Dar: Soko la Mabegi Karume laungua moto alfajiri ya Aprili 8, 2022

Tipstipstor

JF-Expert Member
Nov 29, 2021
1,531
3,331
Vibanda vya wafanyabiashara wadogo 'Machinga' na mama lishe zaidi ya 30 vimeteketea kwa moto katika Soko la Karume Jijini Dar es Salaam, asubuhi ya leo Aprili 8, 2022.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam (ACP), Muliro Jumanne Muliro amekiri kutokea kwa moto huo na kusema chanzo cha moto hakijajulikana lakini uchunguzi unaendelea, japo taarifa za awali zilionyesha kuwa moto ulianza kwenye kibanda kimoja na kisha kusambaa.

"Kwa mazingira yalivyo pale, vibanda vingi vimebanana na vipo kila baada ya hatua mbili, hivyo moto unapotokea ni rahisi kusambaa, bahati nzuri ni kuwa umeshadhibitiwa, na watu wa usalama wapo eneo la tukio," amesema Muliro.

Naye, Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Ilala, Elisa Mugisha amesema timu yake imeudhibiti moto huo ambao pia umeunguza mabanda ya wafanyabiashara wa mabegi.

=================================

Majira ya muda wa saa 11 alfajiri ya leo, moto umewaka na kuteketeza soko la wamachinga wauza mabegi karume.

Matukio ya picha

IMG_20220408_060829.jpg

Moto bado unaendelea kuwaka huku vikosi vya zimamoto na uokoaji vikiendelea na harakati ya kuuzima

IMG_20220408_060916.jpg
 
Moto bado unaendelea kuwaka huku vikosi vya zimamoto na uokoaji vikiendelea na harakati ya kuuzima

View attachment 2179976
Please my president Samia, rudisha vikosi vyote vya uookaji including Fire Brigade kwa local government's, kila Halmashauri iwe na kikosi chake cha uookaji na ondoa uaskari kwenye vikosi hivi, hii itaongeza ufanisi wa huduma hizi
 
Hilo jeshi la zimamoto na uokoaji lifumuliwe na lenyewe.

Yaani eneo moja linaungua kwa interval ya miezi ila kila siku eneo linateketea?

Huu si utoto huu?

Au basi acheni kufanya jeshi liajiri 4 za mwisho pekee.

Na zile kamati zilizoundwa members wakamatwe.
 
Hilo jeshi la zimamoto na uokoaji lifumuliwe na lenyewe.

Yaani eneo moja linaungua kwa interval ya miezi ila kila siku eneo linateketea...
Kwanza soko hilo lilikuwa na vifaa vya kuzimia moto? Hili jeshi si linatakiwa kufanya ukaguzi huo?
 
Back
Top Bottom