Msaada kisima changu kimejaa chura

Msaada kisima changu kimejaa chura

Wana JF ninapoishi mimi sina access na maji ya bomba ambayo unalipia bili kwahiyo nimeamua kuchimba kisima na maji nimepata tatizo vyura wamegeuza ndio makazi yao wapo wengi hadi kero, sasa kuna madhara yoyote kutumia maji ambayo vyura wanaishi humo?

Natumia kuoga, kufulia na kuoshea vyombo, sipikii wala sinywi ingawa natamani kuanza kupikia.
Kwani chura makazi yake wapi? Uwaandalie makazi halafu ulalamike
 
nenda idara ya maji, waeleze tatizo.......utapata suluhu....ila kumbuka visima vina tozo ya serikali....jipange....
 
Fuga tu Samaki Mkuu, hao Vyura watageuzwa Chakula Asubuhi tu.
 
Mkuu weka chlorine ila tafuta mtaalamu akapime maji yako kabla ya kuweka chlorine ili ajuwe chemical properties ya maji yako
 
Ata akiweka sato wa 5 wakubwa kiasi wanauwa vyura wote
Akiweka Sato hatayatumia tena hayo maji maana litageuka kuwa bwawa la samaki. Sato wana tabia ya kuzaliana kwa haraka hivyo watajaa kwenye hicho kisima, pia sina uhakika kama Sato ataweza kuwameza vyura wakubwa. Bora atupiemo Kambale.
 
Natafuta madume mawili, sichanganyi jinsi maana unaweza solve tatizo la chura ukaweka tatizo la kambale
Kambale ata ukichanganya jinsia Haina tabu,hawawezi zaliana kwenye icho kisima,wataishia kugongana tu,ukikosa hao kambale nicheki pm
 
Back
Top Bottom