Msaada juu ya kaka yangu, nifanyeje?

Msaada juu ya kaka yangu, nifanyeje?

Mmelea wenyewe vibaya

Eti nipeleke demu nikalale nae kwa dada/shemeji

Halafu sio mmoja mademu lukuki

Mnaishi kizungu sio? Hamna namna mfundisheni maza nae uzungu.....

Adabu gani hio kenge bluu
I wonder
 
Mi nimeolewa miaka miwili iliopita lakini kutokana kutafta maisha mme wangu anaishi nchi za nje kutafta maisha nakweli mungu mwena tunaendelea vyema pamoja kwamba hayuko hapa.

Alimchukuaga kakaangu kamtaftia kazi huko kakaangu kutokana natabia yake nakujingiza katika kazi flani akawa deported

Kutokana kwamba nimtu wastarehe sana hela aliokua nayo ilivyoisha tukakubalina pamoja na mme wangu aje tuishi pamoja hapa Arusha maana hakuna watu wengi sana nyumbani.
Sasa kilichonifanya niandike hii post kakaangu anabadilisha wasichana mpaka naogopa kila siku lazima alete mwanamke napia alishawahi kumleta sister hadi.

Kwaupande wangu naumia jinsi anavyo chezea watoto wawatu wengine wanakua namatumaini kwamba atawaoa kumbe hana huu mpango. Ambao tumezoweana kwa haraka wananipigia cm wakilia juu yake wala hata yy hana habari
Namweshim sana maana he is over 35 kwahyo amenizidi ka miaka 10. Natafta jinsi yakuongea nae nashindwa
Naomba mnisaidie nifanyeje aweze kuwa na msichana moja tu basi hata wawili sio kukutana kwenye corridor na sura mpya kila cku.

Lakini pia tangu j. Mosi iliopita alileta mwanamke moja nimkubwa kama mamayetu kama 45-50 alafu cjawahi kuona akika na mwanamke mda mrefu hivo amejichubua vibaya sema mstarabu alafu anjituma sana jikoni. Pili huyu mama msafi sana pamoja kwamba ni mnene ila anajitahidi kazi hapa napale Sasa naona kakaangu kafika kwamara yakwanza naona akitoka kazini kuwahi nyumbani kumchukua bibie nakwenda Mjini kupooza koo. Sina shida nahuyu mama sema mamaangu mwezi wa10 anakuja nyumbani nahuyu mama naona ndo kafika hadi naona anazungmzia kuweka banda lakuku.

Ebu naomba mnishauri jinsi yakumwambia either aondokena huyu mamaake mlezi maana yetu nae sio habba atokubali kwa jinsi navyo mjua mama pia ana pressure, au huyu mama aondoke mwenyewe maana kaka hata hajigusi wala kumhofia maza. Nifanyeje wakuu
Wewe na kaka yako nyote watoto wa mama
 
Kaka over 35 mama mzazi between 45-50 hata kwa mimba za utotoni ni ngumu kumeza, mama awe na miaka 45 mtoto wake over 35 duh... chai ya rangi
 
So unamaanisha mwanaume mwenye ndevu zake anaishi kwa shemeji yake siyo?
 
Hivi inakuaje mwanaume uchukue demu uende kumgongea kwa sista? Uyo sista anae ku ruhusu atakua ana akili timamu kweli au chizi? Kaka ako hana makosa sababu anaonekana wazi tu aliwai kuugua maralia sugu ikampanda kichwani.
 
KWANZA NAKUOMBA MUNGU NIEPUSHE NA MWANAMKE WA HIVI HATA KWENYE KIZAZI CHANGU.

Kuna mtu hapo juu kakuambia ukweli ukasema amejibu kwa hisia sio ushauli tho hata wewe unambeba uyo kakako kwa hisia sio uhalisia.

Najaribu kuwaza kama mnawatoto humo ndani sijui mnatengeneza kizaz cha haina gani hasa kwa watoto wa kiume!.

Dada hakuna maamuzi utaweza fanya daima kwa kutotaka kuonekana mbaya, otherwize unaenda kua kwenye kundi la WANAFIKI.

Pia nachokiona upotayari kuambiwa vile ambavyo ushajishauri tiyari ila hauko tayari kushauriwa.

Kwa maana iyo leo na kesho mumeo asipokuwepo(mungu aepushe) means ukitaka kumtoa kaka yako akalialia kua ndo malipo unayomlipa hayo then utakubali kubeba iyo character yake maana usidanganye watu CHARACTER ndo imebeba wasifu wote wa mtu.

Kama kaka anakupa ugumu ivo ni vipi kesho watoto wako uliowazaa/utaowazaa wakikua na baba akawa hayupo wakanza tabia kama za mjomba wao utaweza kiwamanage? Utawakatazaje na leo hii wanaona haya, je wakija mdugu wa mume wakaiga utaweza kuwamanage? Je utalaumu?

Mi naona bado mentally unautoto haujawa matured enough kua mama na kiongozi msaidizi wa familia, wamekupa JOHO kabla hujagraduate, hata uyo kaka yako bado kijana tuu ila unampa heshima na ukubwa asio kua nao. Daima huwezi kumlea mtu mzima, huwezi kulipa fadhira kwa kukumbatia ujinga, maana hata yeye hawez kukulipa unavyombeba leo kwenye nyumba yake. Hatulipani mema kwa kutukuza maovu, tunalipana mema kwa wema, Kwanini unashidwa kuusema KWELI juu batiri kisa huonekane mzuri! huo ni UNAFIKI daraja la kwanza. Kila kitu kinamipaka na mtu akishavuka mipata lazima apokee matokeo.

Ok mi ushauri wangu ni kua kwanza msimfukuze tho najua hamuwezi/mtashidwa. Inabidi kwanza huende kwa viongozi sahihi wa dini yako wakumentol, ukiwakosa nambie nitakudirect, wakufundishe kujielewa position yako ya kua mke wa mtu na namna ya kulinda heshima ya mumewako nyumba yako na familia yako in general kama mke/mwanamke.

Sababu tatzo haliko kwa kaka yako, tatizo lipo kwako. We ukishajitambua vizuri bas utaweza kuishi na watu vizuri na zaidi ukimtanguliza mungu.

JARIBU KUA MTU BORA NA SIO KUA MTU MZURI.

(AN-NISAAI-5)

Wala msiwape wasio na akili mali yenu ambayo Mwenyezi Mungu ameyajaalia yawe ni kiamu yenu.


YOHANA 2:12-

“..kawakuta mle hekaluni watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao. Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazitawanya sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao. Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, “Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!”.
 
JamiiForums2144198311.gif
 
Back
Top Bottom