weka hata nyama kidogo,
uliiona katika TV Video za Library au You Tube?
ngoja waje wakupe Summary maana km ni hii fuatlia kwenye Wikipedia huwa wanaelezea pia unaweza kuitafsiri hiyo summary kwa Kiswahili, anzia kwenye Plot na Cast
View attachment 1766988 View attachment 1766990
Tenet (film) - Wikipedia
en.wikipedia.org
Ndo hiyo mkuu.
Nimeiangalia jana naona tu mapicha picha.
Niliiangalia majuzi hapa, na tumeisubiri muda sana toka ilivyoanza kutengenezwa. Jinsi ilivyoisha inaonekana itaendelea ya pili.Now naangalia Mortal Kombat
WAKUU MPO POA
Leo nilikuwa na watch movie inaitwa TENET.
Kusema la ukweli hii movie sijaielewa.
Ningependa kwa mkuu aliyebahatika kuiangalia just anipe hata kasummary kidogo kuhusu hii movie.
Umefafanua vyema sanaTENET
Spoiler Alert
kama haujaiangalia ukaichek kwanza.
Ntajaribu Kuielezea kwa kadri ntakavyoweza
Cha kujua kuwa hii Movie ni War kati ya Future na present kuwa future wamemind kwa sababu watu wa past( ambao ndio sisi yetu present) wamefanya maamuzi mabaya wakasababisha mazara kwa future kama climate change na mengineyo ambayo yakapelekea vita kwahyo future ikabuni Technology ya kurudi past inaitwa Inversion unaweza uka invert watu na objects kutoka future kuja past sema sasa huku past inverted object au person anakuwa anaenda kinyume nyume si kwa sababu kawa inverted, ila yeye aliekuwa inverted anaona kuwa anaenda kawaida sasa wewe ambao hauko inverted ndio unamuona kuwa anarudi nyuma nyuma. Sijui nime make sense
PLOT,
Agent Wa CIA anaitwa Protagonist ndio Main character na Ndio maana ya protagonist crazy right , kwahyo kwenye hii Mission Protagonist anakamatwa na bad guys anateswa kuepuka kutoa siri anakunywa kile kidonge akijua ni sumu ili afe asitoe siri shockingly kumbe sio sumu ilikuwa ni test ya kuona kama yuko Loyal(muaminifu) kuwa recruited na Organization inayoitwa Tenet(jina la movie) hio taasisi imekuwa created na yye mwenyewe in future
Protagonist ataenda kukutana na watu maana hii movie watu wanakutana sema story short ataenda kukutana na huyu Mwanasayansi mwanamama ambae atamuonyesha risasi ambazo ziko inverted( ziko zinaenda kinyume na mda zimetengenezwa kutoka future iko hivi mfano kuokota msumari inabidi uimagine kama unaangusha msumari in reality unauokota sijui kama namake sense? you get the idea) so ikabidi watafute risasi hizo zimetoka wapi ndio wakaenda kwa yule Mama wa kihindi Priya wakati huo Kaongezeka Neil (Robert Pattinson jamaa wa Twilight ile Vampire Movie) so wakagundua kua Priya alimuuzia Silaha jamaa Sator Russian guy yule.
So hapo Protagonist akaenda London akakutana na mke wa sator akawa anamwambia drama zake kuhusu mme wake gaidi anavyo mblack mail kuhusu fake drawing aliyoiuza yule mwana mama anauza ma drawings kama ulivyoona blackmailing kwa kiswahili sina neno lake.
Baada ya hapo wakapanga kwenda kuiba ile drawing airport hapo ni protagonist na Neil wakavamiwa na watu wawili wenye mask ambao wako inverted wamevaa mask ukiwa inverted unavaa mask na wale watu ni futureselves ya wale jamaa walikua wanazile mask pia wasionekane sura ili wakirudi past wasionane yani watu wawili kwenye timeline moja italeta annihilation(yeap sina maelezo mengi physics yenyewe nnayo ya advance level elimu ya Tz)
Kat alimuintroduce Protagonist kwa sator mara akamuokoa maisha yake bla bla wakawa patner nn ikabidi waende kuchukua case yenye ile Plutonium kukatokea na ile car chase pale kwenye ile scene ya heist ambayo kuna inverted cars nn ilikuwa mind blowing. Protagonist na Neil wakaiba ile Case Mara wakaja wakavamiwa na Mchizi Sator ambae yuko inverted huku kamchukua Kat(mke wake) mateka,
..... Mambo mengi yakatokea the point mwishon ni kwamba huyu sator alikuwa anaumwa cancer kwahyo akakusanya vipande tisa vya algorithm ( device ambayo ilikuwa inaweza kusababisha global destruction), so kumzuia ikabidi Troops zisafiri past pale kuna Neil na Protagonist kwenda kuilinda ile Algorithm na kuaminisha kuwa sator kafanikisha Mission yake kumbe sio ambao atauliwa na inverted Kat ambae baada ya kumuua mme wake ataruka kwenye boti kama unakunbuka mwanzon Kat alimuona mwanamke anaruka kwenye ile yatch. so vipande vya algorithm watavisambaratisha viwe tofauti maana visiwe pamoja, Lastly jua kuwa Tenet ilianzishwa na Protagonist Na Neil inasemekana kuwa ni mtoto wa yule MaMa -Kat kumbuka ana kadogo kale alikokuwa anakapeleka shule considering Neil alipokutana na Protagonist alikuwa anajua favourite drink yake na kuwa protagonist huwa hanywi akiwa anafanya kazi inaonekana kuwa wanajuana in the future.
Nimejaribu kuandika ndefu as i can it turned out muda wa kuandika sana haupo, sema sorry kama bado haieleweki, whatsoever...sio lazima uelewe kila kitu na kama umepata kamwanga inatosha, poa _Gudluck
Hizo movie mtu asikudanganye kuwa kaelewa. Mpaka upate ABC zake wikipedia au kwenye mitandao inayozielezea. Hata utulie lazima zitakuacha.Kila mtu ukimuuliza anasema unatakiwa utulie na utumie akili, tumetulia na kutumia akili bado hatujaelewa. Basi tumekubali hatuna akili mtuelezee sasa.