Simkumbuki Wakili mnafiki kuliko Marando

Simkumbuki Wakili mnafiki kuliko Marando

Unafiki upo hapo Jasusi. Tena ni dhahiri kabisa. Na kisiasa it's a bad look.

Na mimi kama mpiga kura nina haki kabisa ya kutumia sababu hiyo kumuona yeye ni mnafiki na asiyestahili kura yangu. Utapingaje ufisadi kwenye majukwaa ya kisiasa halafu mahakamani ugeuke na kuwa mtetezi wa hao hao watu unaowachana kwenye majukwaa ya kisiasa? It's stupid.

Na mfano wako wa daktari na dadaye hata haulingani na unafiki wa Marando.......

Acha uvivu wa kufikiri ndugu yangu, tofautisha siasa na kazi ya mtu...mbona mawakili hao hao ndio mnawakimbilia pale ndugu zenu wakiwa na kesi nzito kama wizi, rushwa, mauaji.....si muwaache waozee jela......kazi ni kazi na siasa ni siasa
 

Mkuu kuwa mwelewa ushahidi unaoongelewa hapa ni ule wa mawasiliano ya Maranda na Baba yako Jeetu Patel.

Nape bana,kwa kujipendekeza hajambo,Jeetu Patel ni baba yake kwa kuwa ana fweza,Dr Slaa ni babu yake kwa kuwa nimpinzani wake wakati hawa watu wapo lika moja.......

Mkuu umeweka sawasawa kisu kwenye mfupa. Leo Nape anajinasibu kuwa Jeetu Patel ni baba yake?! (Najua si vibaya kuwa na baba muhindi halafu yeye mswahili wa Manzese) Halafu Samweli Sitta (67) mwenye umri mkubwa kuliko Dr Slaa (63) kwa Nape ni Mzee lakini Dr Slaa ambaye ni mdogo kwa Sitta yeye ni babu?! Logically, huyu jamaa ana mtindio wa mawazo kama sio vision disorder.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Nape tunaomba ujibu kwanza hili halafu uje na mambo mengine! Je wewe si Miongoni mwa waasi wa CCM mpaka kufikia kuanzisha CCJ? Kama swala la kumiliki kadi ni la kipuuzi Kwa nini ulilianzisha dhidi ya Dr Slaa? Je Leo ndio umegundua suala la kadi ni la kipuuzi? Je utatumia njia gani kuwaaminisha watu kwamba suala la kadi ni la kipuuzi wakati wewe ndio muasisi wa upuuzi huo? Je unakubaliana na maoni ya watu wengi kwamba Dr Slaa yuko sahihi?
 
Hata mimi nimeshangazwa... Inawezekana hajui anachokiongea...

Kamanda Heche alipokuwa arusha aliwaeleza wananchi wasi wasi wake juu ya Nape kama kweli ni mtoto wa Mzee moses nauye kutokana na kutorandana kitabia hata kidogo. sasa leo kaja yeye mwenyewe jukwaani kumtaja baba yake kuwa ni fisadi Jitu petel! Hongera nape kwa kutuweka wazi watanzania.
 
Kama unaona Marando anafanya kosa kupinga ufisadi kwenye majukwaa wakati huohuo hugeuka na kuwatetea watuhumiwa wa ufisadi mahakamani.Je unasemaje kuhusu serekali ambayo hupinga mauaji kwa nguvu zote lakini anapotokea mtu anaua tena na ushahidi upo mzuri wa kuonyesha kuwa mtuhumiwa aliuwa kweli.lakini kesi inapopelekwa mahakamani serekali yenyewe inayopinga mauaji hugeuka na kuanza kumtetea muuaji ili ashinde kesi tena kwa kutumia kodi za wananchi.
 
Nape,
Tatizo lako ni kwamba una tendency ya kuanzisha mada halafu tukianza kukuuliza maswali unasepa. Inakuwa vigumu kwa watu makini kuchangia kwa sababu hiyo.......

Sahihi sana mkuu;
... anakera sana kwa hii tabia!
 
NAPE J. PATEL! vipi babako mdogo SUBHASH PATEL anaendeleaje? Sasa kama Marando ni mnafiki,anawatetea mafisadi wa EPA, mbona wewe wanakulea kama mtoto wao? Hauoni kama hizo hela wanazokupa ni za kifisadi?
 
Du! Kwa style hiyo, tusijekushangaa hata Mohamed Dewji na Manji wanaitwa baba na Nape.
 
Kusoma India hadi Nnauye anaanza kusahaulika. Nape Jeetu Nauye Patel
 
Kaona maswali yamemkwaza na kumzidia na wale vijana wake wa mitandaoni pale Lumumba wamelala hawamtetei Bosi wao, kwa nini asile kona Nape kilaza?
Akili nyepesi always uja na mambo mepesi yasiyo na mashiko, ni kweli angetuwekea ushahidi wa Mzee Marando kumjibu Jeetu Patel angalau leo Nape angetudhihirishia kuwa ameiva kimkakati na tusingekuwa na shaka na habari yake, Nikionacho ni kuwa ameamua kutuletea siasa kwenye hii thread! Nilicho na uhakika nacho ni kwamba ushiriki wake katika kuanzisha chama cha CCJ utabaki kuwa ukweli mpaka atakapokiri mbele ya kadamnasi.

