Msaada juu ya kaka yangu, nifanyeje?

Msaada juu ya kaka yangu, nifanyeje?

Mwambie kaka yako atafute kwake...kwani si ana kazi yake?
 
Mi nimeolewa miaka miwili iliopita lakini kutokana kutafta maisha mme wangu anaishi nchi za nje kutafta maisha nakweli mungu mwena tunaendelea vyema pamoja kwamba hayuko hapa.

Alimchukuaga kakaangu kamtaftia kazi huko kakaangu kutokana natabia yake nakujingiza katika kazi flani akawa deported

Kutokana kwamba nimtu wastarehe sana hela aliokua nayo ilivyoisha tukakubalina pamoja na mme wangu aje tuishi pamoja hapa Arusha maana hakuna watu wengi sana nyumbani.
Sasa kilichonifanya niandike hii post kakaangu anabadilisha wasichana mpaka naogopa kila siku lazima alete mwanamke napia alishawahi kumleta sister hadi.

Kwaupande wangu naumia jinsi anavyo chezea watoto wawatu wengine wanakua namatumaini kwamba atawaoa kumbe hana huu mpango. Ambao tumezoweana kwa haraka wananipigia cm wakilia juu yake wala hata yy hana habari
Namweshim sana maana he is over 35 kwahyo amenizidi ka miaka 10. Natafta jinsi yakuongea nae nashindwa
Naomba mnisaidie nifanyeje aweze kuwa na msichana moja tu basi hata wawili sio kukutana kwenye corridor na sura mpya kila cku.

Lakini pia tangu j. Mosi iliopita alileta mwanamke moja nimkubwa kama mamayetu kama 45-50 alafu cjawahi kuona akika na mwanamke mda mrefu hivo amejichubua vibaya sema mstarabu alafu anjituma sana jikoni. Pili huyu mama msafi sana pamoja kwamba ni mnene ila anajitahidi kazi hapa napale Sasa naona kakaangu kafika kwamara yakwanza naona akitoka kazini kuwahi nyumbani kumchukua bibie nakwenda Mjini kupooza koo. Sina shida nahuyu mama sema mamaangu mwezi wa10 anakuja nyumbani nahuyu mama naona ndo kafika hadi naona anazungmzia kuweka banda lakuku.

Ebu naomba mnishauri jinsi yakumwambia either aondokena huyu mamaake mlezi maana yetu nae sio habba atokubali kwa jinsi navyo mjua mama pia ana pressure, au huyu mama aondoke mwenyewe maana kaka hata hajigusi wala kumhofia maza. Nifanyeje wakuu
miaka 35 anaish kwa shemeji hadi analeta mchumba humo humo hamna kitu tena humo
samaki mkunje angali mbichi
mtimueni msimpe favour za kipuuzi ayajue maisha
ww unahisi unampenda kwa msaada unaompa bt ukweli ni unamuharibu mm 20 yrs tyr nilikua na maisha yangu
 
Kukaa na kaka MTU anamiaka zaidi ya 35 eti mnaishi naye tena Wa kiume nimekushangaa sana.
 
Mwambie apange chumba chake plz huo ndo ushauri Wangu maana kwetu miaka kumi na nane tu! Anaanza kujitegemea.
 
Mi nimeolewa miaka miwili iliopita lakini kutokana kutafta maisha mme wangu anaishi nchi za nje kutafta maisha nakweli mungu mwena tunaendelea vyema pamoja kwamba hayuko hapa.

Alimchukuaga kakaangu kamtaftia kazi huko kakaangu kutokana natabia yake nakujingiza katika kazi flani akawa deported

Kutokana kwamba nimtu wastarehe sana hela aliokua nayo ilivyoisha tukakubalina pamoja na mme wangu aje tuishi pamoja hapa Arusha maana hakuna watu wengi sana nyumbani.
Sasa kilichonifanya niandike hii post kakaangu anabadilisha wasichana mpaka naogopa kila siku lazima alete mwanamke napia alishawahi kumleta sister hadi.

Kwaupande wangu naumia jinsi anavyo chezea watoto wawatu wengine wanakua namatumaini kwamba atawaoa kumbe hana huu mpango. Ambao tumezoweana kwa haraka wananipigia cm wakilia juu yake wala hata yy hana habari
Namweshim sana maana he is over 35 kwahyo amenizidi ka miaka 10. Natafta jinsi yakuongea nae nashindwa
Naomba mnisaidie nifanyeje aweze kuwa na msichana moja tu basi hata wawili sio kukutana kwenye corridor na sura mpya kila cku.

Lakini pia tangu j. Mosi iliopita alileta mwanamke moja nimkubwa kama mamayetu kama 45-50 alafu cjawahi kuona akika na mwanamke mda mrefu hivo amejichubua vibaya sema mstarabu alafu anjituma sana jikoni. Pili huyu mama msafi sana pamoja kwamba ni mnene ila anajitahidi kazi hapa napale Sasa naona kakaangu kafika kwamara yakwanza naona akitoka kazini kuwahi nyumbani kumchukua bibie nakwenda Mjini kupooza koo. Sina shida nahuyu mama sema mamaangu mwezi wa10 anakuja nyumbani nahuyu mama naona ndo kafika hadi naona anazungmzia kuweka banda lakuku.

