Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,890
Niwapatie background kidogo: Gazeti la Jumatano la Raia mwema lilipata matangazo toka Hazina kuhusu masuala haya ya malipo ya walimu na hivyo likachapisha matangazo hayo na ndiyo msingi wa email hii:
Mwandishi bulogu yake: kijana; nyegerage, karibuni, hiki ndo kijiwe chetu sema utakachokusema!!
My Take:
Natumaini Raia Mwema watachapa hiyo barua.
MwanaKijiji,
Nyagerage anapaswa kufahamu kuwa bila matangazo magazeti hayawezi kujiendesha. RaiaMwema sio gazeti la kupata faida, ni gazeti la huduma zaidi ili tupate kusoma makala kama za kina Lula etal.
Matangazo ambayo raiamwema imepata wiki iliyopita yaweza kusaidia kuchapa raia mwema kwa wiki kama tano zijazo na hivyo kutusaidia kupata ambacho hatupati kutoka magazeti mengine - habari za uchambuzi na uchunguzi.
Ninashauri tu kwa raiamwema kuwa inapotokea kuna matangazo mengi kama yale, basi waongeze ukubwa wa gazeti kwani wasomaji tunaonewa kwa kukosa makala. Pia waandishi wa makala kazi zao zakosa nafasi.
Barua hiyo ichapwe, lakini with a note ya mhariri kuwa gazeti haliendeshwi kwa mauzo tu ya gazeti bali kwa matangazo.
Mmesikia kuwa serikali imetoa notice kwa wizara kutopeleka matangazo yake kwa vyombo vya habari vya Mengi? Lengo ni kuua vyombo hivi na kumfanya Mengi aache kusimamia habari za ufisadi. Tanzania mtangazi mkuu ni Serikali - wanaJF tujue hilo.