Comrade Kagame,

Napela Nnauye ni miongoni mwa nguzo za ccm iliyopo sasa ni miongoni mwa Vijana wasioshindwa kirahisi. NAAMINI HAJAUKIMBIA UZI ALIOUANZISHA BALI YUPO KU-SCAN ile document ya Marando na Patel.

Napela Nnauye, fanya haraka sasa kaka. Wengine tunataka tuichangie hoja kwa ushahidi mahsusi.
 
Dr Slaa anasimama mwembe yanga temeke anataja orodha ya mafisadi halafu Marando anasimama mahakamani kuwatetea hao mafisadi, huu ni unafiki.
 
Tusipokuwa makini tutafikiria kwa akili ya Nape,mimi naona wewe Nape na Marando wote ni wanafiki ila wewe ni mnafiki mbaya kwasababu ni kijana.

Mwaka jana ulituimbia nyimbo za kujivua gamba na kuwataka mafisadi wajitathmini,watafakari kisha wachukue hatua ya kujiondoa chamani kabla ya kuwaandikia barua. Hadi Rostam Aziz alijiuzulu na kulaani siasa zako uchwara.

Lakini siku hizi unaongea tofauti kabisa eti kuhuisha chama huku ukila sahani moja na Lowassa na Chenge uliokuwa ukiwatuhumu wewe na vijana wako ili wajiondoe kwenye chama.

Je wewe Nape siyo Mnafiki? Je,si kweli kwamba heshima ya ccm imeshuka kutokana na kukumbatia watuhumiwa ufisadi? Mwisho, Marando amekutuhumu kuhusu kadi (siasa), mbona wewe unasisitiza ushahidi unaohusu scanned document (law profession) ya Marando?
 
'Akibisha ' hapo ndiyo tatizo lilipo , hakuna kusubiri , weka ushahidi , vinginevyo tutajua ni yaleyale ya siku 90 !
 
Mkuu hapa ndio nazidi kuamini kuwa wewe ni kilaza. Unakumbuka ile "Innocent until proven guilty"?
Kama hukumbuki waulize vizuri wanasheria (hii sio siasa) watakueleza.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Nadhani wewe ndo utakuwa "KILAZA" kama mnalijua hivyo kwa nini kila siku mnaimba flani fisadi hata kabla hajahukumiwa na mahakama.
 
ni vema kutoa uthibisho kama upo. Hii inapunguza maswali lakini pia inajenga heshima ya mtoa hoja
 
nape wewe n muongo, mzandiki,mftini,mgombanishi,leo unalalamika nini kumbe mkuki kwa nguruwe,uluvyomsingiizia mzee wa watu dr slaa kwamba anailipia kadi ya ccm mpaka leo ulisikia raha sana kwenye moyo wako,ili hali uanajua kuwa mwana chanama wa vyama ni kosa kisheria mbona haukumshtaki kama ankadi mbili zote ni hai? kwanza tuambie yule hawara yako aliyekuwa chanel 10 umemtorosha anatumia hela zetu au?
 
wewe uliwataka wajivue magamba kwenye chama chenu, ukiwataka wawaachie chama chenu, mkikutana mnapeana mikono, unajichekesha huku unainamisha kichwa chini kwa kuona aibu. sasa hiv huo wimbo ndo umekuishia kbs.

huu sio unafiki.
 
Acha ubaguzi,yeye binafsi kachgua kumuita hivyo na Marando Kamuita Mzee wake mbona ukulalalmika alipomuita Mzee Marando kwa ubini huo!!!au basi kwa kuwa ni Nape basi!!Ebu tuwe tunawekana sawa kwenye yale ya msingi,semeni vitu vitakavyompa Nape nafasi ya kuendelea kuwepo hapa afunguke!!!Vinginevyo mnachangia watu kama Nape kuhalalisha kulikimbia Jukwaa kwa Msingi ya kuwa JF imevamiwa.Na ushahidi ni watu kama wewe.sometime ukiwa great thinker unajiongeza!!!1

acha hizo uliza mambo ya msingi kama data ya mawasiliano ya Mzee Marando na Jittu patel, hayo ndio maneno ya msingi!!Usiulize swali as if Mrs amekwambia muuulize Nape swali hili Jeetul Pael ni Babako?"Wewe tukikuliza Bhavick ni Bhaji? utasemaje?

hivi wewe umewai kumsoma Nappe akifunguka hapa zaidi ya kuleta propaganda zake na kukimbia.?
 
Tunahitaji kujua kwa undani maswala yanayohusu kesi ya EPA na jinsi CCM ilivyohusika, Marando is playing two roles kwenye hizo case kama informer wa CHAMA na kama wakili kwa taaluma yake!

Kama hawataki watuhumiwa wamnyime kazi! Ila hatuwezi kuacha kusema wezi wa EPA! Nnauye Jr alipaswa kujibu tuhuma zake za kadi mbili asitoe mapovu ya ku attack watu bila kujibu hoja!
 
wewe uliwataka wajivue magamba kwenye chama chenu, ukiwataka wawaachie chama chenu, mkikutana mnapeana mikono, unajichekesha huku unainamisha kichwa chini kwa kuona aibu. sasa hiv huo wimbo ndo umekuishia kbs.

huu sio unafiki.
Hamna tofauti na mnavyowaita masalia lakini wakikutana na Hao Viongozi wao wanacheka na kula pamoja...siasa waachie wenyewe wanasiasa
 
Back
Top Bottom