Ebu naomba mnishauri jinsi yakumwambia either aondokena huyu mamaake mlezi maana yetu nae sio habba atokubali kwa jinsi navyo mjua mama pia ana pressure, au huyu mama aondoke mwenyewe maana kaka hata hajigusi wala kumhofia maza. Nifanyeje wakuu
Kaka yako ni hasara nawe pia bila kumsahau mumeo

Nyie mkaka wa miaka 35 anakaa kwenu na mnamruhusu analeta wanawake ndani??
 
Kilichobaki ni wewe na kaka yako kuwa deported kijijini kwenu na mmeo.Familiya yenu ni ya ajabu mno,kitu la miaka 35 limechukuliwa na shemeji kutafutiwa kazi nje alafu linazingua mpaka linarudishwa,alafu bila aibu linafikia tena kwa shemeji na kama haitoshi linabadilishia wanawake hapo.Huyo mmeo hana ndugu wanaokutembelea hapo na kuwasiliana na ndugu yao?.Narudia mtakuwa deported kijijini kwenu wewe na kaka yako.
 
Lijitu lina miaka 35,linaishi kwa Dada...ajabu sana si uliambie liende kijijin likakate mkaa...
Alafu hiyo tabia mmemuendekeza mwachen tu aendelee na mama kubwa wake si mmekubal hapo kwako ni lodge hata humuonyi?
 
SPIRIT OF LUST is disturbing your loved broda. ntakusaidia kumwombea aisee NiPM JINA LAKE NIANZE KAZI THIS TIME.
 
I wish you knew me kuna member humu wananifaham am not of that type. Pili baba yetu alishaaga dunia kaka kachukua majukum ya kunisomesha. Sikutaka kuliongelea hili maana hafanyi kwasasababu alinisomesha hajawahi kunisimanga hata cku moja

Ila kama kakaangu namweshim sana. Najua hata humu sio wote mna ndugu zenu. Wakubwa huwezi out of nowhere kuanza kufukuza. Ndomaana nimeomba usahauri
Huyo ndo wakusomesha mtu?
 
Mtoa mada samahani,familiya yako ni wenyeji wa mkoa gani?.
 
Nimesoma, nilipofika hapo kwenye "anazungumzia kuweka banda la kuku" ikabidi ni pause kwanza nicheke....usikute ndiye aliyeweka ule uzi wa vifaranga vya kuchi.

Au unamkata sana jicho akaona atafute mbinu ya kukwambia "hapa ndio nimefika shoga"
 
Kosa lako ni kumfanya kaka yako awe tegemezi anamatatizo gani 35yrs kuishi kwa shemeji??
 
Havina uhusiano. Tafautisha character, behaviour na personality. Naomba tu ushauli wako. Alafu huko nyuma hakuwa hivyo
Kama ni kukusomesha alikusomesha wewe siyo mmeo.Mwanamke mpumbavu huivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe.Mmeo haifurahii hali hiyo,unadhani watu wa familiya yake wanaweza kukutembelea hapo kwa namna hiyo?.Mmeigeuza Nyumba kuwa danguro alafu unasema eti anakaangiza.Vitabia vya malezi ya pwani ndo vijana wanalelewa kijinga hivyo.Mkoa ninaotoka mimi hili ni jambo la aibu mnoo,Katika ukoo wenu hakuna wanaume wenye ajili kumuondoa japo?.eti alinisomesha,upuuzi huo.Kaka yako amelelewa na mama yenu katika hali ya kutokuwa responsible ndio maana hana hata familiya wala kupanga chumba kimoja kiburugwa.
 
Kumbe ni wewe? Habari za moshono? Pole sana, duh kudeal na huyo bro ako ni ngumu,jaribu kumueleza waziwazi kuwa mama anakuja na haitaleta picha nzuri yeye alale hapo na mzigo wake tena umri sawa na mama,akishindwa kuelewa mwambie mumeo,mumfukuze yawezekana anafanya hao mambo kisa hana mizigo ya kulipia utilities kodi ya pango,umeme,maji na taka n.k akitoka kwenda kujitegemea akili itasogea
 
Kama ni kukusomesha alikusomesha wewe siyo mmeo.Mwanamke mpumbavu huivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe.Mmeo haifurahii hali hiyo,unadhani watu wa familiya yake wanaweza kukutembelea hapo kwa namna hiyo?.Mmeigeuza Nyumba kuwa danguro alafu unasema eti anakaangiza.Vitabia vya malezi ya pwani ndo vijana wanalelewa kijinga hivyo.Mkoa ninaotoka mimi hili ni jambo la aibu mnoo,Katika ukoo wenu hakuna wanaume wenye ajili kumuondoa japo?.eti alinisomesha,upuuzi huo.Kaka yako amelelewa na mama yenu katika hali ya kutokuwa responsible ndio maana hana hata familiya wala kupanga chumba kimoja kiburugwa.
Umeongea kwa hisia kuliko ushauri. Nini shida mkuu. Ndomana awali ckutaka kulizungumzia hilo
 
Back
Top Bottom