Msanii Soggy Doggy ajiunga CHADEMA

Msanii Soggy Doggy ajiunga CHADEMA

Pamoja na kwamba ninapenda mabadiliko, lakini hii sio sahihi na siafiki. Umaarufu sio uongozi. Huyu Soggy hivi bungeni ataenda kufanya nini? Jamani, ebu tuwe wakweli; hivi tunamuweka kwenye mizani gani tukimsoma Soggy kupitia kwenye ujumbe wa nyimbo zake? Kweli ana uwezo wa kuchambua masuala mtambuka yanayoikabili nchi?


CHADEMA, ni heri kuliacha jimbo kwa CCM (kama kuna mgombea bora) kama kuliko kupoteza nguvu na fedha kwa mtu ambaye sio sahihi.
Mkuu umenena yaani CDM kweli hakina viongozi hata huyu muhuni? Kweli kazi mmnayo
 
Wasanii sasa wameitambua kweli na wamepata ujasiri. Uoga pembeni na sasa wanathubutu.
 
kwani hawa VINEGA si walikuwa CHADEMA tangu zamani? Sasa mbona wanajiunga tena mmoja mmoja?
 
Welcome kamanda, speed ile ile kwenye kona120
 
hajipange.. Kubambikiwa kesi, kupigwa mabom na risas si mambo ya ajabu kutoka kwa chama kinacho ongozwa na Msomali na Savimbi.
 
Baada ya kufulia kwenye music wanakimbilia kwenye siasa.

Si kama wewe ulivyokimbia kwenye sheria baada ya kufulia na ukakimbilia kuuza poda! Ngoja wachina wakukamate tena tuone mshua ataweka pondi nini?
 
Mliwabeza sana wasanii wakati wanazuunguka na CCM kwenye mikutano na kampenizao leo hii mmeona ni wa muhimu. Kweli naamini ccm ndio baba wa demokrasia na mfano wa kuigwa ktk siasa.
Kweli naamini ccm ndio baba wa demokrasia na mfano wa kuigwa ktk siasa!

52fghv.jpg
 
Yaani hata wewe unawadharau watu wa segerea sana inabidi utuombe radhi maana huwezi kuwa kiongozi wetu. Umeacha ile tabia ya Mangwair? Maana wewe upo Kama the late kila mmoja anajua hilo
 
Huyu kijana ni mmoja wa wasanii waliokataa muda mrefu dhuluma inayofanywa na clouds entertainment wakaja na issue ya VINEGA akiwa na Sugu, Mkoloni na wengine. Sasa lady jd nae ndani
 
Karibu kamanda, hakuna kulala mpaka ukombozi wa kweli

Kamanda mla unga? Asije akawa Kama Mangwair maana Ule mchezo wake hajaacha. Huwezi pata kitu unapoteza muda wako bure lakini hata wewe huna cha kupoteza maana huna Mbele wala nyuma najua muziki haupo nawe tena
 
Uwiiiiiii sasa baaaaasi.
Siasa ya tanzania imevamiwa na wavuta bangi.Huyo jamaa karakata nzima wanamjua kwa kuvuta bangi na kunywa gongo,na ata kule radio uhuru walimtimua kwa sababu za ulevi,hapa Arusha aliwahi kufanya kazi kwenye radio moja hivi,siku moja akawa na kipindi cha mangoma ya usiku,akapanga ma 'CD'kwenye automatic player kisha akaenda zake disco 7x7,ngoma ilipofika saa 8 usiku ikakata,tajiri(boss wake)kasubilia dk 10kitu hakiungi,akaamua kupiga simu akaambiwa jamaa katoka tangu saa4 usiku.Kwa kumuonyesha kwamba kachukia ikabidi tajiri aende mwenyewe kukimbiza kipindi mpaka alfajiri,jamaa alivyorudi saa 11 akakabidhiwa na barua ya kutemwa mzigo.
Sasa hao ndio wawakilishi wetu bungeni lol.
 
Kwani huyo MAKONGORO alishawahi kufanya nini, waache wananchi wataamua wenyewe???

Simtetei Makongoro, lakini kwa vigezo vya uongozi huwezi mlinganisha na Soggy! Tuache siasa, mimi napenda mabadiliko bila kuuweka uongozi rehani.

Hili sio suala la Makongoro atoke, ni suala la nani anamtoa ili tupate kiongozi wa kusukuma agenda za maendeleo. Mpaka sasa CHADEMA wana timu nzuri ya wabunge: Mnyika, Zitto, Lema, Wenje, Mdee nataja kwa uchache, wenye weledi wa hali ya juu. Tunahitaji wengine wa kariba hii.
 
Back
Top Bottom