sajo

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
3,022
5,254
Msanii mkongwe wa Hip Hop nchini, Salutaba Mwakimwagile maarufu kama Salu T amefariki dunia jijini Mbeya leo tarehe 15 Aprili 2023. Msanii huyo amefariki akiwa anaendelea kupewa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Akitoa taarifa ya awali, Msanii mwingine wa HipHop, Taikun Ally maarufu kama Mchizi Mox ameeleza kuwa jumanne tarehe 12 Aprili 2023, Salu T akiwa mkoani Mbeya katika harakati zake za maisha, alipata ajali ya gari iliyomsababishia majeruhi na maumivu ya mgongo. Imeelezwa kuwa hali ya Salu T ilikuwa mbaya na hivyo kupewa rufaa ya kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili lakini hali yake haikuruhusu kusafiri na hivyo aliendelea kubaki hospitali ya Rufaa Mbeya mpaka umauti ulipomkuta.


Salu T amewahi kutamba na ngoma kama Chunga Sana aliomshirikisha msanii AY (2006) na kutayarishwa na Producer Lindu.


na ngoma nyingine nyingi, ikiwa ni pamoja na album iitwayo HAZINA.


Mchizi Mox ameeleza kuwa msiba wa Salu T upo nyumbani kwao marehemu mitaa ya Round about ya Mbuyuni, Kinyerezi Dar es Salaam na mazishi yanatajiwa kufanyika Jumatatu tarehe 17 Aprili 2023 jijini Dar es Salaam.

Pole kwa familia ya Salu T na wanaHipHop wote.

Mungu ailaze pema roho ya Salu T.
download (3).jpeg
download (4).jpeg

 
Msanii mkongwe wa Hip Hop nchini, Salu T amefariki dunia jijini Mbeya leo tarehe 15 Aprili 2023. Msanii huyo amefariki akiwa anaendelea kupewa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Akitoa taarifa ya awali, Msanii mwingine wa HipHop, Taikun Ally maarufu kama Mchizi Mox ameeleza kuwa jumanne tarehe 12 Aprili 2023, Salu T akiwa mkoani Mbeya katika harakati zake za maisha, alipata ajali ya gari iliyomsababishia majeruhi na maumivu ya mgongo. Imeelezwa kuwa hali ya Salu T ilikuwa mbaya na hivyo kupewa rufaa ya kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili lakini hali yake haikuruhusu kusafiri na hivyo aliendelea kubaki hospitali ya Rufaa Mbeya mpaka umauti ulipomkuta.


Salu T amewahi kutamba na ngoma kama Chunga Sana aliomshirikisha msanii AY (2006) na kutayarishwa na Producer Lindu.


na ngoma nyingine nyingi, ikiwa ni pamoja na album iitwayo HAZINA.


Mchizi Mox ameeleza kuwa msiba wa Salu T upo nyumbani kwao marehemu mitaa ya Round about ya Mbuyuni, Kinyerezi Dar es Salaam na mazishi yanatajiwa kufanyika Jumatatu tarehe 17 Aprili 2023 jijini Dar es Salaam.

Pole kwa familia ya Salu T na wanaHipHop wote.

Mungu ailaze pema roho ya Salu T.

M.A.P Salu T
 
Msanii mkongwe wa Hip Hop nchini, Salu T amefariki dunia jijini Mbeya leo tarehe 15 Aprili 2023. Msanii huyo amefariki akiwa anaendelea kupewa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Akitoa taarifa ya awali, Msanii mwingine wa HipHop, Taikun Ally maarufu kama Mchizi Mox ameeleza kuwa jumanne tarehe 12 Aprili 2023, Salu T akiwa mkoani Mbeya katika harakati zake za maisha, alipata ajali ya gari iliyomsababishia majeruhi na maumivu ya mgongo. Imeelezwa kuwa hali ya Salu T ilikuwa mbaya na hivyo kupewa rufaa ya kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili lakini hali yake haikuruhusu kusafiri na hivyo aliendelea kubaki hospitali ya Rufaa Mbeya mpaka umauti ulipomkuta.


Salu T amewahi kutamba na ngoma kama Chunga Sana aliomshirikisha msanii AY (2006) na kutayarishwa na Producer Lindu.


na ngoma nyingine nyingi, ikiwa ni pamoja na album iitwayo HAZINA.


Mchizi Mox ameeleza kuwa msiba wa Salu T upo nyumbani kwao marehemu mitaa ya Round about ya Mbuyuni, Kinyerezi Dar es Salaam na mazishi yanatajiwa kufanyika Jumatatu tarehe 17 Aprili 2023 jijini Dar es Salaam.

Pole kwa familia ya Salu T na wanaHipHop wote.

Mungu ailaze pema roho ya Salu T.

Nasikia alikuwa ni Shabiki mkubwa sana wa Yanga SC hivyo huenda mambo yakawa yameshatiki kwa Babu.

Simba SC Kesho mkipona sijui kwani nasikia tena kuna Mchezaji wao Kafiwa na Baba yake Mzazi.

Shikamooni Yanga SC na huyo Babu.
 
Ewe Mungu wangu nasema asante kwasababu,
Kukua kwangu baba na mama walipita tabu,
Sikuwa mstaarabu nilikuwa na shaka na imani yangu,
Vipi dini zote waanzilishi wazungu na waraabu,
Jamii ambazo ziliwatesa zetu mababu,
Walichanganya hatari nyingi hawakuwa na adabu,
Walinyang'anya mali nyingi ikiwemo dhahabu,
Je watu hawa wao hawakukanywa na vitabu,
Hapo sielewi mweza wa yote nipe jawabu,
Mola nimekosa najua nina gadhabu,
Kwa mema yangu machache naomba unipe thawabu niishi vyema nikifa uniepushie adhabu..

Salu tee - shukrani (Faraja records)

Pumzika kwa amani kaka mkubwa.
 
Back
Top Bottom