Msiba wa dada mkwe unaibua maswali mengi yanayohitaji majibu

Msiba wa dada mkwe unaibua maswali mengi yanayohitaji majibu

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,621
Reaction score
6,510
Kuna msiba uliotokea ila umeibua maswali mengi ya chinichini. Kwa jicho langu la kijasusi najiuliza maswali hapa ambayo bado yanakosa majibu.

Kwanza, huyo dada mkwe anaitwa nani, mbona taarifa nyingi za huo msiba hazitaji jina lake?

Pili, mbona hatujaonyeshwa picha ya marehemu wakati wa uhai wake?

Tatu, kwa nini huo msiba haujafanyika kwa familia ya mhusika, yaani huyo marehemu dada mkwe?

Nne, huyo marehemu dada mkwe hakuwa na familia? Hakuwa na mume? Hakuwa na mtoto/watoto?

Tano, kuna uwezekano wowote kuwa huo msiba wa dada mkwe ulikuwa ni bosheni la kupotezea ule msiba mwingine ili mtu fulani asije kuulizwa kwa nini hakwenda kule msibani akakutana na watu walionuna?

Najiuliza tu kwa jicho langu la kijasusi. Tusaidiane kupata majibu.
 
Duuu kama tumefikia hapo ni pabaya sana.....kisa mali na madaraka mnaua kila mtu bila hatia
 
Back
Top Bottom