndiyo sababu kuu ya matatizo ya Watanzania! Anaona hiyo ni hoja yenye tija hata kuliko nini kiwe kwenye Katiba na yumkini atahitaji suala hili la Dr. Slaa kurudisha kadi liwe la Kikatiba! Hawa ndiyo vijana wetu wa Tanzania wanaotuvusha mwaka 2012

Wa pili ni kijana machachari na mweledi wa vitabuni Mh. Zitto Kabwe. Zitto amefanya shughuli nyingi na kuamsha hoja mbalimbali zilizolenga kumweka yeye binafsi kwenye fikra za Watanzania kama Rais ajaye. Katika kufikia azma hii, mpango mkakati wake unaonyesha kutojali miiko, taratibu na maadili ya Kitaasisi na Kijamii. Mpaka sasa, ushahidi wa kimazingira unamuonyesha kama mtu anayefadhiri uasi dhidi ya chama chake ilimradi tu apate upenyo wa kutimiza lengo lake. Zitto ndiye aliyeasisi kampeni ya Ujana/Umri/Rika na Urais wa 2015 akitaka umri wa kugombea ushushwe hadi maika 35
[MENTION]Zitto[/MENTION] "Umri wa kugombea urais, Rwanda wenzetu wanaruhusu miaka 35, Burundi miaka 35, Kenya miaka 35, Marekani miaka 35, Afrika Kusini miaka 35…Sisi ni ushamba tu, hakuna sababu ya kuweka umri mkubwa," alisema Zitto ambaye wakati akianza kuchangia alitania akisema kuwa itakapofika mwaka 2015 atakuwa na umri wa miaka 39.
Lakini hivi karibuni akihojiwa na JF alioonyesha kutokuwa nadhifu wa kile analichoanzisha kwa kuleta hoja mpya akitaka kila mpiga kura awe na aweze pia kugombea!
Kila raia mwenye haki ya kupiga kura awe na haki ya kupigiwa kura! Tatizo ni nini?
Ni mtu yuleyule aliwahi kuandika haya:
[MENTION]Zitto[/MENTION] Mimi ninaamini kabisa kuwa Rais ajaye wa Tanzania ni lazima atokane na kizazi cha baada ya uhuru. … Hili ni Taifa la vijana. ….… .Wazee wameishi maisha yao. Wameishi yetu na sasa tunataka kuwakopesha maisha ya watoto wetu?
Baada ya kauli zake kumuelemea akageuka na kuandika hivi:
Ubaguzi wa aina yeyote ile ni ushamba, ujinga na upuuzi tu.

Zitto hana tofauti na Nape Nnauye ambaye kila anayemuita au kumlinganisha na Baba yake na kudai kumuheshimu kwa maneno; kivitendo humdhihaki na kumpa dharau ya hali ya juu.

Mfano soma hii sehemu ya ufafanuzi wa Nnauye Jr:
… MAREHEMU KYARUZI NI SAWA NA BABA YANGU....
Halafu soma na vitendo alivyomfanyia huyo amfananishae na Baba yake!
Nape aliingia Bukoba tarehe 25/05/2012. …baada ya hapo alielekea Missenyi ambako tunaarifiwa alikuwa na mikutano ya hadhara. … Labda ili Watanzania muweze kupima vema uelewa na akili za Nape, tuwafahamishe kuwa Missenyi ndiko iliko Kyaka na ambako maziko ya Dr. Kyaruzi yamefanyika. Tunashindwa kuelewa, hiyo mikutano ilikuwa safisha njia ya mazishi au inahusiana vipi na mtu aliyepeleka ujumbe wa maombolezo?

Linalochanganya zaidi ni hili la Jumamosi tarehe 26/05/2012. Hii ndiyo siku ambayo Dr. Kyaruzi alipumzishwa rasmi kaburini alale kwa amani. Lakini kwa Nape akiwa Kyaka hii ilikuwa siku maalumu ya kufungua matawi na kutangaza operation yake mpya ya kisiasa iitwayo "Vua Gamba, vua Gwanda, Vaa Uzalendo"…...

Mfano wa pili pale Nnauye Jr anapokiri kwa kinywa kumheshimu Dr. Slaa ilhali kivitendo ana mdhihaki!
…. Nape ambaye amekiri kumheshimu Dk Slaa kama babu yake...
Nadhani Mohamed Mtoi kamjibu vema hapa:
...Leo Nape anajinasibu kuwa Jeetu Patel ni baba yake?! (Najua si vibaya kuwa na baba muhindi halafu yeye mswahili wa Manzese) Halafu Samweli Sitta (67) mwenye umri mkubwa kuliko Dr Slaa (63) kwa Nape ni Mzee lakini Dr Slaa ambaye ni mdogo kwa Sitta yeye ni babu?! Logically, huyu jamaa ana mtindio wa mawazo kama sio vision disorder.

Ondoka upesi mwaka 2012. Safisha uondoke na upuuzi pamoja na upumbafu wa vijana na ujana wao. Hata kama watatambua ukweli kuwa kuja kwa 2013 kunawasogeza karibu na rika la uzee ambalo wanalitusi, wanalidhihaki na kulikejeri, usiwaruhusu kujongea huko. Waachie wanaotaka mabadiliko kivitendo wavuke kwenda mwaka mpya. Wanafiki na waasi wasifike hata dalajani.

Nakuaga mwaka wa Ujana na Upumbafu; Kwa heri ya kuonana mwaka 2012!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom