Msamvu, Morogoro: Vibanda 8 vya biashara katika eneo la Stendi ya Mabasi vyateketea kwa moto

wewe tena!? Nimepamis hapo.. Sema naonaga kelele sana ... Sijakaa miaka almost 2! Mambo vip boss!.. Jumamosi kama utakuwepo tukae hapa Don! Ndio chimbo nalolipenda ati!
Si unajua wazee wa matukio
Mm nna nyota ya kukutana na matukio, visanga basi shidaa tu
Kelele si ndy poa hulali pale pako poa kama unataka kukesha

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Hebu chukua tahadhari mkuu, jikinge. Bado tunakuhitaji sana.

Ni hitilafu ya umeme au chanzo ni nini? Walifanikiwa kuuzima kwa wakati kabla madhara makubwa kutokea?

Shukrani
Hajafa mtu.... Sema Mali ziliharibika
Sisi tulikuwa Ndani bado tunapiga masanga
Uzuri wengine wakiwa vyombo ndy akili inazidi kuchaji...
Yah Yawezekana chanzo ni umeme mkuu

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Msamvu B iko kata ya Kihonda Maghorofani, Iko mbali sana na Msamvu Stand,

Msamvu stand ndio sehemu ilipotokea ajali,

Huyo mwamba alisema Itigi, Itigi nibar/guest house vijana walikuwa wanajiponea iko Msamvu

Sasa anadhani Itigi ni mtaa, ilhali hakuna mtaa wa Itigi, Msamvu
Kwamba ajali ilitokea Msamvu stendi bro?
 
Moto ambao haujafahamika umesababishwa na nini umewaka na kuteketeza vibanda vya biashara takriban 8 katika eneo la stendi ya Msamvu, usiku wa kumakia leo

Akizungumza baada ya kuudhibidti moto huo, Kamanda wa Uokoaji na Zimamoto mkoani humo, Godluck Zerote amesema hakuna mtu aliyedhurika bali mali peke yake

Amesema eneo hilo vibanda hivyo vimebanana sana vikiwa zaidi ya 20 hivyo baada ya kuudhibiti moto ndio wataanza kuangalia thamani ya mali na chanzo cha moto

View attachment 1464111
Duh, Mungu atunusuru
 
Majanga yatupe somo kuboresha jeshi la zima moto, tozo ni nyingi kuanzia mfanyabiashara duka,.... nashauri tozo hizo ziwe kama Bima, ili ikitokea ajali wahanga wafidiwe.
Wafanyabiashara wajifunze kuweka insurance kwenye mali zao (biashara), vile vile watu wajiwekee insurance kwa nini wategemee wengine wawafanyie hivyo? Tozo zinazokatwa ni kwa mujibu wa sheria haziwezi kuwa insurance.
 
Aisee alafu mara nyingi ajali za moto huwa zinatokea usiku, sijajua hapa huwa ni kwa nini hasa!
Huu ni utaalamu wa viongozi wetu katika kuondoa eneo la biashara ambalo halina mpangilio mzuri, matukio mengi ni ya kupangwa believe me.
 
Halikuanguka hapo msamvu...Ni mitaa ya Itigi.
Au ulikuwepo eneo la tukio?
Ni sawa na ajali itokee pale ubungo maji halafu useme imetokea ubungo stand kiufupi sio msamvu ila ni Kama km 0.5 toka msamvu zamani palikuwa na kiwanda Cha uchapishaji nyuma yake pana Gest mpya nzuri na hapo hapo pana bar karibu na mafundi wa kutengeneza magari kwahiyo sio msamvu kabisa.
 
Back
Top Bottom